• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

Wakazi wa kijiji cha Tangazo wafaidika na Kliniki tembezi ya kifua kikuu

 

wananchi wa kata ya Tangazo wakipata huduma ya uchunguzi wa ugonjwa wa TB (Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa Kata ya Tangazo, Mtwara, wameishukuru serikali kwa kuwaletea kliniki tembezi ya uchunguzi wa kifua kikuu, hatua iliyowapunguzia gharama na kurahisisha upatikanaji wa matibabu, huku wakitaka kampeni hizo ziendelee vijijini.

Na Musa Mtepa

Wananchi wa Kata ya Tangazo, mkoani Mtwara, wameipongeza serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kupeleka kliniki tembezi ya uchunguzi wa ugonjwa wa kifua kikuu (TB) katika kijiji chao, hatua waliyoeleza kuwa imepunguza gharama na kurahisisha upatikanaji wa huduma za matibabu.

Wakizungumza na Jamii FM Radio, wakazi wa kata hiyo wamesema huduma hizo zimekuwa mkombozi kwao, hasa kwa kuzingatia hali ngumu ya kiuchumi inayowakabili.

Sauti ya Bi Salma Mpando na Ismail Kambutu wakazi wa kata ya Tangazo

Wengine walioeleza shukrani zao ni pamoja na Mzee Mtalika Lilala na Abdala Salum Kibokotwe wa Kijiji cha Tangazo ambapo pamoja na yote wamependekeza kliniki tembezi hizo ziongezwe kwa magonjwa mengine

Sauti ya Mzee Mtalika Lilala na Abdala kibokotwe wakazi wa Kijiji cha Tangazo

Kwa upande wake, Mratibu wa Kifua Kikuu na Ukoma Mkoa wa Mtwara, Dkt. Maikoadi Skoni, amesema kliniki tembezi hiyo ilizinduliwa rasmi Agosti 1, 2025, katika Viwanja vya Mkanaledi, Manispaa ya Mtwara Mikindani. Kampeni hiyo inalenga kufikia halmashauri zote tisa za mkoa wa Mtwara.

Sauti ya 1 Dkt Maikoni Skoni mratibu wa TB na Ukoima mkoa wa Mtwara

Amesisitiza kuwa huduma hizo zinatolewa bure, na wagonjwa wote watakaobainika huunganishwa moja kwa moja na vituo vya afya vya karibu ili kupata matibabu zaidi.

Sauti ya 2 Dkt Maikoni Skoni mratibu wa TB na Ukoima mkoa wa Mtwara

Naye Dkt. Boniface Jengela, Mratibu wa TB na Ukoma katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, amesema lengo kuu la kampeni hiyo ni kuwafikia wananchi wanaoishi mbali na vituo vya afya na kuwatambua mapema wanaoonesha dalili za kifua kikuu.

Aidha Dkt Boniface amebainisha kuwa dalili wanazozinaglia ni pamoja na  kukohoa zaidi ya wiki mbili,kutoka jasho wakati wa usiku na viashiria vingine  huku akiwataka Wananchi kuitikia kwa uwingi maeneo yote yatakayopitia na kampeni hiyo.

Sauti ya Dkt Boniface Jengela mratibu wa kifua kikuu na ukoma Mtwara D

Kampeni hii ni sehemu ya juhudi za serikali kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu nchini ifikapo mwaka 2030.

Share:

Mchango wa wazazi, walezi kupunguza watoto wa mtaani

 

Mmoja wa wadau akizungumza katika kipindi. Picha na mwandishi wetu

“Mtaa hauna mtoto ila watoto wanatoka kwenye jamii zetu wenyewe”

Jamii inapaswa kuzingatia malezi bora ya watoto na kupunguza au kuacha kabisa kutelekeza familia zao jambo ambalo linapelekea watoto wengi kushindwa kupata malezi bora na huduma stahiki katika ngazi ya familia na kupelekea watoto hao kukimbilia mitaani ili kujitafutia mahitaji na hapo ndipo linapozaliwa jina la Watoto wa mitaani.

Kiuhalisia mtaa hauna mtoto ila watoto wanatoka kwenye jamii zetu wenyewe na zipo sababu nyingi zinazopelekea tatizo hili ambalo limekuwa kubwa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwemo Mtwara, 

Kwakuliona hilo Jamii FM Radio tumekuandalia kipindi kinachoangazia Mchango wa wazazi na walezi katika kupunguza watoto wa mtaani, Kipindi hiki kimekutanisha Teresia Ngonyani Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mtwara, Torai Kibit- Meneja miradi KIMAS, Martin Kasembe -Mzazi na Hamis Chikambu Kiongozi wa dini ya kiislamu 

Bonyeza hapa Kusikiliza

Share:

SDA yataka usawa kwa wenye ulemavu

 

Washirika wa warsha iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Sport Development Aid (SDA) (Picha na Mwanahamisi Chikambu)

Ni warsha kujadili changamoto na fursa kwa watu wenye ulemavu, ikiwakutanisha viongozi wa serikali na wadau wa maendeleo, lengo ni kuimarisha elimu jumuishi na kuondoa mitazamo potofu.

Na Mwanahamisi Chikambu

Katika juhudi za kuendeleza elimu jumuishi na kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu, Shirika lisilo la Kiserikali la Sport Development Aid (SDA), linalojihusisha na kuwawezesha mabinti kupaza sauti, limeandaa warsha maalum ya siku moja iliyofanyika Mkoani Mtwara.

Warsha hiyo imelenga kujadili changamoto na fursa zinazohusu watu wenye ulemavu, ikiwakutanisha viongozi mbalimbali wa serikali na wadau wa maendeleo, ikiwa ni pamoja na wakuu wa idara kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara na Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara (Mtwara DC), maafisa elimu, afisa michezo na utamaduni, afisa ustawi wa jamii, watendaji wa kata, wakuu wa shule za sekondari, pamoja na wawakilishi kutoka vyama vya watu wenye ulemavu na baadhi ya walemavu wenyewe.

Akizungumza wakati wa warsha hiyo, Meneja wa Mradi kutoka SDA, Bi. Jacline Mpunjo, amesema kuwa licha ya watu wenye ulemavu kuwa sehemu ya jamii, bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazowazuia kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Sauti ya… Meneja wa Mradi kutoka SDA, Bi. Jacline Mpunjo

Wadau wote walioshiriki warsha hiyo wameeleza umuhimu wa kuwatambua watu wenye ulemavu kama sehemu ya nguvu kazi ya taifa, wakisisitiza hitaji la kuwepo kwa sera jumuishi, pamoja na kuondoa mila na mitazamo potofu zinazowatenga.

Sauti ya washiriki

Warsha hiyo imehitimishwa kwa madhumuni ya pamoja ya kuhakikisha utekelezaji wa mpango wa elimu jumuishi na upatikanaji wa huduma bora kwa watu wenye ulemavu, hususan katika sekta ya elimu na ustawi wa jamii.

Share:

Makala: Mabadiliko ya tabianchi na athari za uchumi

Hali ya barabara ya Mtwara kuwelekea Dar es Salaam kabla ya kuharibika. Picha na Amua Rushita

“Tunatoa wito wa kuchukua hatua za pamoja, utunzaji wa miundombinu, kuboresha miundombinu, kuwahamisha watu kutoka maeneo hatarishi na kuimarisha elimu ya tabianchi

Na Musa Mtepa,

Mabadiliko ya hali ya hewa yanaathiri maisha ya Watanzania, hasa katika mikoa ya Kusini kama Mtwara na Lindi, makala hii maalum inamulika madhara ya tabianchi ikiwemo mafuriko ya mara kwa mara, uharibifu wa makazi na kusimama kwa shughuli za kiuchumi na usafiri.

Kupitia ushuhuda wa wananchi na kauli za viongozi wa serikali, makala inaonyesha hatua zilizochukuliwa kama ujenzi wa madaraja makubwa lakini pia inaibua maswali kuhusu ufanisi wake wa muda mrefu. Je, tuna mikakati ya kweli ya kukabiliana na mabadiliko haya?

Tunatoa wito wa kuchukua hatua za pamoja, utunzaji wa miundombinu, kuboresha miundombinu, kuwahamisha watu kutoka maeneo hatarishi, na kuimarisha elimu ya tabianchi. Ustawi wa mikoa ya kusini na mustakabali wa taifa uko mikononi mwetu sote.

Bonyeza hapa kusikiliza makala haya

Share:

Mzee mlemavu wa macho aomba msaada wa makazi Mtwara

Mwonekano wa nje wa nyumba anayoishi mzee Salumu Somba mlemavu wa macho katika kijiji cha Nyengedi Mtwara Vijijini (Picha na Musa Mtepa)

Mzee Salumu Somba mkazi wa Mnyengedi, Mtwara, mlemavu wa macho, anaomba msaada wa makazi, mavazi, na mahitaji ya msingi kwa ajili ya familia yake kutokana na hali ngumu ya maisha.

Na Musa Mtepa

Mzee Salumu Somba, mkazi wa Kijiji cha Mnyengedi kata ya Mkunwa katika Halmashauri ya Mtwara Vijijini, anaomba msaada kutoka kwa wadau na wasamaria wema ili apate makazi bora na mahitaji ya msingi ya kibinadamu.

Mzee Somba ni mlemavu wa macho ambaye anaeleza kuwa maisha anayopitia kwa sasa ni magumu mno kutokana na hali yake ya ulemavu, ukosefu wa makazi bora, mavazi na upatikanaji wa chakula cha uhakika kwa familia yake.

Sauti ya 1 mzee Salumu Somba Mlemavu wa macho

Mzee huyo mwenye mke mmoja na watoto wawili wanaosoma darasa la kwanza na la tatu, anasema kwa sasa nyumba yake imeharibika kiasi kwamba wakati wa mvua hunyeshewa akiwa ndani na familia yake, hali inayowaweka kwenye mazingira hatarishi kiafya na kimaisha.

Sauti ya 2 mzee Salumu Somba Mlemavu wa macho
Mzee Salumu Somba akiwa ameketi barazani mwa nyumba yake (Picha na Musa Mtepa0

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyengedi, Bi Lukia Mnyachi, amesema alifahamishwa kuhusu hali ya Mzee Somba na mwanakijiji mmoja. Baada ya kutembelea eneo analoishi mzee huyo na kujionea mazingira halisi, aliamua kuanzisha jitihada za kumsaidia.

Sauti ya 1 Lukia Mnyachi mwenyekiti wa Kijiji

Aidha Bi Lukia amesema baada ya kupata mchango kutoka kwa umoja wa wenyeviti akaanza mchakato rasmi wa kujenga nyumba kwa ajili ya Mzee Somba kwa kuendelea kushirikisha viongozi wengine wa juu ambao kwa namna moja au nyingine wameendelea kumuunga mkono katika kulifanikisha hilo.

Sauti ya 2 Lukia Mnyachi mwenyekiti wa Kijiji

Licha ya hatua hizo, bado kuna uhitaji mkubwa wa msaada zaidi kwa familia hiyo — hasa vifaa vya msingi kama kitanda, magodoro, mashuka na mavazi kwa watoto wake.

Sauti ya 3 Lukia Mnyachi mwenyekiti wa Kijiji

Baadhi ya wakazi wa kijiji hicho wamejitokeza kwa moyo mmoja kushiriki katika jitihada za kumjengea Mzee Somba banda la muda, huku wakiendelea kuomba msaada zaidi kutoka kwa wadau wa maendeleo na mashirika ya kijamii.

Sauti ya baadhi ya wananchi wa Nyengedi
Mwenyekiti wa kijiji cha Nyengedi Bi Lukia Mnyachi akiwa na mzee Salumu Somba mlemavu wa macho baada ya kutembelea nyumbani kwake(Picha na Musa Mtepa)

Kwa wale wanaotaka kuchangia au kumsaidia Mzee Somba na familia yake, wanaombwa kuwasiliana na uongozi wa Kijiji cha Mnyengedi au kupitia kituo cha Jamii FM Radio kwa maelekezo zaidi.

Share:

Mfahamu mwanamke pekee kinyang’anyiro cha udiwani kata ya Chuno

 

Mariamo Chibwalo (Pichani) akizungumza na Mwanaidi kopakopa (aliyeshika kinasa sauti) kuhusu kuwania nafasi ya uongozi katika kata ya Chuno iliyopo Mkoani Mtwara nchini Tanzania. Picha na Mpiga Picha wetu

Kata ya Chuno iliyopo Manispaa ya Mtwara Mikindani yenye jumla ya watia nia 10 wanaowania nafasi ya udiwani, Mariam Chibwalo ndiye mwanamke pekee aliyejitokeza kuomba ridhaa ya chama.

Na Mwanaidi Kopakopa

Kujiamini na uzoefu katika siasa ni miongoni mwa silaha kuu anazozitumia Mariam Chibwalo, mkazi wa Kata ya Chuno katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, mkoani Mtwara. Mariam ni mmoja wa watia nia kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo katika kata hiyo yenye jumla ya watia nia 10 wanaowania nafasi ya udiwani, yeye ndiye mwanamke pekee aliyejitokeza kuomba ridhaa ya chama.

Dhamira yake ni kutimiza ndoto na maono aliyojiwekea kwa ajili ya ustawi wa jamii yake, Kwa mujibu wa Mariam, moja ya ndoto zake ni kuiona Kata ya Chuno ikipiga hatua mpya katika nyanja mbalimbali hasa za uchumi, elimu na maendeleo ya kijamii yanayoonekana wazi.

Analenga kuhakikisha makundi ya wanawake na vijana yanashiriki kikamilifu katika maamuzi pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ili kuhakikisha hakuna kundi linalobaki nyuma katika safari ya maendeleo ya kata hiyo.

Sikiliza Mahojiano na Mwandishi wetu kwa kubonyeza hapa

Share:

SDA yapongezwa kukuza sauti za mabinti Mtwara

Mkurugenzi wa SDA Thea Swai akizungumza mbele ya washiriki wakati wa utambulisho wa mradi wa Girls Speak Out season three katika ukumbi TCIA mjini Mtwara (Picha na Mwanahamisi Chikambu)

Mradi wa Kuwawezesha Mabinti Kupaza Sauti umepongezwa kwa kuleta mabadiliko chanya kwa wasichana Mtwara kwa kuwaongezea ujasiri, sauti na ushiriki katika maamuzi muhimu. Awamu ya tatu imezinduliwa Julai 2025, ikilenga kufikia mabinti wengi zaidi na kushirikisha jamii kwa upana.

Na Mwanahamisi Chikambu

Afisa Utamaduni wa Mkoa wa Mtwara, Bi. Fatma Mtanda, amepongeza Shirika la Maendeleo ya Michezo (SDA) kwa mchango wao kupitia mradi wa Kuwawezesha Mabinti Kupaza Sauti, unaolenga kuimarisha nafasi ya mtoto wa kike katika jamii.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa awamu ya tatu ya mradi huo uliofanyika leo Julai 23, 2025 kwenye ukumbi wa TCCIA, Bi. Mtanda amesema mradi huo umeleta mabadiliko chanya kwa mabinti kwa kuwajengea uwezo wa kujiamini, kujieleza na kushiriki kwenye maamuzi yanayohusu maisha yao.

Sauti ya Bi Fatma Mtanda Afisa Utamaduni Mkoa wa Mtwara

Washiriki wa mafunzo hayo wameeleza jinsi elimu waliyoipata kupitia mradi huo ilivyowasaidia kuboresha mbinu za kushughulikia changamoto za kijinsia, hasa kwa wanafunzi wa kike. Wamesema mafunzo yamewasaidia kutambua njia bora za kuwasaidia wasichana kushinda vizingiti vya kijamii na kimfumo.

Sauti ya washiriki wa mafunzo

Kwa upande mwingine, baadhi ya makungwi walioshirikishwa katika utekelezaji wa mradi huo wameeleza namna walivyopokea elimu ya kutoa mafundisho chanya kwa mabinti, bila kuendeleza mila na desturi zinazowanyima haki au kuwawekea mipaka ya kimaendeleo.

Sauti ya Makungwi walioshiriki mafunzo hayo

Akizungumza kwa niaba ya SDA, Mkurugenzi wa Shirika hilo Bi. Thea Swai ameeeleza kuwa awamu hii ya tatu ya mradi itatekelezwa kuanzia mwaka 2025 hadi 2028, ikiwa na lengo la kufikia mabinti wengi zaidi, kuongeza idadi ya walimu na watendaji wanaopatiwa mafunzo pamoja na kushirikisha makundi mbalimbali ya jamii katika kuwawezesha wasichana kupaza sauti zao.

Sauti ya Thea Swai mkurugenzi mtendaji wa SDA
Share:

Mwili wakutwa ukining’inia kwenye mkorosho Lindi

Omari Bakari Hidobelele (35), mkazi wa Madangwa, Lindi, amekutwa amejinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali. Polisi wamesema marehemu alikuwa na msongo wa mawazo. Familia imeshangazwa na tukio hilo, ikieleza kuwa hakuwa na matatizo yoyote. Polisi wamehimiza jamii kusaidia wenye changamoto za afya ya akili

Na Musa Mtepa

Mtu mmoja aliefahamika kwa jina Omari Bakari Hidobelele(35) mkazi wa Kijiji Cha madangwa kata ya Sudi halmashauri ya Mtama mkoani Lindi amekutwa amejinyonga hadi kufa kwa kutumia mkanda wa suruali yake.

Akitihibitisha tukio hilo Daktari wa Zahanati ya kijiji cha Mtegu Jackine Joseph Sita amesema kwa mujibu wa vipimo vilivyofanyika inonekana kuwa na alama zinazo thibitisha kujinyonga kupitia kifo chake .

Sauti ya Jackline Joseph Sita Daktari wa Zahanati ya Mtegu

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa kijiji hicho, Bw. Salumu Hassani Kuku, kijana huyo alitoweka tangu saa tatu asubuhi ya Julai 21, 2025. Jitihada za kumtafuta zilianza mara moja bila mafanikio hadi siku iliyofuata, Jumanne ya Julai 22, ambapo alikutwa akiwa amejinyonga kwenye mti wa mkorosho majira ya saa mbili asubuhi.

Sauti ya Salumu Hassani Kuku Mwenyekiti wa kijiji cha Madangwa

Bibi wa marehemu, Bi. Fatuma Ahmadi Liyai, amesema familia imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hiyo, lakini wamelazimika kuikubali kama sehemu ya maisha.

Aidha, Bi. Fatuma amesema tangu Omari aliporejea kutoka Kilwa, hakuwa na matatizo yoyote wala migogoro na mtu yeyote, jambo linaloendelea kuwashangaza.

Sauti ya Bi Fatuma Liyai Bibi wa Marehemu

Kwa upande wake, Jeshi la Polisi mkoa wa Lindi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu alikuwa anapitia hali ya msongo wa mawazo kwa kipindi cha muda mrefu, jambo linalodhaniwa kuwa chanzo cha uamuzi huo wa kujiua.

Jeshi la Polisi pia limetoa wito kwa jamii kuhakikisha wanaimarisha usaidizi wa kisaikolojia kwa watu wanaoonesha dalili za msongo wa mawazo au matatizo ya afya ya akili, na kutoa taarifa mapema kwa wataalamu husika ili kusaidia kuzuia matukio ya aina hii.

Share:

MTWARA: "Ni Marufuku matumizi ya Msumeno wa Mnyonyoro (chainsaw)"


Serikali ya wilaya ya Mtwara, mkoani Mtwara imepiga marufuku matumizi ya msumeno wa Mnyonyoro(chainsaw)ambayo inadaiwa kuwa chanzo cha uvunaji holela wa miti Wilayani humo. 

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa wilaya ya Mtwara,Evod Mmanda wakati akizungumza katika uzinduzi wa zoezi la upandaji wa Miti katika wilaya hiyo ambapo pia amezitaka halmashauri zote katika wilaya ya Mtwara kuzuia na kudhibiti uvunaji holela wa miti kwani hali hiyo inasababisha uharibifu mkubwa wa mazingira.

"Mtu anayemiliki Chainsaw hana tofaut na mtu anayemiliki mtambo wa gongo" alisema Mmanda na kulngezea "utaratibu wa kuvuna miti unafahamika lazima uombe kibali kuanzia ngazi ya kijiji na kijiji waandike muhtsari walete wilayani hata kama ni mwembe wako lazima ufuate utaratibu huo"  Mmanda amesema

kuwa utaratibu huo si wake bali utaratibu wa kisheria na hivyo atakayekiuka atachukuliwa hatua Kali za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani.  Awali kaimu katibu tawala wa Wilaya ya Mtwara,Fransis Mkuti akisoma taarifa ya upandaji miti katika wilaya hiyo kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2017 had machi mwaka huu amesema kuwa jumla ya miti 594876 imepandwa.

John G Massawe,Jamii FM
Share:

MTWARA: MKUU WA MKOA ATANGAZA KIAMA KWA WALE WOTE WANAOHUJUMU ZAO LA KOROSHO MKOANI HUMO


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mh Gelasius Byakanwa ameamuru kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Tandahimba kuwakamata viongozi wote wa vyama 35 vya msingi waliosababisha kulipa malipo hewa kwa wakulima ambao hawajauza korosho, yenye  thamani ya Shilingi Milioni 395.

Mh Byakanwa amesema hayo wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari mkoa hapa, baada ya kukabidhiwa ripoti ya kamati ya uchunguzi wa zao la korosho Wilaya ya Tandahimba, na kuibaini madudu mengi kwenye wilaya hiyo, na kuakikisha wote waliohusika kuchukuliwa hatua za kisheria na mkulima mmoja mmoja analipwa pesa yake.

Mkuu wa Mkoa amesema, pia kamati ya uchunguzi  wamebaini takribani Bilioni 3 hazijalipwa kwa wakulima zimecheleweshwa na wameamuru ndani ya wiki ijayo vyama hivyo viakikishe vinawalipa wakulima wote kwa pesa zilizopo kwenye akaunti husika.

Pia Mh Byakanwa ameamuru kamati ya ulinzi na usalama kumkamata  Meneja wa Chama kikuu cha ushirika cha Tandahimba na Newala(TANECU) Mohamed Nassoro na mtunza ghala wa chama hicho Msafiri Zombe kutokana na upotevu korosho kwenye ghala kuu ambazo ni mali ya vyama 5 vya ushirika ambazo ni takribani tani 194.

Kamati hiyo ya uchunguzi wa zao la korosho Wilayani Tandahimba, iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa ikiwa chini ya Mwenyekiti wake Jackline Kasondela ambae ni Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

Na Gregory Millanzi.



Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>