
“Mtaa hauna mtoto ila watoto wanatoka kwenye jamii zetu wenyewe”
Jamii inapaswa kuzingatia malezi bora ya watoto na kupunguza au kuacha kabisa kutelekeza familia zao jambo ambalo linapelekea watoto wengi kushindwa kupata malezi bora na huduma stahiki katika ngazi ya familia na kupelekea watoto hao kukimbilia mitaani ili kujitafutia mahitaji na hapo ndipo linapozaliwa jina la Watoto wa mitaani.
Kiuhalisia mtaa hauna mtoto ila watoto wanatoka kwenye jamii zetu wenyewe na zipo sababu nyingi zinazopelekea tatizo hili ambalo limekuwa kubwa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwemo Mtwara,
Kwakuliona hilo Jamii FM Radio tumekuandalia kipindi kinachoangazia Mchango wa wazazi na walezi katika kupunguza watoto wa mtaani, Kipindi hiki kimekutanisha Teresia Ngonyani Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mtwara, Torai Kibit- Meneja miradi KIMAS, Martin Kasembe -Mzazi na Hamis Chikambu Kiongozi wa dini ya kiislamu






No comments:
Post a Comment