
“Tunatoa wito wa kuchukua hatua za pamoja, utunzaji wa miundombinu, kuboresha miundombinu, kuwahamisha watu kutoka maeneo hatarishi na kuimarisha elimu ya tabianchi“
Na Musa Mtepa,
Mabadiliko ya hali ya hewa yanaathiri maisha ya Watanzania, hasa katika mikoa ya Kusini kama Mtwara na Lindi, makala hii maalum inamulika madhara ya tabianchi ikiwemo mafuriko ya mara kwa mara, uharibifu wa makazi na kusimama kwa shughuli za kiuchumi na usafiri.
Kupitia ushuhuda wa wananchi na kauli za viongozi wa serikali, makala inaonyesha hatua zilizochukuliwa kama ujenzi wa madaraja makubwa lakini pia inaibua maswali kuhusu ufanisi wake wa muda mrefu. Je, tuna mikakati ya kweli ya kukabiliana na mabadiliko haya?
Tunatoa wito wa kuchukua hatua za pamoja, utunzaji wa miundombinu, kuboresha miundombinu, kuwahamisha watu kutoka maeneo hatarishi, na kuimarisha elimu ya tabianchi. Ustawi wa mikoa ya kusini na mustakabali wa taifa uko mikononi mwetu sote.






No comments:
Post a Comment