Wakazi wa kijiji cha Tangazo wafaidika na Kliniki tembezi ya kifua kikuu

 

wananchi wa kata ya Tangazo wakipata huduma ya uchunguzi wa ugonjwa wa TB (Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa Kata ya Tangazo, Mtwara, wameishukuru serikali kwa kuwaletea kliniki tembezi ya uchunguzi wa kifua kikuu, hatua iliyowapunguzia gharama na kurahisisha upatikanaji wa matibabu, huku wakitaka kampeni hizo ziendelee vijijini.

Na Musa Mtepa

Wananchi wa Kata ya Tangazo, mkoani Mtwara, wameipongeza serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kupeleka kliniki tembezi ya uchunguzi wa ugonjwa wa kifua kikuu (TB) katika kijiji chao, hatua waliyoeleza kuwa imepunguza gharama na kurahisisha upatikanaji wa huduma za matibabu.

Wakizungumza na Jamii FM Radio, wakazi wa kata hiyo wamesema huduma hizo zimekuwa mkombozi kwao, hasa kwa kuzingatia hali ngumu ya kiuchumi inayowakabili.

Sauti ya Bi Salma Mpando na Ismail Kambutu wakazi wa kata ya Tangazo

Wengine walioeleza shukrani zao ni pamoja na Mzee Mtalika Lilala na Abdala Salum Kibokotwe wa Kijiji cha Tangazo ambapo pamoja na yote wamependekeza kliniki tembezi hizo ziongezwe kwa magonjwa mengine

Sauti ya Mzee Mtalika Lilala na Abdala kibokotwe wakazi wa Kijiji cha Tangazo

Kwa upande wake, Mratibu wa Kifua Kikuu na Ukoma Mkoa wa Mtwara, Dkt. Maikoadi Skoni, amesema kliniki tembezi hiyo ilizinduliwa rasmi Agosti 1, 2025, katika Viwanja vya Mkanaledi, Manispaa ya Mtwara Mikindani. Kampeni hiyo inalenga kufikia halmashauri zote tisa za mkoa wa Mtwara.

Sauti ya 1 Dkt Maikoni Skoni mratibu wa TB na Ukoima mkoa wa Mtwara

Amesisitiza kuwa huduma hizo zinatolewa bure, na wagonjwa wote watakaobainika huunganishwa moja kwa moja na vituo vya afya vya karibu ili kupata matibabu zaidi.

Sauti ya 2 Dkt Maikoni Skoni mratibu wa TB na Ukoima mkoa wa Mtwara

Naye Dkt. Boniface Jengela, Mratibu wa TB na Ukoma katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, amesema lengo kuu la kampeni hiyo ni kuwafikia wananchi wanaoishi mbali na vituo vya afya na kuwatambua mapema wanaoonesha dalili za kifua kikuu.

Aidha Dkt Boniface amebainisha kuwa dalili wanazozinaglia ni pamoja na  kukohoa zaidi ya wiki mbili,kutoka jasho wakati wa usiku na viashiria vingine  huku akiwataka Wananchi kuitikia kwa uwingi maeneo yote yatakayopitia na kampeni hiyo.

Sauti ya Dkt Boniface Jengela mratibu wa kifua kikuu na ukoma Mtwara D

Kampeni hii ni sehemu ya juhudi za serikali kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu nchini ifikapo mwaka 2030.

Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>