
Kata ya Chuno iliyopo Manispaa ya Mtwara Mikindani yenye jumla ya watia nia 10 wanaowania nafasi ya udiwani, Mariam Chibwalo ndiye mwanamke pekee aliyejitokeza kuomba ridhaa ya chama.
Na Mwanaidi Kopakopa
Kujiamini na uzoefu katika siasa ni miongoni mwa silaha kuu anazozitumia Mariam Chibwalo, mkazi wa Kata ya Chuno katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, mkoani Mtwara. Mariam ni mmoja wa watia nia kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo katika kata hiyo yenye jumla ya watia nia 10 wanaowania nafasi ya udiwani, yeye ndiye mwanamke pekee aliyejitokeza kuomba ridhaa ya chama.
Dhamira yake ni kutimiza ndoto na maono aliyojiwekea kwa ajili ya ustawi wa jamii yake, Kwa mujibu wa Mariam, moja ya ndoto zake ni kuiona Kata ya Chuno ikipiga hatua mpya katika nyanja mbalimbali hasa za uchumi, elimu na maendeleo ya kijamii yanayoonekana wazi.
Analenga kuhakikisha makundi ya wanawake na vijana yanashiriki kikamilifu katika maamuzi pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ili kuhakikisha hakuna kundi linalobaki nyuma katika safari ya maendeleo ya kata hiyo.
Sikiliza Mahojiano na Mwandishi wetu kwa kubonyeza hapa






No comments:
Post a Comment