• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

TADB yazijengea uwezo redio za jamii Tanzania


Mwenyekiti wa mtandao wa redio za jamii Tanzania (TADIO) ndugu Baptist  akizungumza katika mafunzo hayo

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) inaendesha semina kwa wamiliki na wahariri wa redio za kijamii zipatazo 50 ikiwemo Jamii FM Radioo ya Mtwara toka Tanzania Bara na Zanzibar kuanzia tarehe 23 hadi 25,Mei 2026, Lengo kuu likiwa ni kukuza uelewa juu ya majukumu ya TADB pamoja na kuonesha fursa zinazopatikana katika benki hiyo.

Aidha, washiriki wamejengewa uwezo wa kuripoti masuala ya maendeleo ya sekta ya kilimo, fedha za kilimo, na nafasi ya taasisi za kifedha katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa kilimo nchini. 

Mafunzo hayo yataimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya habari vya kijamii na TADB katika kuhamasisha uelewa wa umma kuhusu fursa za uwezeshaji wa kifedha kwa wakulima, wafugaji, wavuvi na wadau wengine wa mnyororo wa thamani katika sekta ya kilimo.


Semina hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Jengo la Mkandarasi Jijini Dodoma na kufunguliwa rasmi na Mkurugenzi wa Mipango, Ushauri na Mahusiano ya Taasisi TADB, ndugu Mkani Waziri, ambaye amesisitiza umuhimu wa vyombo vya habari katika kuelimisha jamii kuhusu mchango wa sekta ya fedha kwenye maendeleo ya kilimo na uchumi wa taifa kwa ujumla.

Mbali na elimu hiyo wanahabari hao wamepatiwa vyeti ikiwa ni njia ya kutambua mchango wao katika jamii pamoja na materials mbalimbali yatakayosaidia kutangaza fursa zinazopatikana TADB ili wakulima wote nchini waweze kunufaika nazo.



Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>