• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

Mashamba 15 yashambuliwa na viboko Mnuyo

 

Sehemu ya mashamba ya wakulima wa kijiji cha Mnuyo kata ya Msimbati yaliyoshambuliwa na Viboko (Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa kijiji cha Mnuyo mkoani Mtwara wamelalamikia mashambulizi ya viboko mashambani, wakiiomba serikali kuchukua hatua za haraka kuwalinda na kuzuia hatari ya baa la njaa.

Na Musa Mtepa

Wananchi wa Kijiji cha Mnuyo, kata ya Msimbati, Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, mkoani Mtwara, wameiomba serikali kupitia mamlaka zinazohusika na wanyamapori kufika kijijini hapo ili kuwaondolea changamoto ya wanyama aina ya viboko wanaoshambulia mashamba yao ya mpunga.

Wakizungumza na Jamii FM Redio Aprili 10,2026, wananchi hao wamesema kuwa katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakikumbwa na changamoto kubwa ya viboko kuvamia mashamba yao ya mpunga nyakati za usiku, hali inayowatishia baa la njaa siku za usoni.

Sauti ya wakulima wa mpunga Kijiji cha Mnuyo

Aidha, wananchi hao wameiomba serikali kuwasaidia kwa haraka kutatua changamoto hiyo, ambayo imekuwa kubwa kwao kiasi cha baadhi yao kukata tamaa ya kuendelea na shughuli za kilimo kutokana na uwepo wa wanyama hao.

Sauti ya wakulima wa mpunga Kijiji cha Mnuyo
Kinyesi cha Mnyama Boko kikionekana pembezoni mwa shamba la Mpunga (Picha na Musa Mtepa)

Kwa upande wake, mwenyekiti wa Kijiji cha Mnuyo, Yusuf Salumu, amekiri kupokea taarifa za uwepo wa wanyama hao katika eneo hilo, akisema tayari amezifikisha katika Halmashauri ya Wilaya kwa ajili ya hatua zaidi.

Aidha, mwenyekiti huyo amesema viboko hao wanaotoka Mto Ruvuma wameshashambulia mashamba 15 ya wakulima wa kijiji hicho, huku akiomba mamlaka zinazohusika na wanyamapori kuchukua hatua za haraka kuwaondoa wanyama hao.

Sauti ya Yusuf Salumu, mwenyekiti wa Kijiji cha Mnuyo
Share:

Manispaa ya Mtwara Mikindani yaimarisha ulinzi wa mtoto

 

Fatu Mapua, Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Mtwara Mikindani akiongoza mdahalo wa wadau juu ya ulinzi na usalama wa mtoto uliofanyika Aprili 11,2026 katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. (Picha na Musa Mtepa)

Jamii imetakiwa kushiriki kikamilifu kulinda watoto dhidi ya ukatili, kupitia elimu na ushirikiano wa . wadau mbalimbali, ili kuhakikisha usalama wa watoto chini ya miaka 18 katika Manispaa ya Mtwara Mikindani

Na Musa Mtepa

Jamii imeaswa kila mmoja kusimama katika nafasi yake ili kuhakikisha usalama na ulinzi wa mtoto vinakuwa kipaumbele, kwa lengo la kumuweka salama dhidi ya vitendo vya ukatili na matukio hatarishi.

Wito huo umetolewa Aprili 11, 2026, katika mdahalo uliowakutanisha wadau mbalimbali, wakiwemo mawakala wa magari ya abiria, madereva wa bodaboda, washereheshaji wa sherehe (MC), ma-DJ na waandishi wa habari.

Mdahalo huo ulioandaliwa na Idara ya Ustawi wa Jamii ya Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, ulikuwa na lengo la kupunguza na hatimaye kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya watoto wenye umri chini ya miaka 18 katika manispaa hiyo.

Wakizungumza katika mdahalo huo, washiriki wameipongeza halmashauri kwa kuandaa mdahalo huo, wakisema umewawezesha kupata maarifa muhimu ambayo wataenda kuyafanyia kazi katika shughuli zao za kila siku.

Aidha, wamesema mbali na kuwa sehemu ya kutoa elimu kwa jamii kuhusu matukio hatarishi kwa watoto, wametoa wito kwa halmashauri kupitia viongozi wa mitaa kuendelea kutoa elimu kuhusu ulinzi wa watoto pamoja na vihatarishi vinavyochangia ukatili huo, ikiwemo watoto kuhusishwa katika matukio ya usiku, kuhudhuria kumbi za starehe na kushiriki shughuli za mitaani.

Sauti ya wajumbe walioshiriki katika mdahalo

Akizungumzia tuhuma za baadhi ya madereva wa bodaboda kuhusishwa na matukio ya ukatili kwa watoto, Hance Bruno, dereva bodaboda kutoka kata ya Shangani, amekiri kuwepo kwa baadhi yao wenye tabia hiyo, huku akiahidi kwenda kulifanyia kazi suala hilo katika kituo chake. Pia ametoa wito kwa wazazi kuwa makini na watoto wao, hasa katika kipindi cha sikukuu.

Sauti ya Hance Bruno Dereva bodaboda kata ya Shangani

Kwa upande wake, Fatu Issa Mapua, Afisa Ustawi wa Jamii wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, amesema miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na matukio ya ukatili yaliyojitokeza ndani ya manispaa hiyo na kupanga mikakati ya baadaye ili kuwasaidia watoto kuwa salama katika maeneo yao.

Sauti ya Fatu Issa Mapua afisa ustawi Manispaa ya Mtwara Mikindani

Aidha, Bi. Mapua amesema matukio ya ukatili bado yapo katika Manispaa ya Mtwara Mikindani, ndiyo maana wamekuwa wakikutana na makundi mbalimbali ili kuwapatia elimu na kuiwezesha jamii kutoa taarifa pale matukio yanapotokea. Ameongeza kwa kutoa wito kwa wananchi kwamba usalama na ulinzi wa mtoto ni jukumu la kila mmoja.

Sauti ya Fatu Issa Mapua afisa ustawi wa Jamii Manispaa ya Mtwara Mikindani
Share:

Makato ya korosho kikwazo mradi wa soko Mnyahi

 

Mwonekano wa soko la zamani la kijiji cha Mnyahi kata ya Milangominne halmashauri ya mji Nanyamba mkoani Mtwara ambalo wakulima wa zao la korosho wanakatwa shilingi 20 kwa kila kilo moja inayouzwa ili fedha ijenge soko jipya (Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa Mnyahi Mtwara walalamikia kuchelewa kwa ujenzi wa soko licha ya makato ya korosho, wakitupia lawama viongozi wa kijiji na mfumo wa ukusanyaji fedha.

Na Musa Mtepa

Wananchi wa kijiji cha Mnyahi, kata ya Milangominne mkoani Mtwara, wameulalamikia uongozi wa kijiji pamoja na Halmashauri ya Mji Nanyamba kwa kuwa kikwazo cha kutokamilika kwa miradi ya maendeleo inayoanzishwa na kijiji hicho, inayotegemea makato ya zao la korosho linalolimwa katika eneo hilo.

Wakizungumza na Jamii FM Radio, wananchi hao wamesema kuwa takribani miaka mitatu sasa imepita tangu walipokubaliana katika mkutano wa kijiji kukatwa shilingi 20 kwa kila kilo moja ya korosho, ili fedha zitakazopatikana ziweze kuwezesha ujenzi wa soko jipya kijijini hapo.

Sauti ya wananchi wa kijiji cha Mnyahi

Aidha, wananchi hao wamesema kuwa changamoto inayosababisha kuchelewa kwa ujenzi wa soko hilo ipo katika serikali ya kijiji, wakidai kuwa baadhi ya viongozi hawawajibiki ipasavyo, hususan katika uendeshaji wa mikutano ya kijiji. Pia wameomba viongozi wakuu wa vyama vinavyowaweka madarakani viongozi wa vijiji kuwafuatilia kwa karibu utendaji wao wa kazi baada ya uchaguzi.

Sauti ya 2 wananchi wa kijiji cha Mnyahi

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kijiji cha Mnyahi, Hamisi Salumu Mpangu, amesema kuwa changamoto kubwa ya upatikanaji wa fedha hizo kwa wakati na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inatokana na matatizo anayokutana nayo mtendaji wa kijiji katika kutumia mfumo wa NeST, hali inayochangiwa na umri pamoja na uelewa mdogo wa matumizi ya mfumo huo.

Sauti ya Hamisi Salumu Mpangu, Mwenyekiti wa kijiji cha Mnyahi
Mwenyekiti wa kijiji cha Mnyahi Bw Hamisi Salumu Mpangu akitolea maelezo juu ya malalamiko ya wananchi wa kijiji hicho(Picha na Musa Mtepa)

Akitolea ufafanuzi juu ya malalamiko ya wananchi wa kijiji cha Mnyahi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Nanyamba, Mhe. Hassani Ali Mauji, amesema kuwa fedha hizo hukusanywa awali na MAMCU, na baada ya msimu kumalizika hufanya makusanyo ya pamoja ya halmashauri yote na kuziingiza katika akaunti ya halmashauri. Baadaye, mkurugenzi huzipeleka katika akaunti za vijiji kulingana na kiwango cha fedha kilichokusanywa.

Aidha, amesema kuwa ili viongozi wa kijiji waweze kutoa fedha hizo, ni lazima kuwepo na muhtasari wa vikao vya mikutano ya kijiji unaoeleza matumizi ya fedha hizo katika miradi ya maendeleo ya wananchi. Ameongeza kuwa jukumu la ufuatiliaji wa taratibu hizo ni la mtendaji wa kijiji husika.

Sauti ya Hassani Ali Mauji, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Nanyamba

Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>