• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

Waandishi wa habari watahadharishwa kuzingatia weledi uchaguzi mkuu

Amua Rushita akiendelea na mafunzo na Waandishi wa habari wa kituo cha Jamii fm redio yaliyofanyika leo August 15,2025 katika kituoni hapo (Picha na Musa Mtepa)

 Mafunzo kwa waandishi wa Jamii FM Redio yamewahimiza kuzingatia weledi, usalama kazini na kujikinga na uhalifu mtandaoni kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025

Na Musa Mtepa

Waandishi wa habari wametakiwa kuwa makini na kuzingatia weledi wa taaluma yao, hususan kuelekea katika kipindi cha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 nchini.

Wito huo umetolewa leo, Agosti 15, 2025, na mkufunzi Amua Rushita wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari wa kituo cha Jamii FM Redio kuhusu ulinzi na usalama katika kipindi cha uchaguzi. Amesema kuwa waandishi wanapaswa kuchukua tahadhari wanapokuwa kazini ili kuepuka hatari zinazoweza kujitokeza.

Sauti ya 1 Amua rushita mkufunzi wa mafunzo

Akifafanua, Amua amesema mafunzo hayo yamejikita katika maeneo matatu makuu: kuzingatia taratibu wakati wa kuhudhuria mikutano ya vyama vya siasa, kujikinga na uhalifu mtandaoni kupitia vifaa vya kidijitali, na kuimarisha ustawi wa kisaikolojia kwa waandishi wa habari wakiwa kazini.

Sauti ya 2 Amua rushita mkufunzi wa mafunzo

Waandishi wa habari wa Jamii FM Redio, Shaibu Omari na Msafiri Kipila, wameeleza kufurahia mafunzo hayo, wakisema yamegusa moja kwa moja namna ya kuboresha usalama wao na kufuata taratibu sahihi wakati wa mchakato wa uchaguzi.

Sauti ya msafiri kipila na Shaibu Omari

Kwa upande wake, Mwanahamisi Chikambu, mwandishi wa habari wa kituo hicho, amesema ameongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kuvaa mavazi yanayomtambulisha mwandishi wa habari, pamoja na kujitambulisha kwa viongozi wa usalama kwenye eneo la tukio ili kurahisisha utambuzi endapo changamoto itatokea

Sauti ya Mwanahamisi Chikambu Mwandishi

Mafunzo haya ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari ni sehemu ya mradi wa usalama wa mwandishi wa habari kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025 nchini ambayo yanasimamiwa na umoja wa Klabu za waandishi wa habari nchini (UTPC).

Share:

Jamii inachangiaje kuwalinda, kuwatunza watu wenye ulemavu?

Hamisi Mshamu Bakari akiwa na biadhaa zake za mtumba. Picha na Msafiri Kipila

“Hamisi Bakari anakiri kuwa changamoto kubwa anayokumbana nayo ni ukosefu wa eneo maalum la kufanyia biashara, kama angepata sehemu hiyo rasmi basi angeweza kupiga hatua zaidi za kimaendeleo kwa kuwa angeendesha biashara yake kwa utulivu na kujiimarisha zaidi kiuchumi”

Na Msafiri Kipila

Katika harakati za kujikwamua na umasikini, watu wenye ulemavu wameendelea kuonyesha juhudi na uthubutu mkubwa wa kushiriki katika shughuli za maendeleo kama walivyo watu wengine katika jamii. Licha ya changamoto mbalimbali zinazowakabili, bado wengi wao wamejiajiri na kufanya biashara ndogondogo ili kujitegemea kiuchumi na kuondoa dhana potofu kuwa ulemavu ni mwisho wa uwezo wa mtu.

Hamisi Mshamu Bakari ni miongoni mwa watu hao. Ni mlemavu wa mguu ambaye amejikita katika biashara ya kuuza viatu na nguo za mtumba kwa zaidi ya miaka 20. Akiwa na azma ya kubadili maisha yake, Hamisi hutembea umbali mrefu kila siku kutoka Mtawanya Juu hadi Magomeni, ambako huchukua bidhaa zake kabla ya kuzitembeza mitaani kwa ajili ya kuziuza. Safari hizo ndefu, licha ya hali yake ya ulemavu, zinadhihirisha kiwango kikubwa cha uvumilivu, bidii na kujituma alichonacho.

Hamisi Mshamu Bakari akiwa kwenye makazi yake. picha na Msafiri Kipila

Hata hivyo, Hamisi anakiri kuwa changamoto kubwa anayokumbana nayo ni ukosefu wa eneo maalumu la kufanyia biashara. Anasema kama angepata sehemu hiyo rasmi, basi angeweza kupiga hatua zaidi za kimaendeleo kwa kuwa angeendesha biashara yake kwa utulivu na kujiimarisha zaidi kiuchumi. Anaeleza kuwa msaada wa aina hiyo ungekuwa chachu kubwa ya mafanikio kwa watu wenye ulemavu, ambao mara nyingi hukosa fursa za msingi zinazoweza kuwainua kiuchumi.

Kupitia simulizi hii, jamii inapaswa kutambua kuwa watu wenye ulemavu hawahitaji huruma, bali wanahitaji fursa, mazingira rafiki na msaada wa kweli utakaowawezesha kujitegemea. Kama jamii itawekeza kwao, kwa kuwapatia maeneo ya biashara, mikopo au mafunzo ya ujasiriamali, basi watakuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya taifa letu. Kisa cha Hamisi kinatoa somo la matumaini, lakini pia changamoto inayohitaji hatua za haraka.

 Bonyeza hapa kusikiliza makala haya

Share:

Mtamba aibuka kidedea kura za maoni CUF Mtwara Vijijini

Mh.Shamsia Azizi Mtamba mshindi wa kura za maoni CUF Mtwara Vijijini(Picha na Musa Mtepa)

Mh. Shamsia Mtamba ashinda kura za maoni CUF Mtwara Vijijini kwa kura 334 kati ya 374, akimuacha Abdull Mahupa nyuma kwa kura 39

Na Musa Mtepa

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini, Mh. Shamsia Azizi Mtamba, ameibuka mshindi katika uchaguzi wa kura za maoni wa Chama Cha Wananchi (CUF), uliofanyika leo kwenye ukumbi wa mikutano wa Paris, mjini Mtwara.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Msimamizi wa uchaguzi Bw. Masudi Muhina amesema jumla ya kura 374 zilipigwa ambapo Mh. Shamsia Mtamba alipata kura 334, huku mpinzani wake Abdull Bakari Mahupa akijizolea kura 39. Kura moja iliharibika.

Sauti ya Bw Masud Muhina msimamizi wa uchaguzi wa CUF

Akizungumza baada ya kutangazwa kwa matokeo, Abdull Mahupa alikubali kushindwa na kumpongeza Mh. Shamsia kwa ushindi huo. Aidha, aliwaomba wanachama wa CUF kuvunja makundi na kuungana kwa pamoja kumpa ushirikiano Shamsia katika harakati za kulirudisha jimbo hilo mikononi mwa chama katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Sauti ya Abdull Mahupa mshindi wa pili wa kura za maoni CUF
Diwani mstaafu wa kata ya Ndumbwe ambae alikuwa mgombea ubunge kupitia CUF Mtwara vijini katika uchaguzi wa kura ya maoni kwa ujumbe Mh. Abdull Mahupa(Picha na Musa Mtepa)

Kwa upande wake, Mh. Shamsia Mtamba amewashukuru wajumbe wa mkutano kwa kuendelea kumuamini na kumchagua tena kuwa mgombea wa jimbo hilo, huku akiwaomba kuendelea kushirikiana naye katika kampeni zijazo.

Sauti ya Shamsia Azizi Mtamba mshindi wa kura za maoni

Kabla ya uchaguzi, wagombea walipata fursa ya kunadi sera zao mbele ya wajumbe wa mkutano huo, sambamba na kujibu maswali mbalimbali kutoka kwa wanachama – hatua iliyowapa nafasi ya kueleza kwa kina mikakati yao ya kuimarisha maendeleo ya jimbo la Mtwara Vijijini.

Sauti ya wagombea wakinadi sera zao mbele ya wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya CUF
Share:

Wenye ulemavu wanapojikomboa kupitia biashara

 

Hamisi Mshamu Bakari akifanya mahojiano na Msafiri kipila (mwenye kinasa sauti). Picha na Musa Mtepa

“Hamisi Bakari anakiri kuwa changamoto kubwa anayokumbana nayo ni ukosefu wa eneo maalumu la kufanyia biashara, kama angepata sehemu hiyo rasmi basi angeweza kupiga hatua zaidi za kimaendeleo kwa kuwa angeendesha biashara yake kwa utulivu na kujiimarisha zaidi kiuchumi”

Na Msafiri Kipila

Katika harakati za kujikwamua na umasikini, watu wenye ulemavu wameendelea kuonyesha juhudi na uthubutu mkubwa wa kushiriki katika shughuli za maendeleo kama walivyo watu wengine katika jamii. Licha ya changamoto mbalimbali zinazowakabili, bado wengi wao wamejiajiri na kufanya biashara ndogo ndogo ili kujitegemea kiuchumi na kuondoa dhana potofu kuwa ulemavu ni mwisho wa uwezo wa mtu.

Hamisi Mshamu Bakari ni miongoni mwa watu hao. Ni mlemavu wa mguu ambaye amejikita katika biashara ya kuuza viatu na nguo za mtumba kwa zaidi ya miaka 20. Akiwa na azma ya kubadili maisha yake, Hamisi hutembea umbali mrefu kila siku kutoka Mtawanya Juu hadi Mangomeni, ambako huchukua bidhaa zake kabla ya kuzitembeza mitaani kwa ajili ya kuziuza. Safari hizo ndefu, licha ya hali yake ya ulemavu, zinadhihirisha kiwango kikubwa cha uvumilivu, bidii na kujituma alichonacho.

Mke wa Hamisi Mshamu Bakari akizungumza na mwandishi wa makala haya. picha na Musa Mtepa

Hata hivyo, Hamisi anakiri kuwa changamoto kubwa anayokumbana nayo ni ukosefu wa eneo maalumu la kufanyia biashara. Anasema kama angepata sehemu hiyo rasmi, basi angeweza kupiga hatua zaidi za kimaendeleo kwa kuwa angeendesha biashara yake kwa utulivu na kujiimarisha zaidi kiuchumi. Anaeleza kuwa msaada wa aina hiyo ungekuwa chachu kubwa ya mafanikio kwa watu wenye ulemavu, ambao mara nyingi hukosa fursa za msingi zinazoweza kuwainua kiuchumi.

Kupitia simulizi hii, jamii inapaswa kutambua kuwa watu wenye ulemavu hawahitaji huruma, bali wanahitaji fursa, mazingira rafiki na msaada wa kweli utakaowawezesha kujitegemea. Kama jamii itawekeza kwao, kwa kuwapatia maeneo ya biashara, mikopo au mafunzo ya ujasiriamali, basi watakuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya taifa letu. Kisa cha Hamisi kinatoa somo la matumaini, lakini pia changamoto inayohitaji hatua za haraka.

 Bonyeza hapa kusikiliza makala haya

Share:

Kuruthumu apatiwa msaada wa kununua kiatu maalum

Bi. Kuruthumu Seifu Mohamed akiwa ameketi na kiatu maalumu. Picha na Msafiri Kipila

“Kuruthumu amepatiwa msaada wa shilingi 300,000 kwa ajili ya gharama za ununuzi wa kiatu hicho maalumu. Huu ni mwanzo mpya kwa maisha yake, kwani sasa ataweza kushiriki ipasavyo katika shughuli za kila siku bila kikwazo kikubwa cha utembeaji”

Na Msafiri Kipila

Katika jamii yenye changamoto mbalimbali, watu wenye ulemavu mara nyingi hukumbwa na hali ngumu ya maisha, hususan kwa wale wanaohitaji vifaa maalumu ili kuweza kuendesha maisha yao ya kila siku. Hali hiyo imekuwa ikiwakwamisha katika kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kijamii na kiuchumi. Hata hivyo, kuna nuru ya matumaini kupitia moyo wa huruma kutoka kwa wadau na viongozi wa jamii.

Miongoni mwa walionufaika na msaada huo ni Bi. Kuruthumu Seifu Mohamed, mama mwenye ulemavu wa mguu ambaye kwa muda mrefu amekuwa akihitaji kiatu maalumu ili aweze kutembea kwa urahisi. Kupitia juhudi za wadau wa haki na maendeleo ya watu wenye ulemavu, Kuruthumu amepatiwa msaada wa shilingi 300,000 kwa ajili ya gharama za ununuzi wa kiatu hicho maalumu. Huu ni mwanzo mpya kwa maisha yake, kwani sasa ataweza kushiriki ipasavyo katika shughuli za kila siku bila kikwazo kikubwa cha utembeaji.

Akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake na Wasichana Wenye Ulemavu Mtwara Mikindani, amethibitisha kuwa fedha hizo zimepokelewa rasmi na kumfikia mhusika. Aidha, ametumia fursa hiyo kuhamasisha jamii iendelee kujitokeza kusaidia watu wenye ulemavu, kwani bado kuna changamoto nyingi zinazowakabili.

Bi. Kuruthumu Seifu Mohamed akipokea kiasi cha shilingi laki tatu. Picha na Musa Mtepa

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mtwara, Mhe. Anastazia Wambura, ameeleza kuguswa na hali wanayopitia watu wenye ulemavu. Amesema kuwa amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha watu hao wanapata usaidizi unaowasaidia kujikwamua kimaisha. “Nimekuwa nikifanya hivi mara kwa mara, lengo ni kuhakikisha watu wenye ulemavu wanashiriki katika shughuli za maendeleo kama watu wengine,” alisema Mhe. Wambura.

Msaada huu kwa Bi. Kuruthumu ni mfano hai wa jinsi mshikamano wa kijamii na uongozi wenye maono unavyoweza kuleta mabadiliko katika maisha ya watu wanaohitaji msaada. Ni wito kwa jamii nzima kuendelea kuwathamini, kuwaunga mkono na kuwajumuisha watu wenye ulemavu katika nyanja zote za maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kusikiliza makala haya, Bonyeza Hapa

Share:

Wananchi wa mtaa wa Mkunja Nguo waomba barabara rasmi

 

Sehemu ya Barabara ya Mkunjanguo kuelekea mtaa wa Namdohola ilivyo haribika (Picha na Musa Mtepa)

Uchongaji wa Barabara hiyo itarahisisha huduma kwa wakazi, hususan nyakati za dharura, Mwenyekiti wa mtaa, Bw. Kuladaku, ameunga mkono wazo hilo, akisisitiza mchango wake kwa maendeleo ya vijiji jirani

Na Musa Mtepa

Kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya njia ya kutoka Mkunja Nguo kuelekea Namdohola, mdau wa maendeleo Bw. Ahmadi Issa Chihipu ameiomba Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani kuiangalia kwa “jicho la tatu” na kuichonga rasmi kuwa barabara inayopitika kwa urahisi na usalama kwa wananchi.

Akizungumza na Jamii fm Redio, Bw. Chihipu amesema kuwa njia hiyo imekuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Namdohola, pamoja na vijiji vya jirani vya Litumbo na Mnyengedi vya halmashauri ya Mtwara vijijini , na tayari ameanza kuchukua hatua binafsi kwa kujitolea kufanya usafi na kufyeka ili kuiandaa kwa ajili ya uchongaji, mara tu Halmashauri itakaporidhia.

Ahmadi Chihipu – Mdau wa Maendeleo

Mbali na mchango wake binafsi, Bw. Chihipu ameeleza kuwa moja ya sababu kubwa zilizomsukuma kuibua umuhimu wa barabara hiyo ni changamoto za usafiri nyakati za dharura, hususan wakati wanawake wajawazito wanapopatwa na uchungu wa kujifungua usiku.

2: Ahmadi Chihipu – Mdau wa Maendeleo

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Mkunja Nguo, Bw. Musa Ali maarufu kama Kuladaku, ameunga mkono hoja hiyo na kubainisha kuwa barabara hiyo itakuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi wa maeneo mbalimbali ya jirani.

Musa Kuladaku – Mwenyekiti wa Mtaa wa Mkunja Nguo

Mwenyekiti Kuladaku ametoa wito kwa mamlaka husika kuchukua hatua za haraka kuifanyia kazi ombi hilo, akisisitiza kuwa barabara hiyo ni hitaji la muda mrefu linalogusa maisha ya watu moja kwa moja.

Share:

Wakazi wa kijiji cha Tangazo wafaidika na Kliniki tembezi ya kifua kikuu

 

wananchi wa kata ya Tangazo wakipata huduma ya uchunguzi wa ugonjwa wa TB (Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa Kata ya Tangazo, Mtwara, wameishukuru serikali kwa kuwaletea kliniki tembezi ya uchunguzi wa kifua kikuu, hatua iliyowapunguzia gharama na kurahisisha upatikanaji wa matibabu, huku wakitaka kampeni hizo ziendelee vijijini.

Na Musa Mtepa

Wananchi wa Kata ya Tangazo, mkoani Mtwara, wameipongeza serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kupeleka kliniki tembezi ya uchunguzi wa ugonjwa wa kifua kikuu (TB) katika kijiji chao, hatua waliyoeleza kuwa imepunguza gharama na kurahisisha upatikanaji wa huduma za matibabu.

Wakizungumza na Jamii FM Radio, wakazi wa kata hiyo wamesema huduma hizo zimekuwa mkombozi kwao, hasa kwa kuzingatia hali ngumu ya kiuchumi inayowakabili.

Sauti ya Bi Salma Mpando na Ismail Kambutu wakazi wa kata ya Tangazo

Wengine walioeleza shukrani zao ni pamoja na Mzee Mtalika Lilala na Abdala Salum Kibokotwe wa Kijiji cha Tangazo ambapo pamoja na yote wamependekeza kliniki tembezi hizo ziongezwe kwa magonjwa mengine

Sauti ya Mzee Mtalika Lilala na Abdala kibokotwe wakazi wa Kijiji cha Tangazo

Kwa upande wake, Mratibu wa Kifua Kikuu na Ukoma Mkoa wa Mtwara, Dkt. Maikoadi Skoni, amesema kliniki tembezi hiyo ilizinduliwa rasmi Agosti 1, 2025, katika Viwanja vya Mkanaledi, Manispaa ya Mtwara Mikindani. Kampeni hiyo inalenga kufikia halmashauri zote tisa za mkoa wa Mtwara.

Sauti ya 1 Dkt Maikoni Skoni mratibu wa TB na Ukoima mkoa wa Mtwara

Amesisitiza kuwa huduma hizo zinatolewa bure, na wagonjwa wote watakaobainika huunganishwa moja kwa moja na vituo vya afya vya karibu ili kupata matibabu zaidi.

Sauti ya 2 Dkt Maikoni Skoni mratibu wa TB na Ukoima mkoa wa Mtwara

Naye Dkt. Boniface Jengela, Mratibu wa TB na Ukoma katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, amesema lengo kuu la kampeni hiyo ni kuwafikia wananchi wanaoishi mbali na vituo vya afya na kuwatambua mapema wanaoonesha dalili za kifua kikuu.

Aidha Dkt Boniface amebainisha kuwa dalili wanazozinaglia ni pamoja na  kukohoa zaidi ya wiki mbili,kutoka jasho wakati wa usiku na viashiria vingine  huku akiwataka Wananchi kuitikia kwa uwingi maeneo yote yatakayopitia na kampeni hiyo.

Sauti ya Dkt Boniface Jengela mratibu wa kifua kikuu na ukoma Mtwara D

Kampeni hii ni sehemu ya juhudi za serikali kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu nchini ifikapo mwaka 2030.

Share:

Mchango wa wazazi, walezi kupunguza watoto wa mtaani

 

Mmoja wa wadau akizungumza katika kipindi. Picha na mwandishi wetu

“Mtaa hauna mtoto ila watoto wanatoka kwenye jamii zetu wenyewe”

Jamii inapaswa kuzingatia malezi bora ya watoto na kupunguza au kuacha kabisa kutelekeza familia zao jambo ambalo linapelekea watoto wengi kushindwa kupata malezi bora na huduma stahiki katika ngazi ya familia na kupelekea watoto hao kukimbilia mitaani ili kujitafutia mahitaji na hapo ndipo linapozaliwa jina la Watoto wa mitaani.

Kiuhalisia mtaa hauna mtoto ila watoto wanatoka kwenye jamii zetu wenyewe na zipo sababu nyingi zinazopelekea tatizo hili ambalo limekuwa kubwa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwemo Mtwara, 

Kwakuliona hilo Jamii FM Radio tumekuandalia kipindi kinachoangazia Mchango wa wazazi na walezi katika kupunguza watoto wa mtaani, Kipindi hiki kimekutanisha Teresia Ngonyani Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mtwara, Torai Kibit- Meneja miradi KIMAS, Martin Kasembe -Mzazi na Hamis Chikambu Kiongozi wa dini ya kiislamu 

Bonyeza hapa Kusikiliza

Share:

SDA yataka usawa kwa wenye ulemavu

 

Washirika wa warsha iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Sport Development Aid (SDA) (Picha na Mwanahamisi Chikambu)

Ni warsha kujadili changamoto na fursa kwa watu wenye ulemavu, ikiwakutanisha viongozi wa serikali na wadau wa maendeleo, lengo ni kuimarisha elimu jumuishi na kuondoa mitazamo potofu.

Na Mwanahamisi Chikambu

Katika juhudi za kuendeleza elimu jumuishi na kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu, Shirika lisilo la Kiserikali la Sport Development Aid (SDA), linalojihusisha na kuwawezesha mabinti kupaza sauti, limeandaa warsha maalum ya siku moja iliyofanyika Mkoani Mtwara.

Warsha hiyo imelenga kujadili changamoto na fursa zinazohusu watu wenye ulemavu, ikiwakutanisha viongozi mbalimbali wa serikali na wadau wa maendeleo, ikiwa ni pamoja na wakuu wa idara kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara na Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara (Mtwara DC), maafisa elimu, afisa michezo na utamaduni, afisa ustawi wa jamii, watendaji wa kata, wakuu wa shule za sekondari, pamoja na wawakilishi kutoka vyama vya watu wenye ulemavu na baadhi ya walemavu wenyewe.

Akizungumza wakati wa warsha hiyo, Meneja wa Mradi kutoka SDA, Bi. Jacline Mpunjo, amesema kuwa licha ya watu wenye ulemavu kuwa sehemu ya jamii, bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazowazuia kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Sauti ya… Meneja wa Mradi kutoka SDA, Bi. Jacline Mpunjo

Wadau wote walioshiriki warsha hiyo wameeleza umuhimu wa kuwatambua watu wenye ulemavu kama sehemu ya nguvu kazi ya taifa, wakisisitiza hitaji la kuwepo kwa sera jumuishi, pamoja na kuondoa mila na mitazamo potofu zinazowatenga.

Sauti ya washiriki

Warsha hiyo imehitimishwa kwa madhumuni ya pamoja ya kuhakikisha utekelezaji wa mpango wa elimu jumuishi na upatikanaji wa huduma bora kwa watu wenye ulemavu, hususan katika sekta ya elimu na ustawi wa jamii.

Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>