• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

TPA Mtwara yaongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo

 

Wajumbe na wadau wa mamalaka ya usimamizi wa Bandari wakifuatilia mkutano huo uliofanyika September 29,2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa BOT kanda ya Mtwara

Bandari ya Mtwara imeongeza usafirishaji wa mizigo kwa asilimia 49 kati ya 2023/2024, ikihusisha korosho na makaa ya mawe, huku idadi ya makampuni ya meli ikiongezeka

Na Gregory Milanzi

Mtwara-September 29,2025 – Ukusanyaji na usafirishaji wa mizigo kupitia Bandari ya Mtwara umeongezeka kwa asilimia 49 katika mwaka wa fedha 2023/2024 ikilinganishwa na miaka ya nyuma, hatua inayodhihirisha ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika ukanda wa kusini.

Akizungumza September 29, 2025 kwenye mkutano wa wadau wa bandari hiyo unaoendelea mkoani Mtwara, Meneja wa Bandari ya Mtwara, Ferdinand Nyathi amesema bandari hiyo imesafirisha tani milioni 2.5 za mizigo kwa mwaka 2024/2025 kutoka tani milioni 1.7 kwa mwaka uliopita wa fedha.

Sauti ya Ferdinand Nyathi Meneja wa Bandari Mtwara
Ferdinand Nyath meneja wa Bandari ya Mtwara akiwa katika mkutano wa mamala ya usimamizi wa Bandari kuelekea msimu mpya wa zao la korosho

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wakala wa Meli Tanzania (TASAA), Daniel Mallongo amesema Bandari ya Mtwara ni muhimu sana kwa usafirishaji wa zao la korosho, na kwamba idadi ya makampuni ya usafirishaji wa meli imeongezeka kutoka mawili hadi sita katika misimu mitatu iliyopita.

Sauti ya Daniel Malongo mwenyekiti TASAA

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Emanuel Mrutu amesema Bandari ya Mtwara haifanyi kazi msimu wa korosho pekee, bali imekuwa ikihudumia pia bidhaa nyingine kama makaa ya mawe.

Sauti ya Emanuel Mrutu mwakilishi mkurugenzi TPA

Mkutano huo wa wadau wa bandari unalenga kuangazia fursa na changamoto katika kuendeleza shughuli za usafirishaji kupitia Bandari ya Mtwara.

Share:

Umuhimu wa wanandoa kushiriki elimu ya uzazi wa mpango

 

Picha hii ni kwa msaada wa Mtandao

Karibu usikilize makala maalum ya dakika 13 inayoangazia Umuhimu wa wanandoa kushiriki elimu ya uzazi wa mpango.
Makala hii imeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) na shirika la WELLSPRING, linalotekeleza mradi wa kutoa elimu kuhusu afya ya mama na mtoto, uzazi wa mpango, na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia.

Muandaaji na msimuliaji wa makala hii ni Mwanaidi Kopakopa.

Karibu usikilize makala maalum ya Umuhimu wa wanandoa kushiriki elimu ya uzazi wa mpango.
Share:

Mgombea udiwani Chuno ataka ushirikiano wa wanawake katika siasa

 

Bi Mariamu Chimbwahi akiwa katika studio za jamii fm Redio akizungumza na Wananchi juu ya ushiriki wa wanawake katika Siasa na Changamoto wanazokutananazo (Picha na Musa Mtepa)

Mgombea udiwani Kata ya Chuno kupitia CCM, Mariamu Chimbwahi, amewataka wanawake kuanza uongozi ngazi za chini ili kujijengea uzoefu, huku akihimiza ushirikiano baina yao na kushiriki katika shughuli za kiuchumi ili kujitegemea

Na Musa Mtepa

Wanawake wametakiwa kujitokeza kugombea nafasi za uongozi kuanzia ngazi za chini, ili kujijengea uzoefu na kujiamini kabla ya kuwania nafasi za juu katika uongozi wa kisiasa na kijamii.

Kauli hiyo imetolewa leo, Septemba 29, 2025, na mgombea udiwani wa Kata ya Chuno, Manispaa ya Mtwara Mikindani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mariamu Chimbwahi, wakati akizungumza katika kipindi cha Dira ya Asubuhi kinachorushwa na Jamii FM Radio.

Bi. Chimbwahi amesema licha ya kuwepo kwa jitihada za kuwawezesha wanawake kisiasa, bado ni muhimu kwao kuanza uongozi kutoka ngazi ya chini ili kupata uzoefu wa kusimama jukwaani, kujibu hoja, na kushiriki mijadala ya kisiasa kwa ufanisi.

Sauti ya 1: Mariamu Chimbwahi, Mgombea Udiwani Kata ya Chuno
Mgombea udiwani kata ya Chuno Manispaa ya Mtwara Mikindani Bi Mariamu Chimbwahi akiwa katika Studio za jamii fm Redio(Picha na Musa Mtepa)

Aidha, Mariamu Chimbwahi ametoa wito kwa wanawake kutoa ushirikiano wa dhati kwa wanawake wenzao pindi wanapoamua kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, huku akitaka jamii kuachana na dhana potofu kwamba “adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzake”.

Sauti ya 2: Mariamu Chimbwahi, Mgombea Udiwani Kata ya Chuno

Katika hatua nyingine, Bi. Chimbwahi amesema endapo atafanikiwa kuchaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya Chuno, atahakikisha anawahamasisha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi zitakazowawezesha kujitegemea, kulea familia zao kwa ufanisi, na kuwawezesha watoto kupata elimu bora.

Sauti ya 3: Mariamu Chimbwahi, Mgombea Udiwani Kata ya Chuno
Share:

Watoto kuacha shule chanzo viashiria vya uvunjifu wa amani

 

Maafisa kutokashirika la TASA Tanzania wakiwa katika studio za Jamii fm redio zizopo Mtwara Mjini mtaa wa Naliende (Picha na Musa Mtepa)

Mdondoko wa wanafunzi na ukatili wa kijinsia vyatajwa kuchangia ongezeko la vitendo vinavyohatarisha amani katika jamii , huku wazazi wakilaumiwa kwa kulegeza majukumu ya malezi na ufuatiliaji wa watoto wao

Na Musa Mtepa

Mtwara, Septemba 24, 2025 – Ukatili wa kijinsia pamoja na mdondoko wa wanafunzi mashuleni vimetajwa kuwa miongoni mwa sababu zinazochochea viashiria vya uvunjifu wa amani katika jamii.

Akizungumza katika kipindi Dira ya Asubuhi kinachorushwa na  Jamii FM radio tarehe 24 Septemba, 2025, Afisa Tathmini na Ufuatiliaji kutoka shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Safety Alliance (TASA), Bw. Hamisi Mwinshekhe, amesema wanafunzi wanaokumbwa na changamoto ya kuacha shule hukosa mwelekeo wa maisha, hali inayowafanya kuwa rahisi kushawishika kujiingiza kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani.

Sauti ya Hamisi Mwinshekhe, Afisa Tathmini na Ufuatiliaji – TASA

Bw. Mwinshekhe ameongeza kuwa chanzo kikuu cha mdondoko wa wanafunzi ni kulegalega kwa wazazi katika jukumu la malezi. Ameeleza kuwa baadhi ya wazazi huacha watoto wao kulelewa na mazingira ya mitaani, jambo linalowapelekea vijana hao kujiunga na makundi hatarishi.

Sauti ya Hamisi Mwinshekhe, Afisa Tathmini na Ufuatiliaji – TASA

Kwa upande wake, Mratibu wa Miradi kutoka shirika la TASA, Bi. Betty Chenge, amesema wazazi wengi wamekuwa wakiwaachia walimu jukumu la malezi na ufuatiliaji wa watoto wao, badala ya kushirikiana nao kikamilifu. Hali hiyo, amesema, imekuwa chanzo cha ongezeko la utoro na mdondoko mashuleni.

Sauti ya 1 Betty Chenge, Afisa Miradi – TASA

Aidha, Bi. Chenge ameisisitiza jamii kutambua kuwa malezi ya mtoto si jukumu la mtu mmoja pekee, bali ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha mtoto anapata mahitaji yake ya msingi. Ameongeza kuwa jamii inapaswa kuwasaidia watoto wanaoonesha viashiria vya mienendo hatarishi kwa kuwaelimisha na kuwaongoza katika njia sahihi.

Sauti ya 2 Betty Chenge, Afisa Miradi – TASA

Katika mjadala huo, baadhi ya wasikilizaji waliopiga simu kushiriki kipindi wamelishukuru shirika la TASA kwa elimu waliyopatiwa, huku wakikiri kuwa uzembe wa malezi kutoka kwa baadhi ya wazazi umekuwa chanzo kikuu cha mdondoko wa wanafunzi na kushiriki kwao katika vitendo vinavyohatarisha amani ya jamii.

Sauti za wasikilizaji wakichangia kwa njia ya simu

Shirika la Tanzania Safety Alliance (TASA) kwa sasa linatekeleza mradi wa “Amani Yetu Kesho Yetu” , unaotekelezwa katika kata tano za Halmashauri ya Mtwara Vijijini ambazo ni MadimbaTangazoNalinguMsimbati, na Mahurunga.

Share:

TANESCO kuongeza uzalishaji wa umeme Mtwara

 

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Ngowele akizungumza na vyombo vya Habari wakati wa upokeaji wa mashine za uzalishaji umeme(Picha na Musa Mtepa)

TANESCO kuongeza uzalishaji wa umeme kwa MW 20 katika kituo cha Hiari, Mtwara, kukabiliana na upungufu wa umeme Lindi na Mtwara. Mashine mpya itakamilika ndani ya mwezi mmoja, ikiongeza uzalishaji hadi MW 70

Na Musa Mtepa

Mtwara, Tanzania – Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linatarajia kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme kwa megawati 20 katika kituo cha Hiari, mkoani Mtwara, ikiwa ni juhudi za kukabiliana na changamoto ya upungufu wa umeme katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Mtwara, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Ngowele, amesema kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza nguvu ya uzalishaji wa umeme kufikia megawati 70, kutoka megawati 38 zinazohitajika kwa sasa.

Sauti ya , Bi. Irene Ngowele Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO

Ameongeza kuwa ufungaji wa mashine hiyo mpya unatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha mwezi mmoja, ambapo baada ya kukamilika, itasaidia kuongeza uzalishaji wa umeme wa ziada ukilinganisha na matumizi ya kila siku.

Sauti ya 2, Bi. Irene Ngowele Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO

TANESCO imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa maeneo yote ya Tanzania, na hatua hii inatazamiwa kuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi na shughuli za kiuchumi za mikoa ya kusini.

Share:

Mtwara yapiga hatua dhidi ya talaka holela

 

Ofisi za Door of Hope Tanzania zilizopo katika mtaa wa Kiyangu Manispaa ya Mtwara Mikindani(Picha na Musa Mtepa)

Door of Hope Tanzania imewasilisha mrejesho wa mradi wa “Pinga Ukatili, Jenga Amani na Kizazi Chenye Usawa” mkoani Mtwara, ukilenga kupinga ukatili wa kijinsia na kutoa msaada wa kisheria. Viongozi wamesifu mafanikio, ikiwemo kupungua kwa funga nyumba na talaka holela

Na Musa Mtepa

Shirika lisilo la Kiserikali la Door of Hope Tanzania, linalojihusisha na utetezi, uwezeshaji na usaidizi kwa vijana na wanawake nchini kupitia huduma za msaada wa kisheria bila malipo,limewasilisha mrejesho wa utekelezaji wa mradi wake wa “Pinga Ukatili, Jenga Amani na Kizazi Chenye Usawa” kwa wadau mbalimbali mkoani Mtwara.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa TCCIA, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mheshimiwa Abdalla Mwaipaya, amesema kuwa matukio ya ukatili wa kijinsia, hususan vitendo vya “funga nyumba” vinavyofanywa na baadhi ya wanaume, vimepungua ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Sauti ya Abdala Mwaipaya mkuu wa wilaya ya Mtwara

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Door of Hope Tanzania, Clemence Mwombeki, amesema kuwa lengo la kikao hicho ni kutoa mrejesho wa shughuli zilizotekelezwa kama sehemu ya mwendelezo wa mradi huo, sambamba na kuishauri serikali kuchukua hatua stahiki juu ya changamoto zilizobainika.

Sauti ya Clemence Mwombeki Mkurugenzi Mtendaji wa Door of Hope Tanzania

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, Bi. Athmini Mapalilo, amesema serikali imeanza kutoa mafunzo kwa jamii juu ya matumizi sahihi ya mapato yanayotokana na zao la korosho. Aidha, ametoa rai kwa taasisi za kidini na mashirika ya kiraia kuendelea kutoa elimu kuhusu madhara ya talaka holela na vitendo vya funga nyumba.

Sauti ya Bi. Athmini Mapalilo afisa maendelea ya jamii halmashauri ya wilaya ya Mtwara

Akichangia katika kikao hicho, Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Kata ya Mahurunga, Bi. Asmini Liwowa, pamoja na Bi. Fatuma Shaibu, mkazi wa Chikongola, walisisitiza umuhimu wa wadau kutoa elimu kwa familia kuhusu athari za talaka holela na namna zinavyowaathiri watoto na jamii kwa ujumla.

Sauti ya Asmini Liwowa na Fatuma Shaibu
Share:

CCM Mtwara Mjini yataka mafiga matatu Oktoba 29

 

Rehema Sombi makamu mwenyekiti wa umoja wa vijana (UVCCM) taifa akizungumza na wananchi waliojitokea kwenye uzinduzi wa kampeni wa chama hicho (Picha na Musa Mtepa)

CCM Mtwara Mikindani yazindua kampeni Septemba 14, 2025, kwa wagombea ubunge na udiwani. Rehema Sombi ataka mshikamano na ushindi wa “mafiga matatu” – Diwani, Mbunge, Rais. Joel Nannauka na Arif Primji waahidi maendeleo na huduma bora kwa wananchi kupitia sera za CCM.

Na Musa Mtepa

Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Mtwara Mikindani kimezindua rasmi kampeni zake kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, kwa upande wa mgombea ubunge na wagombea udiwani wa Jimbo la Mtwara Mjini.

Akizungumza kama mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Bi. Rehema Sombi, amewataka wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kudumisha mshikamano na kuhakikisha wanaweka “mafiga matatu” kwa kuchagua madiwani, mbunge na rais kutoka Chama cha Mapinduzi.

QUEIN….2 Rehema Sombi makamu mwenyekiti umoja wa vijana taifa

Kwa upande wake, mgombea ubunge wa Jimbo la Mtwara Mjini kupitia CCM, Dkt Joel Nannauka, amesema kuwa ndoto yake ni kuibadilisha taswira ya Mtwara kutoka kuwa ya mwisho hadi kuwa ya mbele katika maendeleo ya kitaifa.

Sauti ya Dkt Joel Nannauka Mgombea ubunge CCM Mtwara mjini
Makamu Mwenyekiti uvccm Rehema Sombi akimkabidhi Mwongozo wa utekelezaji wa ilani Mgombea ubunge Mtwara Mjini Dkt Joel Nannauka(Picha na Musa Mtepa)

Naye mgombea ubunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini, Arif Primji, amewataka wananchi wa Manispaa ya Mtwara, ambao wanakadiriwa kufikia idadi ya watu 146,772, kuendelea kuiamini CCM kutokana na huduma mbalimbali za kijamii zilizowafikia kupitia serikali ya chama hicho.

Sauti ya Arif Primj Mgombea Ubunge jimbo la Mtwara vijijini
Share:

Wananchi kijiji cha Nyengedi kuchangia 10,000 ujenzi wa shule

 

Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Nyengedi wakisikiliza kwa umakini maelezo ya viongozi wao wa kata na kijiji katika mkutano (Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa Nyengedi wametakiwa kutekeleza kwa uaminifu makubaliano ya kuchangia shilingi 10,000 kwa kila kaya ili kufanikisha ujenzi wa Shule ya Msingi Mnyengedi, mradi unaolenga kuboresha elimu na kupunguza adha ya watoto kutembea umbali mrefu

NA MUSA MTEPA

Wananchi wametakiwa kutekeleza kwa uaminifu makubaliano wanayoyafikia kwa hiari kupitia mikutano ya vijiji, ili kufanikisha malengo ya maendeleo ya pamoja.

Akizungumza kuhusu makubaliano ya kuchangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Mnyengedi, Afisa Tarafa wa Mayanga, Bw. Marco Mapunda amesema wananchi wa kijiji cha Nyengedi wamekubaliana kila kaya ichangie kiasi cha shilingi 10,000.

Aidha Bw Mapunda amesema kwa yeyote ambae atakiuka kutokubali kuchangia atachukuliwa hatua za kisheria kama mwalifu mwingine.

Sauti ya Marco Mapunda afisa tarafa Mayanga

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Nyengedi, Bi Lukia Mnyachi, amesema kijiji hicho hapo awali kilikuwa kitongoji cha Kijiji cha Kawawa, na hivyo walikuwa wakitegemea huduma muhimu kutoka huko.

Aidha amesema kuwa hivyo kutokana na hali hiyo kupitia mikutano ya kijiji wakakubarina kutoa fedha shilingi 10,000 kwa ajili ya kununua uwanja tayari kwa mchakato wa ujenzi wa shule.

Sauti ya Lukia Mnyachi mwenyekiti wa Kijiji

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamepongeza juhudi za mwenyekiti wao na kuahidi kushiriki kikamilifu kwenye mchakato wa maendeleo.

Sauti ya Wananchi wa Nyengedi

Mradi huu wa ujenzi wa shule unalenga kuboresha upatikanaji wa elimu kwa watoto wa kijiji cha Nyengedi na kupunguza changamoto za kutembea umbali mrefu kufuata elimu.

Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>