CCM Mtwara Mjini yataka mafiga matatu Oktoba 29

 

Rehema Sombi makamu mwenyekiti wa umoja wa vijana (UVCCM) taifa akizungumza na wananchi waliojitokea kwenye uzinduzi wa kampeni wa chama hicho (Picha na Musa Mtepa)

CCM Mtwara Mikindani yazindua kampeni Septemba 14, 2025, kwa wagombea ubunge na udiwani. Rehema Sombi ataka mshikamano na ushindi wa “mafiga matatu” – Diwani, Mbunge, Rais. Joel Nannauka na Arif Primji waahidi maendeleo na huduma bora kwa wananchi kupitia sera za CCM.

Na Musa Mtepa

Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Mtwara Mikindani kimezindua rasmi kampeni zake kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, kwa upande wa mgombea ubunge na wagombea udiwani wa Jimbo la Mtwara Mjini.

Akizungumza kama mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Bi. Rehema Sombi, amewataka wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kudumisha mshikamano na kuhakikisha wanaweka “mafiga matatu” kwa kuchagua madiwani, mbunge na rais kutoka Chama cha Mapinduzi.

QUEIN….2 Rehema Sombi makamu mwenyekiti umoja wa vijana taifa

Kwa upande wake, mgombea ubunge wa Jimbo la Mtwara Mjini kupitia CCM, Dkt Joel Nannauka, amesema kuwa ndoto yake ni kuibadilisha taswira ya Mtwara kutoka kuwa ya mwisho hadi kuwa ya mbele katika maendeleo ya kitaifa.

Sauti ya Dkt Joel Nannauka Mgombea ubunge CCM Mtwara mjini
Makamu Mwenyekiti uvccm Rehema Sombi akimkabidhi Mwongozo wa utekelezaji wa ilani Mgombea ubunge Mtwara Mjini Dkt Joel Nannauka(Picha na Musa Mtepa)

Naye mgombea ubunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini, Arif Primji, amewataka wananchi wa Manispaa ya Mtwara, ambao wanakadiriwa kufikia idadi ya watu 146,772, kuendelea kuiamini CCM kutokana na huduma mbalimbali za kijamii zilizowafikia kupitia serikali ya chama hicho.

Sauti ya Arif Primj Mgombea Ubunge jimbo la Mtwara vijijini
Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>