TANESCO kuongeza uzalishaji wa umeme Mtwara

 

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Ngowele akizungumza na vyombo vya Habari wakati wa upokeaji wa mashine za uzalishaji umeme(Picha na Musa Mtepa)

TANESCO kuongeza uzalishaji wa umeme kwa MW 20 katika kituo cha Hiari, Mtwara, kukabiliana na upungufu wa umeme Lindi na Mtwara. Mashine mpya itakamilika ndani ya mwezi mmoja, ikiongeza uzalishaji hadi MW 70

Na Musa Mtepa

Mtwara, Tanzania – Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linatarajia kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme kwa megawati 20 katika kituo cha Hiari, mkoani Mtwara, ikiwa ni juhudi za kukabiliana na changamoto ya upungufu wa umeme katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Mtwara, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Ngowele, amesema kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza nguvu ya uzalishaji wa umeme kufikia megawati 70, kutoka megawati 38 zinazohitajika kwa sasa.

Sauti ya , Bi. Irene Ngowele Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO

Ameongeza kuwa ufungaji wa mashine hiyo mpya unatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha mwezi mmoja, ambapo baada ya kukamilika, itasaidia kuongeza uzalishaji wa umeme wa ziada ukilinganisha na matumizi ya kila siku.

Sauti ya 2, Bi. Irene Ngowele Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO

TANESCO imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa maeneo yote ya Tanzania, na hatua hii inatazamiwa kuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi na shughuli za kiuchumi za mikoa ya kusini.

Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>