
Wananchi wa Nyengedi wametakiwa kutekeleza kwa uaminifu makubaliano ya kuchangia shilingi 10,000 kwa kila kaya ili kufanikisha ujenzi wa Shule ya Msingi Mnyengedi, mradi unaolenga kuboresha elimu na kupunguza adha ya watoto kutembea umbali mrefu
NA MUSA MTEPA
Wananchi wametakiwa kutekeleza kwa uaminifu makubaliano wanayoyafikia kwa hiari kupitia mikutano ya vijiji, ili kufanikisha malengo ya maendeleo ya pamoja.
Akizungumza kuhusu makubaliano ya kuchangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Mnyengedi, Afisa Tarafa wa Mayanga, Bw. Marco Mapunda amesema wananchi wa kijiji cha Nyengedi wamekubaliana kila kaya ichangie kiasi cha shilingi 10,000.
Aidha Bw Mapunda amesema kwa yeyote ambae atakiuka kutokubali kuchangia atachukuliwa hatua za kisheria kama mwalifu mwingine.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Nyengedi, Bi Lukia Mnyachi, amesema kijiji hicho hapo awali kilikuwa kitongoji cha Kijiji cha Kawawa, na hivyo walikuwa wakitegemea huduma muhimu kutoka huko.
Aidha amesema kuwa hivyo kutokana na hali hiyo kupitia mikutano ya kijiji wakakubarina kutoa fedha shilingi 10,000 kwa ajili ya kununua uwanja tayari kwa mchakato wa ujenzi wa shule.
Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamepongeza juhudi za mwenyekiti wao na kuahidi kushiriki kikamilifu kwenye mchakato wa maendeleo.
Mradi huu wa ujenzi wa shule unalenga kuboresha upatikanaji wa elimu kwa watoto wa kijiji cha Nyengedi na kupunguza changamoto za kutembea umbali mrefu kufuata elimu.






No comments:
Post a Comment