MTWARA: WANANCHI KULIPWA FIDIA NDANI YA WIKI MBILI

Image may contain: 32 people, people smiling, crowd and outdoor
Mkuu wa mkoa wa MTWARA MHE GELASIUS BYAKANWA amewahakikishia wananchi wa kata ya NANGOO wilayani MASASI kuwa watalipwa fidia ya maeneo na Mali zilizoharibiwa wakati wa utekelezaji wa mradi wa maji wa MBWINJI unaotumiwa na wananchi wa MASASI na NACHINGWEA.

MKuu wa mkoa ametoa kauli hiyo baaada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa kata hiyo yaliyoainishwa katika makundi matatu ikiwemo watu kulipwa pungufu, kulipwa wasiostahili na wengine kutolipwa kabisa wakati ni wahanga.

Kufuatia hali hiyo BYAKANWA amewaeleza wananchi wa kata hiyo na Kata jirani kuwa atahakikisha kila mtu anayestahili kulipwa analipwa ndani ya miezi MIWILI baada ya uchunguzi wa kutambua waliolipwa wakati hawana sifa kukamilika ambapo ndani ya miezi hiyo miwili watakuwa wamebainika na hatua zitachukuliwa.

MHE BYAKANWA amesema "Nipeni hii miezi MIWILI nikipata kibali kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU tutashughulikia ngazi ya Mkoa kwa kuunda kamati itakayo fanya uchunguzi na kutambua wale wanaostahili na wasiostahili na hatua zitachukuliwa hapahapa bila kusubiri utaratibu wa TAKUKURU ambazo zina chukua unamlolongo mrefu"

Wananchi wametoa malalamiko kuwa kuna watu ambao hawakupitiwa na mradi walilipwa fedha wakati wanaostahili hawajalipwa litafanyiwa kazi haraka na watarudisha fedha hizo ili walipwe wanaostahili.

Akijibu hoja ya kulipa fidia watu hewa Mwakilishi wa ofisi ya TAKUKURU Masasi ameeleza kuwa uchunguzi unaendelea wa kuwabaini watu hao na kwa kijiji cha Liputu kilichopo Kata ya ndanda wilayani humo umekamilka na imebainika kweli kuwa wapo watu ambao walilipwa bila kuwa na maeneo yaliyoathiriwa na mradi.

Aidha MHE. BYAKANWA amemwagiza Mkurugenzi wa MANAWASA kuhakikisha anafungua vioski vya maji vyote vilivyofungwa kwasababu ya wauza maji wamekila hela ili wananchi waendee kupata huduma ya maji kama serikali ya awamu ya tano inavyoelekeza kuwa wananchi lazima wapate maji kwani wanaadhibiwa kwa kosa ambalo hawajatenda.

Pia amemsisitiza Mkurugenzi wa MANAWASA kuhakikisha wale wauza maji wote waliokula fedha wakamatwe ili walejeshe fedha hizo haraka na baada ya wiki mbili zoezi hilo liwe limekamilika.

Image may contain: 10 people, people smiling, outdoorMHE. BYAKANWA amewataka wananchi kutunza vyanzo vya maji na miundombinu ya maji kwani jamii ndio yenye jukumu la kutunza kwa kuto fanya shughuli zozote karibu na vyanzo vya Maji lakini pia kuilinda miundombinu yake kwani serikali inatumia fedha nyingi kutekeleza Miradi hiyo.

Mradi wa Mbwiji ulianza kutekelezwa 2011 mwaka na ulighalimu zaidi ya bilioni 30.

HABARI NA JOINA NZARI- MASASI

Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>