Kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa leo Kiongozi wa ACT, Zitto Kabwe, amesema wakulima hao hulaliwa na wanunuzi wa zao hilo na kulazimika kuuza kilo moja ya maharage kwa bei ya Sh. 700 hadi 800, wakati yakisafirishwa mjini huuzwa Sh. 1800 hadi 2000 kwa kilo.
Amesema kufuatia changamoto hiyo, chama hicho kupitia Diwani wake wa Kata ya Biturana, Barnabas Baranzila wamehamasisha wananchi kuchonga barabara kutoka kwenye vijiji vya kata hiyo hadi makao makuu ya Kata, ili kurahaisha usafirishaji wa mazao na hivyo kupunguza unyonyaji kwenye soko.
Hata hivyo, Zitto amesema ACT itawasaidia wakulima hao kuunda ushirika imara ili kuhakikish ahawanyonywi katika soko la mazao yao.
CHANZO: DEWJBLOG






No comments:
Post a Comment