• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

Watanzania wanufaika na mageuzi ya sheria ya madini

 

Mabadiliko ya sheria ya Madini, zaidi ya Asilimia 97 ya watanzania wajitokeza kufanya kazi kwenye sekta ya madini

Na Gregory Milanzi

Mabadiliko makubwa ya sheria ya madini yaliyofanyika mwaka 2017 yamewezesha watanzania wengi kufanya kazi katika sekta ya madini, ambapo katika migodi migubwa ya madini iliyopo nchini asilimia 97 ya wafanyakazi ni watazania huku asilimia zaidi ya tisini ya uongozi na utawala katika migodi hiyo ni watanzania.

Kabla ya mabadiliko ya sheria ya madini mwaka 2017, idadi ya watanzania waliokuwa wanafanya kazi katika migodi mikubwa ya madini, shughuli za utafutaji na uchakataji wa gesi asilia ilikuwa ni ndogo.

Lakini baada ya kufanyika kwa mabadiliko watanzania wengi wanafanya kazi na kusimamia migodi hiyo.

Kamishina wa madini nchini Terence Ngole akiwa mkoani Mtwara katika warsha ya kuelimisha umma kuhusu shughuli za uwazi na uwajibikaji katika sekta ya madini, mafuta na gesi asilia iliyoandaliwa na Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji Katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) anafafanua zaidi.

Sauti ya 1 TERENCE NGOLE-Kamishina wa Madini

Sheria hiyo inawataka wawekeza kutumia huduma zinazopatikana nchini, na zisizopatikana nchini zihusishe makampuni ya ndani ya nchi, hatua hii imesaidia kuongezeka kwa manunuzi yanayofanywa na watazania.

Sauti ya 2 TERENCE NGOLE-Kamishina wa Madini

Wazawa wanaofanya kazi katika sekta hiyo wanaonesha ufanisi mkubwa na halmashauri zikinufaika zaidi na matokeo ya sheria hiyo.

Sauti ya HIDAYA GARIATANO-Mfanyakazi kampuni ya Gesi Asilia MNP na

Share:

Mahakama yaendelea kuimarisha utoaji wa haki Mtwara

 

Mhe.Edwin Kakolaki Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara akihutubia katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini iliyofanyika viwanja vya Mahakama kanda ya Mtwara(Picha na Musa Mtepa)

Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara imesema inaendelea kuimarisha uwezo wake ili kuhakikisha utoaji wa haki kwa wakati kama sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Kauli hiyo imetolewa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika Mtwara.

Na Musa Mtepa

Katika kutekeleza mipango ya maendeleo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mahakama kwa kushirikiana na Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha uwezo wake ili kusimamia utoaji wa haki kwa wakati kwa taasisi, mashirika na wananchi nchini.

Hayo yameelezwa Februari 2, 2026 na Mheshimiwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara, Edwin Kakolaki, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara.

Sauti ya 1: Edwin Kakolaki – Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara

Mheshimiwa Jaji Kakolaki amesema kuwa katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, muhimili wa Mahakama una nafasi muhimu katika kujenga taifa lenye haki, amani, usalama na utulivu kwa kujenga mazingira salama ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.

Sauti ya 2: Edwin Kakolaki – Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara
Watumishi wa Mahakama wakiwa katika viwanja Mahakama kuu kanda ya Mtwara(Picha na Musa Mtepa)

Aidha, Jaji Kakolaki amesema Mahakama imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika matumizi ya teknolojia, hatua inayochangia kuongeza ufanisi na kasi ya utendaji kazi ikilinganishwa na miaka ya nyuma, jambo linalosaidia wananchi kupata haki kwa wakati.

Sauti ya 3: Edwin Kakolaki – Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara
Mkuu wa wilaya ya Mtwara Abdala Mwaipaya akimkaribisha mkuu wa mkoa wa Mtwara tayari kwa kutoa salamu za mkoa katika maadhimisho hayo(Picha Musa Mtepa)

Akitoa salamu za maadhimisho hayo, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Mkoa wa Mtwara, Lightness Kikao, amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo imebeba uzito mkubwa kwa kuwa inaakisi ukweli kwamba hakuna maendeleo ya kweli bila uwepo wa haki, utawala wa sheria na misingi ya utawala bora.

Sauti: Lightness Kikao – Makamu Mwenyekiti, TLS Mkoa wa Mtwara
Makamu Mwenyekiti, TLS Mkoa wa Mtwara Lightness Kikao akitoa akitoa salamu za TLS (picha na Musa Mtepa)

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrik Sawala, ambaye alikuwa mgeni maalumu katika maadhimisho hayo, amesema utoaji wa haki kwa wakati kwa wananchi utadumisha amani na utulivu katika mkoa wa Mtwara na taifa kwa ujumla, hali itakayowapa wananchi fursa ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo kwa amani.

Sauti: Kanali Patrik Sawala – Mkuu wa Mkoa wa Mtwara
Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanal Patrik Sawala akitoa salamu za mkoa katika maadhimisho ya siku sheria nchini (Picha na Musa Mtepa)
Share:

Matumizi ya mkaa-Makala

 

Mmoja wa wajasiliamali akindaa jiko kwaajili ya kuchoma mahindi ili kupata kipato. Picha na Gregory Millanzi

Ongezeko la watu pamoja na kupanda kwa gharama za nishati mbadala kama gesi na umeme kumeongeza kwa kiasi kikubwa utegemezi wa mkaa.

Na Gregory Millanzi

Kwa miongo mingi, mkaa umekuwa chanzo kikuu cha nishati kwa kaya nyingi, hususani katika maeneo ya mijini na vijijini. Hapo awali matumizi ya mkaa yalionekana kuwa suluhisho rahisi na la gharama nafuu kwa shughuli za kupikia na matumizi mengine ya kila siku. Wananchi waliutumia kwa kiasi na kwa uangalifu, wakitegemea misitu iliyokuwepo kwa wingi wakati huo.

Kadri miaka ilivyopita, ongezeko la watu pamoja na kupanda kwa gharama za nishati mbadala kama gesi na umeme kumeongeza kwa kiasi kikubwa utegemezi wa mkaa. Hali hii imesababisha ukataji mkubwa wa miti kwa ajili ya uzalishaji wa mkaa, jambo ambalo limeathiri vibaya misitu na mazingira kwa ujumla.

Athari za matumizi makubwa ya mkaa sasa zimeanza kujidhihirisha waziwazi. Miongoni mwa athari hizo ni uharibifu wa misitu, mabadiliko ya tabianchi, kuongezeka kwa joto duniani, pamoja na changamoto za kiafya zitokanazo na moshi unaozalishwa wakati wa matumizi ya mkaa majumbani.

Makala haya yanalenga kuelimisha jamii kuhusu madhara ya matumizi ya mkaa na kuhamasisha matumizi ya nishati safi, salama na endelevu ili kulinda mazingira pamoja na afya ya binadamu.

Bonyeza hapa kusikiliza kwa undani zaidi

Share:

Athari za ukataji miti

 

Moja ya miti iliyokatwa katika mazingira. Picha na Gregory Millanzi

Athari za ukataji miti zinaonekana wazi kupitia ukame, mafuriko, na mabadiliko ya tabianchi yanayoathiri moja kwa moja maisha ya binadamu.

Na Gregory Millanzi

Ukataji miti umekuwa tatizo linalokua kwa kasi katika jamii nyingi, hasa maeneo ya vijijini. Hapo zamani, misitu ilikuwa chanzo muhimu cha mvua ya kutosha, hewa safi, na makazi ya wanyama pori. Wananchi waliitegemea misitu kwa mahitaji kama kuni, dawa za asili, na chakula, huku wakihifadhi mazingira yao.

Hata hivyo, kutokana na ongezeko la idadi ya watu pamoja na kuongezeka kwa mahitaji ya ardhi kwa ajili ya kilimo, makazi, na biashara ya mbao, ukataji miti umefanyika kiholela bila juhudi za kupanda miti upya. Matokeo yake yamekuwa makubwa na ya kutisha, yakiwemo kupungua kwa mvua, kuharibika kwa ardhi, kuongezeka kwa joto, pamoja na kutoweka kwa baadhi ya wanyama na mimea.

Kwa sasa, athari za ukataji miti zinaonekana wazi kupitia ukame, mafuriko, na mabadiliko ya tabianchi yanayoathiri moja kwa moja maisha ya binadamu. Simulizi hii inalenga kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa misitu na kuchukua hatua madhubuti za uhifadhi wa mazingira kwa ajili ya ustawi wa kizazi cha sasa na kijacho.

Bonyeza hapa usikilize makala hii inayochambua kwa kina athari za ukataji miti mkoani Mtwara. Makala hii imeandaliwa na kusimuliwa na Gregory Millanzi.

Share:

Mtwara wahimizwa kuzingatia elimu kwa wenye ulemavu

 

Mkurugenzi wa MERODI Frances Chiwango akiwa na wadau wa elimu wakizungumzia umuhimu wa elimu kwa wenye ulemavu(Picha na Musa Mtepa)

Wazazi na walezi mkoani Mtwara wametakiwa kuwapeleka shule watoto wenye ulemavu katika kipindi hiki cha uandikishaji wa Elimu ya Awali na Msingi. Wito huo umetolewa na MERODI kupitia Jamii FM, ikisisitiza elimu jumuishi, ushirikiano wa jamii na msaada wa serikali kwa wazazi wa watoto wenye ulemavu

Na Musa Mtepa

Wazazi na walezi mkoani Mtwara wametakiwa kuweka kipaumbele katika elimu kwa watoto wenye ulemavu kwa kuhakikisha wanawaandikisha katika kipindi hiki cha uandikishaji wa Elimu ya Awali na Msingi kinachoendelea kote nchini.

Wito huo umetolewa leo Januari 29, 2026 na Frances Chiwango, Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na watu wenye ulemavu mkoani Mtwara ya Mtwara Economic Rights Organization for Disabled (MERODI), alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Dira ya Asubuhi kinachorushwa na Jamii FM Radio.

Akizungumza katika kipindi hicho, Chiwango amesema licha ya kuwepo kwa mwamko kwa baadhi ya wazazi na walezi ikilinganishwa na miaka ya nyuma, bado juhudi zaidi zinahitajika ili kuendelea kuwahamasisha wazazi kuwapeleka shule watoto wenye ulemavu.

Sauti ya 1 – Frances Chiwango, Mkurugenzi wa MERODI

Aidha, Chiwango amesema uamuzi wa serikali kuweka mkazo katika elimu jumuishi umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza unyanyapaa kati ya wanafunzi wenye ulemavu na wasio na ulemavu, akitolea mfano safari yake ya kwanza kuelekea shuleni.

Sauti ya 2 – Frances Chiwango, Mkurugenzi wa MERODI

Vilevile, ametoa wito kwa viongozi wa serikali za mitaa pamoja na maafisa ustawi wa jamii kushirikiana kwa karibu na wazazi na walezi ili kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata haki yao ya msingi ya elimu.

Sauti ya 3 – Frances Chiwango, Mkurugenzi wa MERODI

Kwa upande wake, Maximilian Makau, mdau wa elimu na mjumbe wa Bodi ya MERODI, ameitaka jamii kuacha kuwaona watoto wenye ulemavu kama mzigo, akisisitiza kuwa wana uwezo wa kujitegemea na kufanikiwa kama watu wengine endapo watapatiwa fursa sawa.

Sauti ya 1 – Maximilian Makau, Mdau wa Elimu na Mjumbe wa MERODI

Makau pia ameitaka serikali kuwaangalia kwa jicho la pekee wazazi wenye watoto wenye ulemavu, hususan kwa kuwawezesha kupitia mikopo au programu maalumu kama ilivyo kwa makundi mengine maalumu, ili kuwasaidia watoto hao kupata elimu bora.

Sauti ya 2 – Maximilian Makau, Mdau wa Elimu na Mjumbe wa MERODI
Share:

Polisi Mtwara wachunguza tukio la mtoto kujaribu kuua

 

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara ACP Issa Suleiman akitoa taarifa ya matukio mbalimbali ya kihalifu kwa waandishi wa habari yaliyotokea mkoani Mtwara (Picha na Musa Mtepa)

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linachunguza tukio la mtoto wa miaka 12 anayedaiwa kujaribu kumuua mtoto wa miaka 4 wilayani Nanyumbu. Wakati huo huo, polisi wamefanikiwa kukamata watuhumiwa wa nyara za serikali na dawa za kulevya katika oparesheni mbalimbali mkoani humo.

Na Musa Mtepa

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linaendelea kuchunguza tukio la mauaji lililohusisha mtoto, lililotokea katika kijiji cha Masyalele, wilayani Nanyumbu, mkoani Mtwara.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Januari 27, 2026, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Issa Suleiman, amesema mtoto Shabani Muebo (12) anadaiwa kujaribu kumuua mtoto mwenzake Ibrahimu Salumu Kelvine (4), wote wakazi wa kijiji cha Masyalele.

ACP Suleiman amesema tukio hilo lilitokea tarehe 23 Januari, 2026, ambapo mtuhumiwa alimlaghai mhanga aliyekuwa akicheza na watoto wenzake, kisha akaelekea naye katika msitu wa jando wa kijiji hicho na kumjeruhi shingoni kwa kutumia kiwembe kabla ya kumtelekeza katika pori.

Kamanda huyo ameongeza kuwa, Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kina wa tukio hilo, huku mtoto aliyedhurika akiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Misheni ya Ndanda, wilayani Masasi mkoani Mtwara.

Sauti ya 1 – ACP Issa Suleiman, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara

Katika hatua nyingine, ACP Suleiman amesema kupitia doria na misako inayoendeshwa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Askari wa Wanyamapori, watuhumiwa wawili wamekamatwa kwa tuhuma za kupatikana na nyara za serikali aina ya meno ya tembo.

Watuhumiwa hao ni Ignas Aron Mponzi (37), mwalimu wa Shule ya Msingi Namitende, na Dickson Ado (46), mkulima, wote wakazi wa kijiji cha Nangumbu wilayani Ruangwa mkoani Lindi.

 Sauti ya 3 – ACP Issa Suleiman, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara

Vilevile, katika mwendelezo wa oparesheni za kupambana na uhalifu, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara tarehe 17 Januari, 2026, liliwakamata Abas Mohamed Nakiti (49) na Mohamedi Mohamed Nakiti (22), wakulima na wakazi wa kijiji cha Mkachima wilayani Masasi, wakiwa na viroba kumi (10) vya dawa za kulevya aina ya bangi zenye uzito wa jumla wa kilogramu 110.

Sauti ya 4 – ACP Issa Suleiman, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara

Aidha, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limeeleza kuwa linaendelea kufuatilia na kudhibiti mbinu mbalimbali zinazotumiwa kufanya uhalifu, ikiwemo kupambana na usafirishaji, uuzaji na matumizi ya dawa za kulevya, ambavyo ni kinyume na sheria za nchi.

Share:

Mtwara wapewa somo unyonyeshaji bora

 

Viongozi na wadau wakiwa kwenye kikao cha Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za TCCIA mjini Mtwara (Picha na Musa Mtepa)

Jamii Mtwara imehimizwa kunyonyesha watoto maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya mwanzo, kuimarisha makuzi yao, huku wadau wakitathmini huduma za malezi na kupanga mipango kupitia PJT-MMMAM.

Na Musa Mtepa

Jamii mkoani Mtwara imetakiwa kuhakikisha watoto wananyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita ya mwanzo bila kuchanganya na chakula au kinywaji kingine chochote, ili waweze kupata makuzi sahihi.

Wito huo umetolewa January 23,2026 wakati wa kikao cha robo mwaka cha wadau mbalimbali wakiwemo  asasi za kiraia kilicholenga kufanya tathmini ya shughuli zilizotekelezwa kuanzia Oktoba hadi Desemba 2025, pamoja na kupanga mipango kazi ya Januari hadi Machi 2026 kupitia Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za TCCIA mjini Mtwara.

Akizungumza katika kikao hicho, Meneja Mradi kutoka Taasisi isiyo ya Kiserikali ya KIMAS yenye makao makuu yake wilayani Masasi mkoani Mtwara, Torai Kibiti, amesema bado kuna changamoto katika baadhi ya maeneo, ikiwemo uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa mtoto kunyonya maziwa ya mama pekee bila kuchanganya na kitu kingine.

Amesema changamoto hiyo inatokana na imani potofu iliyopo katika jamii kwamba mtoto ambaye hajafikisha miezi sita hawezi kunyonya maziwa ya mama pekee, hali inayohitaji kuongeza juhudi za uelimishaji na hamasa kwa jamii.

Akiwasilisha mada kuhusu chombo cha kupima hali ya utekelezaji na ubora wa utoaji wa huduma za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto (Scorecard), kwa niaba ya Ofisa Ustawi wa Mkoa wa Mtwara, Ofisa Ustawi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, Godlove Miho, amesema chombo hicho kinasaidia wadau kujitathmini na kubaini ubora wa huduma wanazotoa kwa watoto.

Sauti ya Godlove Miho, Ofisa Ustawi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Vituo vya Kulelea Watoto mkoani Mtwara, Selemani Issa Mkonga, amesema ili kufikia malengo ya Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto, jamii haina budi kuwekeza katika uanzishaji wa vituo vya kulelea watoto, kwani idadi iliyopo kwa sasa haitoshelezi mahitaji.

Sauti ya Issa Mkonga, Mwenyekiti wa Vituo vya Kulelea Watoto Mkoa wa Mtwara

Aidha, Issa Mkonga amesema upungufu au kukosekana kwa vituo vya kulelea watoto kumesababisha watoto wengi kukumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo unyanyasaji na vitendo vya ukatili mitaani, na kutoa wito kwa wadau kujitokeza kuanzisha vituo hivyo kwa maslahi ya watoto.

Sauti ya pili ya Issa Mkonga, Mwenyekiti wa Vituo vya Kulelea Watoto Mkoa wa Mtwara

Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM)inalengakuhakikisha watoto wote kuanzia mimba hadi umri wa miaka 8 wanapata malezi, makuzi na huduma bora ili wakuekimwili, kiakili, kihisia na kijamii , ikiwemo Afya na Lishe, Malezi Chanya na Ulinzi wa Mtoto, Elimu ya Awali na Maendeleo ya Akili, Makuzi ya Kihisia na Kijamii na Huduma kwa Watoto Wenye Mahitaji Maalum.

Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>