• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

MTWARA: SERIKALI IMESEMA HAIJARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA BARABARA YA MTWARA MNIVATA

Image may contain: 4 people, people smiling, people standing, beard and outdoor
Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Mh MAKAME MBALAWA amepozungumza na Wananchi wa Kata ya Naliendele Jana Tarehe 4/3/2018 na kumtaka Mkandarasi anaejenga Barabara hiyo kwa kiwango cha Lami kuharakisha ujenzi huo.

Waziri MBALAWA mesema"Haturidhishwi na kasi ya Ujenzi wa barabara hii yenye Urefu wa Km 50 Kutoka Mtwara hadi Kijiji cha Mnivata kwa Thamani ya Tsh Bilioni 89.59 na ndio maana tunatembelea mara kwa mara kumsukuma Mkandarasi huyu afanye kwa kasi tunayoitaka"

Akijibu maswali ya baadhi ya Wananchi waliouliza kuhusu Swala la wenyeji kukosa Ajira ndogondogo na kupewa watu wa Mikoa mingine pamoja na kukosa miundombinu itakayosaidia maji yasituwame katika eneo moja, Waziri huyo amesema atayafanyia kazi kama Serikali.
Image may contain: one or more people, people standing, sky, tree, outdoor and nature 
Waziri Mbalawa aliongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara MH EVOD MMANDA ambae nae alipata nafasi ya kuzungumza na Wananchi hao na kuwasihi waendelee kushirikiana na Mkandarasi huyo ili barabara hiyo iweze kukamilika kwa haraka.

Karim Faida-JAMII FM.


Share:

MTWARA: VIWANDA VYA UBANGUAJI LAZIMA WAPATE KOROSHO GHAFI



Waziri wa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji CHARLES MWIJAGE amevihakikishia Viwanda vya Ubanguaji Korosho MTWARA vinapata malighafi hiyo mwaka mzima kuliko ilivyo hivi sasa ambapo zaidi ya tani laki tatu za korosho ghafi zimesafirishwa nje ya Nchi huku Viwanda hivyo vikifungwa kwa kukosa  malighafi hiyo.

MWIJANGE amesema hayo baada ya kutembelea Shirika linalohudumia viwanda vidogo vidogo SIDO  Mkoani hapa na kukuta kiwanda kinachotumiwa na wanawake kubangua korosho kimefungwa kutokana na kukosa Korosho ghafI


Hata hivyo Waziri MWIJAGE amesema hilo haliwezi kukubalika lazima utaratibu ufanyike  ili sehemu ya Korosho ghafi ibaki Nchini kulinda viwanda hivyo,  


Akiwa mkoani MTWARA waziri huyo  amewakabidhi SUMA JKT kazi ya  ujenzi wa Kiwanda cha wajasiriamali  kitakachojengwa katika ofisi za SIDO MTWARA, Mwakilishi wa SUMA JKT Meja ATUPELE MWAMFUPE ambae ni Meneja wa Kanda ya Kusini amesema watahakikisha watafanya kazi ndani ya muda miezi mitatu kazi itakuwa imekamilika.


Maeneo mengine aliyotembelea na kituo cha uwekezaji , Kiwanda cha kubangua korosho cha Cash nut pamoja na kiwanda cha kuzalisha Cementi cha DANGOTE, na MTWARA CEMENT.

GREGORY MILLANZI- JAMII FM 



Share:

DAR ES SALAAM: JOSEPH BUTIKU: UVCCM MLINDENI RAIS MAGUFULI

Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, ndugu  Joseph Butiku, amewaasa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) pamoja na watanzania kwa ujumla kumlinda Mhe. Rais Magufuli dhidi ya maadui zake ambao walikuwa wakitawanya na kujinufaisha na rasilimali za taifa huku wakiwaacha watanzania kwenye dimbwi la umaskini.
Mzee Butiku ameyasema hayo leo Jumapili Machi 4, 2018, jijini Dar es Salaam, alipokuwa akiwasilisha mada ya Uzalendo na Historia ya Taifa letu kwa Viongozi, ikiwa ni sehemu ya mafunzo maalumu ya uongozi kwaajili ya vijana wa umoja huo kwa ngazi ya kata, wilaya na mkoa inayoendelea jijini Dar es Salaam.
“Uamuzi wa Rais Magufuli wa kuhakikisha rasilimali za taifa letu haziendelei kunyonywa na wezi wa ndani na nje umemletea maadui wengi sana na nyinyi vijana mnayo dhamana kubwa ya kuhakikisha mnamlinda Rais wetu kufa na kupona” amesema Butiku.
Toka Rais Magufuli aingie madarakani na kuanza kusimamia rasilimali za nchi ili ziwanufaishe watanzania wote hasa maskini, kumekuwepo na vilio kutoka kwa wale ambao walikuwa wakinufaika na rasilimali hizo, huku wakifanya kila njia kuhakikisha wanakwamisha juhudi zake, jambo ambalo halijafanikiwa, na kwa mwenendo wa Rais Magufuli inaonekana dhahiri shahiri kuwa mipango ya kumkwamisha haitafainikiwa maana wananchi wengi wamekuwa wakimuunga mkono.
Share:

TAHLISO Yatoa Tamko Kuhusu Wanafunzi Wanaotaka Mwigulu Ajiuzulu Kwa Kifo Cha Akwilina

TAARIFA KWA UMMA
Ndugu waandishi wahabari tunawashukuru sana kwa kukubali wito wetu wakuja kujumuika pamoja nasisi.
 
Leo tarehe 3/3/2018 tumekutana na viongozi wa vyuo vikuu nchi nzima kwa ajili yakujadili changamoto zinazotukabili.
 
Kikao hiki ni cha TAHLISO Baraza Kuu (SENATE) kina husisha Maraisi wa serikali za wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini.
 
Tunatambua kwamba kuna kifo cha mwanafunzi mwenzetu Akwilina Akwilini,mwanafunzi wa chuo cha NIT kilichotokea mwezi wa pili. Tunawashukuru wanafunzi wenzetu kwa utulivu mkubwa na mshikamano waliouonesha tangu msiba ulipotokea, wakati wa kipindi cha majonzi hadi kufikia sasa.
 
Tunamshukuru Mhe.Raisi wa Jamuhuri ya Muunganowa Tanzania kwa kuingilia kati suala hili na kuagiza uchunguzi ufanyike na hatua za kisheria zichukuliwe kwa wote watakaobainika kuhusika na kifo cha Akwilina Akwilini. 
 
Vilevile tunaishukuru Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ukaribu waliouonesha katika kipindi chote cha msiba.

Tunaomba wanafunzi waendelee kuwa watulivu wakati maagizo ya Mh. Raisi yakitekelezwa.
 
Aidha tunapenda jamiii tambue kuwa TAHLISO ndio chombo kikuu cha kuwasemea wanafunzi wote nchi nzima Tanzania na sio kikundi kingine chochote kile. 
 
Vipo vikundi vingi vimejitokeza na kutoa matamko mbalimbali baada ya kifo hiki kutokea, vikundi vingine vikaenda mbali Zaidi kwakuwataka baadhiya watendaji wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani kujiuzulu jambo ambalo linaashiria vikundi hivyo kuongozwa ama kutumika na makundi ya kisiasa, haiwezekani kutaka watendaji wa Serikali wajiuzulu wakati uchunguzi bado unafanyika na matokeo ya uchunguzi huo bado hayajatoka.

Jambo la kusikitisha Zaidi kuna baadhi ya vikundi vimejitangaza kwamba vinaungwa mkono na Maraisi wa Vyuo Vikuu jambo ambalo sio la kweli, Marais wote wa Vyuo Vikuu tuko hapa Dodoma tunaendelea na vikao vyetu vya kujadili changamoto zinazowakabili wanafunziwa Vyuo Vikuu.
 
Tunatoa wito kwa vikundi vyote vinavyojihusisha nakutumia mwamvuliwa Marais wa Vyuo Vikuu kama kinga yao ili kuu hadaa Umma kwamba wanaungwa Mkono, vikundi hivyo viache tabia hiyo vinginevyo tutawachukulia hatua za kinidhamu.
 
TAHLISO tunasubiri matokeo ya Uchunguzi unaofanyika juu ya kifo cha Akwilina na tunaimani wahusika wote watachukuliwa hatua kali zakisheria. 
 
Tunawaomba wanafunzi wote tuendelee kuwa watulivu wakati tukisubiri matokeo hayo na kujiepusha na maandamano na vitendo vyovyote vitakavyo sababisha uvunjifu wa Amani nakuleta mgawanyo miongoni mwa wanafunzi.
 
Hata hivyo namna bora yakufikisha hoja nikutumia njia ya majadiliano kama wasomi badala ya kutumia nguvu ama maandamano kwakutofuata taratibu na madhara yake ni kusababisha vuruguzi sizotakiwa na hatimaye kuhatarisha usalama na hivyo kuathiri jamii kwaujumla wake.
 
Vurugu zozote zitokanazo kwakutozingatia taratibu zinaweza kudhorotesha shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na Uchumiwa Taifa letu.
 
Vile vile zinapoteza mvuto kwawawekezaji wanje na wandani, ikiwemo shughuli za utalii nchini ambazo zinachangia pato la Taifa letu.
 
Athari za Vurugu na kukosekana kwa amani zipo wazi natunaziona kwa nchi nyingine zikiwemo baadhi ya nchi jirani zetu ambao wamekua wakimbizi nchini kwetu kila siku.
 
Tunaona kuwa kama wanataaluma tunajukumu kubwa la kuelimisha jamii na kuwamfano bora wakutumia njia za majadiliano katika kujenga hoja zetu ilizitatuliwe kuliko kutumia njia ya maandamano au vurugu zisizo na ulazimawowote.
 
Taasisi hii ndio yenye dhamana ya kutetea nakusimamia maslahi ya wanafunzi wote wa vyuo na vyuovikuu Tanzania na si vinginevyo.
………………………………….
GEORGE ALBERT MNALI
MWENYEKITI
TAHLISO
Share:

LINDI:::: Waziri Mkuu: Msiuze Ufuta Wenu Mashambani Pelekeni Minadani

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakulima wa ufuta katika mikoa inayolima zao hilo nchini kuuza kwa kutumia njia ya minada na si mashambani.

Ametoa agizo hilo  wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Nachihungo, Narungombe na Chikwale.

Waziri Mkuu ambaye yuko wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi amesema ili wakulima waweze kupata tija ni vema wakauza ufuta wao kwa kupitia minada kama inavyofanyika katika zao la korosho

“Usikubali kumuuzia mtu yeyote ufuta wako ukiwa shambani kwa sababu bei atakayonunulia ni ndogo kulinganisha na soko, naamini ufuta wote ukiuzwa  katika minada mtaona faida.”

Kufuatia agizo hilo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa, Bw. Andrea Chezue aandae utaratibu wa maeneo ya kukusanyia ufuta na kufanyia minada.

Amesema ufuta unaolimwa nchini ni bora na unapendwa sana duniani hivyo wasiwe na wasiwasi. Baadhi ya Mikoa inayolima ufuta kwa wingi ni Lindi, Pwani, Dodoma, Manyara, Kigoma na Singida.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema vijiji vote visivyokuwa na umeme nchini vikiwemo vya wilaya ya Ruangwa vitaunganishiwa katika REA awamu ya tatu.

Amesema wananchi waendelee kuwa na subira kwa sababu tayari mkandarasi ameshaanza kazi ya kuunganisha umeme katika vijiji vingine vya wilaya hiyo na  atafika kwenye maeneo yao.

Alibainisha kuwa mkakati wa Rais Dkt. John Magufuli ni kuhakikisha wananchi wote nchini waunganishiwa nishati ya umeme kwenye majumba yao, hivyo waendelee kuwa na subira na kushirikiana na Serikali yao.

Kuhusu suala la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama alisema, “Huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano, hivyo vijiji vyote vitapata maji”.

Pia alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kote nchini kutunza vyanzo vya maji ili kuliepusha taifa kugeuka jangwa pia miradi inayoletwa na Serikali iwe endelevu.

CHANZO: MPEKUZI BLOG
Share:

KISARAWE WAONGEZA MIKAKATI YA UFAULU SHULENI

Wilaya ya Kisarawe imedhamiria kuongeza kiwango cha ufaulu kwa
wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kwa kuweka mikakati kabambe
itakayowezesha wanafunzi kuwa mahiri katika masomo pamoja na mitihani.
Hayo yamebainishwa na Mbunge wa jimbo la Kisarawe Selemani Jafo
katika sherehe ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi wilayani Kisarawe iliyofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari ya minaki.

Katika sherehe  hiyo, Jafo ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, amewapongeza walimu wa wilaya hiyo kwa kuongeza ufaulu na kwamba inahitajika mikakati mingi zaidi ili wanafunzi wawe mahiri kwenye
mitihani.

Hata hivyo amesema hali ya baadhi ya shule za Kisarawe kuwa miongoni mwa shule kumi za mwisho katika mitihani kwasasa imetoweka.

Aidha Jafo ametoa maelekezo ya ununuzi wa mtambo mkubwa wa kudurufu
mitihani ili suala la uchapishaji wa mitihani ya shule za msingi na sekondari
usiwe tatizo tena.

Jambo hilo limeleta faraja kubwa kwa walimu waliokuwepo katika
sherehe hiyo kwani itawezesha kufanyika kwa mitihani ya kujipima kwa urahisi
wilayani humo.

Mtambo huo mpya unatarajiwa kununuliwa ndani ya wiki hii kwa kuwa fedha zimeshapatikana kutokana na michango kutoka kwa wadau mbalimbali wanao endelea kuchangia kampeni ya “Ondoa Zero Kisarawe” Kampeni hii imeonyesha kuzaa matunda kwani idadi ya wanafunzi waliopata daraja la sifuri imepungua kutoka wanafunzi 457 hadi 256.

Pia wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi daraja la nne wameongezeka na kufikia 163 wakati hapo awali walikuwa chini ya wanafunzi 50.



Share:

SHINYANGA : DC AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga amewataka maafisa watendaji wa vijiji na kata kusoma taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi pamoja na wenyeviti wa vitongoji,mitaa,vijiji na kata kufanya mikutano kwa ajili ya kutatua kero zinazowakabili wananchi.

Matiro ametoa agizo hilo leo Jumatatu Februari 26,2018 wakati wa mkutano wa kusikiliza kero za wananchi akiwa ameambatana na maafisa mbalimbali wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga katika kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.

Alitoa agizo hilo baada ya wananchi kudai kuwa viongozi waliopo katika kata hiyo hawafanyi mikutano kusikiliza kero za wananchi na badala yake wamekuwa wakisubiri uchaguzi ukikaribia ndiyo wanajitokeza.

Mmoja wa wananchi hao,Paul Kashinje (87) alisema viongozi wa eneo hilo hawawajibiki kwa wananchi matokeo yake wamekuwa wakikabiliwa na changamoto lukuki na kutoa tahadhari kuwa kipindi hiki wanataka vitendo zaidi kuliko maneno kwa viongozi hao na wasipobadilika watawashughulikia.

Kufuatia hoja hiyo na zingine,Matiro aliwaagiza viongozi wa vitongoji,vijiji,mitaa na kata kuhakikisha wafanya mikutano na wananchi ili kujadili namna ya kutatua kero zao huku akiagiza maafisa watendaji kusoma taarifa za mapato na matumizi ili kuondoa migongano isiyokuwa ya lazima.

Katika hatua nyingine Matiro alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kujenga nyumba bora badala ya kuishi kwenye nyumba za udongo ambazo ni rahisi kubomoka inaponyesha hata mvua kidogo tu.

Matiro pia aliwataka wananchi kutunza mazingira kwa kupanda miti na kuitunza na kulima zao la mtama badala ya kulima mahindi ambayo ustawi wake siyo mzuri mkoani Shinyanga.

Wakizungumza mbele ya mkuu wa wilaya,wananchi walizitaja baadhi ya kero zao kuwa ni kukosekana kwa eneo la mazishi “makaburi”,ukosefu wa shule,barabara,zahanati,maji,umeme na migogoro ya viwanja.
Share:

DAR ES SALAAM: AWESO AAGIZA WAKANDARASI WANAOTEKELEZA MIRADI YA MAJI VIZURI WALIPWE KWA WAKATI

4Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso ameagiza wakandarasi wote wanaotekeleza vizuri miradi ya maji nchini walipwe fedha zao kwa wakati, bila kucheleweshwa wanapoleta hati zao za madai, wakati alipokua akikagua utekelezaji wa miradi ya maji katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Aweso alisema pamoja na madai yao kulipwa kwa wakati, pia wakandarasi hao wapewe miradi mingine zaidi kama mfano kwa wakandarasi wengine, kwani nia ya Serikali ni miradi iishe kwa wakati na kufanya kazi na wakandarasi wenye uzalendo.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri Aweso alitembelea miradi ya maji ya Hondogo, Kibamba, King’azi A na mradi wa kuchakata majitaka wa DEWAT uliopo Mburahati, unaofadhiliwa na Taasisi ya Kijerumani ya BORDA akiambatana na wataalam kutoka DAWASA na DAWASCO.

Manispaa ya Ubungo imetengewa zaidi milioni 653 kwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji, asilimia 60 ya fedha hizo zikiwa ni mapato yake ya ndani.


Share:

DAR ES SALAAM: KAMANDA MAMBOSASA "OLE WAO WATAKAOFANYA MAANDAMANO"

BOKAMANDA wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amesema ni marufuku kwa mwanachi yoyote kushiriki kwenye maandamano kwani hawapo tayari kuona watu wakiandamana na kusababisa uvunjifu wa amani iliyopo.

Mambosasa ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia mambo mbalimbali na ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa wananchi kutojihusisha na maandamano.

Amefafanua kwenye mitandao ya kijamii kuna baadhi ya watu wanaitumia vibaya na sasa wameanza kuhamasisha maandamano kwa kupanga tarehe ambayo itakuwa Aprili 26 mwaka huu.

“Kwenye mitandao ya kijamii tumeona watu wanahamasisha maandamano.Tunawaambia Polisi hatutakaa kimya na wale ambao wataandamana kitakachotokea wasitulaumu.

“Polisi tumejipanga kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wanakuwa salama na wanafurahia hali ya ulitulivu iliyopo.Wale ambao wanataka kufanya maandano wahesabu hawana bahati na ndio maana tunaomba wananchi wasishiriki kwenye maandamano ambayo yameanza kuhamasishwa kupitia mitandao ya kijamii,”amesema Mambosasa.

Amefafanua Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linataka kuona wananchi wakiendelea na shughuli zao za kimaendeleo na wachache wenye kutaka kuvuruga amani iliyopo haitawavumilia.
CHANZO: FULL SHANGWE

Share:

DAR ES SALAAM: Wanasheria zaidi ya 100 wameanza kupitia na kuchambua malalamiko mbalimbali ya wananchi

IMG_1871WANASHERIA zaidi ya 100 wameanza kupitia na kuchambua  malalamiko mbalimbali ya wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa  lengo la kuhakikisha yanapatiwa majibu.

Hatua hiyo inatokana na wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kufika  kwa Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda na kisha kutoa malalamiko  kuhusu mambo mbalimbali.

Kutokana na malalamiko hayo Makonda aliaahidi kuyashughulikia  na sasa timu hiyo ya wataalamu wa masuala ya sheria wameanza jukumu la kupitia malalamiko ya wananchi hao na kisha kutafuta ufumbuzi wake wa kisheria.

Akizungumza leo, Mwanasheria wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Fabiola Mwingira amesema wanasheria hao wameanza kufanya uchambuzi wa malalamiko hayo na baada ya hapo wataanza  kuyasikiliza kwa kukutanisha pande zote mbili kwa maana ya mtoa malalamiko na anayelalamikiwa.

“Wanasheria hao wameanza kufanya uchambuzi wa malalamiko ya  wananchi kuanzia leo hadi Machi 9 mwaka huu na lengo  kila mwananchi aliyepeleka malalamiko yake basi yapate  ufumbuzi.

“Malalamiko wanayoyashughulikia ni yale ambayo hayako  mahakamani na yaliyo mahakamani basi yatabaki  huko huko yapatiwe ufumbuzi na tayari wamewaandikia barua wahusika,’amesema Mwingira.

Amefafanua baada ya wanashera hao kumaliza kusikiliza  malalamiko hayo, watatoa ushauri wa kisheria ambao utamuwezesha  sasa Mkuu wa Mkoa kutoa uamuzi.

Pia amesema utoaji majibu ya kero za wananchi hao awamu ya pili ,majina yatabandika kwenye geti la ofisi ya Mkuu wa Mkoa ,hivyo wananchi watatangaziwa siku na saa.


Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>