MTWARA: SERIKALI IMESEMA HAIJARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA BARABARA YA MTWARA MNIVATA
Waziri wa
Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Mh MAKAME MBALAWA amepozungumza na Wananchi wa
Kata ya Naliendele Jana Tarehe 4/3/2018 na kumtaka Mkandarasi anaejenga
Barabara hiyo kwa kiwango cha Lami kuharakisha ujenzi huo.
Waziri MBALAWA mesema"Haturidhishwi na kasi ya Ujenzi wa barabara hii yenye
Urefu wa Km 50 Kutoka Mtwara hadi Kijiji cha Mnivata kwa Thamani ya Tsh Bilioni
89.59 na ndio maana tunatembelea
mara kwa mara kumsukuma Mkandarasi huyu afanye kwa kasi tunayoitaka"
Akijibu maswali ya baadhi ya Wananchi waliouliza kuhusu Swala la
wenyeji kukosa Ajira ndogondogo na kupewa watu wa Mikoa mingine pamoja na
kukosa miundombinu itakayosaidia maji yasituwame katika eneo moja, Waziri huyo
amesema atayafanyia kazi kama Serikali.
Waziri Mbalawa aliongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara MH EVOD
MMANDA ambae nae alipata nafasi ya kuzungumza na Wananchi hao na kuwasihi
waendelee kushirikiana na Mkandarasi huyo ili barabara hiyo iweze kukamilika
kwa haraka.
Karim Faida-JAMII FM.
MTWARA: VIWANDA VYA UBANGUAJI LAZIMA WAPATE KOROSHO GHAFI
Waziri wa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji
CHARLES MWIJAGE amevihakikishia Viwanda
vya Ubanguaji Korosho MTWARA vinapata malighafi hiyo mwaka mzima kuliko ilivyo
hivi sasa ambapo zaidi ya tani laki tatu za korosho ghafi zimesafirishwa nje ya
Nchi huku Viwanda hivyo vikifungwa kwa kukosa malighafi hiyo.
MWIJANGE
amesema hayo baada ya kutembelea Shirika linalohudumia viwanda vidogo vidogo
SIDO Mkoani hapa na kukuta kiwanda kinachotumiwa na wanawake
kubangua korosho kimefungwa kutokana na kukosa Korosho ghafI
Hata hivyo Waziri MWIJAGE amesema hilo
haliwezi kukubalika lazima utaratibu ufanyike ili sehemu ya Korosho
ghafi ibaki Nchini kulinda viwanda hivyo,
Akiwa mkoani MTWARA waziri
huyo amewakabidhi SUMA JKT kazi ya ujenzi wa Kiwanda cha
wajasiriamali kitakachojengwa katika ofisi za SIDO MTWARA,
Mwakilishi wa SUMA JKT Meja ATUPELE MWAMFUPE ambae ni Meneja wa Kanda ya Kusini
amesema watahakikisha watafanya kazi ndani ya muda miezi mitatu kazi itakuwa
imekamilika.
Maeneo mengine aliyotembelea na kituo cha
uwekezaji , Kiwanda cha kubangua korosho cha Cash nut pamoja na kiwanda cha
kuzalisha Cementi cha DANGOTE, na MTWARA CEMENT.
GREGORY MILLANZI- JAMII FM
DAR ES SALAAM: JOSEPH BUTIKU: UVCCM MLINDENI RAIS MAGUFULI
Mzee Butiku ameyasema hayo leo Jumapili Machi 4, 2018, jijini Dar es Salaam, alipokuwa akiwasilisha mada ya Uzalendo na Historia ya Taifa letu kwa Viongozi, ikiwa ni sehemu ya mafunzo maalumu ya uongozi kwaajili ya vijana wa umoja huo kwa ngazi ya kata, wilaya na mkoa inayoendelea jijini Dar es Salaam.
“Uamuzi wa Rais Magufuli wa kuhakikisha rasilimali za taifa letu haziendelei kunyonywa na wezi wa ndani na nje umemletea maadui wengi sana na nyinyi vijana mnayo dhamana kubwa ya kuhakikisha mnamlinda Rais wetu kufa na kupona” amesema Butiku.
Toka Rais Magufuli aingie madarakani na kuanza kusimamia rasilimali za nchi ili ziwanufaishe watanzania wote hasa maskini, kumekuwepo na vilio kutoka kwa wale ambao walikuwa wakinufaika na rasilimali hizo, huku wakifanya kila njia kuhakikisha wanakwamisha juhudi zake, jambo ambalo halijafanikiwa, na kwa mwenendo wa Rais Magufuli inaonekana dhahiri shahiri kuwa mipango ya kumkwamisha haitafainikiwa maana wananchi wengi wamekuwa wakimuunga mkono.
TAHLISO Yatoa Tamko Kuhusu Wanafunzi Wanaotaka Mwigulu Ajiuzulu Kwa Kifo Cha Akwilina
Ndugu waandishi wahabari tunawashukuru sana kwa kukubali wito wetu wakuja kujumuika pamoja nasisi.
Leo tarehe 3/3/2018 tumekutana na viongozi wa vyuo vikuu nchi nzima kwa ajili yakujadili changamoto zinazotukabili.
Kikao hiki ni cha TAHLISO Baraza Kuu (SENATE) kina husisha Maraisi wa serikali za wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini.
Tunatambua kwamba kuna kifo cha mwanafunzi mwenzetu Akwilina Akwilini,mwanafunzi wa chuo cha NIT kilichotokea mwezi wa pili. Tunawashukuru wanafunzi wenzetu kwa utulivu mkubwa na mshikamano waliouonesha tangu msiba ulipotokea, wakati wa kipindi cha majonzi hadi kufikia sasa.
Tunamshukuru Mhe.Raisi wa Jamuhuri ya Muunganowa Tanzania kwa kuingilia kati suala hili na kuagiza uchunguzi ufanyike na hatua za kisheria zichukuliwe kwa wote watakaobainika kuhusika na kifo cha Akwilina Akwilini.
Vilevile tunaishukuru Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ukaribu waliouonesha katika kipindi chote cha msiba.
Tunaomba wanafunzi waendelee kuwa watulivu wakati maagizo ya Mh. Raisi yakitekelezwa.
Aidha tunapenda jamiii tambue kuwa TAHLISO ndio chombo kikuu cha kuwasemea wanafunzi wote nchi nzima Tanzania na sio kikundi kingine chochote kile.
Vipo vikundi vingi vimejitokeza na kutoa matamko mbalimbali baada ya kifo hiki kutokea, vikundi vingine vikaenda mbali Zaidi kwakuwataka baadhiya watendaji wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani kujiuzulu jambo ambalo linaashiria vikundi hivyo kuongozwa ama kutumika na makundi ya kisiasa, haiwezekani kutaka watendaji wa Serikali wajiuzulu wakati uchunguzi bado unafanyika na matokeo ya uchunguzi huo bado hayajatoka.
Jambo la kusikitisha Zaidi kuna baadhi ya vikundi vimejitangaza kwamba vinaungwa mkono na Maraisi wa Vyuo Vikuu jambo ambalo sio la kweli, Marais wote wa Vyuo Vikuu tuko hapa Dodoma tunaendelea na vikao vyetu vya kujadili changamoto zinazowakabili wanafunziwa Vyuo Vikuu.
Tunatoa wito kwa vikundi vyote vinavyojihusisha nakutumia mwamvuliwa Marais wa Vyuo Vikuu kama kinga yao ili kuu hadaa Umma kwamba wanaungwa Mkono, vikundi hivyo viache tabia hiyo vinginevyo tutawachukulia hatua za kinidhamu.
TAHLISO tunasubiri matokeo ya Uchunguzi unaofanyika juu ya kifo cha Akwilina na tunaimani wahusika wote watachukuliwa hatua kali zakisheria.
Tunawaomba wanafunzi wote tuendelee kuwa watulivu wakati tukisubiri matokeo hayo na kujiepusha na maandamano na vitendo vyovyote vitakavyo sababisha uvunjifu wa Amani nakuleta mgawanyo miongoni mwa wanafunzi.
Hata hivyo namna bora yakufikisha hoja nikutumia njia ya majadiliano kama wasomi badala ya kutumia nguvu ama maandamano kwakutofuata taratibu na madhara yake ni kusababisha vuruguzi sizotakiwa na hatimaye kuhatarisha usalama na hivyo kuathiri jamii kwaujumla wake.
Vurugu zozote zitokanazo kwakutozingatia taratibu zinaweza kudhorotesha shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na Uchumiwa Taifa letu.
Vile vile zinapoteza mvuto kwawawekezaji wanje na wandani, ikiwemo shughuli za utalii nchini ambazo zinachangia pato la Taifa letu.
Athari za Vurugu na kukosekana kwa amani zipo wazi natunaziona kwa nchi nyingine zikiwemo baadhi ya nchi jirani zetu ambao wamekua wakimbizi nchini kwetu kila siku.
Tunaona kuwa kama wanataaluma tunajukumu kubwa la kuelimisha jamii na kuwamfano bora wakutumia njia za majadiliano katika kujenga hoja zetu ilizitatuliwe kuliko kutumia njia ya maandamano au vurugu zisizo na ulazimawowote.
Taasisi hii ndio yenye dhamana ya kutetea nakusimamia maslahi ya wanafunzi wote wa vyuo na vyuovikuu Tanzania na si vinginevyo.
………………………………….
GEORGE ALBERT MNALI
MWENYEKITI
TAHLISO
LINDI:::: Waziri Mkuu: Msiuze Ufuta Wenu Mashambani Pelekeni Minadani
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakulima wa ufuta katika mikoa inayolima zao hilo nchini kuuza kwa kutumia njia ya minada na si mashambani.
Ametoa agizo hilo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Nachihungo, Narungombe na Chikwale.
Waziri Mkuu ambaye yuko wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi amesema ili wakulima waweze kupata tija ni vema wakauza ufuta wao kwa kupitia minada kama inavyofanyika katika zao la korosho
“Usikubali kumuuzia mtu yeyote ufuta wako ukiwa shambani kwa sababu bei atakayonunulia ni ndogo kulinganisha na soko, naamini ufuta wote ukiuzwa katika minada mtaona faida.”
Kufuatia agizo hilo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa, Bw. Andrea Chezue aandae utaratibu wa maeneo ya kukusanyia ufuta na kufanyia minada.
Amesema ufuta unaolimwa nchini ni bora na unapendwa sana duniani hivyo wasiwe na wasiwasi. Baadhi ya Mikoa inayolima ufuta kwa wingi ni Lindi, Pwani, Dodoma, Manyara, Kigoma na Singida.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema vijiji vote visivyokuwa na umeme nchini vikiwemo vya wilaya ya Ruangwa vitaunganishiwa katika REA awamu ya tatu.
Amesema wananchi waendelee kuwa na subira kwa sababu tayari mkandarasi ameshaanza kazi ya kuunganisha umeme katika vijiji vingine vya wilaya hiyo na atafika kwenye maeneo yao.
Alibainisha kuwa mkakati wa Rais Dkt. John Magufuli ni kuhakikisha wananchi wote nchini waunganishiwa nishati ya umeme kwenye majumba yao, hivyo waendelee kuwa na subira na kushirikiana na Serikali yao.
Kuhusu suala la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama alisema, “Huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano, hivyo vijiji vyote vitapata maji”.
Pia alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kote nchini kutunza vyanzo vya maji ili kuliepusha taifa kugeuka jangwa pia miradi inayoletwa na Serikali iwe endelevu.
CHANZO: MPEKUZI BLOG
KISARAWE WAONGEZA MIKAKATI YA UFAULU SHULENI
Wilaya ya Kisarawe imedhamiria
kuongeza kiwango cha ufaulu kwawanafunzi wa shule za msingi na sekondari kwa kuweka mikakati kabambe
itakayowezesha wanafunzi kuwa mahiri katika masomo pamoja na mitihani.
Hayo yamebainishwa na Mbunge wa
jimbo la Kisarawe Selemani Jafo
katika sherehe ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi wilayani Kisarawe iliyofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari ya minaki.
katika sherehe ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi wilayani Kisarawe iliyofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari ya minaki.
Katika sherehe hiyo, Jafo
ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, amewapongeza walimu wa wilaya
hiyo kwa kuongeza ufaulu na kwamba inahitajika mikakati mingi zaidi ili
wanafunzi wawe mahiri kwenye
mitihani.
mitihani.
Hata hivyo amesema hali ya baadhi
ya shule za Kisarawe kuwa miongoni mwa shule kumi za mwisho katika mitihani
kwasasa imetoweka.
Aidha Jafo ametoa maelekezo ya
ununuzi wa mtambo mkubwa wa kudurufu
mitihani ili suala la uchapishaji wa mitihani ya shule za msingi na sekondari
usiwe tatizo tena.
mitihani ili suala la uchapishaji wa mitihani ya shule za msingi na sekondari
usiwe tatizo tena.
Jambo hilo limeleta faraja
kubwa kwa walimu waliokuwepo katika
sherehe hiyo kwani itawezesha kufanyika kwa mitihani ya kujipima kwa urahisi
wilayani humo.
sherehe hiyo kwani itawezesha kufanyika kwa mitihani ya kujipima kwa urahisi
wilayani humo.
Mtambo huo mpya unatarajiwa kununuliwa
ndani ya wiki hii kwa kuwa fedha zimeshapatikana kutokana na michango kutoka
kwa wadau mbalimbali wanao endelea kuchangia kampeni ya “Ondoa Zero Kisarawe” Kampeni hii imeonyesha kuzaa matunda kwani idadi ya wanafunzi waliopata
daraja la sifuri imepungua kutoka wanafunzi 457 hadi 256.
Pia wanafunzi waliopata daraja
la kwanza hadi daraja la nne wameongezeka na kufikia 163 wakati hapo awali
walikuwa chini ya wanafunzi 50.
SHINYANGA : DC AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE
Matiro ametoa agizo hilo leo Jumatatu Februari 26,2018 wakati wa mkutano wa kusikiliza kero za wananchi akiwa ameambatana na maafisa mbalimbali wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga katika kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.
Alitoa agizo hilo baada ya wananchi kudai kuwa viongozi waliopo katika kata hiyo hawafanyi mikutano kusikiliza kero za wananchi na badala yake wamekuwa wakisubiri uchaguzi ukikaribia ndiyo wanajitokeza.
Mmoja wa wananchi hao,Paul Kashinje (87) alisema viongozi wa eneo hilo hawawajibiki kwa wananchi matokeo yake wamekuwa wakikabiliwa na changamoto lukuki na kutoa tahadhari kuwa kipindi hiki wanataka vitendo zaidi kuliko maneno kwa viongozi hao na wasipobadilika watawashughulikia.
Kufuatia hoja hiyo na zingine,Matiro aliwaagiza viongozi wa vitongoji,vijiji,mitaa na kata kuhakikisha wafanya mikutano na wananchi ili kujadili namna ya kutatua kero zao huku akiagiza maafisa watendaji kusoma taarifa za mapato na matumizi ili kuondoa migongano isiyokuwa ya lazima.
Katika hatua nyingine Matiro alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kujenga nyumba bora badala ya kuishi kwenye nyumba za udongo ambazo ni rahisi kubomoka inaponyesha hata mvua kidogo tu.
Matiro pia aliwataka wananchi kutunza mazingira kwa kupanda miti na kuitunza na kulima zao la mtama badala ya kulima mahindi ambayo ustawi wake siyo mzuri mkoani Shinyanga.
Wakizungumza mbele ya mkuu wa wilaya,wananchi walizitaja baadhi ya kero zao kuwa ni kukosekana kwa eneo la mazishi “makaburi”,ukosefu wa shule,barabara,zahanati,maji,umeme na migogoro ya viwanja.
DAR ES SALAAM: AWESO AAGIZA WAKANDARASI WANAOTEKELEZA MIRADI YA MAJI VIZURI WALIPWE KWA WAKATI
Naibu Waziri Aweso
alisema pamoja na madai yao kulipwa kwa wakati, pia wakandarasi hao wapewe
miradi mingine zaidi kama mfano kwa wakandarasi wengine, kwani nia ya Serikali
ni miradi iishe kwa wakati na kufanya kazi na wakandarasi wenye uzalendo.
Katika ziara hiyo
Naibu Waziri Aweso alitembelea miradi ya maji ya Hondogo, Kibamba, King’azi A
na mradi wa kuchakata majitaka wa DEWAT uliopo Mburahati, unaofadhiliwa na
Taasisi ya Kijerumani ya BORDA akiambatana na wataalam kutoka DAWASA na
DAWASCO.
Manispaa ya Ubungo
imetengewa zaidi milioni 653 kwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa
miradi ya maji, asilimia 60 ya fedha hizo zikiwa ni mapato yake ya ndani.
DAR ES SALAAM: KAMANDA MAMBOSASA "OLE WAO WATAKAOFANYA MAANDAMANO"
Mambosasa
ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia mambo mbalimbali
na ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa wananchi kutojihusisha na maandamano.
Amefafanua
kwenye mitandao ya kijamii kuna baadhi ya watu wanaitumia vibaya na sasa
wameanza kuhamasisha maandamano kwa kupanga tarehe ambayo itakuwa Aprili 26
mwaka huu.
“Kwenye
mitandao ya kijamii tumeona watu wanahamasisha maandamano.Tunawaambia Polisi
hatutakaa kimya na wale ambao wataandamana kitakachotokea wasitulaumu.
“Polisi
tumejipanga kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wanakuwa salama na wanafurahia
hali ya ulitulivu iliyopo.Wale ambao wanataka kufanya maandano wahesabu hawana
bahati na ndio maana tunaomba wananchi wasishiriki kwenye maandamano ambayo
yameanza kuhamasishwa kupitia mitandao ya kijamii,”amesema Mambosasa.
Amefafanua
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linataka kuona wananchi
wakiendelea na shughuli zao za kimaendeleo na wachache wenye kutaka kuvuruga
amani iliyopo haitawavumilia.
CHANZO: FULL SHANGWEDAR ES SALAAM: Wanasheria zaidi ya 100 wameanza kupitia na kuchambua malalamiko mbalimbali ya wananchi
Hatua
hiyo inatokana na wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kufika kwa Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda na kisha kutoa malalamiko
kuhusu mambo
mbalimbali.
Kutokana
na malalamiko hayo Makonda aliaahidi kuyashughulikia na sasa timu hiyo ya wataalamu wa masuala ya sheria wameanza jukumu la
kupitia malalamiko ya wananchi hao na kisha kutafuta ufumbuzi wake wa kisheria.
Akizungumza
leo, Mwanasheria wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Fabiola Mwingira
amesema wanasheria hao wameanza kufanya uchambuzi wa malalamiko hayo na baada
ya hapo wataanza
kuyasikiliza kwa
kukutanisha pande zote mbili kwa maana ya mtoa malalamiko na anayelalamikiwa.
“Wanasheria
hao wameanza kufanya uchambuzi wa malalamiko ya wananchi kuanzia leo hadi Machi 9 mwaka huu na lengo
kila mwananchi
aliyepeleka malalamiko yake basi yapate ufumbuzi.
“Malalamiko
wanayoyashughulikia ni yale ambayo hayako mahakamani na yaliyo mahakamani basi yatabaki huko huko yapatiwe
ufumbuzi na tayari wamewaandikia barua wahusika,’amesema Mwingira.
Amefafanua
baada ya wanashera hao kumaliza kusikiliza malalamiko hayo, watatoa ushauri wa kisheria ambao utamuwezesha
sasa Mkuu wa Mkoa
kutoa uamuzi.
Pia
amesema utoaji majibu ya kero za wananchi hao awamu ya pili ,majina yatabandika
kwenye geti la ofisi ya Mkuu wa Mkoa ,hivyo wananchi watatangaziwa siku na saa.













