• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

SHINYANGA : DC AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga amewataka maafisa watendaji wa vijiji na kata kusoma taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi pamoja na wenyeviti wa vitongoji,mitaa,vijiji na kata kufanya mikutano kwa ajili ya kutatua kero zinazowakabili wananchi.

Matiro ametoa agizo hilo leo Jumatatu Februari 26,2018 wakati wa mkutano wa kusikiliza kero za wananchi akiwa ameambatana na maafisa mbalimbali wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga katika kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.

Alitoa agizo hilo baada ya wananchi kudai kuwa viongozi waliopo katika kata hiyo hawafanyi mikutano kusikiliza kero za wananchi na badala yake wamekuwa wakisubiri uchaguzi ukikaribia ndiyo wanajitokeza.

Mmoja wa wananchi hao,Paul Kashinje (87) alisema viongozi wa eneo hilo hawawajibiki kwa wananchi matokeo yake wamekuwa wakikabiliwa na changamoto lukuki na kutoa tahadhari kuwa kipindi hiki wanataka vitendo zaidi kuliko maneno kwa viongozi hao na wasipobadilika watawashughulikia.

Kufuatia hoja hiyo na zingine,Matiro aliwaagiza viongozi wa vitongoji,vijiji,mitaa na kata kuhakikisha wafanya mikutano na wananchi ili kujadili namna ya kutatua kero zao huku akiagiza maafisa watendaji kusoma taarifa za mapato na matumizi ili kuondoa migongano isiyokuwa ya lazima.

Katika hatua nyingine Matiro alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kujenga nyumba bora badala ya kuishi kwenye nyumba za udongo ambazo ni rahisi kubomoka inaponyesha hata mvua kidogo tu.

Matiro pia aliwataka wananchi kutunza mazingira kwa kupanda miti na kuitunza na kulima zao la mtama badala ya kulima mahindi ambayo ustawi wake siyo mzuri mkoani Shinyanga.

Wakizungumza mbele ya mkuu wa wilaya,wananchi walizitaja baadhi ya kero zao kuwa ni kukosekana kwa eneo la mazishi “makaburi”,ukosefu wa shule,barabara,zahanati,maji,umeme na migogoro ya viwanja.
Share:

DAR ES SALAAM: AWESO AAGIZA WAKANDARASI WANAOTEKELEZA MIRADI YA MAJI VIZURI WALIPWE KWA WAKATI

4Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso ameagiza wakandarasi wote wanaotekeleza vizuri miradi ya maji nchini walipwe fedha zao kwa wakati, bila kucheleweshwa wanapoleta hati zao za madai, wakati alipokua akikagua utekelezaji wa miradi ya maji katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Aweso alisema pamoja na madai yao kulipwa kwa wakati, pia wakandarasi hao wapewe miradi mingine zaidi kama mfano kwa wakandarasi wengine, kwani nia ya Serikali ni miradi iishe kwa wakati na kufanya kazi na wakandarasi wenye uzalendo.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri Aweso alitembelea miradi ya maji ya Hondogo, Kibamba, King’azi A na mradi wa kuchakata majitaka wa DEWAT uliopo Mburahati, unaofadhiliwa na Taasisi ya Kijerumani ya BORDA akiambatana na wataalam kutoka DAWASA na DAWASCO.

Manispaa ya Ubungo imetengewa zaidi milioni 653 kwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji, asilimia 60 ya fedha hizo zikiwa ni mapato yake ya ndani.


Share:

DAR ES SALAAM: KAMANDA MAMBOSASA "OLE WAO WATAKAOFANYA MAANDAMANO"

BOKAMANDA wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amesema ni marufuku kwa mwanachi yoyote kushiriki kwenye maandamano kwani hawapo tayari kuona watu wakiandamana na kusababisa uvunjifu wa amani iliyopo.

Mambosasa ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia mambo mbalimbali na ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa wananchi kutojihusisha na maandamano.

Amefafanua kwenye mitandao ya kijamii kuna baadhi ya watu wanaitumia vibaya na sasa wameanza kuhamasisha maandamano kwa kupanga tarehe ambayo itakuwa Aprili 26 mwaka huu.

“Kwenye mitandao ya kijamii tumeona watu wanahamasisha maandamano.Tunawaambia Polisi hatutakaa kimya na wale ambao wataandamana kitakachotokea wasitulaumu.

“Polisi tumejipanga kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wanakuwa salama na wanafurahia hali ya ulitulivu iliyopo.Wale ambao wanataka kufanya maandano wahesabu hawana bahati na ndio maana tunaomba wananchi wasishiriki kwenye maandamano ambayo yameanza kuhamasishwa kupitia mitandao ya kijamii,”amesema Mambosasa.

Amefafanua Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linataka kuona wananchi wakiendelea na shughuli zao za kimaendeleo na wachache wenye kutaka kuvuruga amani iliyopo haitawavumilia.
CHANZO: FULL SHANGWE

Share:

DAR ES SALAAM: Wanasheria zaidi ya 100 wameanza kupitia na kuchambua malalamiko mbalimbali ya wananchi

IMG_1871WANASHERIA zaidi ya 100 wameanza kupitia na kuchambua  malalamiko mbalimbali ya wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa  lengo la kuhakikisha yanapatiwa majibu.

Hatua hiyo inatokana na wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kufika  kwa Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda na kisha kutoa malalamiko  kuhusu mambo mbalimbali.

Kutokana na malalamiko hayo Makonda aliaahidi kuyashughulikia  na sasa timu hiyo ya wataalamu wa masuala ya sheria wameanza jukumu la kupitia malalamiko ya wananchi hao na kisha kutafuta ufumbuzi wake wa kisheria.

Akizungumza leo, Mwanasheria wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Fabiola Mwingira amesema wanasheria hao wameanza kufanya uchambuzi wa malalamiko hayo na baada ya hapo wataanza  kuyasikiliza kwa kukutanisha pande zote mbili kwa maana ya mtoa malalamiko na anayelalamikiwa.

“Wanasheria hao wameanza kufanya uchambuzi wa malalamiko ya  wananchi kuanzia leo hadi Machi 9 mwaka huu na lengo  kila mwananchi aliyepeleka malalamiko yake basi yapate  ufumbuzi.

“Malalamiko wanayoyashughulikia ni yale ambayo hayako  mahakamani na yaliyo mahakamani basi yatabaki  huko huko yapatiwe ufumbuzi na tayari wamewaandikia barua wahusika,’amesema Mwingira.

Amefafanua baada ya wanashera hao kumaliza kusikiliza  malalamiko hayo, watatoa ushauri wa kisheria ambao utamuwezesha  sasa Mkuu wa Mkoa kutoa uamuzi.

Pia amesema utoaji majibu ya kero za wananchi hao awamu ya pili ,majina yatabandika kwenye geti la ofisi ya Mkuu wa Mkoa ,hivyo wananchi watatangaziwa siku na saa.


Share:

MTWARA: (HABARI PICHA) Wazri Mkuu Kassim Majaliwa azindua kituo cha afya Chiwale

PMO_0269
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi wa jengo la wazazi katika kituo cha afya Chiwale, Wilayani Masasi, akiwa ameanza ziara yake ya kikazi ya siku tatu, Mkoani Mtwara  Februari 26, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_0271
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe  wakati akiweka jiwe la msingi katika kituo cha afya Chiwale, akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku tatu, Mkoani Mtwara  Februari 26, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_0286
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua wodi ya wazazi katika kituo cha afya Chiwale, mara baada ya kuweka jiwe la msingi kituoni hapo, akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku tatu, Mkoani Mtwara  Februari 26, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_0320
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongea na wananchi wa Chiwale, Wilayani Masasi, mara baada ya kuweka jiwe la msingi la jengo la wazazi katika kituo cha afya Chiwale. Februari 26, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Share:

DAR ES SALAAM: Wema Sepetu Alinambia anavuta Bangi kwa starehe

Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu imeendelea na kesi inayomkabili muigizaji Wema Sepetu ambapo Ofisa wa Polisi WP Mary ameieleza mahakama kuwa mnamo Februari 4, 2017 Wema alimwambia anatumia bangi kwa ajili ya starehe na si kuuza

WP Marry ambaye ni shahidi wa tatu ameyaeleza hayo wakati akiongozwa na Wakili wa serikali Costantine Kakula, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.

WP Marry amedai kuwa Wema alimueleza maneno hayo wakati walipokuwa njiani kuelekea nyumbani kwake kumkagua.

Amedai kuwa February 4, 2017 aliagizwa kumtoa Wema Mahabusu na kwenda kumfanyia upekuzi nyumbani kwake akiwa na OC CID na Maofisa wengine wa Polisi.

Amedai kuwa wakiwa wanajiandaa kuondoka Central Polisi kuelekea kwa Wema Bunju Basihaya, wakiwa kwenye gari kuelekea huko alimuuliza Wema kuhusu tuhuma zinazomkabili kwamba anahusika na biashara ya Dawa za kulevya au kutumia.

Amedai kuwa Wema alijibu “Sijishughulishi na kuuza ila natumia bangi kama starehe”.

WP Marry amedai kuwa baada ya kumuuliza Wema alimwambia mara yake ya mwisho kuvuta Bangi ilikuwa Jumatatu ambapo swali hilo aliulizwa February 4,2017.

Alieleza kuwa walipofika nyumbani kwa Wema waligonga geti na kufunguliwa na mdada wa kazi ambapo walivyoingia ndani walikuta kuna mdada mwingine wa kazi.

WP Marry amedai kuwa kabla ya kuingia ndani Wema aliomba kumpigia simu dada yake ili awepo wakati wa kufanya ukaguzi ambapo dada yake alifika na kujitambulisha kwa jina la Nuru Sepetu.

WP Marry ameeleza kuwa wakati Wema anampigia simu dada yake alitoka dada mmoja wa kazi kumfuata mjumbe ambapo alikuja naye na kujitambulisha kwa jina la Steven Ndaho.

Amedai baada ya dada yake Wema kufika alitaka kuwapekua kabla ya kuingia ndani ambapo Nuru aliwapekuwa wote kabla ya kuingia ndani.

Amedai baada ya kumaliza upekuzi walirudi Central polis, February 8,2017 saa nne asubuhi alipewa maelekezo na Inspekta Wille kwamba aende na Wema kwa Mkemia Mkuu wa serikali kwa ajili ya kuchukuliwa sampuli ya mkojo.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi March 12 na 13, 2018 kwaajili ya kuendelea na ushahidi.
Share:

MBEYA: Mawakilii wa Sugu Wajipanga Kukata Rufaa

Baada ya mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga kuhukumiwa kifungo cha miezi mitano jela, wakili wao Peter Kibatala amesema wanakusudia kukata rufaa.

Sugu na Masonga wamehukumiwa adhabu hiyo leo Februari 26,2018 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Michael Mteite.

Wawili hao wamehukumiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli, kosa walilotenda kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 30,2017 eneo la Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Kibatala amesema baadaye watatoa taarifa ya nini kinaendelea ila wanakusudia kukata rufaa.

Baada ya hukumu kutolewa viongozi wa Chadema waliokuwepo mahakamani waliingia kwenye magari yao na kuelekea katika ofisi za chama hicho Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Wakati wa usomwaji wa hukumu hiyo, nje ya jengo la mahakama ulinzi uliimarishwa kukiwa na askari waliotanda hadi maeneo ya jirani.

Sugu ni mbunge aliyeweka rekodi ya kupata kura nyingi kuwashinda wabunge wote wa majimbo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Katika uchaguzi huo, Sugu alipata kura 108,566 akiwaacha wapinzani wake kugawana kura 57,690.

Hukumu imetolewa na hakimu Mteite aliyesikiliza shauri hilo baada ya upande wa mashtaka na wa utetezi kukamilisha ushahidi Februari 9,2018.

Jamhuri iliwasilisha mashahidi watano na kielelezo kimoja cha sauti iliyodaiwa kurekodiwa na shahidi wa tano, Inspekta Joram Magova.

Upande wa utetezi uliwasilisha mashahidi sita wakiwamo Sugu na Masonga waliokana kutamka maneno waliyoshtakiwa kuyatoa.

Washtakiwa walitetewa na mawakili Sabina Yongo, Boniface Mwabukusi na Hekima Mwasipu kabla ya kujitoa na kazi hiyo kufanywa na Kibatala.

Kwa mara ya kwanza, Sugu na Masonga  walifikishwa mahakamani Januari 16 na kusomewa mashtaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande aliyeeleza upelelezi ulikuwa umekamilika na walikuwa tayari kuendelea na usikilizaji.
CHANZO: MPEKUZI
Share:

IRINGA: Wahamiaji 83 wa Ethiopia wapandishwa kizimbani

Wahamiaji 83 raia wa Ethiopia na Mtanzania mmoja mkazi wa Tukuyu wamefikishwa Mahakama ya Mkoa Iringa huku wahamiaji hao wakituhumiwa kuingia nchini bila kibali.

Akisoma mashtaka hayo leo Februari 26, 2018, wakili wa Serikali, Godfrey Ngwijo amesema raia hao wanakabiliwa na shtaka la kuingia nchini kinyume na kifungu cha sheria namba 45(i) kifungu (1) ,(2) kilichofanyiwa marekebisho 2016.

Ngwijo amesema Februari 23, 2018 saa moja jioni katika kijiji cha Mazombe wilayani Kilolo, wahamiaji 83 wasio na vibali walikamatwa na kufikishwa kituo cha polisi kwa kuingia nchini kinyume na sheria ambapo dereva wa lori walilopanda  hakupatikana baada ya kukimbia.

Amesema wahamiaji hao walikamatwa wakiwa katika hali mbaya kutokana na kukaa sehemu ya nyuma ya lori hilo ambako hakuna hewa ya kutosha, joto kali na kutokula chakula kwa muda mrefu.

Baadhi ya wahamiaji hao leo wamefikishwa hospitali ya mkoa kupata matibabu.

Wakili huyo amesema kati ya waliofika mahakamani kusomewa mashtaka yao, watatu  walishindwa kufika kwa sababu bado wako hospitali wanaendelea na matibabu.

Mtanzania aliyekutwa katika gari hiyo, Hassan Mwalusanjo akituhumiwa kusafirisha wahamiaji hao kwa kutumia lori mali ya Gabriel Mwakyambiki mkazi wa Tukuyu kinyume na sheria, alikana kosa hilo.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, David Ngonyani ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 2, 2018.
CHANZO: MPEKUZI
Share:

MBEYA: Mbunge Joseph Mbilinyi 'sugu' Kahukumiwa Miezi Mitano Jela

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya imemuhukumu Miezi Mitano jela Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite ambapo amesema ameridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mteite amesema kuwa Mahakama imejikita katika sehemu kuu nne.

Amesema kuwa sehemu hizo ni kama washtakiwa walitamka Maneno ya fedheha, pia kama maneno waliyoyatoa yamebeba maudhui ya fedheha, pia kama maneno hayo yana mlenga Rais pamoja washtakiwa kama wana hatia ama lah.

Katika hukumu hiyo iliyochukua zaidi ya saa moja Hakimu Mteite amesema amejiridhisha pasina kuacha shaka juu ya ushahidi wa mashahidi watatu wa upande wa mashtaka.

Hakimu Mteite amesema Mahakama inakubaliana na hoja ya kwamba washtakiwa walitamka maneno ya fedheha dhidi ya Rais kutokana na ushahidi wa upande wa mashtaka ambao waliwasikia washtakiwa na kuwaona wakati wakitamka.

“Katika kesi hii mashahidi wengi ni askari, hivyo ni dhahiri wametoa maneno hayo,” -Hakimu Mteite

Pia kuhusu maneno hayo kumlenga Rais Magufuli, Hakimu Mteite amesema maneno hayo ya fedheha ni ya kitaifa, kwani masuala yanayogusa watu kuuawa ni ya kitaifa na ndio maana washtakiwa walitamka maneno (Rais Wetu).

“Tujiulize ni Rais yupi waliyemzungumzia ni wa Simba, Yanga ama Mbeya City hivyo Rais aliyezungumziwa hapa ni Magufuli kwani hakuna Magufuli mwingine anayetuongoza,”-Hakimu Mteite

Hakimu Mteite amesema kwa imani yake washtakiwa wana hatia.

“Kutokana na upande wa utetezi kuomba nafuu ya adhabu na upande wa mashtaka kutaka itolewe adhabu kali, nawahukumu miezi mitano jela,” -Hakimu Mteite.

CHANZO: MPEKUZI
Share:

MTWARA: Waziri Mkuu Aiagiza TAKUKURU Kuwakamata Aliiyekuwa Mkugenzi wa Halimashauri Masasi na Mweka Hazina

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Mtwara Bw. Stephen Mafipa  kumtafuta popote alipo na kumkamata aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Masasi Bw. Fortunatus  Kagoro  kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha.

Mbali na Bw. Kagoro pia Kaimu Mweka Hazina Bw. Heri Hamad Afisa Mipango Bi Teresia Nsumba  nao ameagiza wakamatwe na baada ya uchunguzi watakaobainika kwamba hawajahusika na ubadhilifu huo watarudishwa kazini. "Lazima fedha za Serikali zitumike kama ilivyokusudiwa."

Watendaji hao wanadaiwa kutumia sh. bilioni 1.8 zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Mji wa Masasi kwa kuchora mchoro na kujenga msingi katika maeneo mawili tofauti.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatatu, Februari 26, 2018) wakati akizungumza na watumishi na Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Masasi na Halmashauri ya wilaya ya Masasi akiwa kwenye ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara.

Amesema mwaka 2014  Serikali ilipeleka sh milioni 575 wilaya Masasi kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Halmashauri hiyo na fedha hizo ziliishia kutumika  katika hatua za maandalizi ya awali ikiwa ni pamoja na kutengeneza michoro ya jengo.

Waziri Mkuu amesema 2016/2017 Serikali ilipeleka tena sh. bilioni 1.25 kwa ajili ya ujenzi huo, ambapo Halmashauri hiyo ilienda kutafuta eneo lingine na kufanya tena shughuli zilizokuwa zimefanyika na kuanza ujenzi ambao umeishia katika msingi na fedha zimeisha.

Pia amewataka watendaji hao kutotumia fedha za makusanyo ya ndani kwa ajili ya kuziba pengo la fedha za mradi huo ambazo baadhi yake hazijulikani zilipo na amewaagiza Madiwani kutoruhusu jambo hilo.

"Madiwani msikubali kutumia fedha za makusanyo ya ndani kupeleka kwenye ujenzi wa miradi ya maendeleo ambayo tayari Serikali ilishatoa fedha ya ujenzi wake.

Amesema Serikali inahitaji kuona fedha za maendeleo zinazopelekwa katika Halmashauri mbalimbali nchini zinatumika kama ilivyoelekeza na si vinginevyo na Serikai haitakuwa na mzaha kwa mtumishi atakayezitumia vibaya.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, FEBRUARI 26, 2018.
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>