Wanasalamu Kanda ya Kusini wamsaidia mwenye ulemavu

 

Mwakilishi wa Wanasalamu Kanda ya Kusini akikabidhi godoro na daftari kwa Mzee Somba ikiwa ni mchango wa umoja huo (Picha na Musa Mtepa)

Wanasalamu Kanda ya Kusini kwa kushirikiana na Jamii FM wametoa msaada wa godoro na vifaa vya shule kwa Mzee Salumu Somba, mlemavu wa macho na mkazi wa Mnyengedi, baada ya kuguswa na hali yake kupitia kipindi cha Sikika. Wametoa wito kwa jamii kushirikiana kusaidia wenye uhitaji.

Na Musa Mtepa

Umoja wa Wanasalamu Kanda ya Kusini kwa kushirikiana na wadau wa Jamii FM Radio, leo Oktoba 15, 2025, wametoa msaada wa godoro na vifaa vya shule kwa familia ya Mzee Salumu Somba, mkazi wa Kijiji cha Mnyengedi,Mzee Somba ni mlemavu wa macho na anaishi katika mazingira ya kipato duni.

Akizungumza kwa niaba ya umoja huo wakati wa kukabidhi msaada, Bi Mwanahawa Nayopa (Mrs. Machela) amesema kuwa walipata taarifa za hali ngumu ya maisha ya Mzee Somba kupitia kipengele cha Sikika, kinachorushwa hewani na Jamii FM Radio kupitia kipindi cha Dira ya Asubuhi.

Kupitia taarifa hiyo, waliguswa na hali ya familia hiyo, hasa watoto wa Mzee Somba wanaosoma katika Shule ya Msingi Mwenge, na wakaamua kuchangishana fedha kwa ajili ya kununua godoro pamoja na vifaa vya shule.

Sauti ya Mwanahawa Nayopa – Mwakilishi wa Wanasalamu Kanda ya Kusini

Aidha, Bi Nayopa ameishukuru Jamii FM Radio kwa mchango wake mkubwa wa kuibua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi, hususan watu wenye uhitaji maalum. Ametoa wito kwa jamii nzima kuendeleza moyo wa kusaidiana kwani kusaidia wenye uhitaji si jukumu la mtu mmoja bali ni la jamii nzima.

Sauti ya Mwanahawa Nayopa – Mwakilishi wa Wanasalamu Kanda ya Kusini

Kwa upande wake, Mzee Salumu Somba amewashukuru Wanasalamu kwa msaada waliompatia, huku akiwaombea baraka tele kutoka kwa Mungu huku akisema kuwa msaada huo umempa faraja kubwa na kuwaomba waendelee kuwa na moyo huo wa huruma kwa wengine wenye mahitaji kama yake au hata zaidi.

Sauti ya Mzee Salumu Somba – Mlemavu wa Macho

Naye Ebby Hamisi, Mtendaji wa Kijiji cha Mnyengedi, ametoa shukrani zake kwa Umoja wa Wanasalamu kanda ya kusini kwa kuguswa na hali ya Mzee Somba na kutoa rai kwao kwa kutokata tamaa kutokana na maneno ya kubezwa au kudhihakiwa, bali waendelee kufanya mema kwa jamii.

Sauti ya Ebby Hamisi – Mtendaji wa Kijiji cha Mnyengedi

Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>