Wanafunzi DIS waitembelea Jamii FM Mtwara

 

Amua Rushita meneja na mtaalamu wa TEHAMA akitoa maelekezo jinsi redio inavyofanya kazi kutokea studio hadi kufikia kwa wasikilizaji(Picha na Musa Mtepa)

Wanafunzi wa Kidato cha Pili wa Dar es Salaam Independent School wametembelea Jamii FM Radio Mtwara kujifunza kuhusu vyombo vya habari na athari za mitandao ya kijamii , ikiwa ni sehemu ya somo la Mtazamo wa Kidunia (Global Perspective).

Na Musa Mtepa

Mtwara —-Wanafunzi wa Kidato cha Pili kutoka Dar es Salaam Independent School (DIS) leo, Oktoba 7, 2025, wametembelea kituo cha kurushia matangazo cha Jamii FM Radio kilichopo Mtwara, kwa lengo la kujifunza kwa vitendo kuhusu vyombo vya habari, hususan redio na mitandao ya kijamii.

Akizungumza kuhusiana na ujio huo, Meneja na Mtaalamu wa Masuala ya TEHAMA kutoka Jamii FMAmua Rushita, amesema kuwa wanafunzi hao wamefika kituoni hapo ili kujifunza namna mitandao ya kijamii inavyoathiri vyombo vya habari (Traditional Media), pamoja na jinsi jamii inavyoweza kupata taarifa sahihi kupitia vyombo vya habari.


Sauti ya Amua Rushita – Meneja wa Jamii FM

Amua ameongeza kuwa moja ya sababu zilizowavutia wanafunzi kutembelea Jamii FM ni kutokana na namna vipindi vya redio hiyo vinavyogusa makundi yote ya jamii moja kwa moja.

Sauti ya Amua Rushita – Meneja wa Jamii FM

Kwa upande wake, Mwalimu, Donald kutoka Dar es Salaam Independent School, ameishukuru Jamii FM kupitia kwa Amua Rushita kwa kutoa elimu ya kina kuhusu aina mbili za vyombo vya habari   faida na changamoto zake kwa jamii .

Pia amesema kuwa moja ya mambo waliokuja kujifunza Mtwara ni somo la Mtazamo wa Kidunia (Global Perspective), ambalo limejikita katika kueleza jinsi mitandao ya kijamii inavyoathiri Jamii hususani kwa upande wa vyombo vya habari.

Sauti ya Mr. Donald – Mwalimu, Dar es Salaam Independent School

Nao wanafunzi wa DIS wamesema kuwa ziara hiyo imewasaidia kuelewa kwa undani namna vyombo vya habari vinavyofanya kazi, na nafasi ya redio kama chanzo cha habari kinachoaminika katika jamii.

Sauti ya Wanafunzi wa Dar es Salaam Independent School
Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>