Viongozi Mkunwa wagusa maisha ya mzee Somba

 

Afisa mtendaji wa kata ya Mkunwa Bi Rachael Pether wa pili kutokea kulia akiwa katika picha ya pamoja wakati wa kukabidhi msaada wa Godoro kwa familia ya Mzee Salamu Somba (Picha na Musa Mtepa)

Viongozi wa Kata ya Mkunwa wametoa msaada wa godoro, sabuni na taa kwa familia ya Mzee Salumu Somba ili kusaidia kupunguza changamoto za maisha zinazoikabili familia hiyo.

Na Musa Mtepa

Viongozi na watendaji wa vijiji katika Kata ya Mkunwa wametoa msaada wa godoro, sabuni na taa kwa familia ya Mzee Salumu Somba, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za mwenyekiti wa Kijiji cha Nyengedi katika kusaidia familia hiyo inayokabiliwa na hali ngumu ya maisha.

Akizungumza na Jamii FM Radio leo Oktoba 9, 2025 wakati wa kukabidhi msaada huo, Afisa Mtendaji wa Kata ya Mkunwa, Bi Rechal Bernadater Pether, amesema kuwa uongozi wa Kijiji cha Nyengedi uliwasilisha taarifa juu ya hali ya familia hiyo katika ofisi ya kata, na baada ya kutembelea familia hiyo walijiridhisha kuhusu uhitaji wa msaada.

Aidha, Bi Rechal ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza na kusaidia familia hiyo ambayo inakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi.

Sauti ya Bi Rechal Bernadater Pether, Mtendaji wa Kata ya Mkunwa

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Nyengedi, Bi Ebby Hamisi, ameushukuru uongozi wa kata kwa kuguswa na changamoto zinazowakabili wananchi wao, akibainisha kuwa msaada huo utasaidia kupunguza kwa kiasi fulani matatizo yanayoikumba familia hiyo.

Hata hivyo, Bi Ebby amesema kuwa pamoja na msaada huo, familia ya Mzee Somba bado inakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwemo watoto wake wa shule ya msingi kukosa mahitaji muhimu ya shule, na hali ya kulala chini kwa kutumia matambala ardhini.

Sauti ya Bi Ebby Hamisi, Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Nyengedi

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyengedi, Bi Lukia Mnyachi, ameushukuru uongozi wa kata kwa msaada huo, akisema umeleta faraja na kupunguza changamoto kwa familia ya Mzee Somba.

Sauti ya Bi Lukia Mnyachi, Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyengedi

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Mzee Salumu Somba ameushukuru uongozi wa kata pamoja na mwenyekiti wa kijiji kwa jitihada zao za kuwafikia na kuwasaidia, akieleza kuwa hali yao kwa sasa imeimarika ukilinganisha na kipindi cha nyuma.

Sauti ya Mzee Salumu Somba, mlemavu wa macho

Mzee Salumu Somba ni mkazi wa Kijiji cha Nyengedi kilichopo Kata ya Mkunwa, Halmashauri ya Mtwara Vijijini, mkoani Mtwara. Hapo awali alikuwa akiishi katika nyumba chakavu isiyo na paa imara, hali iliyosababisha yeye na watoto wake watatu wenye umri kati ya miaka 5 hadi 8 kulala wakiwa wazi kwa mvua na jua.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Kijiji cha Nyengedi, kupitia kwa Mwenyekiti wake Bi Lukia Mnyachi, ulijitahidi na kufanikisha ujenzi wa nyumba mpya kwa familia hiyo. Hata hivyo, familia hiyo iliendelea kukosa vitanda na kulazimika kulala chini, hali iliyowalazimu viongozi hao kuandaa msaada wa godoro na mahitaji mengine ya msingi.

Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>