Malezi duni yatajwa sababu ya mimba mashuleni Mtwara

 

Baadhi ya wananchi wa kata ya Naliendele wakishiriki mdahalo huo(Picha na Mohamed Masanga)

Mdahalo ulioandaliwa na Jamii FM umebainisha kuwa mimba mashuleni husababishwa na malezi duni, kutokuwepo kwa uangalizi wa karibu kutoka kwa wazazi, pamoja na ushiriki wa jamii hafifu katika kulinda watoto wa kike

Na Musa Mtepa

Inaelezwa kuwa ukosefu wa malezi na maandalizi bora kwa watoto kutoka kwa wazazi umeendelea kuwa moja ya sababu kuu zinazochangia wanafunzi wa kike kupata mimba wakiwa bado shuleni.

Hayo yamebainika katika mdahalo ulioandaliwa na Jamii FM Radio Oktoba 8, 2025, uliokuwa na kaulimbiu “Jamii Inashiriki Vipi Katika Kutokomeza Mimba Shuleni.

Maafisa usafirishaji (bodaboda) kutoka stendi ya Bajaji, kata ya Naliendele, wameeleza kuwa mimba nyingi zinazopatikana shuleni huchangiwa na wazazi kulega katika malezi, ikiwemo kuruhusu watoto kushiriki matukio ya usiku kama vile vigodoro, ambayo huwapeleka katika mazingira hatarishi.

Sauti ya maafisa usafirishaji – kata ya Naliendele

Hata hivyo, baadhi ya wazazi wamepinga kauli hiyo wakisema si wazazi wote huruhusu watoto wao kwenda kwenye vigodoro. Shaibu Abdala Kupela na Brandina Chilumba, ambao ni wazazi, wamesema kuwa kuna sababu nyingine nyingi zinazochangia mimba shuleni, ikiwemo wazazi kutengana bila sababu za msingi, hali inayosababisha watoto kukosa uangalizi wa kutosha.

Sauti za wazazi wakichangia mjadala

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Pachoto “A”, Bw. Sadi Abdala Kombo, amesema kuwa ili kuondokana na tatizo la mimba mashuleni, ni lazima wazazi wasimame imara katika kulea watoto wao na kutambua wajibu wao kama walezi.

Sauti ya Sadi Kombo – 1 Mwenyekiti wa Mtaa wa Pachoto A

Aidha, Mwenyekiti huyo amesisitiza kuwa viongozi wa mitaa wana wajibu wa kukutana na wazazi mara kwa mara kwa ajili ya kujadiliana namna ya kuwasaidia watoto kuishi salama na kujitambua wakiwa shuleni.

Sauti ya Sadi Kombo – 2 Mwenyekiti wa Mtaa wa Pachoto A

Kwa upande mwingine, Judith Chitanda kutoka shirika la Nerio Paralegal pamoja na Sajenti Esta kutoka dawati la jinsia, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara, wameitaka jamii kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa pale mtoto anapopata ujauzito ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya wahusika na kusaidia kutokomeza mimba mashuleni.

Sauti ya Judith Chitanda na Sajent Esta – Dawati la Jinsia, Jeshi la Polisi
Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>