Mwenyekiti wa kijiji aongoza ujenzi nyumba ya mwenye ulemavu Mtwara

 

Nyumba mpya aliyojengewa mzee Zomba mlemavu wa macho kwa jitihada za mwenyekiti wa kijiji cha Mnyengedi Bi lukia Mnyachi(Picha na Musa Mtepa)

Familia ya Mzee Salumu Zomba, mwenye ulemavu wa macho, yamekabidhiwa nyumba mpya baada ya kuishi kwenye kibanda kibovu, juhudi zilizowezeshwa na viongozi wa kijiji cha Mnyengedi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Na Musa Mtepa

Baada ya kuishi katika mazingira hatarishi kwa muda mrefu, familia ya Mzee Salumu Ismail Zomba, ambaye ni mlemavu wa macho, mkazi wa Kijiji cha Mnyengedi kata ya Mkunwa mkoani Mtwara, hatimaye imekabidhiwa nyumba mpya yenye vyumba viwili na ukumbi, ikiwa ni matokeo ya juhudi za pamoja zilizoongozwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyengedi, Bi Lukia Mnyachi.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa nyumba hiyo, Mtendaji wa Kijiji cha Mnyengedi, Bi Ebby Hamisi, amesema kuwa familia ya Mzee Zomba hapo awali ilikuwa ikiishi katika kibanda kibovu ambacho hakikutoa hifadhi ya kutosha dhidi ya mvua na jua, hali iliyowaathiri hasa watoto waliokuwa wakiishi katika mazingira hayo.

Sauti ya 1 Bi Ebby Hamisi Mtendaji wa Kijiji cha Nyengedi

Aidha, Bi Ebby ameeleza kuwa licha ya mafanikio ya ujenzi huo, familia hiyo bado inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kimaisha. Alitoa shukrani kwa wadau wote waliosaidia kufanikisha ujenzi huo, wakiwemo kituo cha redio cha Jamii FM kilichopo Naliendele, Mtwara.

Sauti ya 2 Bi Ebby Hamisi Mtendaji wa Kijiji cha Nyengedi

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Afisa Tarafa wa Mayanga, Bw. Marco Mapunda, amewapongeza wote waliojitolea katika kusaidia familia hiyo na kusema kuwa kitendo hicho ni mfano bora wa mshikamano wa kijamii na namna viongozi wanavyoweza kuwa chachu ya maendeleo kwa watu wenye uhitaji.

Sauti ya 1 Marco Mapunda afisa tarafa tarafa ya Mayanga
Marco Mapunda akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye kukabidhi nyumba ya Bw Zomba (Picha na Musa Mtepa)

Pia afisa tarafa ameahidi kuzibeba na kuzifanyia kazi changamoto zote zilizowasishwa kupitia risala iliyosomwa na afisa mtendaji wa Kijiji cha Nyengedi Bi Ebby Hamisi kwa kuziwasilisha katika ofisi ya mkuu wa wilaya na kuona namna ya kuisaidia familia hiyo

Sauti ya 2 Marco Mapunda afisa tarafa tarafa ya Mayanga

Kwa upande wake, Bi Lukia Mnyachi, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyengedi, alielezea jinsi alivyoguswa na hali ya maisha ya Mzee Zomba na kuamua kuanzisha juhudi za kutafuta msaada ili kumjengea nyumba.

Sauti ya Bi Lukia Mnyachi Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyengedi
Mwenyekiti wa kijiji cha Nyengedi akielezea jitihada zilizofanyika hadi kukamilika kwa ujenzi wa Nyumba ya Mzee Salumu Zomba mlemavu wa Macho na Mkazi wa kijiji cha Mnyengedi mkoani Mtwara(Picha na Musa Mtepa)

Mzee Salumu Zomba, akizungumza kwa furaha, ameshukuru kwa jitihada kubwa zilizofanywa na viongozi na wadau waliomsaidia kupata makazi bora. Hata hivyo, ametumia nafasi hiyo kuomba msaada zaidi wa vitanda, magodoro, na mahitaji ya watoto wake wanaosoma.

Sauti ya Mzee Salumu Zomba mlemavu wa macho
Mzee Salumu Zomba akiwa na mke wake wakiwa katika picha ya pamoja kwenye kibanda walichokuwa wanaishi na watoto wao kabla ya Mwenyekiti wa kijiji Bi Lukia Mnyachi kufanikisha ujenzi wa Nyumba Mpya(Picha na Musa Mtepa)

Majirani wa Mzee Zomba pia wameelezea hali ngumu ya maisha anayopitia, wakisisitiza kuwa kwa kuwa ni mlemavu wa macho, anahitaji msaada wa mara kwa mara kutoka kwa jamii na serikali.

Sauti ya majirani wa Mzee Zomba
Mwonekano wa awali wa Nyumba ya Mzee Zomba kabla hajaporomoka na Mvua na kujenga kibanda kidogo cha kuishi (Picha na Musa Mtepa)
Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>