JWTZ yaadhimisha miaka 61 kwa shughuli za kijamii, michezo Mtwara

 

vikosi vya jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ ) wakiwa katika maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwake katika viwanja vya Nangwanda Sijaona Mjini Mtwara(Picha na Musa Mtepa)

JWTZ limeadhimisha miaka 61 tangu kuanzishwa kwake kwa kushiriki shughuli za kijamii ikiwemo uchangiaji damu na mpira wa kirafiki dhidi ya Jeshi la Polisi, katika viwanja vya Nangwanda Sijaona, Mtwara

Na Musa Mtepa

Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) leo Septemba 1, 2025, limeadhimisha miaka 61 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1964, kufuatia kuondoka kwa jeshi la kikoloni.

Maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, yakiongozwa na Mkuu wa Vikosi na Vikundi vya JWTZ mkoa wa Mtwara (Base Commander), Kanali James Simon Mwakinyuke.

Kanali Mwakinyuke amesema kuwa maadhimisho hayo ni kumbukizi ya kuzaliwa kwake ambapo kuelekea katika maadhimisho hayo huambatana na ufanyaji wa shughuli mbalimbali za kijamii

Sauti ya 1 Kanali James Mwakinyuke mkuu wa vikosi vya JWTZ Mtwara
Kanali James Simon Mwakinyuke akizungumza na Waandishi wa habari katika kilele cha maadhimisho ya kuzaliwa kwa JWTZ yaliyofanyika katika viwanja vya Nangwanda Sijaona mjini Mtwara(Picha na Musa Mtepa)

Aidha, Kanali Mwakinyuke amesema katika kilele cha maadhimisho ya mwaka huu, Jeshi la Wananchi mkoani Mtwara limejitoa kushiriki katika zoezi la uchangiaji wa damu kupitia Mfuko wa Damu Salama – Kanda ya Kusini, pamoja na kucheza mechi ya kirafiki ya mpira wa miguu kati ya JWTZ na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara.

Sauti ya 2 Kanali James Mwakinyuke mkuu wa vikosi vya JWTZ Mtwara
Miongoni mwaafisa wa Jeshi la Wananchi la Tanzania akiwa katika hatua za mwisho za vipimo tayari kwa kuchangia Damu katika mfuko wa taifa wa Damu Salama (Picha na Musa Mtepa)

Huu ni utaratibu wa kawaida kwa JWTZ mkoani Mtwara ambapo Mwaka jana walifanya usafi katika eneo la Mashujaa na tukachangia damu katika Zahanati ya Jeshi ya 665 Alignment.

Maadhimisho haya ni sehemu ya mwendelezo wa JWTZ kushirikiana na jamii kwa njia za kijamii na kijeshi, ikiwa ni pamoja na kudumisha amani na mshikamano ndani ya nchi.

Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>