Wanachama CCM Msimbati watishia kujiondoa uanachama

 

Wanachama wa CCM wakiwa katika ofisi ya chama wakipinga kuondolewa kwa jina la Rashidi Linkoni aliyeshinda kwenye kura za maoni(Picha na Musa Mtepa)

Wanachama zaidi ya 150 wa CCM Msimbati wamelalamikia kuondolewa kwa jina la Rashidi Linkoni aliyeshinda kura za maoni, wakitishia kurudisha kadi zao, huku viongozi wa wilaya wakisisitiza maamuzi ya kamati ya siasa

Na Musa Mtepa

Zaidi ya wanachama 150 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Msimbati, wilayani Mtwara Vijijini, wameonesha kutoridhishwa na kitendo cha kuondolewa jina la Rashidi Omari Linkoni, aliyeshinda kura za maoni kwa kura 116, na kurejeshwa jina la Abrehemani Hamisi aliyeshika nafasi ya pili kwa kura 101.

Wanachama hao, wakizungumza na Jamii FM Agosti 17, 2025, wamesema hatua hiyo ni dharau kwa maamuzi ya wajumbe na kutishia kurudisha kadi za chama.

Sauti ya Wanachama wa CCM Kata ya Msimbati
Baadhi ya kadi za Wanachama wa CCM wa kata ya Msimbati zilizo rejeshwa na kutupwa baada ya wanachama kutoridhishwa na kitendo cha kuenguliwa mgombea aliyepitishwa na wajumbe Kwenye kura za maoni

Mzee Musa Ali maarufu kama Mzee Chituka, muasisi wa CCM kata ya Msimbati, amesema kitendo hicho kimekwenda kinyume na maamuzi ya wajumbe na akashauri uongozi wa wilaya kufika Msimbati kufanya mazungumzo na wanachama waliomchagua Linkoni.

Sauti ya Mzee Musa Ali muasisi wa CCM kata ya Msimbati
Mzee Musa Ali muasisi wa CCM kata ya Msimbati (Picha na Musa Mtepa)

Kwa upande wake, Salumu Uchumi, mwenyekiti wa CCM tawi la Liumo, alithibitisha kuwa hadi kufikia Agosti 17, zaidi ya wanachama 150 walikuwa tayari wamerudisha kadi zao za uanachama kutokana na uamuzi huo.

Sauti ya Salumu Uchumi Mwenyekiti CCM tawi la Liumo

Rashidi Omari Linkoni, diwani mstaafu aliyeenguliwa licha ya kuongoza kura za maoni, amesema amepokea kwa namna yake maamuzi ya viongozi wa wilaya, lakini hana budi kuyakubali.

Sauti ya Rashidi Linkoni Diwani mstaafu
Rashidi Linkon aliyekuwa Diwani wa kata ya Msimbati akizungumza baada ya wanachama kuandamana wakihitaji kurejeshwa kwa jina lake lililochaguliwa kwenye kura za maoni(Picha na Musa )

Naye Shahame Masudi Ahmadi, katibu wa CCM kata ya Msimbati, amekiri jina la Abrehemani Hamisi kurudi badala ya Linkoni na kueleza kuwa ni maamuzi ya Kamati ya Siasa ya Wilaya, huku akiwataka wanachama kuwa watulivu na kufuata maelekezo ya viongozi wa juu.

Sauti ya Shame Masudi Ahmadi Katibu wa CCM kata ya Msimabti

Akizungumzia hali hiyo, Hamisi Wanyama, katibu wa siasa na uenezi CCM Mtwara Vijijini, amesema wajumbe walimteua Linkoni kwenye kura za maoni, lakini kamati ya siasa wilaya ina mamlaka ya kubadili jina endapo itaona inafaa. Aidha, ameongeza kuwa malalamiko ya wanachama ni ishara ya utovu wa nidhamu na kutoifuata itikadi ya chama.

Sauti ya 1 Hamisi Wanyama katibu wa Siasa na uenezi wilaya

Wanyama amebainisha kuwa taarifa za wanachama kurudisha kadi ameziona mitandaoni na hajapokea rasmi, lakini endapo zitafikishwa watazipokea, huku akiahidi kufika Msimbati kuzungumza na wanachama husika.

Sauti ya 2 Hamisi Wanyama katibu wa Siasa na uenezi wilaya
Katibu wa Siasa na uenezi CCM Mtwara Vijijini Hamisi Wanyama akitolea ufafanuzi juu ya malalamiko ya wanachama wa CCM kata ya Msimbati
Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>