• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

Jamii yahimizwa kuepuka hisia katika kutatua migogoro

 

Afisa ufuatiliaji na tathmini kutoka shirika la TASA Hamisi Mwinshehe akiwa katika studio za Jamii fm Mtwara

Afisa wa TASA, imeitaka  jamii kutenga muda wa kufikiria na kutoa maamuzi sahihi katika kutatua migogoro, ikisisitiza kuepuka hisia na kutoegemea upande wowote

Na Musa Mtepa

Jamii imetakiwa kutenga muda wa kufikiria, kuchakata na kutoa maamuzi sahihi katika kutatua migogoro inayowakabili katika maeneo yao.

Hayo yamesemwa na Afisa Tathmini na ufuatiliaji kutoka shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Safety Alliance (TASA) linalofanya kazi katika Manispaa ya Mtwara–Mikindani, Hamisi Rashidi Mwinshekhe, kupitia kipindi cha Dira ya Asubuhi kinachorushwa na kituo cha redio cha Jamii FM Mtwara.

Amesema kuwa mgogoro ni hali ya kuwepo kwa mivutano ya kimawazo au kimtazamo, hivyo ni muhimu jamii kutenga muda wa kutosha wakati wa mchakato wa utatuzi ili kuhakikisha kila upande unaridhika na maamuzi yatakayofikiwa.

Sauti ya 1: Hamisi Mwinshekhe – Afisa Tathmini na Ufuatiliaji, TASA

Aidha, Mwinshekhe amesema kuwa kumekuwa na sababu mbalimbali zinazosababisha kuibuka kwa migogoro katika jamii, ambazo kwa namna moja au nyingine ni muhimu kuepukika ili kujenga jamii imara na yenye amani.

Sauti ya 2: Hamisi Mwinshekhe – Afisa Tathmini na Ufuatiliaji, TASA

Ameongeza kuwa kuna mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kutatua migogoro, ikiwemo kuepuka matumizi ya hisia, kuonesha huruma, pamoja na kutoegemea upande wowote katika mgogoro unaoendelea.

Sauti ya 3: Hamisi Mwinshekhe – Afisa Tathmini na Ufuatiliaji, TASA

Shirika la TASA kwa sasa linatekeleza mradi wa “Amani Yetu, Kesho Yetu” katika kata tano za Halmashauri ya Mtwara Vijijini, ambazo ni Nalingu, Madimba, Msimbati, Tangazo na Mahurunga.

Mradi huu unalenga kuelimisha jamii, hususan vijana, kuhusu athari za uvunjifu wa amani na umuhimu wa kudumisha utulivu katika maeneo yao.

Share:

Wakulima wa mwani Naumbu walia na soko

 

Mwonekano wa zao la Mwani likiwa limeanikwa baada ya kuvunwa kutoka shambani (Baharini) Picha na Musa Mtepa

Serikali imeombwa kuongeza wanunuzi wa zao la mwani ili kuboresha ushindani wa soko huku wakulima wakilalamikia bei ya shilingi 800 ambayo haiendani na gharama za uzalishaji na usafirishaji kutoka baharini

Na Musa Mtepa

Wakulima wa mwani kutoka Kijiji cha Naumbu, Kata ya Naumbu, Halmashauri ya Mtwara Vijijini wameiomba Serikali pamoja na wadau wa zao hilo kuhakikisha kunakuwepo na ongezeko la wanunuzi ili kuongeza ushindani wa soko.

Wakizungumza na Jamii FM Radio , wakulima hao wamesema kuwa bei ya mwani inayofikia shilingi 800 kwa kilo haiendani na gharama pamoja na mahitaji yao ukilinganisha na uzalishaji wanaoufanya.

Wamesisitiza kuwa ongezeko la wanunuzi litaongeza ushindani na hivyo kusaidia kupandisha bei ili waweze kunufaika zaidi na zao hilo.

Aidha, wameeleza kuwa ili kuzalisha na kufikisha mwani nchi kavu, hulazimika kugharamia usafirishaji kutoka baharini, hivyo kwa bei ya shilingi 800 kwa kilo hawawezi kupata kipato kinachokidhi mahitaji yao.

Sauti ya wakulima wa mwani Naumbu Kusini

Akizungumzia hali ya uzalishaji wa mwani katika kijiji hicho, mkulima Bi Bibie Ali Kitenge amesema kuwa wamekuwa wazalishaji wakubwa wa zao hilo, huku wakizalisha kila baada ya siku 45.

Sauti ya Bi Bibie Kitenge mkulima wa Mwani

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Naumbu Kusini, Bw. Selemani Shineni, amesema soko la mwani bado ni changamoto kubwa, hali inayosababisha kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wakulima wanaoomba watafutiwe soko lenye tija.

Sauti ya 1 – Selemani Shineni, Mwenyekiti Naumbu Kusini

Aidha, Shineni ameiomba halmashauri, kupitia maafisa uvuvi, kutowazuia wanunuzi wengine wanaojitokeza kununua mwani. Amesema kuwa kama kuna vigezo wanunuzi wanashindwa kuvifuata, wanapaswa kuelezwa ili wavifuate na hatimaye waweze kununua, jambo litakalowezesha wakulima kunufaika na zao lao.

Sauti ya 2 – Selemani Shineni, Mwenyekiti Naumbu Kusini
Share:

SDA yaadhimisha IDPWD kwa usafi wa mazingira

 

Shirika la SDA wakiwa pamoja na watu wenye ulemavu katika zoezi la usafi wa mazingira. Picha na Msafiri kipila

Ikiwa leo ni Siku ya Watu wenye Ulemavu Duniani, siku hii imeambatana na mabadiliko ya tabianchi na uwepo wa mabadiliko hayo kuna athari kwa watu wenye ulemavu.

Na Grace Hamisi

Shirika lisilo la kiserikali Sports Development Aids (SDA) kupitia mradi wake wa mazingira leo tarehe  03/12/2025, wameadhimisha siku ya watu wenye ulemavu duniani kwa kushirikiana na watu wenye ulemavu kufanya usafi eneo la fukwe ya bahari na kutoa elimu namna ya kutunza takataka mkoani Mtwara.

Akizungumza mkurugenzi wa shirika hilo Tea Swai, ameelezea namna walivyoshirikiana na watu wenye ulemavu kufanya usafi huo na kutoa elimu jinsi ya kutunza mazingira pamoja namna ya  kupunguza ukatili kwa watu wenye ulemavu.

Sauti ya Tea Swai – Mkurugenzi wa SDA

Nae Afisa afya Mazingira Salome Mayala, amepongeza kwa kile ambacho kimefanyika kwani kinahamasisha watu kuweza kutunza mazingira na kujikinga na madhara yanayopatikana kwa kuchafua mazingira.

Sauti ya Afisa afya Mazingira Salome Mayala

Kwa upande wake mtaalamu wa masuala ya walemavu na saikolojia, mwalimu Chris Mkwela amesema ikiwa leo ni siku ya watu wenye ulemavu imeambatana na mabadiriko ya tabia ya nchi na uwepo wa mabadiliko hayo kuna athari kwa watu wenye ulemavu kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika la umoja wa mataifa ambalo linahusika kupunguza hatari na majanga.

Sauti ya mwalimu Chris Mkwela – mtaalamu wa masuala ya walemavu na saikolojia

Hata hivyo Amani Danfod Kazumari ambae ni mtu mwenye ulemavu ameshukuru shirika la SDA kwa kuwakutanisha pamoja na kufanya usafiri eneo la fukwe ya bahari ambapo alikuwa mazingira sio mazuri.

Sauti ya Amani Danfod Kazumari

Fatuma Mpondomoka mkazi wa likombe ameomba taasisi nyingine pia kuwaweka karibu watu wenye ulemavu katika shughuli mbalimbali ikiwemo siku hizi muhimu na kuwapa taarifa mapema ili wa wao waweze kujiandaa na kuonyesha vile ambavyo wanavifanya kwani wanaweza.

Sauti ya Fatuma Mpondomoka
Share:

Wafanyabiashara Mtwara walia na ongezeko la tozo

 

Baadhi ya wafanyabiashara wakifuatilia kwa umakini mkutano wa ushirika wa Wafanyabiashara uliofanyika November 15, 2025 viwanja vya Mashujaa Manispaa ya Mtwara Mikindani (Picha na Musa Mtepa)

Wafanyabiashara wa Mtwara wamelalamikia ongezeko la tozo na ushuru linalodaiwa kupandisha bei za bidhaa, huku wakitaka serikali kupitia upya kanuni hizo. Manispaa imesisitiza kuwa tozo zinatekelezwa kwa mujibu wa sheria na iko tayari kushughulikia malalamiko kupitia majadiliano

Na Musa Mtepa

Wafanyabiashara mjini Mtwara wamelalamikia ongezeko la ushuru unaoendelea kutungwa katika biashara zao, wakieleza kuwa hatua hiyo inaathiri bei za bidhaa na kuhatarisha uwezo wa mlaji wa mwisho kumudu bidhaa hizo.

Wakizungumza Novemba 15, 2025 katika mkutano wa Ushirika wa Wafanyabiashara (WABISOKO) uliofanyika katika viwanja vya Mashujaa, Manispaa ya Mtwara Mikindani, wafanyabiashara hao wamesema mkutano huo umewezesha kutoa taarifa za maendeleo ya ushirika pamoja na changamoto zinazowakabili.

Akielezea hali ya tozo wanazokutana nazo wanapoingiza bidhaa ndani ya manispaa, Selemani Kadege amesema kuwa endapo serikali haitapitia upya ushuru unaotozwa, bidhaa zitaendelea kuwa ghali na hivyo kumuumiza mlaji wa mwisho.


Sauti ya Selemani Kadege, mfanyabiashara Soko Kuu Mtwara

Kwa upande wake, Asha Abilahi, mfanyabiashara wa Soko la Chuno, amesema kuwa wamekuwa wakitozwa ushuru katika vizuizi vya barabarani, ambapo baadhi ya watendaji hawatoi risiti, hali ambayo imekuwa kero kwao. Ameiomba serikali kufuatilia suala hilo kwa umakini zaidi.


Sauti ya 1 Asha Abilahi, mfanyabiashara Soko la Chuno

Aidha, Bi. Asha ameiomba serikali kuhakikisha wafanyabiashara wakubwa wa vyakula, minada na nguo wanapelekwa Soko la Chuno ili kulihuisha na kuongeza mzunguko wa biashara, badala ya wafanyabiashara kufanyika nje ya eneo la soko hilo.


Sauti ya 2 Asha Abilahi, mfanyabiashara Soko la Chuno

Akitoa ufafanuzi kuhusu tozo hizo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, Rugembe Maiga amesema kuwa ushuru unaotozwa unatokana na sheria iliyopitishwa kwa kuzingatia taratibu. Ameongeza kuwa iwapo kuna malalamiko au changamoto, manispaa ipo tayari kukaa na wafanyabiashara kupitia maeneo yenye matatizo.

Amesisitiza kuwa kwa sasa sheria tayari imetungwa, hivyo wafanyabiashara wanapaswa kuendelea kulipa kodi, ada na ushuru kwa viwango vilivyowekwa mpaka pale maboresho yatakapofanyika na kupitishwa na mamlaka husika.

Sauti ya Rugembe Maiga Mwakilishi wa mkurugenzi Manispaa ya Mtwara Mikindani
Share:

Mtwara kutenga milioni 500 kuboresha Soko Kuu

 

Bw. Rugembe Maiga akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya Manspaa ya Mtwara Mikindani katika mkutano wa WABISOKO(picha na Musa Mtepa)

Manispaa ya Mtwara–Mikindani imetangaza mpango wa kutenga zaidi ya shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuboresha Soko Kuu la Mtwara, ikilenga kuboresha miundombinu na mazingira ya biashara huku wafanyabiashara wakiyakaribisha maboresho hayo na kuomba kupewa kipaumbele baada ya ujenzi kukamilika

Na Musa Mtepa

Zaidi ya shilingi milioni 500 zinatarajiwa kutengwa kwa ajili ya kuanza mchakato wa uboreshaji wa ujenzi wa Soko Kuu la Mtwara, hatua inayolenga kuwawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao katika mazingira bora na yenye hadhi inayolingana na Manispaa ya Mtwara–Mikindani.

Akimwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara–Mikindani kwenye mkutano wa Ushirika wa Wafanyabiashara wa Soko Kuu (WABISOKO) uliofanyika Novemba 15, 2025 katika Viwanja vya Mashujaa, Bw. Rugembe Maiga amesema kuwa pamoja na jitihada nyingi zilizofanywa na serikali, bado wanatambua kuwa soko hilo ni chakavu na linahitaji maboresho ili liendane na hadhi ya manispaa.

Sauti ya Rugembe Maiga, mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara–Mikindani

Aidha, Bw. Rugembe amesema kuwa mbali na mipango ya ujenzi mpya, tayari wameanza kushughulikia baadhi ya changamoto zilizokuwa zikiwakabili wafanyabiashara ikiwemo uboreshaji wa huduma za choo, maeneo ya kufanyia biashara pamoja na mitaro ya kupitisha maji.

Sauti ya Rugembe Maiga, mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara–Mikindani

Wakizungumzia mpango huo, wafanyabiashara wa soko hilo, Selemani Kadege na Ramadhani Mtumba, wameishukuru serikali kwa hatua hizo za maboresho, huku wakitoa ombi la kupewa kipaumbele wafanyabiashara waliopo sasa mara baada ya ujenzi kukamilika.


Sauti ya Selemani Kadege na Ramadhani Mtumba – Wafanyabiashara
Share:

DC Mtwara awataka wajasiriamali kuwajibika kwa mikopo

 

DC Mwaipaya akizungumza na wajasiliamali na wafanyabiashara wa soko kuu mtwara wakati wa mkutano wa WABISOKO katika viwanja vya Mashujaa jana November 15,2025 (Picha na Musa Mtepa)

Mkuu wa Wilaya Abdala Mwaipaya amesisitiza uwajibikaji huo kwenye mkutano wa WABISOKO na kuwapongeza wafanyabiashara kwa kudumisha amani na kuwasilisha changamoto zao kwa utulivu. Makamu Mwenyekiti Rashidi Johana amewasilisha maendeleo na changamoto za ushirika.

Na Musa Mtepa

Wajasiriamali wametakiwa kutimiza wajibu wao katika kufanikisha upatikanaji na urejeshaji wa mikopo inayotolewa na serikali kupitia benki washirika, ili kuwezesha watu wengine kunufaika na huduma hiyo.

Kauli hiyo imetolewa Novemba 15, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Abdala Mwaipaya, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Ushirika wa Wafanyabiashara wa Soko Kuu Mtwara (WABISOKO) uliofanyika katika viwanja vya Mashujaa, Manispaa ya Mtwara–Mikindani.

Mwaipaya amesema kuwa serikali inatekeleza wajibu wake, lakini ni muhimu kwa wajasiriamali kama walengwa wa mikopo hiyo kuhakikisha wanatimiza masharti na vigezo vinavyohitajika ili kupata na kurejesha mikopo ipasavyo.

Sauti ya 1: Abdala Mwaipaya, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara

Aidha, DC Mwaipaya ametumia nafasi hiyo kuwashukuru wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kwa kudumisha amani na utulivu katika kipindi cha uchaguzi mkuu uliopita. Pia amewapongeza viongozi wa jumuia hiyo kwa kuwa watulivu na kuwasilisha changamoto zao bila kuanzisha vurugu au fujo.

Sauti ya 2: Abdala Mwaipaya, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Ushirika wa Wafanyabiashara wa Soko Kuu Mtwara (WABISOKO), Bw. Rashidi Issa Johana, amesema kuwa dhamira kuu ya mkutano huo ni kuwapa wanachama taarifa ya maendeleo tangu viongozi wa sasa walipochukua madaraka, pamoja na changamoto na mafanikio yaliyopatikana.

Sauti ya Rashidi Issa Johana, Makamu Mwenyekiti WABISOKO
Wajasiliamali wakiwa kwenye mkutano wa WABISOKO (Picha na Musa Mtepa)
Share:

PPRA yatoa mafunzo kwa makundi maalumu Mtwara

 

Makundi maalumu washiriki wa mafunzo yaliyotolewa na PPRA November 12,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Benjamini Mkapa kilichokuwa chuo cha ualimu Mtwara wakifuatilia kwa umakini mafunzo hayo(Picha na Musa Mtepa)

PPRA imeendesha mafunzo kwa makundi maalumu mkoani Mtwara kuhusu taratibu za ununuzi wa umma, yakilenga kuongeza uelewa na ushiriki wao katika zabuni za serikali. Mafunzo hayo yamezinduliwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Bahati Geuzye, na yataendelea hadi Desemba katika halmashauri zote za mkoa

Na Musa Mtepa

Mtwara, Novemba 12, 2025Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imeendesha mafunzo maalumu kuhusu taratibu za manunuzi ya umma kwa makundi maalumu yakiwemo watu wenye ulemavu, kwa lengo la kuongeza uelewa na ushiriki wao katika zabuni za serikali.

Akifungua mafunzo hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Bi. Bahati Geuzye, amesema mafunzo hayo ni fursa muhimu na ya kipekee kwa wadau kutoka makundi maalumu kujifunza kuhusu sheria, kanuni na taratibu za ununuzi wa umma.

Sauti ya 1 – Bi. Bahati Geuzye, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara
Katibu tawala mkoa wa Mtwara Bi Bahati Geuzye akikibidhi hati ya TRA kwa wajasiliamali wakati wa mafunzo ya PPRA (Picha Musa Mtepa)

Aidha, Bi. Geuzye amesema zaidi ya asilimia 70 ya bajeti ya serikali hutumika kwenye ununuzi wa umma, hivyo ni muhimu kwa wananchi wote wenye sifa kushiriki na kunufaika na miradi ya maendeleo kupitia mfumo rasmi wa serikali.

Sauti ya 2 – Bi. Bahati Geuzye, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara

Kwa upande wake, Afisa Ununuzi kutoka PPRA, Bw. Magnus Steven, amesema mafunzo hayo yalianza Novemba 10, 2025, na yataendelea hadi mwezi Desemba katika halmashauri zote za Mkoa wa Mtwara.

Sauti ya 1 – Magnus Steven, Afisa PPRA
Afisa Ununuzi kutoka PPRA, Bw. Magnus Steven akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya mafunzo hayo(Picha na Musa Mtepa)

Bw. Steven ameongeza kuwa lengo ni kujenga uelewa na kuimarisha uaminifu kati ya makundi maalumu na serikali, ili waweze kushiriki kikamilifu na kunufaika na zabuni mbalimbali.

Sauti ya 2 – Magnus Steven, Afisa PPRA

Washiriki wa mafunzo hayo wamesema wamepata uelewa mkubwa kuhusu namna zabuni za serikali zinavyotangazwa na nafasi ya watu wenye ulemavu katika mchakato huo, huku wakiahidi kuwa mabalozi wa kutoa elimu zaidi kwa jamii.

Sauti ya washiriki wa mafunzo
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>