• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

DAR ES SALAAM: Rais Magufuli Katengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba la Taifa(NHC)

Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Blandina Nyoni na kuivunja bodi hiyo. katika taarifa hiyo iliyotolewa leo ikulu jijini dar es salaam haijaeleza sababu za kuvunja Bodi hiyo na kutengua nafasi ya Mkurugenzi huyo. Uteuzi wa Mwenyekiti na bodi nyingine utafanyika baadaye.
Share:

DAR ES SALAAM: Mei Mosi Kitaifa Kufanyika Jijini Arusha....Mgeni Rasmi Anatarajiwa Kuwa Rais Magufuli

Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (Tuico), kimeanza maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei mosi), yanayotarajiwa kufanyika kitaifa mkoani Arusha.

Mwenyekiti wa Tuico taifa, Paulo Sangeze, alisema, mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Rais John Magufuli.

Akizungumza katika semina ya kuelimisha na kubadilishana uzoefu, iliyowashirikisha viongozi wa matawi mbalimbali ya  Tuico mwishoni mwa wiki, iliyofanyika jijini hapa, Mwenyekiti wa Tuico taifa, Sangeze, alisema Shirikisho la Vyama vya Huru vya Wafanyakazi nchini (Tucta), limekiteua chama chao kuwa mratibu wa shughuli zote za Mei mosi kwa mwaka huu.

Alisema baada ya kupewa fursa hiyo wanafanya vikao vya maandalizi na tayari wamepanga maadhimisho hayo kwa mwaka huu, yatafanyika mkoani Arusha katika Uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid.

Katibu wa Tuico, Boniface Nkakatisi, alisema maandalizi hayo yanaenda na mialiko ya wageni watakaohudhuria ikiwamo wafanyakazi mbalimbali nchini, wanachama  wa Tuico, mabalozi kutoka nchi mbalimbali duniani.
Share:

DAR ES SALAAM: RC Makonda atoa taarifa kuhusu tukio la kushambuliwa kwa afisa ubalozi wa Syria

TAARIFA YA MKUU WA MKOA DAR ES SALAAM KUHUSU TUKIO LA KUSHAMBULIWA KWA AFISA UBALOZI WA SYRIA.
Kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar Es Salaam nimeshtushwa na taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Afisa Ubalozi wa Syria ameshambuliwa na kuporwa kiasi kikubwa cha fedha leo mchana Jijini Dar Es Salaam. Taarifa hiyo imeenda mbali zaidi na kusema kwamba Dar Es Salaam sio salama na kueleza watu wawe makini zaidi.

Nawaomba sana wananchi wa Dar es Salaam muendelee kuwa watulivu na mkielewa kwamba Mkoa wenu ni salama salama sana. Vyombo vya usalama vinalifanyia kazi tukio hili na taarifa za awali nilizopokea zinaonyesha tukio hili linaweza kuwa limepangwa na watu wa ndani. Tunafuatilia zaidi kujua kwa nini Afisa huyo hakuomba ulinzi wa polisi akiwa amebeba kiasi hicho kikubwa cha fedha na pia kwa nini dereva wake amekimbia.

Kwa hali ilivyo mpaka sasa kuna uwezekano ikawa ni tukio la kupangwa na watu wa ndani. Hatutaruhusu watu wachache wachafue taswira ya Mkoa wetu.

Uchunguzi ukifikia sehemu nzuri taarifa rasmi itatolewa na vyombo vyetu vya usalama. Ulinzi na usalama wa wananchi wetu ni muhimu sana.

Mh. Paul Makonda
Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam
Share:

IRINGA: Hatimaye Abdul Nondo amefikishwa Mahakamani

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo amesafirishwa usiku wa kuamkia leo Machi 21, 2018 kupelekwa mkoani Iringa.

Taarifa zilizotolewa na wakili wake, Jebra Kambole leo Jumatano Machi 21, 2018 zinaeleza kuwa sasa Nondo yupo Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa.

Nondo anadaiwa kutoweka katika mazingira ya kutatanisha Machi 6, 2018 na siku inayofuata akaonekana mjini Mafinga, wilayani Mufindi, Iringa ambako alishikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo na baadaye kurejeshwa Dar es Salaam.

Tangu akamatwe Nondo hajawahi kuzungumza na wakili wake wala mtu yeyote wa karibu yake jambo ambalo limekuwa likipingwa na watetezi wa haki za binadamu.

Jana, Jebra alisema kuwa wamefungua kesi kwa ajili ya kuiomba mahakama mambo matatu, kwanza kumpa dhamana Nondo, pili kutoa amri ya kuwapa mawakili haki ya kuonana na Nondo na kingine ni kuitaka mahakama itamke mwanafunzi huyo wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) ameshikiliwa  kinyume cha sheria.
Share:

MTWARA: Madiwani watatu wamuunga Mkono Rais Magufuli kwa kuhama chama


Madiwani Watatu wa kata za Nalingu Shaibu Mtavanga (CUF), Muungano HASSAN HASSAN LIKUTU (CHADEMA) na nanguruwe ERISHA WALLA (CUF, ) kutoka halmashauri ya mtwara vijijini Mkoani MTWARA, wamejiuzulu nyadhifa zao na kujiunga na chama cha Mapinduzi (CCM) .
Madiwani hao kwa pamoja wameamua kujiunga na chama cha mapinduzi (ccm) ili kuunga mkono juhudi za Rais John Pombe Magufuri.
Wakiongea wa Nyakati tofauti wamethibitisha kuwa wameamua wenyewe bila kushurutishwa wala kurubuniwa na mtu yeyote.
Katibu mwenezi wa wilaya Mtwara vijijini  SELEMANI SANKWA amethibitisha kuwapokea madiwani hao mbele ya waandishi wa habari  hapo jana.
Share:

Miili ya watu wawili yaokotwa katika mto Arusha

Watu wawili ambao ni wanandoa wamefariki dunia katika Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha baada ya kuchukuliwa na mafuriko katika mto Piyaya Kata ya Piyaya wilayani humo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Yusuph Ilembo amesema miili hiyo imeonekana leo majira ya asubuhi baada ya maji ya mto huo wa msimu kupungua.

Aidha, Kamanda Ilembo amewataja marehemu hao kuwa ni Ormins Sunguyo na mkewe Nembris Sunguyo ambao walikuwa na mtoto wa mdogo aliyefahamika kwa jina la Oloosukuta Sunguyo ambaye alinusurika kifo.

Kamanda Ilembo alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi katika mkoa wa Arusha kuchukua tahadhari kipindi hiki cha mvua na kuepuka kuvuka mito wakati maji yanafurika.
Share:

BINA ameitaka TBS kuchunguza kemikali bandia wanazouziwa Wachimbaji wadogo

Serikali kupitia Shirika la Viwango nchini, TBS limetakiwa kuchunguza kemikali bandia zinazouzwa na wafanyabiashara wasio waaminifu kwa wachimbaji wadogo wa madini hali inayosababisha hasara kwa wachimbaji hao.

Rais wa Shirikisho la wachimbaji wadogo wa madini nchini, (FEMATA) Bw John Bina amesema hayo baada ya kikao kilichowakutanisha wachimbaji wadogo Mkoani Geita kwa lengo la kujadili namna Serikali inavyoweza kufanikisha ujenzi wa soko la madini kwa kanda ya ziwa.

Alisema baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakiuza kemikali bandia kwa wachimbaji wadogo na hivyo kuwasababishia hasara.“Tunaomba serikali na TBS kuangalia sanaa haya madawa ambayo yanaingia nchini kuhakikisha wanachunguza kemikali hizi kwani kwa sasa uzalishaji unashuka kwa kiasi kikubwa wa madini ,na nyie wachimbaji niwaombe muwe mnachunguza kabla ya kununua kwani kweli mnaingia hasara kubwa sanaa”Alisisitiza Bina.

Mmoja wa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu Bw Nuru Shabani alisema kwa kuuziwa Kemikali hizo bandia amekuwa akiathirika katika shughuli zake.“Kiukweli tunaathirika sanaa na hili halina ubisha sasa hivi unaweza kununua tani moja ya kaboni unakuta inapitisha bila ya kushika mali inamaana hadi iwe na pipim kuanzia mia saba hadi mia nane ,Ila kwa sasa nashukuru walau serikali imetambua mchango wetu na imetuthamini mimi nilikuwa naomba kupitia Kitengo chetu tuwe na wasimamizi ambao watatusaidia kubaini kemikali hizi”Alisema Nuru.

Bw John Bina ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya kushughulikia kero za wachimbaji wadogo alisema pamoja na matatizo hayo lakini wachimbaji hao wamekubaliana kuanzishwa kwa soko la madini Mkoani Mwanza ili kudhibiti vitendo vya utoroshwaji wa madini.
Share:

DAR ES SALAAM: Hospitali ya Temeke yathibitisha kumpokea kijana aliyejeruhiwa kwa risasi

Siku moja baada ya Mwananchi kuripoti habari ya Alex Suke (18) anayedaiwa kupigwa risasi na polisi waliokuwa wakituliza vurugu eneo la Buguruni Relini Ijumaa iliyopita, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa Temeke Dk Amani Malima, amethibitisha kumpokea kijana huyo.

Akizungumza jana na mwandishi wetu, Dk Malima alisema madaktari wanaendelea kumpatia matibabu na kubainisha kuwa juzi alishindwa kuthibitisha tukio hilo kwa maelezo kuwa hakuwepo ofisini, “Yupo wodi namba saba lakini kamuone Dk Mwita ambaye yuko zamu atakupa ushirikiano,”alisema.

Mwananchi lilipowasiliana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Emmanuel Lukula kwa njia ya simu alisema, “hilo suala ni la zamani sana wewe ndo unaulizia leo? Kwa sasa nipo nje ya ofisi nitakutafuta baadaye kidogo.”

Awali, mwandishi wetu alimtafuta Dk Mwita ambaye alikuwa zamu katika wodi namba saba alikolazwa kijana huyo.

Baada ya kufika wodini hapo saa saba mchana alishuhudia madaktari wakifanya maandalizi kwa ajili ya kumpeleka kijana huyo kwenye chumba cha upasuaji jambo lililozuia mahojiano wakati huo.

Mwandishi wetu aliweka kambi kwa muda hospitalini hapo kwa ajili ya kuzungumza na daktari huyo na kujibiwa na wasaidizi wake kuwa ana majukumu mengi, si rahisi kupata muda wa kuzungumza na mwanahabari.

Mama wa kijana huyo, Aghata Mwangamba alisema madaktari walimueleza kuwa mwanae atafanyiwa upasuaji wa mkono ambao ulijeruhiwa kwa risasi huku akilalamikia mzigo wa gharama za matibabu. “Leo (jana) analalamika sana mkono tofauti na jana (juzi) na madaktari wameniambia leo (jana) watamfanyia upasuaji mwingine wa mkono ambao ulijeruhiwa na risasi,” alisema.

Alisema wameiomba Serikali iwasaidie katika matibabu kwani hadi sasa ametumia Sh900,000 katika matibabu.

“Mtoto wangu hana bima na mimi ni mjane gharama ni kubwa na uwezo wangu kwa sasa umekuwa mdogo,” alisema mama huyo na kubainisha kuwa anategemea genge kuendesha maisha yake.

Bibi wa kijana huyo, Subira Mwakajila alisema familia imepata pigo kwa kujeruhiwa kijana huyo, “Sisi hatuoni haja ya kupelekana mahakamani lakini tunataka kujua hatma ya kijana wetu kiafya na kimasomo,”alisema.

Kijana huyo alipigwa risasi wakati polisi wakiwatawanya watu maeneo ya Buguruni Relini Ijumaa iliyopita.

Juzi baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo akiwamo Juma Liwanje walieleza kuwa kijana huyo alipigwa risasi kutokana na vurugu zilizotokea eneo la Buguruni Relini baada ya askari kufyatua risasi kuwatawanya watu wakiwamo madereva bodaboda.
Share:

DAR ES SALAAM: Mbarawa asema ujenzi reli ya kisasa kutoka Dar-Moro umefikia asilimia tisa

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro umefikia asilimia tisa, utakamilka baada ya miezi 30.

Akizungumza leo Machi 14, 2018 katika uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro hadi Makutopora mkoani Dodoma, Mbarawa amesema ujenzi kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro utakamilika Novemba 2019.

“Reli iliyopo sasa ya upana wa mita moja miundombinu yake imechoka sana treni huenda kwa kasi ya Kilometa 30 kwa saa. Rais (John Magufuli) ninaomba nikuhakikishie kuwa wizara ya ujenzi itaendelea kuwasimamia wakandarasi,” amesema.

“Tutahakikisha wakandarasi wanamaliza kazi ya ujenzi wa reli hii kwa wakati na kuhakikisha ubora. Hivi ninavyokuambia wakandarasi wanafanya kazi usiku na mchana kwa siku saba kwa wiki.”
Chanzo: muungwana
Share:

DAR ES SALAAM: Rais Magufuli asema Wananchi kulipa kodi isiwe kero kwao

Rais John Magufuli amesema wananchi kulipa kodi isiwe kero kwao, bali heshima na kuitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwa makini.

Akizungumza leo Machi 14, 2018 mjini eneo la Ihumwa nje kidogo ya Mkoa wa Dodoma wakati akizindua ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro hadi Makutopora, Rais Magufuli amesema baadhi ya kodi wananchi hukwepa kulipa kodi kutokana na namna zinavyotozwa na viwango kuwa juu.

“Kuna watu TRA siyo wazuri, Kamishna wa TRA na Waziri wa Fedha  shughulikieni hili. Mtu kulipa kodi isiwe ni kero bali heshima,” ameagiza.

Kuhusu ujenzi wa reli hiyo, Rais Magufuli amesema katika awamu zote za ujenzi itagharimu Sh15 trilioni.

“Ukiachilia mbali mradi huu, Serikali itaendelea kutekeleza miradi mingine ya miundombinu. Hapa Dodoma tunajenga barabara za mizungumko, kazi ya designing (usanifu) inafanyika na itakuwa kwa kiwango cha lami ili kweli Dodoma ionekane makao makuu ya nchi,” amesema.
Chanzo: muungwana
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>