Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imesema mwanzoni mwa mwezi machi hadi mei mwaka huu, mvua za wastani na za masika zinatarajiwa kunyesha.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, ambapo ameeleza mwelekeo wa mvua katika kipindi cha msimu wa masika.
Ametaja maeneo ambayo mvua hizo zinatarajiwa kuanza kunyesha mwanzoni mwa mwezi Machi, ikiwemo Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Unguja, Pemba na Uakanda wa Pwani ya Kaskazini.
Dkt. Kijazi amezitaka sekta mbalimbali kuchukua tahadhari kwa kujiandaa vyema na kuutumia utabiri huo, kwa kuwa mvua hizo zitaleta athari kutokana na vipindi vifupi vya mvua kubwa vinavyoweza kusababisha mafuriko.
Pia, ametaka wananchi kutumia kipindi hicho vizuri kwa kufanya kilimo na usalama wa mifugo, wanayammapori na chakula.







No comments:
Post a Comment