Jeshi la Polisi limesema siku ya uchaguzi wa mdogo wa ubunge kwa jimbo la Kinondoni kutakuwa na ulinzi mkali ili kuhakikisha mchakato wote wa masuala ya uchaguzi unafanyika katika misingi ya sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi.
Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, RPC Jumanne Mlilo wakati akizungumza na wanahabari.
“Rai ya Jeshi la Polisi kwa wananchi ni kujitokeza kwa wingi siku hiyo ili wawekutekeleza haki yao ya kikatiba kwa kufuata sheria na taratibu watakazoelekkezwa siku hiyo na wahusika wa uchaguzi bila kuleta vurugu au wao kuwa chanzo cha vurugu,” amesema.
RPC Mlilo amesema, siku hiyo kila kituo cha kupigia kura kitakuwa na polisi wa kawaida na wa FFU, kutakuwa na maji ya washawasha, huku doria ikifanyika kila sehemu itayoongozwa na askari maalumu wa kushughulikia waleta fujo.
“Jeshi halitasita kuchukua hatua za haraka za kisheria kwa mtu yeyote au kikundi chochote chenye nia ya kufanya vitendo vyovyote ambavyo ni kinyume na kanuni au sheria ya uchaguzi,” amesema.







No comments:
Post a Comment