• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

PPRA yatoa mafunzo kwa makundi maalumu Mtwara

 

Makundi maalumu washiriki wa mafunzo yaliyotolewa na PPRA November 12,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Benjamini Mkapa kilichokuwa chuo cha ualimu Mtwara wakifuatilia kwa umakini mafunzo hayo(Picha na Musa Mtepa)

PPRA imeendesha mafunzo kwa makundi maalumu mkoani Mtwara kuhusu taratibu za ununuzi wa umma, yakilenga kuongeza uelewa na ushiriki wao katika zabuni za serikali. Mafunzo hayo yamezinduliwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Bahati Geuzye, na yataendelea hadi Desemba katika halmashauri zote za mkoa

Na Musa Mtepa

Mtwara, Novemba 12, 2025Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imeendesha mafunzo maalumu kuhusu taratibu za manunuzi ya umma kwa makundi maalumu yakiwemo watu wenye ulemavu, kwa lengo la kuongeza uelewa na ushiriki wao katika zabuni za serikali.

Akifungua mafunzo hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Bi. Bahati Geuzye, amesema mafunzo hayo ni fursa muhimu na ya kipekee kwa wadau kutoka makundi maalumu kujifunza kuhusu sheria, kanuni na taratibu za ununuzi wa umma.

Sauti ya 1 – Bi. Bahati Geuzye, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara
Katibu tawala mkoa wa Mtwara Bi Bahati Geuzye akikibidhi hati ya TRA kwa wajasiliamali wakati wa mafunzo ya PPRA (Picha Musa Mtepa)

Aidha, Bi. Geuzye amesema zaidi ya asilimia 70 ya bajeti ya serikali hutumika kwenye ununuzi wa umma, hivyo ni muhimu kwa wananchi wote wenye sifa kushiriki na kunufaika na miradi ya maendeleo kupitia mfumo rasmi wa serikali.

Sauti ya 2 – Bi. Bahati Geuzye, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara

Kwa upande wake, Afisa Ununuzi kutoka PPRA, Bw. Magnus Steven, amesema mafunzo hayo yalianza Novemba 10, 2025, na yataendelea hadi mwezi Desemba katika halmashauri zote za Mkoa wa Mtwara.

Sauti ya 1 – Magnus Steven, Afisa PPRA
Afisa Ununuzi kutoka PPRA, Bw. Magnus Steven akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya mafunzo hayo(Picha na Musa Mtepa)

Bw. Steven ameongeza kuwa lengo ni kujenga uelewa na kuimarisha uaminifu kati ya makundi maalumu na serikali, ili waweze kushiriki kikamilifu na kunufaika na zabuni mbalimbali.

Sauti ya 2 – Magnus Steven, Afisa PPRA

Washiriki wa mafunzo hayo wamesema wamepata uelewa mkubwa kuhusu namna zabuni za serikali zinavyotangazwa na nafasi ya watu wenye ulemavu katika mchakato huo, huku wakiahidi kuwa mabalozi wa kutoa elimu zaidi kwa jamii.

Sauti ya washiriki wa mafunzo
Share:

Wakulima waomba bei bora zaidi ya Korosho

 

Viongozi wa Bodi ya Korosho,TANECU na Serikali wakiwa katika uzinduzi wa rasmi wa mnada wa Korosho msimu wa 2025/2026 katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Tandahimba (Picha na Musa Mtepa)

Wakulima wa korosho wilayani Tandahimba wamepokea kwa mitazamo tofauti bei ya zao hilo katika mnada wa kwanza wa msimu 2025/2026, ambapo kilo moja imenunuliwa kwa bei ya juu ya shilingi 3,520 na ya chini shilingi 2,550, huku wakitaka wanunuzi kuongeza bei ili kuendana na gharama za uzalishaji

Na Musa Mtepa

Wakulima wa zao la korosho wamepokea kwa mitazamo tofauti bei ya zao hilo kupitia mnada wa kwanza uliofanyika tarehe 8 Novemba 2025, wilayani Tandahimba, mkoani Mtwara. Katika mnada huo, bei ya juu kwa kilo moja ya korosho imeuzwa kwa shilingi 3,520 na kwa shilingi 2,550 kwa bei ya chini.

Mnada huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba, kupitia Chama Kikuu cha Ushirika cha Tandahimba na Newala (TANECU), ambapo zaidi ya tani 26,000 za korosho zimeuzwa.

Wakulima wameishukuru serikali na vyama vya ushirika kwa kufanikisha mnada huo, huku wakitoa wito kwa wanunuzi kuongeza bei ya korosho ili iendane na gharama kubwa za uzalishaji wa zao hilo.

Sauti ya wakulima wa korosho wilayani Tandahimba
Wakulima wa zao Korosho wakifuatilia mwenendo wa soko la korosho katika mnada wa kwanza wa uzinduzi wa msimu wa korosho nchini uliofanyika wilayani Tandahimba(Picha na Musa Mtepa)

Bi. Tatu Mahupa mkulima wa korosho amefurahi kufanyika kwa mnada huo huku akiwataka wakulima kutumia vizuri fedha watakazopata kutokana na mauzo ya korosho, kwa kuweka bajeti nzuri ya matumizi na kuepuka matumizi yasiyo ya lazima, ili ziweze kusaidia katika mahitaji muhimu ya familia ikiwemo elimu ya watoto.

Sauti ya Tatu Mahupa, mkulima wa korosho, Mchichira.

Akiongoza mauzo katika mnada huo, Mwenyekiti wa TANECU Ltd, Karim Chipola, amewapongeza wakulima kwa mwitikio wao mkubwa. Amesema kati ya tani 26,000 na kilo 254 zilizouzwa, Tandahimba imechangia tani 18,102 na Newala tani 8,152, zikiuzwa kwa bei ya juu ya shilingi 3,520 na bei ya chini shilingi 2,550 kwa kilo.

Sauti ya Karim Chipola, Mwenyekiti wa TANECU.
Mwenyekiti wa TANECU,Ltd akizungumza na wakulima waliojitokeza kwenye mnada huo(Picha na Musa Mtepa)

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), Bw. Godfrey Marekano, amesema matarajio yao ni kuona idadi ya wanunuzi inaongezeka katika minada inayofuata ili kuongeza ushindani na hatimaye kuinua bei ya korosho kwa manufaa ya wakulima.

Sauti ya Godfrey Marekano, Afisa Mtendaji Mkuu wa TMX.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Ndugu Frances Alfred, amesema mnada huo ni wa kwanza kitaifa kwa msimu wa 2025/2026, na ndio unaoashiria mwenendo wa soko la kimataifa la korosho kwa mwaka huu.

Sauti ya – Frances Alfred, Mkurugenzi Mkuu wa CBT
Share:

Makala: mabinti wa Mtwara wavunja ukimya

Bi Thea Swai akizungumza katika moja ya vikao vya wadau. Picha na Mwanahamisi Chikambu

“Wasichana wanajifunza kwamba sauti yao ina thamani, na kwamba wao pia wana nafasi muhimu katika jamii hasa mabinti wa Mtwara”

Na Mwanahamisi Chikambu

Katika dunia ya sasa inayokua kwa kasi kutokana na maendeleo ya teknolojia, bado mtoto wa kike wa Kiafrika anakabiliwa na vikwazo vingi vinavyomnyima nafasi ya kuonekana, kusikika, na kushiriki kikamilifu katika maamuzi yanayohusu maisha yake.

Lakini mkoani Mtwara, hali inaanza kubadilika, Sauti za wasichana zinapata nguvu mpya kupitia mradi wa Binti Paza Sauti (Girls Speak Out) mpango unaolenga kuwajengea uwezo mabinti kujieleza, kushiriki katika maamuzi, na kuvunja ukimya kuhusu changamoto zinazowakabili kila siku kupitia michezo

Kupitia mradi huu, wasichana wanajifunza kwamba sauti yao ina thamani, na kwamba wao pia wananafasi muhimu katika jamii, Karibu katika makala haya, tujifunze kwa pamoja namna ambavyo mabinti wa Mtwara.

Bonyeza hapa kusikiliza

Share:

CBT yaruhusu usafirishaji wa korosho Saa 24

 

Gari lililobeba Korosho kutoka vya vya ushirika likishusha katika Ghala kuu tayari kwa ajili ya Mnada (Picha Kwa Msaada wa Mtandao)

Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) imeruhusu usafirishaji wa korosho saa 24 kwa mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara ili kuharakisha uondoaji wa mizigo na kuongeza ufanisi wa Bandari ya Mtwara. Katika mnada wa kwanza, TANECU iliuza tani 26,000 kwa bei ya juu ya Sh. 3,520 kwa kilo

Na Musa Mtepa

Tandahimba-Mtwara, Novemba 8, 2025 Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) imeruhusu magari yote yanayosafirisha korosho kutoka mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara kufanya usafirishaji wa korosho masaa 24, usiku na mchana.
Hata hivyo, mikoa mingine itaendelea kusafirisha korosho kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa 12 jioni kama kawaida.

Hatua hiyo inalenga kuharakisha uondoaji wa mizigo kwenye maghala makuu ili kutoa nafasi kwa korosho nyingine za wakulima kuingia ghalani kwa ajili ya minada inayofuata.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi rasmi wa msimu wa minada wilayani Tandahimba, Mkurugenzi Mkuu wa CBT, Ndugu Frances Alfred, amesema kuwa ruhusa hiyo inahusisha mikoa inayosafirisha korosho kupitia Bandari ya Mtwara au maghala makuu yaliyopo mjini Mtwara.

Sauti ya Frances Alfred – Mkurugenzi Mkuu wa CBT

Aidha, Ndugu Frances amesema kuwa sababu kubwa ya kutoa ruhusa hiyo ni kuhakikisha korosho zinatoka kwa haraka katika maghala makuu ili korosho nyingine za wakulima ziweze kuingizwa kwa ajili ya minada inayofuata.
Ameeleza kuwa hatua hiyo pia inalenga kuongeza mzunguko wa malori, kuboresha ufanisi wa Bandari ya Mtwara katika kurahisisha usafirishaji wa korosho nje ya nchi, pamoja na kuwavutia wanunuzi zaidi kushiriki katika minada mingine ijayo ya zao hilo.

Sauti ya Frances Alfred Mkurugenzi wa CBT
Mkurugenzi mkuu wa CBT ndugu Frances Alfred akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kufanyika kwa mnada wa Kwanza 2025/2026 uliofanyika wilayani Tandahimba ,mkoani Mtwara.(Picha na Musa Mtepa)

Novemba 8, 2025, mnada wa kwanza wa zao la korosho umefanyika katika wilaya ya Tandahimba, ambapo Chama Kikuu cha Ushirika cha Tandahimba na Newala (TANECU Ltd) kimefanikiwa kuuza korosho tani 26,000 na kilo 254.

Bei ya juu katika mnada huo ilikuwa shilingi 3,520 kwa kilo, huku bei ya chini ikiwa shilingi 2,550 kwa kilo.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa TANECU, Ndugu Karim Chipola, katika jumla hiyo ya korosho zilizouzwa, Tandahimba imechangia tani 18,102, huku Newala ikichangia tani 8,152.

Share:

Wadau wanashiriki vipi kutatua changamoto za watu wenye ulemavu

 

Wadau wenye ulemavu wakiwa katika mafunzo. Picha na Mwnahamisi Chikambu

Tutahakikisha elimu jumuishi inatekelezwa kwa vitendo ili kutatua changamoto zinazowakabili wanafunzi wenye ulemavu na kuboresha kiwango cha elimu mkoani Mtwara

Na Msafiri Kipila

Shirika lisilo la kiserikali Sport Development Aid (SDA) kwa kushirikiana na Jamii FM, linaendelea kuhimiza jamii kuwashirikisha na kuwatambua watu wenye ulemavu katika juhudi za kutatua changamoto zinazowakabili.

Kupitia programu zake, SDA imetoa mafunzo maalum kwa baadhi ya watendaji na walimu wanaofundisha wanafunzi wenye ulemavu, ili wawe mabalozi wa kutoa elimu na kuibua uelewa katika jamii. Lengo ni kuwasaidia wale wanaowaficha watu wenye ulemavu majumbani, jambo linalowanyima haki zao za msingi kama vile elimu.

Kasimu Samuel Shabani, mwalimu wa Shule ya Sekondari Chekeleni iliyoko Mtwara Vijijini, amesema kuwa yeye kama mwalimu atahakikisha elimu jumuishi inatekelezwa kwa vitendo ili kutatua changamoto zinazowakabili wanafunzi wenye ulemavu na kuboresha kiwango cha elimu mkoani Mtwara.

Kwa upande wake, Jackline Mpunjo, Meneja Mradi wa SDA, amesema wameamua kuendesha mpango huo baada ya kubaini kuwa jamii nyingi bado hazijawatambua ipasavyo watu wenye ulemavu. Amesema ni muhimu kuwashirikisha kikamilifu ili waweze kutimiza malengo yao ya kila siku na kujenga jamii yenye usawa na fursa sawa kwa wote.

Bonyeza hapa kusikiliza Makala haya

Share:

CUF yaahidi maendeleo kwa Wananchi wa kata ya Madimba

 

Mgombea Ubunge katika Jimbo la Mtwara Vijijini Kupitia tiketi ya CUF Shamsia Azizi Mtamba akinadi sera mbele ya wananchi wa kata ya Madimba(Picha na Musa Mtepa)

Mgombea Ubunge wa Mtwara Vijijini kupitia CUF, Shamsia Azizi Mtamba, amewataka wananchi wa Kata ya Madimba kuendelea kumuamini na kumpa kura, akiahidi kuendeleza maendeleo na kulinda kura zao dhidi ya propaganda za kisiasa

Na Musa MtepaMtwara–Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini anaetetea nafasi hiyo kupitia tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Shamsia Azizi Mtamba, amewaomba wananchi wa Kata ya Madimba kutokufanya kosa la kumchagua mgombea mwingine zaidi yake.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo, Oktoba 27, 2025, katika Kijiji cha Madimba, Shamsia amewataka wananchi hao kuendelea kumuamini ili aweze kuendeleza juhudi za kuleta maendeleo katika kata hiyo.

Sauti ya Shamsia Mtamba, Mgombea Ubunge Jimbo la Mtwara Vijijini

Aidha, Shamsia ametumia nafasi hiyo kuwatoa hofu wananchi wa Madimba akisema kuwa amejipanga kulinda kura zake, huku akiwataka wananchi kupuuza propaganda zinazoenezwa na baadhi ya wanasiasa ya kuwa hata akishinda hatotangazwa.

Sauti ya Shamsia Mtamba, Mgombea Ubunge Jimbo la Mtwara Vijijini

Kwa upande wake, mgombea udiwani wa Kata ya Madimba kupitia tiketi ya CUF, Bashiru Mchamba, amewaomba wananchi wampe kura ili aweze kushirikiana nao katika kuleta maendeleo na ustawi wa kata hiyo.

Sauti ya Bashiru Mchamba, Mgombea Udiwani Kata ya Madimba

Wakizungumza kuhusu mwenendo wa kampeni, baadhi ya wananchi wa Kata ya Madimba wamesema baadhi ya wagombea wameonyesha kugusa changamoto zinazowakabili, zikiwemo miundombinu ya barabara, huduma za afya, elimu na upatikanaji wa maji safi.

Sauti ya Wananchi wa Kata ya Madimba
Share:

Hospitali ya kanda yaibua furaha Mtwara

 

Mwonekano wa mbele wa Hospitali ya Rufaa kanda ya Kusini iliyojengwa kata ya Mitengo Manispaa ya Mtwara Mikindani(Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa Mtwara wameishukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kujenga Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini, hatua iliyowapunguzia gharama na safari za kwenda Dar es Salaam kutafuta huduma za kibingwa, huku wakiiomba serikali kuendelea kuboresha huduma hizo kwa manufaa ya wananchi wa kusini

Na Musa Mtepa

Wananchi mkoani Mtwara wameishukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kuboresha huduma za afya kupitia Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini iliyojengwa katika Kata ya Mitengo, Manispaa ya Mtwara-Mikindani.

Wakizungumza Oktoba 25, 2025, wananchi hao wamesema kuwa kabla ya kujengwa kwa hospitali hiyo, walilazimika kusafiri umbali mrefu hadi Dar es Salaam kufuata huduma za kibingwa. Wameeleza kuwa kwa sasa wanapata huduma hizo karibu, jambo lililopunguza kwa kiasi kikubwa gharama za matibabu na usafiri.

Aidha, wameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya, hatua inayowanufaisha wakazi wa mikoa ya kusini pamoja na wananchi wa nchi jirani kupata huduma bora katika hospitali hiyo.

Sauti ya Wananchi wa Mtwara

Bi Hawa Mpai na Bi Hajrati Kuluthumu Mtonya, ambao ni miongoni mwa wagonjwa wanaopata matibabu katika hospitali hiyo, wameeleza kuridhishwa kwao na huduma zinazotolewa huku wakiiomba serikali kuendelea kuimarisha huduma za kibingwa ili kuwaondolea wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu.

Sauti ya Bi Hawa Mpai na Bi Hajrati Kuluthumu

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Dkt. Benedect Ngaiza, amesema Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini ina madaktari bingwa na madaktari bingwa wabobezi pamoja na vifaa tiba vya kisasa, ikiwemo vifaa vinavyopatikana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Amesema kuwa upatikanaji wa huduma hizo umewezesha wananchi wa mikoa ya kusini kupata matibabu bora bila kulazimika kusafiri hadi Dar es Salaam.

Sauti ya Dkt. Benedect Ngaiza – Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara
Chumba cha Dialysis kilichopo katika hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini (Picha na Musa Mtepa)
Share:

Dkt. Nanauka aahidi kuimarisha uchumi Mtwara

 

Mgombea Ubunge jimbo la Mtwara mjini Dkt Joel Nanauka akinadi sera zake mbele ya wananchi wa eneo la kokobichi ,kata ya Rahaleo Manispaa ya Mtwara Mikindani(Picha na Musa Mtepa)

Dkt. Joel Nanauka, mgombea ubunge Mtwara Mjini kwa tiketi ya CCM, ameahidi kuimarisha uchumi wa mji huo, kukuza ajira na kuwawezesha wajasiriamali endapo atachaguliwa. Pia amesisitiza utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo kwa kushirikiana na Serikali

Na Musa Mtepa

Mtwara, Oktoba 20, 2025 – Mgombea ubunge wa Jimbo la Mtwara Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Joel Nanauka, amewaahidi wananchi kuwa iwapo atachaguliwa kuwa Mbunge, atahakikisha anaweka kipaumbele katika kuimarisha uchumi wa mji huo ili kuongeza ajira na kipato kwa wakazi wake.

Akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika katika eneo la Kokobichi, Kata ya Rahaleo, Manispaa ya Mtwara Mikindani, Dkt. Nanauka amesema kuwa Ilani ya CCM inaelekeza utekelezaji wa miradi mikubwa inayotarajiwa kuifanya Mtwara kuwa kitovu cha uchumi wa ukanda wa kusini, na kusaidia hata nchi jirani kupitia huduma na bidhaa zitakazotokana na miradi hiyo.

Sauti ya Dkt. Joel Nanauka, mgombea ubunge Mtwara Mjini

Aidha, Dkt. Nanauka ameeleza kuwa akipewa dhamana ya kuwa Mbunge kwa miaka mitano ijayo, atahakikisha ofisi yake inakuwa na utaratibu maalum wa kuwawezesha wajasiriamali, hasa vijana na wanawake, kwa kuwapatia mafunzo, vifaa na elimu ya biashara ili kuongeza tija katika shughuli zao za kiuchumi.

Sauti ya Dkt. Joel Nanauka, mgombea ubunge Jimbo la Mtwara Mjini

Kwa upande wake, mgombea udiwani wa Kata ya Rahaleo, Ndugu Edward Kapwapwa, amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, bado kata hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo tatizo la mafuriko katika eneo la Nandope wakati wa masika, linalowasababishia wananchi usumbufu mkubwa.

Kapwapwa ameongeza kuwa tayari Serikali kupitia Manispaa ya Mtwara Mikindani imesaini mikataba ya TACTC kwa ajili ya ujenzi wa mifereji ya maji katika mitaa mbalimbali yenye changamoto, ikiwemo Nandope, ili kutatua tatizo hilo kwa njia ya kudumu.


Sauti ya Edward Kapwapwa, mgombea udiwani Kata ya Rahaleo

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Mtwara, Ndugu Mohamedi Abdala (Mudy Ray), amewahakikishia wananchi kuwa Dkt. Nanauka ni kiongozi mwenye moyo wa unyenyekevu na atawajibika kwa bidii katika kuwahudumia wananchi wa Mtwara Mjini.

Sauti ya Mohamedi Abdala (Mudy Ray), Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Mkoa wa Mtwara
Mjumbe wa Halmashauri kuu CCM mkoa wa Mtwara Mohamed Abdala (Mudy Ray) akimnadi mgombea ubunge jimbo la Mtwara Mjini Dkt Joel Nanauka katika viwanja vya Kokobichi kata ya Rahaleo ,Manispaa ya Mtwara Mikindani(Picha na Musa Mtepa)

Katika hatua nyingine, baadhi ya vijana wa Mtwara Mjini wamewataka wananchi kujitokeza kwa wingi Oktoba 29, 2025 siku ya uchaguzi ili kutimiza haki yao ya kikatiba kwa kwenda kupiga kura na kumchagua kiongozi wanayemwamini huku wakihimiza kuepuka upotoshaji unaosambazwa mitandaoni.

Sauti ya baadhi ya vijana wa Mtwara Mjini
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>