• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

Bajeti ya Mwaka 2018/19 ni Trilioni 32.476

Serikali imepanga kukusanya na kutumia Sh32.476 trilioni mwaka ujao wa fedha wa 2018/19.

Akiwasilisha mapendekezo ya Serikali ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na kiwango cha ukomo wa bajeti kwa mwaka 2018/19, waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema ukomo wa bajeti umezingatia upatikanaji wa mapato.

Dk Mpango amesema katika mwaka huo Serikali imepanga kutumia Sh20.468 trilioni kwenye matumizi ya kawaida sawa na asilimia 63 ya bajeti yote.

Matumizi hayo amesema yanajumuisha Sh10 trilioni zitakazolipa deni la Taifa na Sh7.369 trilioni mishahara ya watumishi wakati Sh3.094 trilioni zikielekezwa kwenye matumizi mengine.

Dk Mpango amesema Serikali itatumia Sh12 trilioni sawa na asilimia 37 kutekeleza miradi ya maendeleo.

Kiasi hicho, amesema kinajumuisha Sh9.876 trilioni sawa na asilimia 82.3 kutoka vyanzo vya ndani na Sh2.13 trilioni sawa na asilimia 17.7 kutoka nje.

Jumla ya mapato ya ndani pamoja na makusanyo ya halmashauri yanatarajiwa kuwa Sh20.894 trilioni ambayo ni sawa asilimia 64 ya bajeti yote.

“Kati ya mapato hayo yatokanayo na kodi yanatarajiwa kuwa Sh18 trilioni sawa na asilimia 13.6 ya Pato la Taifa,” amesema.

Amesema mapato yasiyo ya kodi yanatarajiwa kufika Sh2.158 trilioni wakati vyanzo vya halmashauri vikikusanya Sh735.6 bilioni.

Mpango amesema vyanzo vingine vinavyotarajiwa kufanikisha utekelezaji wa bajeti hiyo ni misaada na mikopo yenye masharti nafuu kiasi cha Sh2.676 trilioni kutoka kwa washirika wa maendeleo ambazo ni sawa na asilimia nane ya bajeti hiyo.

Katika mwaka ujao, amesema Serikali inatarajia kukopa Sh5.793 trilioni kutoka soko la ndani ambazo kati ya hizo, Sh4.6 trilioni zitatumika kulipia hati fungani na dhamana za Serikali zinazoiva.

Sh1.193 trilioni zinazozidi kwenye mikopo hiyo ya ndani ambazo ni sawa na asilimia 0.9 ya Pato la Taifa, amesema ndilo deni jipya.

“Ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miundombinu, Serikali inatarajia kukopa Sh3.111 trilioni kutoka soko la nje,” amesema.
Share:

Serikali yasema deni la Taifa ni himilivu

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema hadi Desemba 2017, deni la Taifa lilikuwa limefikia Sh47.756 trilioni na tathmini zinaonyesha bado ni himilivu.

Akiwasilisha mapendekezo ya Serikali ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na ukomo wa bajeti ya Serikali kwa mwaka 2018/19 mjini hapa leo Machi 13, 2018, Dk Mpango amesema deni la nje lilikuwa  Sh34.148 trilioni sawa na asilimia 71.5 na deni la ndani ni Sh13.607 trilioni sawa na asilimia 28.5.

Hata hivyo amesema uwiano wa deni hilo na Pato la Taifa kwa mwaka wa fedha 2017/18 ni asilimia 34.4 ikilinganishwa na ukomo ambao ni asilimia 56.

“Uwiano wa deni la nje na mauzo ya nje ni asilimia 81.1 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 150. Hii inamaanisha kuwa uwezo wetu wa kulipa deni bado ni imara,” amesema.

Amesema Serikali inaendelea kuchukua tahadhari kwa kukopa kwenye vyanzo vyenye masharti nafuu kuhakikisha mikopo hiyo inaelekezwa kwenye miradi ya maendeleo.
Share:

Rais wa Ufaransa apongeza utendaji kazi wa serikali ya Tanzania

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana amekutana na kuzungumza na Balozi mpya wa Ufaransa nchini Mhe. Frederic Clavier ambaye aliongozana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) Bw. Emmanuel Baudran.

Katika mazungumzo hayo ambayo yalifanyika Ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Balozi Clavier aliwasilisha salaam za Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na kusema, “Rais wa Ufaransa ana uhakika na Tanzania ijayo na anaunga mkono jitihada za maendeleo zinazofanywa na Rais Magufuli.”

Balozi huyo mpya wa Ufaransa nchini ambaye amekutana na kuzungumza na Mheshimiwa Makamu wa Rais aliipongeza Tanzania kwa kuwa mstari wa mbele katika masuala mbali mbali ya Kimataifa na kusema “Tanzania ni nchi yenye utulivu na Amani kitu ambacho kinaipa taswira nzuri Umoja wa Mataifa”.

Mhe. Balozi alimjulisha Makamu wa Rais kwamba Ufaransa imekusudia kuimarisha uhusiano zaidi na Tanzania wa Uchumi na Siasa na kuanzisha majadiliano mbali mbali katika masuala ya Mazingira,Mabadiliko ya Tabia Nchi.

Balozi Clavier alimjulisha Makamu wa Rais kuwa mwezi ujao kutakuwa na ugeni wa wafanya biashara kati ya 30 au 40 kutoka nchi ya Ufaransa ambao watakuja kujionea fursa mbali mbali za kibiashara na uwekezaji zinazopatikana nchini Tanzania.

Mhe. Balozi alimuelezea Makamu wa Rais azma ya Ufaransa kushirikiana na Vyuo Vikuu vya Tanzania katika kuanzisha na kuendesha kozi mbali mbali kwa manufaa ya pande zote mbili.

Mwisho aliipongeza Serikali kwa mapambano dhidi ya rushwa na urasimu jambo litakalo wavutia wawekezaji wengi nchini.

Aidha, Bw. Emmanuel Baudran Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa alisema Shirika lao linakusudia kuanzisha kiwanda cha vifaa vya umeme wa jua (solar) mkoani Shinyanga pia shirika hilo limeshafanya miradi ya uboreshaji maji taka katika manispaa ya Temeke na wanaendelea na mikakati ya uanzishwaji wa miradi mingine.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alimshukuru na kumpongeza Balozi wa Ufaransa kwa kazi nzuri wanazofanya hapa nchini.

Alimhakikishia kwamba Serikali ya Tanzania ipo tayari kutoa ushirikiano kwa mambo yote muhimu yenye maslahi kwa wananchi.

Wakati huohuo Makamu wa Rais alikutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa WFP nchini Mhe. Michael Danford.
Share:

Serikali ya Nigeria yatamani kufanya mazungumzo na Boko Haram

Serikali ya Nigeria imesema ina mpango wa kutumia njia ya mazungumzo badala ya kutumia nguvu za kijeshi ili kuwaokoa wasichana 110 waliotekwa katika mji wa Daptch hivi karibuni pamoja na wale waliotekwa mjini Chibok mwaka 2014.

Ofisi ya Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari imesema ingependa kuwapata wasichana waliotekwa Chibok na Daptch wakiwa hai.

Utekaji huo ndio mkubwa zaidi kufanywa na kundi la wanamgambo la Boko Haram lenye itikadi kali ya Jihadi, tangu lilipowateka wasichana wa shule 270 katika mji wa chibok mwaka 2014.

Hata hivyo, taarifa iliyowahi kutolewa na vyombo vya habari vya kiusalama ilidai kuwa takribani wasichana 100 waliachiliwa huru na Boko Haram baada ya kulipwa fidia na serikali.
Share:

Viongozi Watatu Mtandao wa wanafunzi Tanzania (TSNP) Waitwa Polisi

Viongozi watatu wa nafasi za juu katika Mtandao wa wanafunzi Tanzania (TSNP) wameitikia wito wa kufika kwa mpelelezi wa makosa ya Jinai (DCI) Jijini Dar es Salaam leo asubuhi kwa lengo la kuhojiwa kutokana na tukio la Abdu Nondo.

Hayo yamebainishwa na taarifa iliyotolewa na Afisa Habari- TSNP, Hellen Sisya baada ya kupita siku moja tokea Jeshi la Polisi kupitia Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa kuwataka viongozi hao kufika katika ofisi za DCI.

"Tumepokea taarifa ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam inatofautiana kabisa na ile ya Iringa juu ya kuonekana kwake. Hata hivyo, kabla ya taarifa ya uchunguzi kulitanguliwa na matamko ya viongozi wa juu waliodai kuwa Abdul Nondo alijiteka mwenyewe jambo ambalo kwa vyevyote lingeathiri uchunguzi wa jeshi la polisi", amesema Hellen.

Pamoja na hayo, Hellen ameendelea kwa kusema "pamoja na mapungufu yote tunaamini Nondo atatendewa haki atakapofikishwa mahakamani".
Chanzo: mpekuzi
Share:

TEMEKE : DC ASHUSHA NEEMA KWENYE SEKTA YA AFYA, ULINZI NA ELIMU

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva ameeleza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama tawala CCM ambapo ametaja miradi inayojengwa kwenye sekta ya elimu, afya pamoja na ulinzi na usalama.
Wakati akitoa ripoti ya utekelezaji wa ilani hiyo kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM- UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala, Lyaniva amesema ofisi yake inahakikisha inaimarisha hali ya ulinzi na usalama, ambapo kwa sasa inajenga vituo vikubwa viwili vya Polisi maeneo ya Chamanzi na Toangoma, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Kwa upande wa sekta ya afya, Lyaniva amesema kuna vituo viwili vya afya vya kisasa vinajengwa katika Kata ya Yombo na Majimatitu ambapo vitakuwa na wodi ya kinamama na vyumba vya operesheni, ili kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali za Temeke na Zakhiem.
Kuhusu sekta ya elimu, Lyaniva amesema wanaongeza madarasa kwenye baadhi ya shule za msingi ili kupunguza msongamano wa wanafunzi hali iliyosababisha na utekelezwaji wa sera ya elimu bila malipo ambapo wazazi wengi wamekuwa na mwamko wa kuwaandikisha watoto wao shule.
“Suala la elimu bila malipo wananchi wameliitikia vizuri sana sababu wameweza kujitokeza wengi kuwaandikisha watoto wao shule, shule ya Majimatitu imeongoza kwa uandikishaji, ikifuati mbande. Palipokuwa na elimu ya malipo watu walikuwa majumbani wengi sana, nina uhakika hatutakuwa na watoto nyumbani, sasa hivi uhalifu umepungua hatuna kundi la kumi nje kumi ndani kwa kuwa watoto wanaenda shule,” amesema.
Share:

MWENYEKITI, AFISA MTENDAJI MBARONI KWA KUKODISHA RAIA WA BURUNDI HEKARI 100

Watu watano ambao ni raia wa Burundi na Afisa Mtendaji pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha Kikurazo kilichopo wilayani Kakonko mkoani Kigogo, wanashikiliwa na Polisi kwa kosa la kuwakodisha mashamba zaidi ya hekari 100 raia hao wa Burundi.
Viongozi hao walikamatwa jana baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Kakonko kufanya operesheni ya ukaguzi wa usalama wa mipaka ya Tanzania.
Mkuu wa Wialaya ya Kakonko, Kanali Hosea Ndagala alisema awali walipata taarifa za tukio kutoka kwa raia wema kwamba kuna warundi wanaokuja kwenye mipaka ya nchi kinyume na sheria.
“Baada ya kukuta hali hiyo waliamua kumkamata Mwenyekiti wa Kijiji na Mtendaji na baadhi ya warundi waliokuwa katika mashamba hayo na wanaendelea na mahojiano na polisi baada ya hapo watafikishwa mahakamani,” alisema.
Share:

DAR ES SALAAM: Upande Wa Mashtaka Wafunga Ushaidi Kesi Ya Wema Sepetu

Upande wa Jamhuri katika kesi inayomkabili msanii wa filamu nchini, Wema Sepetu na wenzake jana ulidai mahakamani kuwa umefunga ushahidi dhidi ya mashtaka kutumia na kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi kwa msanii huyo.

Madai hayo yalitolewa jana na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam wakati wa kusikiliza ushahidi wa shahidi wa nne na wa tano mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Awali, shahidi wa nne, mjumbe wa nyumba 10, Steven Ndonde alidai mahakamani hapo kuwa siku ya tukio aliitwa kushuhudia upekuzi nyumbani kwa Sepetu.

Alidai kuwa wakati upekuzi unaendelea walikuta kipisi cha msokoto katika chumba cha nguo na viatu cha msanii huyo na chumba cha mfanyakazi wake walikuta kipisi kingine.

Hata hivyo, shahidi huyo alipohojiwa na wakili wa utetezi Albart Msando alikana kuwakuta washtakiwa wote wakiwa na dawa za kulevya aina ya bangi katika upekuzi huo.

Shahidi wa tano, Koplo wa Polisi Robert (31), alidai kuwa Februari 4, 2017 alipokea maagizo kutoka kwa bosi wake ya kupeleka vielelezo kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ikiwamo msokoto mmoja na vipisi viwili vya dawa za kulevya idhaniwayo kuwa bangi.

"Nilipeleka, vilipokelewa ofisi ya mkemia mkuu, baada ya kupokelewa niliandika barua kuhusu vielelezo hivyo," alidai Koplo Robert.

Kakula alidai baada ya kuita mashahidi watato dhidi ya washtakiwa upande wa Jamhuri imefunga kesi yao.

"Mheshimiwa hakimu tunaiachia mahakama iamue sisi upande wa Jamhuri tumefunga kesi yetu..." Alidai Kakula.

Wakili Msando aliomba upande wa utetezi kuwasilisha hoja za kama washtakiwa wana kesi ya kujibu au la ndani ya siku 10.

Upande wa Jamhuri ulidai utawasilisha majibu Aprili 3, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa.

Mbali na Sepetu, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Angelina Msigwa na Matrida Abbas.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

Inadaiwa kuwa Februari 4, mwaka jana katika makazi ya Wema huko Kunduchi Ununio, washtakiwa hao walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Ilidaiwa kuwa Februari mosi, mwaka jana katika eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam, Sepetu alitumia dawa za kulevya aina ya bangi. Washtakiwa walikana mashitaka.
Share:

ARUSHA: Mwakyembe Kuwashitaki kwa Waziri Mkuu Maofisa Habari Wazembe

Waziri  wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema atawasilisha kwa Waziri Mkuu majina ya maofisa habari wazembe, ili watumbuliwe.

Alisema hayo kufuatia uzembe unaofanywa na baadhi yao huku wakibweteka kukaa maofisini bila kufanya kazi.

Alisema maofisa habari wasiojituma ni sawa na kuwa na maofisa habari hewa, ambao wanakula mishahara wasioifanyia kazi, jambo ambalo hakubaliani nalo.

Dk. Mwakyembe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano wa kazi wa siku tano wa maofisa habari, mawasiliano na uhusiano serikalini, unaofanyika jijini Arusha, aliwataka kubadilika na kutekeleza malengo waliojiwekea.

"Kweli naangalia tovuti za halmashauri zipo tisa tu zinazofanya vizuri, zingine wahusika wamelala; na mikoa 18 tu inafanya vizuri kuhabarisha, sasa hawa wengine wajitathmini vinginevyo nitapeleka majina yao kwa Waziri Mkuu, ili watumbuliwe, tutoe ajira kwa wengine," alisema.

Aliwataka wafanye kazi ya kuhabarisha wananchi kazi zinazofanywa na serikali, ili wasitumbuliwe.

Alisema hata wizara husika pia wapo wazembe nao atapeleka taarifa ngazi ya juu ili wachukuliwe hatua, lengo kazi nzuri zinazofanywa na serikali zitambulike kwa wananchi na kuziba mianya kwa wapotoshaji wa taarifa za serikali.

Dk. Mwakyembe aliwataka maofisa habari hao kujituma na kutoa taarifa za kazi zinazofanyika kila siku kwenye mitandao ya kijamii na endapo watazuiwa na mtu yeyote, wawafichue hata kwa siri ili wizara ishughulike na muhusika.

Naye Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa (UN), Alvaro Rodriguez, aliwataka maofisa habari hao kubadilika na kuleta tija kwa taifa baada ya mkutano huo kuisha.

Alisema dunia sasa imeunganishwa kwa teknolojia, hivyo ni vema jamii ikapata taarifa zilizo sahihi kwa wakati.

Aidha, alisema serikali pia inahitaji kusikiliza jamii na sauti za wananchi, ili kupiga hatua katika kufikia Tanzania ya Viwanda.

“Sisi kama wadau tunahitaji kusikia zaidi habari za wananchi wa vijijini, ili tuone jinsi wanavyobadilika katika hali walizonazo,” alisema.
Share:

DAR ES SALAAM: Sababu za mashahidi Kutofika Mahakamani kesi ya Mfanyakazi wa TRA anaemiliki magari 19

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imesema itaanza kusikiliza ushahidi wa Jamhuri dhidi ya kesi inayomkabili Ofisa Msaidizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Jennifer Mushi anayekabiliwa na tuhuma za kumiliki magari 19 na kuishi maisha ya juu kuliko kipato chake kama mtumishi yenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 530.8.

Kesi hiyo ilipangwa kusikilizwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi.

Hata hivyo, upande wa Jamhuri uliomba mahakama kupanga tarehe nyingine kwa kuwa mashahidi hawajapatikana kutokana na kuwa na majukumu mengine.

Wakili wa Serikali Vitalis Peter alidai kuwa kutokana na mashahidi kuwa na majukumu mengine ya serikali wameshindwa kuwapata kwenda kutoa ushahidi dhidi ya mshtakiwa huyo.

Hakimu alisema mahakama yake itaanza kusikiliza ushahidi wa Jamhuri Aprili 9.

Katika kesi ya msingi, Peter alidai kati ya Machi 21, 2016 na Juni 30 mwaka huo mahali tofauti jijini Dar es Salaam, akiwa mtumishi wa TRA, mshtakiwa huyo alikutwa akimiliki mali zisizolingana na kipato chake, kinyume na sheria ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Alitaja mali hizo kuwa ni magari 19 ya Toyota Rav4, Toyota Dyna Truck, Toyota Vitz, Suzuki Carry, Toyota Ipsum, Toyota Wish, Toyota Mark II, Toyota Regius, Toyota Estima, Toyota Alex, Toyota Noah, Toyota Crown, Toyota Hiace, Toyota Estima, Toyota Passo na Suzuki Carry, yote yakiwa na thamani ya Sh. milioni 197.6.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kati ya Machi 21, 2012 na Machi 30, 2016 jijini Dar es Salaam akiwa mwajiri wa TRA aliishi maisha ya hali ya juu tofauti na kipato chake, yenye thamani ya Sh. 333,255,556.24.

Mshtakiwa alikana mashtaka hayo na yuko nje kwa dhamana.
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>