Viongozi hao walikamatwa jana baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Kakonko kufanya operesheni ya ukaguzi wa usalama wa mipaka ya Tanzania.
Mkuu wa Wialaya ya Kakonko, Kanali Hosea Ndagala alisema awali walipata taarifa za tukio kutoka kwa raia wema kwamba kuna warundi wanaokuja kwenye mipaka ya nchi kinyume na sheria.
“Baada ya kukuta hali hiyo waliamua kumkamata Mwenyekiti wa Kijiji na Mtendaji na baadhi ya warundi waliokuwa katika mashamba hayo na wanaendelea na mahojiano na polisi baada ya hapo watafikishwa mahakamani,” alisema.






No comments:
Post a Comment