DKT. #SLAA: "NITAFANYA KAZI KWA MOYO WANGU WOTE”


Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemuapisha Muhidin Mboweto kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Dkt. Wilbrod Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden.
Baada ya kuapishwa, Dkt. Slaa amemshukuru Rais Magufuli kwa uteuzi huo na kuahidi kutumia nafasi hiyo vyema ili kuisaidia nchi kuingia katika uchumi wa kati.
“Nikushuru wewe Mhe. Rais kwa imani uliyonayo kwangu, bila shaka una vigezo vyako ulivyotazama, umeona kwamba ninastahili katika nafasi hii, na kama nilivyoapa ninaomba kusema kwamba sitakuangusha. Hakuna heshima kubwa Taifa linaweza kukupatia kama kulitumia,” alisema Dkt. Slaa na kuongeza.
“Katika ulimwengu wa sasa diplomasia kubwa ni ya kiuchumi, ninakushuru kwamba umenipeleka mahali ninaweza kutoa mchango wangu, nifanye kazi kwa moyo wangu wote, kwa uwezo wangu wote, kwa akili yangu yote na Mwenyezi Mungu akinisaidia niweze kutoa mchango katika safari hii ya kujenga uchumi wa Tanzania, hasa Tanzania ya viwanda, Tanzania inayolenga kuingia kwenye uchumi wa kati.”
Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>