DKT. KIGWANGALLA ASHTUKIZA BODI YA UTALII (TTB)

#Waziri wa Maliasili na Utaliii, Dkt. #Hamisi #Kigwangalla leo Februari 20, 2018, 
amefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Makao makuu ya Bodi ya Utalii 
Tanzania (TTB) Jijini Dar es Salaam na kuitaka kufanya kazi kwa kasi na ubunifu 
zaidi. 

Akizungumza na viongozi wa Bodi hiyo, Dkt. kigwangalla amewataka kuongeza kasi zaidi katika 
kutangaza Utalii wa Tanzania ikiwa ni pamoja na kuanzisha studio ya kimataifa 
ya kutangaza vivutio vya Tanzania ndani na nje ya nchi kwa kutumia lugha 
mbalimbali za Kimataifa. 

Aidha,amewataka kuharakisha zoezi la uwekaji wa mabango yanayotangaza Utalii wa Tanzania katika 
viwanja vya ndege hususani uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu #Nyerere Dar 
es Salaam (JNIA). 
Hata hivyo amewataka pia kujikita zaidi katika matumizi ya mitandao ya kijamii kwa 
kuhakikisha inahuishwa mara kwa mara. 
Pamoja na hayo, ameiagiza bodi hiyo, kushirikisha wadau mbalimbali wanaotoa huduma za 
Utalii ikiwemo madereva taxi na Marubani kwa kuwapa elimu ya kutangaza 
utambulisho wa Tanzania kupitia Utalii na vivutio vilivyopo.

Akiwa katika ofisi hizo ndani ya jengo la Utalii House, alikagua ofisi mbalimbali za 
bodi hiyo pamoja na zile za Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na 
kupata maelezo machache kutoka wa maafisa wa Shirika hilo.
Share:

No comments:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>