• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

AGCOT yataka mageuzi ya kilimo mikoa ya Kusini

 

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi Zainab Telack akizungumza na wadau wa kilimo katika mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara (picha na Musa Mtepa)

“Kama tunaweza uzalisha zaidi ya bilioni 260 kwa zao moja, tunashindwa nini kutegemewa”

Na Musa Mtepa

Wadau wa kilimo wametakiwa kushirikiana kwa umoja katika kumsaidia mkulima kuzalisha kilimo chenye tija kwa kuwawezesha kulima kwa njia za kisasa, ikiwemo kuwapatia vitendea kazi bora vya kilimo.

Hayo yamesemwa Februari 20, 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack, wakati akifungua Warsha ya Wadau wa Kilimo ya kujenga uelewa wa pamoja kuhusu uendelezaji na ukuzaji wa Shoroba za Kilimo kwa mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara, iliyofanyika mjini Mtwara.

Bi. Telack amesema kuwa mafanikio yaliyopatikana katika zao la korosho, ambapo wakulima wamezalisha zaidi ya shilingi bilioni 260, yanaonesha kuwa inawezekana pia kuongeza uzalishaji wa mazao mengine endapo wakulima watawezeshwa kulima kisasa. Amesisitiza matumizi ya matrekta na zana bora za kilimo ili kuwawezesha wakulima kulima mashamba makubwa zaidi na kuongeza tija.

Sauti ya Bi Zainab Telack mkuu wa mkoa wa Lindi

Aidha, amewataka wakuu wa wilaya, wakuu wa idara za kilimo na sekta binafsi kutumia warsha hiyo kama fursa ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuweka mikakati imara ya utekelezaji wa mageuzi ya sekta ya kilimo kwa mikoa ya kusini na taifa kwa ujumla.

Sauti ya Bi Zainab Telack mkuu wa mkoa wa Lindi

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kuendeleza Kilimo kwa utaratibu wa Shoroba Tanzania (AGCOT), Geoffrey Kirenga, amesema lengo la warsha hiyo ni kuimarisha ushirikiano kati ya sekta binafsi na sekta ya umma pamoja na kuongeza ukaribu baina yao ili kukuza sekta ya kilimo.

Sauti ya Geoffrey Kirenga mkurugenzi wa AGCOT

Kirenga ameongeza kuwa katika warsha hiyo ameguswa na hoja zilizotolewa na sekta binafsi pamoja na viongozi wa halmashauri kwamba mwaka 2026 huenda malengo ya uzalishaji yasifikiwe kama ilivyotarajiwa kutokana na uhaba wa mbegu bora za ufuta. Amesema hali hiyo inaashiria kuongezeka kwa idadi ya wakulima wa zao hilo ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Sauti ya Geoffrey Kirenga mkurugenzi wa AGCOT

Kwa upande wao, Mkuu wa Idara ya Kilimo Halmashauri ya Masasi, James Chitumbi, pamoja na Mkuu wa Idara ya Kilimo Halmashauri ya Nachingwea, Rafael Magetu, wamesema warsha hiyo imewapa manufaa makubwa, ikiwemo namna ya kukabiliana na changamoto ya uhaba wa mbegu bora za mazao ya chakula na biashara kwa kuongeza juhudi za uzalishaji ili kufikia kilimo chenye tija.

Wakuu wa Idara ya Kilimo halmashauri ya Nachingwea na Masasi

Akifunga warsha hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brig Jenerali ,Ahmed Abbas, ametoa wito kwa wakuu wa wilaya kwenda kujifunza mbinu za kilimo-biashara zinazotekelezwa mkoani Lindi ili kukuza kilimo mseto na biashara katika Mkoa wa Ruvuma.

Sauti ya Brig Ahmed Abbasi mkuu wa mkoa wa Ruvuma

Warsha hiyo ya siku moja imewakutanisha wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakuu wa idara za kilimo, sekta binafsi pamoja na wadau wa kilimo kutoka mikoa ya Lindi, Ruvuma na Mtwara. Lengo kuu lilikuwa kujenga uelewa wa pamoja kuhusu uendelezaji na ukuzaji wa Shoroba za Kilimo katika mikoa hiyo.

Share:

Mtwara kuadhimisha kitaifa siku ya Skauti Duniani

 

Kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara ambae pia mkuu wa mkoa wa Lindi Bi Zainab Telack akizungumza na vyombo vya habari leo ofisini kwake mjiniMtwara(Picha na Musa Mtepa)

Mkoa wa Mtwara utaadhimisha Siku ya Skauti Duniani Februari 22, 2026, kumuenzi Robert Baden-Powell. Maadhimisho hayo yatajumuisha mafunzo, huduma za jamii na kampeni za uzalendo, huku vijana 400 wakitarajiwa kunufaika na elimu mbalimbali. Wananchi wamealikwa kushiriki katika viwanja vya Nangwanda Sijaona

NA Musa Mtepa

Mkoa wa Mtwara unatarajia kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Skauti Duniani yatakayofanyika Februari 22, 2026, ikiwa ni sehemu ya kumuenzi mwanzilishi wa harakati za Skauti Duniani, Robert Baden-Powell.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zainab Telack, amesema kuwa maadhimisho hayo ni sehemu ya historia ya zaidi ya miaka 100 ya Skauti, yenye lengo la kuwajenga vijana katika misingi ya uzalendo, uwajibikaji na kuipenda nchi yao.

Bi. Telack ameeleza kuwa katika kuelekea kilele cha maadhimisho hayo, tayari shughuli mbalimbali zimeanza kufanyika kupitia vijana wa Skauti, ikiwemo kambi za mafunzo ya ukakamavu, utoaji wa huduma za jamii pamoja na shughuli za utunzaji wa mazingira. Aidha, Februari 21, 2026, vijana hao wanatarajiwa kushiriki mafunzo yanayohusu uwajibikaji, uzalendo na masuala ya usalama.

Sauti ya 1 Bi Zainab Telack kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara

Katika hatua nyingine, Bi. Telack ametumia fursa hiyo kuwaalika wananchi wote wa Mtwara kushiriki kwa pamoja katika maadhimisho hayo yatakayofanyika katika Viwanja vya Nangwanda Sijaona, mjini Mtwara.

Sauti ya 2 Bi Zainab Telack kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara

Kwa upande wake, Naibu Kamishina wa Skauti Mkoa wa Mtwara, Sofia Malandi, amesema kuwa kufanyika kwa maadhimisho hayo kumeleta fursa mbalimbali kwa vijana na kwa mkoa kwa ujumla. Amefafanua kuwa elimu tofauti zinaendelea kutolewa, ikiwemo elimu ya kupinga rushwa na kuimarisha uzalendo, ambapo jumla ya vijana 400 wanatarajiwa kunufaika na mafunzo hayo.

Sauti ya Sofia Mlandi naibu kamishina wa Skauti mkoa wa Mtwara
kamishina wa Skauti mkoa wa Mtwara Sofia Mlandi akizungumzia shughuli zinazofanyika kuelekea maadhimisho hayo(Picha na Musa Mtepa)

Naye Afisa Utamaduni wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mratibu wa maadhimisho hayo, Bi. Fatuma Mtanda, amesema kuwa maadhimisho hayo yanatarajiwa kuhudhuriwa na wageni kutoka mikoa mbalimbali ikiwemo Lindi, Ruvuma, Mbeya, Mjini Magharibi na Pwani. Ameongeza kuwa mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Bi. Zainab Telack.

Sauti ya Fatuma Mtanda mratibu wa maadhimisho
Mratibu wa maadhimisho ya siku ya Skauti Duniani , Bi. Fatuma Mtanda akitolea ufafanuzi juu ya wageni watarajiwa na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo(Picha na Musa Mtepa)
Share:

Paka wa ajabu aibua taharuki Mtwara vijijini

 

Paka wa ajabu aliyekutwa amekufa baada ya kudhaniwa kujipiga kwenye nyumba ya Bi Maimuna Abilahi mkazai wa kijiji cha Nangumi(Picha na Musa Mtepa)

Wananchi wa kitongoji cha Shangani, Nangumi, wamekumbwa na taharuki baada ya paka kupatikana amekufa na kuvalishwa hirizi katika nyumba ya mkazi mmoja. Tukio hilo limeibua hofu na maswali, huku viongozi wa kijiji wakieleza kusikitishwa na hali hiyo isiyo ya kawaida

Na Musa Mtepa

Wananchi wa kitongoji cha Shangani, kijiji cha Nangumi, kata ya Mayanga wilayani Mtwara Vijijini, wamekumbwa na taharuki baada ya kuonekana kwa paka aliyekufa huku mwilini mwake akiwa amevalishwa hirizi.

Tukio hilo limetokea alfajiri ya leo, Februari 17, 2026, katika nyumba ya Maimuna Abilahi, mchuuzi wa samaki na mkazi wa kijiji hicho.

Wakizungumza na Jamii FM Radio, baadhi ya wananchi wa Nangumi wameeleza kushangazwa na tukio hilo, huku wakilihusisha na imani za kishirikina. Wamedai kuwa paka huyo alionekana akiwa amejitupa katika eneo la nyumba hiyo, na baada ya kuchunguzwa alikutwa na hirizi shingoni na kiunoni.

Sauti ya wananchi wa Nangumi

Akizungumzia tukio hilo, Maimuna Abilahi, mmiliki wa nyumba hiyo, amesema alipata taarifa za tukio hilo kupitia simu alipokuwa feri kununua samaki kwa ajili ya biashara yake. Ameeleza kuwa aliondoka nyumbani mapema asubuhi akitumia mlango wa nyuma, ambao ni tofauti na eneo alikokutwa paka huyo.

Sauti ya Maimuna Abilahi, mmiliki wa nyumba

Kwa upande wake, baba mzazi wa Maimuna, mzee Abilahi Issa Mohamedi, amesema baada ya kupata taarifa hizo alifika eneo la tukio na kisha kumpigia simu mwanawe kumjulisha. Ameeleza kuwa walikubaliana kumchoma moto paka huyo majira ya saa kumi jioni.

Alipoulizwa sababu ya kusubiri hadi saa kumi jioni, mzee Abilahi amesema ni maagizo ya wataalamu, akidai kuwa paka huyo ni wa aina ya kipekee.

Sauti ya mzee Abilahi Issa Mohamedi

Naye mwenyekiti wa kijiji cha Nangumi, Musa Salumu Nassoro, ameeleza kusikitishwa na tukio hilo, akisema linaweza kujenga taswira mbaya kwa kijiji hicho. Ameongeza kuwa katika kipindi chote cha uongozi wake hajawahi kushuhudia wala kusikia tukio la aina hiyo katika kijiji cha Nangumi.

Sauti ya Musa Salumu Nassoro, mwenyekiti wa kijiji cha Nangumi
Share:

CBT yasisitiza wakulima upogoleaji na utibuaji wa Mashamba ya Mikorosho

 

Mwonekano wa shamba la mikorosho lilotibuliwa ili kurahisisha maji kupenya ardhini na kuifikia mizizi ya Mikorosho(Picha na Musa Mtepa)

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania, Frances Alfred, amewataka wakulima kuzingatia upogoleaji na utibuliaji wa mashamba kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Amesema ruzuku za pembejeo zimeongeza uzalishaji, huku akisisitiza umuhimu wa kudumisha ubora wa korosho ili kupata bei nzuri sokoni

Na Musa Mtepa

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Frances Alfred, amewataka wakulima kuendelea na zoezi la upogoleaji wa matawi ya mikorosho pamoja na utibuliaji wa mashamba yao ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi yanayosababisha upungufu wa maji katika mikorosho.

Ameyasema hayo Februari 11, 2026, alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Dira ya Asubuhi kinachorushwa na Jamii FM Radio, kilichopo Naliendele, Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara. Amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, moja ya changamoto kubwa iliyoikabili zao la korosho ni mabadiliko ya tabianchi, yakiwemo mvua zisizotabirika na hali ya baridi isiyotarajiwa.

Sauti ya Frances Alfred, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT)

Aidha, amesema mmea wa mkorosho unahitaji maji ya kutosha ili uweze kufyonza virutubisho kutoka kwenye udongo kwa ufanisi. Kutokana na taarifa za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) zinazoonesha uwepo wa mvua za chini ya wastani, amewasisitiza wakulima kupogoa na kutibua mashamba yao ili kukabiliana na changamoto hiyo.

Sauti ya Frances Alfred, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT)

Hata hivyo, amesema pamoja na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, uwepo wa pembejeo za ruzuku zinazotolewa na Serikali umechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la uzalishaji wa zao hilo. Ameeleza kuwa uzalishaji umeongezeka kutoka tani 300,010 mwaka 2023/2024 hadi tani 528,000 mwaka 2024/2025, hatua inayochangiwa na ruzuku hizo.

Sauti ya Frances Alfred, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT)

Katika hatua nyingine, amewataka wakulima wanaokabiliwa na bei ndogo kuendelea kusimamia ubora wa zao la korosho kuanzia ngazi ya vyama vya msingi hadi kwa mkulima mmoja mmoja, ili waweze kupata bei nzuri na kuongeza manufaa yatokanayo na zao hilo.

Sauti ya Frances Alfred, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT)
Share:

“Kwanini uzito wa korosho utofautiane na malipo yake ?’’

 

Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndugu Frances Alfred akiwa katika studio za Jamii FM Radio akishiriki Mubashara kipindi cha Dira ya Asubuhi akizungumzia hali na mwenendo wa zao la korosho katika msimu uliopita na mwelekeo katika msimu ujao (Picha na Grace Hamisi)

Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania, Frances Alfred, ametaka wakulima walipwe kulingana na uzito uliopokelewa na wahusika wa upungufu wawajibike baada ya wakulima kulalamikia tofauti ya uzito wa mazao kati ya Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) na ghala kuu, hali inayosababisha upungufu wa malipo

Na Musa Mtepa

Wakulima wa zao la korosho wamehoji kitendo cha baadhi ya Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) kupunguza kiwango cha uzito wa korosho kilichopimwa ghalani, hali inayosababisha tofauti ya malipo baada ya korosho hizo kuuzwa katika ghala kuu.

Wakichangia katika kipindi cha Dira ya Asubuhi kinachorushwa na Jamii FM Radio Februari 11, 2026, wakulima hao wamesema uzito unaopimwa wanapowasilisha mzigo kwenye vyama vya msingi huwa tofauti na uzito unaokuja kuzingatiwa baadaye wakati wa malipo. Wamedai kuwa wanapohoji  hali hiyo kwa makatibu wa vyama wanaambiwa inatokana na tofauti ya mizani inayotumika kupimia kwenye vyama vya msingi na ile ya ghala kuu.

Sauti ya Wakulima wa Korosho

Akijibu hoja hiyo mubashara katika kipindi hicho, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania, Ndugu Frances Alfred, amesema mkulima anapaswa kulipwa kulingana na uzito wa korosho zilizopokelewa katika chama cha msingi, na hapaswi kupunguziwa malipo kwa sababu yoyote.

Sauti ya Frances Alfred Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Korosho

Aidha, amesisitiza kuwa iwapo kutatokea upungufu wa uzito wakati wa usafirishaji kutoka chama cha msingi kwenda ghala kuu, mhusika aliyesimamia mzigo huo anapaswa kuwajibika na kufidia tofauti hiyo, badala ya mzigo huo kuhamishiwa kwa mkulima. Ameeleza kuwa vitendo vya namna hiyo ni sawa na wizi.

Sauti ya 2 Frances Alfred Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Korosho

Pia ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wakulima kuripoti changamoto zozote wanazokutana nazo kwa Bodi ya Korosho, pamoja na kuendelea kushirikiana na maafisa kilimo katika maeneo yao ili kuhakikisha wanazalisha korosho zenye ubora na zinazoweza kupata soko lenye tija zaidi.

Sauti ya 3 Frances Alfred Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Korosho
Share:

97% ya watanzania wanafanya kazi sekta ya madini

 

Washiriki wakiwa katika warsha. Picha na Gregory Millanzi

Mabadiliko makubwa ya sheria ya madini yaliyofanyika mwaka 2017 yameleta mafanikio makubwa kwa Watanzania katika sekta ya madini, ambapo katika migodi mikubwa ya madini iliyopo nchini asilimia 97 ya wafanyakazi ni Watanzania na zaidi ya asilimia tisini ya uongozi na utawala pia unashikiliwa na Watanzania.

Na Gregory Millanzi

Mabadiliko makubwa ya sheria ya madini yaliyofanyika mwaka 2017 yamewezesha watanzania wengi kufanya kazi katika sekta ya madini, ambapo katika migodi migubwa ya madini iliyopo nchini asilimia 97 ya wafanyakazi ni watazania huku asilimia zaidi ya tisini ya uongozi na utawala katika migodi hiyo ni watanzania.

Kabla ya mabadiliko ya sheria ya madini mwaka 2017, idadi ya watanzania waliokuwa wanafanya kazi katika migodi mikubwa ya madini, shughuli za utafutaji na uchakataji wa gesi asilia ilikuwa ni ndogo.

Lakini baada ya kufanyika kwa mabadiliko watanzania wengi wanafanya kazi na kusimamia migodi hiyo.

Kamishina wa madini nchini Terence Ngole akiwa mkoani Mtwara katika warsha ya kuelimisha umma kuhusu shughuli za uwazi na uwajibikaji katika sekta ya madini, mafuta na gesi asilia iliyoandaliwa na Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji Katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) anafafanua zaidi.

Sauti ya Terence Ngole -Kamishina wa Madini

Sheria hiyo inawataka wawekeza kutumia huduma zinazopatikana nchini, na zisizopatikana nchini zihusishe makampuni ya ndani ya nchi, hatua hii imesaidia kuongezeka kwa manunuzi yanayofanywa na watazania.

Sauti ya Terence Ngole – Kamishina wa Madini

Wazawa wanaofanya kazi katika sekta hiyo wanaonesha ufanisi mkubwa na halmashauri zikinufaika zaidi na matokeo ya sheria hiyo.

Sauti ya Hidaya Gariatano – Mfanyakazi kampuni ya Gesi Asilia MNP
Share:

Watanzania wanufaika na mageuzi ya sheria ya madini

 

Mabadiliko ya sheria ya Madini, zaidi ya Asilimia 97 ya watanzania wajitokeza kufanya kazi kwenye sekta ya madini

Na Gregory Milanzi

Mabadiliko makubwa ya sheria ya madini yaliyofanyika mwaka 2017 yamewezesha watanzania wengi kufanya kazi katika sekta ya madini, ambapo katika migodi migubwa ya madini iliyopo nchini asilimia 97 ya wafanyakazi ni watazania huku asilimia zaidi ya tisini ya uongozi na utawala katika migodi hiyo ni watanzania.

Kabla ya mabadiliko ya sheria ya madini mwaka 2017, idadi ya watanzania waliokuwa wanafanya kazi katika migodi mikubwa ya madini, shughuli za utafutaji na uchakataji wa gesi asilia ilikuwa ni ndogo.

Lakini baada ya kufanyika kwa mabadiliko watanzania wengi wanafanya kazi na kusimamia migodi hiyo.

Kamishina wa madini nchini Terence Ngole akiwa mkoani Mtwara katika warsha ya kuelimisha umma kuhusu shughuli za uwazi na uwajibikaji katika sekta ya madini, mafuta na gesi asilia iliyoandaliwa na Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji Katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) anafafanua zaidi.

Sauti ya 1 TERENCE NGOLE-Kamishina wa Madini

Sheria hiyo inawataka wawekeza kutumia huduma zinazopatikana nchini, na zisizopatikana nchini zihusishe makampuni ya ndani ya nchi, hatua hii imesaidia kuongezeka kwa manunuzi yanayofanywa na watazania.

Sauti ya 2 TERENCE NGOLE-Kamishina wa Madini

Wazawa wanaofanya kazi katika sekta hiyo wanaonesha ufanisi mkubwa na halmashauri zikinufaika zaidi na matokeo ya sheria hiyo.

Sauti ya HIDAYA GARIATANO-Mfanyakazi kampuni ya Gesi Asilia MNP na

Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>