• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

Wafuasi Chadema waliokamatwa msibani kupandishwa Mahakamani

Wafuasi zaidi ya 10  wa Chadema waliokamatwa wakiwa nyumbani kwa mwanachama mwenzao kuhani msiba wanatarajiwa kupandishwa kizimbani muda mfupi ujao.

Watu hao, leo Machi 14, 2018 tayari wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza na kuwekwa katika mahabusu mahakamani hapo kusubiri kukamilika kwa taratibu za kimahakama ili wasomewe mashtaka dhidi yao.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi watu hao walikamatwa eneo la Mabatini Machi 13, 20018  baada ya kutokea kutoelewana kati yao na askari polisi.

Amesema askari hao walikuwa wakifuatilia nyendo za wafuasi hao  tangu walipokuwa wakikusanyika kutoka sehemu mbalimbali za Jiji la Mwanza kwenda nyumbani kwa wanachama mwenzao kwa kile kinachodaiwa ni kuhani msiba.

Katika tukio hilo, polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kutawanya kundi la watu zaidi ya 500 waliokuwa kwenye eneo hilo.
Share:

Sakata la Nondo Polisi watofautiana

Jeshi la polisi nchini limetofautiana katika taarifa zake kuhusu kupatikana kwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo ambapo RPC wa Iringa alisema kijana huyo alifika mwenyewe kituo cha polisi huku Mambosasa akipinga hilo.

Katika taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire Machi 8, 2018 imeonyesha kutofautiana na kauli iliyotolewa jana Machi 13, 2018 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, kamanda Juma Bwire alisema haya.

"Jana tarehe 7 mwezi wa tatu majira ya saa moja Abdul Nondo alifika katika kituo cha polisi Mafinga wilaya ya Mufindi na kuelezea kuwa ametekwa na watu wasiofahamika, jeshi la polisi mkoa wa Iringa limefungua jalada la uchunguzi ili kubaini ukweli kama alikuwa ametekwa na kama kweli alikuwa ametekwa tunaahidi kwamba sisi jeshi la polisi tukiwapata watuhumiwa sheria itachukua mkondo wake" alisema kamanda Bwire

Taarifa ya RPC wa Iringa imeonyesha kukinzana na taarifa aliyotoa jana Kamanda Mambosasa ambaye amedai kuwa Abdul Nondo hakuripoti sehemu yoyote ile na kudai kuwa walimkuta akiendelea na shughuli zake.

"Mnamo tarehe 7 Machi mwaka huu jeshi la polisi kanda Malaamu ya Dar es Salaam lililetewa taarifa kutoka polisi mkoa wa Iringa kwamba mwanafunzi huyo aliyekuwa amedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana alipatikana mkoani humo wilaya ya Mafinga akiwa na afya njema na mwenye kujitambua akiendelea na shughuli zake na wala hakuripoti tukio lolote kabla ya kukamatwa ili kuthibitisha kile kilichokuwa kikisemwa ametekwa na watu wasiojulikana. Hakuripoti mahali popote si kwa Mwenyekiti wa Mtaa, si kwa Afisa Mtendaji wa Kata, wala kituo chochote cha polisi mkoani Iringa bali alikamatwa akiwa Mafinga akiendelea na shughuli zake" alisisitiza Mambosasa 

Mpaka sasa jeshi la polisi linaendelea kumshikilia Abdul Nondo, kwani kwa mujibu wa wakili wa mwanafunzi huyo anasema kwamba mpaka jana Machi 14, 2018 hajafanikiwa kukutana wala kuongea na mteja wake.
Share:

ZANZIBAR: Nyama kutoka Afrika Kusini yateketezwa na ZFDA

Mamlaka ya Chakula na Dawa Zanzibar (ZFDA), imeteketeza  kilo 48 za nyama kutoka Afrika Kusini baada ya Serikali kusitisha uingizaji nyama kutoka nchini humo kutokana na mlipuko wa bakteria wa listeria.

Ilibainika kuwa nyama hizo ziliingizwa nchini kinyume cha sheria, Nyama hizo ni mali ya kampuni ya Qamar ya Vingunguti jijini Dar es Salaam, ilikamatwa Uwanja wa wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Karume mwishoni mwa wiki iliyopita.

Akizungumza leo Machi 14 wakati wa zoezi hilo, mkuu wa kitengo cha uchambuzi wa hatari zinazotokana na chakula wa ZFDA, Aisha Suleiman amesema kilichosababisha kuteketezwa kwa nyama hiyo ni katazo lililotolewa na ZFDA baada ya kutokea mlipuko wa ugonjwa wa listeriosis.

Amesema ZFDA ndiyo yenye majukumu ya kuhakikisha wananchi wanapata chakula salama, Aisha amesema uamuzi ya katazo hilo umetokana na uwapo wa maradhi ya Listeriosis nchini Afrika Kusini, hivyo ofisi yao imepiga marufuku uingizwaji nyama, maziwa na samaki kutoka nchi hiyo.

 Bakteria wa listeria, wanaosababisha maradhi ya listeriosis, wamesababisha vifo vya watu zaidi ya 180 Afrika Kusini.

Amesema katazo hilo si kwa Zanzibar pekee bali na Tanzania bara na nchi nyingine kutokana na utaratibu wa biashara kimataifa.

“Hili katazo siyo sisi tu, ni utaratibu wa kimataifa kwamba kutokana na maradhi ya listeriosis bidhaa za nyama, samaki, maziwa ni marufuku kuingizwa nchini sasa hii kampuni ya Qamar LTD ya Dar es Salaam wao waliamua kuingiza nyama hiyo, tumeikamata na kuiangamiza.” amesema Aisha.
Chanzo Muungwana
Share:

Rais Magufuli: Mimi nasema tuzaliane tu

Rais John Magufuli amesema idadi kubwa ya watu nchini haina budi kuendana na maendeleo kwani watu wanapokuwa wengi wanakuwa na sauti na hivyo akawataka Watanzania waendelee kuzaliana.

“Juzi tuliambiwa kwa sasa tumefikia watu milioni 55, watu wanasema kwa nini tunazaliana, mimi nasema tuzaliane tu,” amesema.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Machi 14, wakati wa uzinduzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge), Makutupora, Dodoma.

“Lakini idadi hiyo ya watu ni lazima wachape kazi, mfano Denmark ina watu milioni tano lakini wana maendeleo mpaka wanazisaidia nchi nyingine zenye watu milioni 55 kama Tanzania,” amesema.

Amesema ujenzi wa reli utatoa ajira za moja kwa moja zaidi ya 30,000 na zisizo za moja kwa moja 600,000.
Share:

Wafariki kwa kusombwa na maji mtoni wakijinadi wanajeshi

Picha kwa mujibu wa mtandao
WATU watatu wakiwamo wawili ambao walijinadi kuwa wana mafunzo ya kijeshi, wamefariki dunia mkoani Dodoma katika matukio mawili tofauti ya kusombwa na mafuriko.

Vifo hivyo vimesababishwa na mvua kubwa zilizonyesha usiku wa juzi.

Katika tukio la kwanza lililotokea Nzuguni Manispaa ya Dodoma, Diwani wa Kata ya Nzuguni, Aloyce Luhega, alisema kuwa katika eneo hilo watu wawili waliojinadi kuwa na mafunzo ya kijeshi walisombwa na mafuriko wakati wakitoka katika majukumu yao ya kazi majira ya jioni.

Alisema kuwa wakati wakirudi nyumbani, watu hao walifika katika eneo lenye kivuko ambapo pamejengwa daraja la chini ambalo lilikuwa limejaa maji kutoka na mvua iliyokuwa ikiendelea kunyesha juzi jioni.

Alieleza kuwa watu hao ambao bado hawajajulikana majina yao, walipofika katika eneo hilo watu waliwashauri wasivuke hadi maji yatakapopungua, lakini walikaidi na kudai kuwa wanaweza kuvuka.

“Walikwenda hadi katikati wakarudi kama mara tatu hivi, lakini mwisho wake wakasema wao wanaweze kuvuka kwa kuwa walishapitia jeshi, lakini wakati wakielekea kuvuka nguvu ya maji iliwashinda na kuwasomba huku tukiwaangalia,” alisema na kuongeza:

“Hatukuwa na la kufanya, tukawafuatilia, lakini kutokana na giza hatukuweza kuwapata hadi leo hii (jana) asubuhi ndipo tumeweza kuwapata wote wawili.”

Alisema miili ya marehemu polisi wameichukua kwa ajili ya hatua nyingine, ikiwamo waliopotelewa na ndugu zao kuitambua.

“Sasa hivi polisi wanalishughulikia suala hili, sisi kama serikali ya kata tumetoa ushirikiano ikiwa ni pamoja na kuitafuta miili hiyo hadi kuipata, hatua nyingine wenzetu wa polisi wataifanyia kazi, nitoe wito kwa wananchi wakati huu wa mvua kuwa waangalifu na kuchukua tahadhari,” alisema Luhega.

Katika tukio jingine, mkazi mmoja wa Kijiji cha Chibwegele Kata ya Mtera Wilaya Mpwapwa, aliyetambulika kwa jina moja la Martha, amefariki dunia baada ya nyumba yake kumwangukia kutokana na mvua iliyonyesha.

Mvua hiyo pia imesababisha kaya 40 za Kitongoji cha Chungu kukosa mahali pa kuishi, baada ya nyumba zao kusombwa.

Diwani wa kata hiyo, Amoni Kodi, alisema mkazi huyo aliyepoteza maisha alikutwa na mkasa huo akiwa ndani ya nyumba yake.

Alisema baada ya kuangukiwa na nyumba majirani walifanikiwa kwenda kumuokoa, lakini walimkuta amefariki dunia huku akiwa amevunjika miguu.

Diwani huyo alisema waathirika wamehifadhiwa na majirani huku serikali ya kata kwa kushirikiana na kamati ya maafa ya wilaya ikijipanga jinsi ya kuwasaidia.

“Waathirika wote wamepatiwa hifadhi na majirani  na kwa upande wa serikali ya kata na wilaya tunajipanga jinsi ya kuzisaidia kaya hizo kama vile chakula, maturubai na mabati hatua ambayo tunaamini itawasaidia, “alisema Kodi .

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, alipoulizwa alisema hana taarifa za kutosha juu ya matukio hayo na kuahidi kutoa taarifa rasmi baadaye.

Vifo hivyo ni mwendelezo wa matukio ya majanga ya mvua za mafuriko zinazoendelea katika maeneo kadhaa nchini.

Watu watano wameripotiwa wamepoteza maisha wakiwamo ndugu wawili ndani ya siku tatu katika matukio ya kufa maji katika mvua za mafuriko wilaya za Handeni na Lushoto mkoani Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, juzi alithibitisha kutokea kwa vifo vinne vilivyotokana na mafuriko na cha mtu mmoja aliyepigwa na radi.

Bukombe alisema Jumamosi 10 jioni wilayani Lushoto watu wawili ambao ni ndugu, Kassim Yahaya na Awadh Yahaya, wakazi wa Kitongoji cha Mbugui Chini walikufa maji wakivuka mto Lukundo.

Naye Mwamini Ally (46), mkazi wa Kijiji cha Rangwi alikufa kwa kusombwa na maji ya mto Ngurumo.Tukio lingine lilitokea Ijumaa jioni katika Kijiji cha Zavuza Kata ya Kiva wilayani Handeni ambapo Mwanahawa Rajab (60) alikufa kwa kusombwa na maji katika bonde la Bangala na Shaban Juma (30), mkazi wa Kijiji cha Mwamgodi Kata ya Msasa wilayani humo alikufa kwa kupigwa na radi. 
Share:

Kufanya mapenzi na ng'ombe kwamponza

Kijana Joseph Koech Alias Mnandi (25) wa Baringo huko Kenya ameuawa kwa kushambuliwa na wananchi wenye hasira kali baada ya kukutwa akifanya mapenzi na ng'ombe

Habari kutoka katika vyombo vya habari nchini humo zinadai kwamba Kijana huyo alijitetea kuwa alilazimika kufanya mapenzi na ng'ombe kutokana na ukweli kwamba wasichana wengi wameathirika na virusi vya UKIMWI
Wakati akipokea kipigo Bw. Mnandi aliwasihi watu hao wasimuue, wamuache alipe gharama za kosa hilo kwa kutoa kipande chake cha ardhi.
Vijana wenye hasira walimshambulia kwa makofi, mawe na vijiti na kumwacha na majeraha makubwa ambayo yalipelekea kifo chake alipokuwa amefikishwa katika hospitali ya Eldama-Ravine.
Kiongozi wa eneo la Torongo Edwin Ronoh amesema huyo mtu anafanya kazi kama mfanyakazi wa kawaida kwa miller mtaa wa eneo la msitu wa Sawich ambapo ameongeza kwamba familia (wamiliki wa ng'ombe) huyo ilikuwa na wakati mgumu wa kumtafuta ng'ombe wao aliyepotea katika misitu ya Sawich.
Amedai kuwa mtuhumiwa huyo  alifunga pembe za ng'ombe juu ya mti na  na miguu ya nyuma juu  ili kuzuia mtafaruku.
Chanzo: eatv
Share:

Askari Magereza waendelea kusota rumande

ASKARI Magereza 11 Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga wanaodaiwa kumuua mwanakijiji, Aloys Makalla, wanaendelea kusota mahabusu, baada ya kesi yao kuahirishwa.

Kesi hiyo iliahirishwa tena jana kwa mara ya nne na Mahakama ya Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga.

Askari hao wanaotuhumiwa kumuua Makalla, mkazi wa Kijiji cha Kerenge, Kata ya Kerenge, Wilaya ya Korogwe.Hakimu  Mfawidhi wa Mahakama hiyo,  Albert Nyang’ali, ambaye alisoma shtaka hilo la mauaji kama mlinzi wa  amani, alisema sababu ya kuendelea kutajwa shauri hilo bila kupangiwa kusikilizwa ni kutokana na baadhi ya vipengele kufanyiwa marekebisho.

Nyang’ali aliwataja askari hao ambao wapo mahabusu ya Gereza la Wilaya ya Korogwe ni P. 5377 Inspekta Makere, A. 4921 RSM (Mkuu wa Nidhamu) Mokiwa Shadrack Lugendo, A. 7367 Sajenti Mussa Mdoe Seif, B. 5919 Koplo Lazaro Stephen Nyato, B. 5486, Koplo Ramadhan Yusuph, B. 7087 WDR Robert Alfred, B. 7980 Fidirishi Cosmas Joseph, B. 7248 WDR Alphonce Revocatus, B. 8911 WDR Mbesha Naftari,  B. 9747 WDR Michael Elias Michael na B. 8533 WDR Hamis Halfa Msola.Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa watuhumiwa wote kwa pamoja Januari 22, 2018 katika Kijiji cha Kerenge wilayani Korogwe walimuua Aloyce Makalla maarufu kama Mapi.Katika kesi hiyo namba 2 P I ya mwaka 2018, watuhumiwa wote walikana shtaka, lakini hawakutakiwa kujibu chochote kwa vile mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za mauaji.Shauri hilo limepangwa kutajwa tena Machi 26, mwaka huu. Hii ni mara ya nne kesi hiyo kutajwa huku, watuhumiwa wote wakirejeshwa rumande.
Share:

Fahamu chanzo cha watu kupata upofu wa maisha

Daktari bingwa wa upasuaji wa macho kutoka hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt.Neema Daniel Kanyaro amedai ugonjwa wa presha ya macho ni moja kati ya magonjwa yanayopelekea mtu kupata upofu wa maisha endapo hatopata tiba mapema.

Dkt. Kanyaro amebainisha hayo kupitia kipindi cha Supamix kinachorushwa kupitia East Africa Radio baada ya kuwepo wimbo kubwa la watu kupata ugonjwa huo, huku wengine wakidhani unatokana na magonjwa ya kurithi kifamilia kama yalivyo mengine yanayojulikana.

"Shinikizo la jicho au presha ya jicho ni moja kati ya magonjwa yanayoleta upovu wa kudumu. Hili tatizo linawaathiri watu wote nikiwa namaanisha kwamba mtoto anaweza akazaliwa nalo kama ile sehemu yake ya kutolea machozi haitakuwa vizuri. Tunasisitiza sana jamii kufahamu ugonjwa huu wa presha ya macho ni lazima upime", amesema Dkt. Kanyaro.
Share:

Orodha ya wenyekiti na makamu wenyekiti kamati ya kudumu ya bunge 2018-2020

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ametoa orodha ya majina ya Wabunge mbalimbali ambao wameteuliwa katika kamati mbalimbali za kudumu za Bunge ambao wataongoza kwa kipindi cha mwaka 2018-2020.

Wabunge mbalimbali wameteuliwa kuongoza kamati hizo za kudumu kwa kipindi hiko cha mwaka ambapo baadhi ya wabunge walioteuliwa ni  Mhe. Nnape Nnauye, Mhe. Andrew J. Chenge, Mhe. Emmanuel Mwakasaka na wengine.

Kufahamu wabunge hao na kamati zao angalia chati iliyopo hapa chini ikibainisha majina ya wenyekiti na makamu wao.
Share:

Wazee CHADEMA Waomba Kukutana na Rais Magufuli

Baraza la Wazee wa Chadema limemuomba Rais John Magufuli kukutana na  wazee ili kubadilishana nao mawazo sambamba na kumpa ushauri wa masuala mbalimbali yanayoendelea nchini.

Akizungumza leo Jumanne Machi 13, 2018 katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, katibu mkuu wa baraza hilo, Roderick Lutembeka amesema kumekuwa na mambo mengi yanayopigiwa kelele, ni vyema rais akakutana na wazee ili wamueleza mambo hayo.

“Ni lazima kama Taifa tuchukue hatua mapema kabla hatujachelewa. Rais Magufuli akubali kuitikia wito wa kukutana na wazee ambao watakuwa na ujasiri wa kumshauri ili kuepusha Taifa kuingia kwenye majanga,” amesema.

Amesema suala la wazee kukutana na rais, kimekuwa ni kilio cha muda mrefu na kwamba nchini Kenya viongozi wameweza kukaa meza moja na kumaliza tofauti zao.

“Lazima tukae tujue mustakabali wa Taifa hatuwezi kusema hakuna tatizo. Tunamtaka akutane na wazee, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa tuzungumze kwa kuwa hii ni nchi yetu wote na si ya chama kimoja,” amesema.

Amesema mambo yanayopaswa kuzungumziwa ni suala la Katiba Mpya, hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Amesema pia matukio ya watu kutekwa na kuuawa yameongezeka, “miezi sita iliyopita tulizungumzia mambo haya lakini naona ndio yanaongezeka.”

“Wazee tumeumizwa mno kuhusu suala la Abdul Nondo hasa pale Waziri wa Mambo ya Ndani (Mwigulu Nchemba) alipotoa kauli kuwa kijana huyu alijiteka. Tulitegemea polisi wafanye uchunguzi, sasa kama waziri mhusika tayari ameshatoa hukumu tutegemee nini kwa hawa polisi. Tunajenga nini ndani ya mioyo ya hawa vijana ambao walijitoa kumtetea kijana mwenzao kama si chuki.”
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>