• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

MWANZA: Ekari tatu za bangi zateketezwa kwenye hifadhi


Zaidi ya ekari tatu za bangi zimeteketezwa kwenye msitu wa hifadhi ya Maisome iliyopo katika kisiwa cha Maisome Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza .

Kwa mujibu wa Katibu Tawala Wilaya ya Sengerema, Alan Mhina, bangi hiyo ilikuwa imelimwa kwenye sehemu ya msitu huo wenye ukubwa wa hekta 12,800, na kwamba, iliteketezwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya katika operesheni maalum ya kukomesha kilimo cha zao hilo haramu.

Kwa upande wake, Meneja Wakala wa Misitu Tanzania, TSF, Wilaya ya Sengerema, Bw. Urio Jeremiah, amesema, operesheni hiyo pia imelenga kukomesha shughuli nyingine za kibinadamu zinazotishia uhai wa hifadhi hiyo.

Share:

DAR ES SALAAM: Serikali yaanza mazungumzo na kampuni ya Bharti Airtel


 Kamati Maalum iliyoundwa na Rais Dkt. Magufuli na Kampuni ya Bharti Airtel yameanza rasmi leo tarehe 12 Machi, 2018 Jijini Dar es Salaam. 

kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na kurugenzi ikulu lengo ni kuweka mazingira safi ya mawasiliano kati ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Bharti Airtel

Share:

MAREKANI: Mkutano wa 62 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW umeanza leo


Mkutano wa 62 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW umeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.

Maudhui ya mkutano huo wa wiki mbili ni changamoto na fursa katika kufikia usawa wa jinsia na kuwezesha wanawake na wasichana waishio vijijini.

Akizungumza katika ufunguzi wa kamisheni hiyo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani Katibu Mkuu wa umoja huo Antonio Guterres amesema huu ni wakati muhimu kwa kuhakikisha madaraka na usawa unamfikia mwanamke na hususani wa Kijijjini ambaye amekuwa akisahaulika

Naye mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na wanawake, UNWomen, Phumzile Mlambo-Ngucka amesema maudhui hayo yanazingatia ukweli kwamba kampeni nyingi za kumkwamua mwanamke na msichana zinaangazia zaidi wale waishio mijini.

“Kwa msing iwa kutokumuacha nyuma mtu yeyote ni kuhakikisha hakuna anayeachwa nje. Moja ya michango mikubwa zaidi ya kufanikisha ajenda 2030 ni kuondoa ukosefu wa usawa unaokabili wanawake na wasichana waishio vijijini, ” amesema Bi. Mlambo-Ngucka.

Wakati wa mkutano mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwemo vikwazo vinavyokabili wanawake wa vijijini na mwelekeo bora ili wajikwamue.

Zaidi ya washiirki 8000 watahudhuria wakiwakilisha mashirika zaidi ya 1200 ya kiraia. Halikadhalika viongozi wa serikali za nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa pamoja na vijana.

Share:

DAR ES SALAAM: Wakili ashindwa kuonana na Abdul Nondo


Mwanasheria Jebra Kambole na Wakili wa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo amefunguka na kusema kuwa mpaka sasa ameshindwa kuonana wala kuongea na mteja wake huyo ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi.

Wakili huyo amesema kuwa amejaribu kufika ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ili kujua hali ya mteja wake pamoja na kuweza kuongea naye lakini ameshindwa.

"Mpaka sasa sijafanikiwa kuzungumza wala kumuona kwa sababu mara ya mwisho wakati tunafanya mazunguzo na DCI ambaye ana mamlaka juu ya hilo kwa sababu Abdul Nondo alikuwa anashikiliwa ofisini kwake mpaka dakika ya mwisho, tulipokwenda ofisini kujaribu kumuona akasema sisi huyu mtu tunamshikilia kama kama mlalamikaji lakini siyo kama mtuhumiwa kwa hiyo nyinyi kama Mawakili hamtakiwi kumhoji ila tukiona kwamba huyu mtu ni mtuhumiwa basi tutawaita muweze kuongea naye na kusikiliza maelezo yake, sisi tulimweleza tunahitaji kumuona ili tuweze kujua afya yake ili tuweze kurejesha mrejesho kwa familia na Watanzia wengine kwa ujumla ambao wanahofia juu ya usalama wake akasema yupo salama" alisema Kombole

Aidha Wakili huyo aliendelea kudai kuwa mpaka sasa Abdul Nondo anashikiliwa kinyume na sheria kwa kuwa sheria ya makosa ya jinai haitoi ruhuusa kwa jeshi la polisi kumshikilia mlalamikaji.

"Anayeshikiliwa ni mtuhumiwa lakini mpaka siku ya leo hajaachiwa kama ni mtuhumiwa kweli kwa sababu mtu ambaye anakwenda kutoa taarifa polisi anaachiwa arudi nyumbani huwezi kushikiliwa huko polisi na kwa kuwa wao wanasema wanamshikilia ana haki ya kupata uwakilishi kwa sababu kwa mujibu wa sheria yetu ya mwenendo wa makosa ya jinai sura namba 20 ya sheria za Tanzania, kifungu cha tano kinasema kwa muda gani mtu atakuwa chini ya dola au polisi, mtu ambaye amewekwa chini tu akiwa hana uhuru wa kwenda anakotaka huyo ina maana yupo chini ya ulinzi kwa hiyo kama upo chini ya ulinzi una haki ya kupata wakili kuweza kuongea naye na kujua nini kinaendelea na hatma yake na kupata fursa ya kuongea na ndugu zake na familia lakini fursa hiyo kwa Nondo haijapatikana kwani saizidi ni zaidi ya masaa 10 yamepita akiwa ameshikiliwa na jeshi la polisi" alisema Kombole

Mbali na hilo Wakili huyo amesema kuwa mpaka sasa wao hawajui Abdul Nondo ameshikiliwa kwa sababu zipi na kusema kuwa kijana huyo ameshikiliwa kinyume na sheria, kinyume cha Katiba, kinyume cha haki za binadam na kinyume na utaratibu wetu kama taifa kiujumla.
CHANZO: EATV
Share:

BURUNDI: Pierre Nkurunzinza atangazwa kuwa kiongozi wa kudumu chama tawala cha CNDD/FDD Burundi

Chama tawala nchini Burundi CNDD/FDD kimemtangaza Rais Pierre Nkurunzinza kama kiongozi mkuu wa kudumu au kiongozi wa milele ndani ya chama hicho.

Uamzi huo umefikiwa baada ya vikao vya siku tatu vya mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika katika eneo la Buye anakozaliwa Bwana Nkurunziza Kaskazini mwa nchi hiyo.

Uamuzi huo pia unachukuliwa wakati Burundi inajiandaa kufanya marekebisho ya katiba ili kumruhusu Rais Nkurunzinza kuendelelea kuongoza taifa hilo hadi mwaka 2034.

Taaarifa fupi ya chama cha CNDD/FDD imesema vikao hivyo vilinuwia kuimarisha chama tawala na taasisi zake.

Lakini pia chama hicho tawala kimechukua uamuzi wa kumuongezea hadhi na kumpa cheo cha juu Rais Nkurunziza na hivyo kumtangaza kuwa ni kiongozi mkuu wa kudumu ndani ya chama.

Kwenye hafla na makundi ya utamaduni ya chama tawala, katibu mkuu wa CNDD/FDD Bwana Evariste Ndayishimiye aliutangazia umati azimio hilo alolitaka kuwa ni muhimu mno katika uhai wa chama tawala.

Tangazo hili la chama tawala CNDD/FDD kumfanya Rais Nkurunzinza kama Kiongozi Mkuu wa Kudumu linajiri wakati Burundi inajiandaa kwa kura ya maoni kuhusu Marekebisho ya Katiba baadae mwezi Mei. Kati ya mambo mengi katiba hiyo ikipitishwa itamuwezesha Rais Nkurunzinza kuweza kuwania Urais mpaka mwaka wa 2034.

Wadadisi wengi wa siasa za Burundi wanaamini kuwa hatua hii ya chama tawala inanuwia kumalizia mapema mjadala wa mtetezi wa kiti cha Urais kwa niaba ya Chama hicho na kuonyesha mustakabali wa uongozi kabla hata uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2020.

Lakini pia uamzi huo unapeleka ujumbe kwa wafuasi wa CNDD/FDD na haswa viongozi wenye nia pengine ya kuwania nafasi hiyo na hivyo kujaribu kukiepusha chama tawala na mpasuko kama ilivyotokea mwaka wa 2015 katika mzozo kuhusu muhula wa sasa wa Rais Nkurunzinza.

Isitoshe kwa Wachanganuzi wa siasa za bado wanaiona hatua hii ya Rais Nkurunziza kutangazwa Kiongozi wa maisha kama dalili tosha ya jinsi kiongozi huyo alivyokidhibiti chama cha CNDD/FDD.

CHANZO: MUUNGWANA BLOG
Share:

NANYUMBU: wafanyakazi 50 kuchukuliwa hatua


Katibu tawala wa wilaya ya NANYUMBU mkoani MTWARA, SALUM PALANGO , March 10 mwaka huu 2018 katika Siku ya Mazoezi Kitaifa, amemuagiza Kaimu Mkurugenzi wa wilaya hiyo NDG. HAMZA SEIF MNALIWA, kuwachukulia hatua za Kinidhamu watumishi wapatao 50 wa Kata ya LIKOKONA,  walioshindwa kuhudhuria katika Mazoezi hayo yanayofanyika nchi nzima kila Jumamosi ya Wiki ya pili ya mwanzo mwa Mwezi.
PALANGO amebainisha hatua hizo za kinidhamu kuwa ni pamoja na kuwapa barua za kujieleza wafanyakazi hao, za  kwanini hatua za kinidhamu zisichukuliwe dhidi yao.
Katika hatua nyingine Katibu tawala huyo kijana machachari pindi awapo kazini,  amemuagiza Mratibu Elimu KATA kuhakikisha MCHAKAMCHAKA kwa wanafunzi unarudishwa kama zilivyo taratibu za kawaida .
“Wanafunzi wamenithibitishia Kuwa hawakimbii tena mchakamchaka, ambao ni muhimu kwa ukuaji wa Afya ya mwili na akili zao na hivyo kuimarisha taaluma zao, mratibu hakikisha mchakamchaka unarudi kama kawaida” amesema PALANGO

Ni utamaduni wa Wilaya ya NANYUMBU kufanya Mzunguko wa Mazoezi katika Kila Kata za Wilaya hiyo na Mwezi huu ilikuwa ni Zamu ya KATA ya LIKOKONA.
Mazoezi hayo yamehudhuriwa na wakuu wa Idara, Wananchi, DIWANI wa KATA, Kaimu Mkurugenzi,Walimu na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari LIKOKONA na Shule mbili za Msingi na Mgeni rasmi alikuwa ni Katibu Tawala Wilaya SALUM PALANGO,  ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo Wilaya na Katibu wake ni Afisa Utamaduni/ Afisa Michezo wa Wilaya.
Share:

TARIME: Nondo afananishwa na Viongozi


Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche amewataka watanzania kupiga kelele ili sheria ichukue mkondo wake hasa katika masuala ya watu kubambikiwa kesi
Mh. Heche ameamua kusema hayo baada ya Mwanafunzi Abdul Nondo kupotea jijini Dar es salaam kisha kupatikana huko Iringa  na habari tofauti zikiibuka kwamba alijiteka na kudaiwa kwamba alitoa taarifa za uongo.
Kutokana na taarifa hizo Mbunge wa Heche amesema kwamba "Kama viongozi  wanabambikiziwa kesi mchana kweupe sio ngumu kwao kumtengenezea huyu kijana kesi".
Ameongeza kuwa "Ni  wajibu wa Watanzania wote kupiga kelele sheria ifuatwe kwenye sakata hili".
Nondo, ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) aliripotiwa kutoweka katika mazingira ya kutatanisha tangu siku ya Machi 8 , ambapo amepatikana akiwa ametupwa barabarani Mafinga mkoani Iringa
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire, amesema Nondo amepatikana akiwa salama bila jeraha lolote wala kupigwa lakini wamefungua jalada hilo kwa ajili ya uchunguzi na mpaka sasa bado yupo kituoni hapo na iwapo atabainika alidanganya atashughulikiwa kama wahalifu wengine.
Share:

DAR ES SALAAM: SERIKALI YAONGEZA HUDUMA ZA MATIBABU YA UGONJWA WA FIGO

SERIKALI kupitia Wizara wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imeongeza wigo wa kutoa huduma za matibabu ya ugonjwa wa figo nchini kwa kuongeza vituo vya usafishaji damu hadi kufikia vituo  zaidi ya 17, na kufanya mafunzo kwa madaktari bingwa ili kuongezea nguvu madaktari bingwa 13 waliopo.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile wakati wa matembezi ya Siku ya figo duniani ambayo yamefanyika mapema leo katika viwanja vya Farasi Oysterbay jijini Dar es salaam.
“Wataalamu tunao 13 kwa upande wa madaktari, tumeiona hiyo changamoto kama Serikali, tumeongeza wigo wakufanya mafunzo kwa madaktari bingwa, na hivi karibuni tutatangaza ufadhili kupitia Serikali, vile vile tumetenga fedha kwaajili ya kuwafundisha madaktari ili kuweza kufanya matibabu ya figo” alisema Dkt. Ndugulile.
Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kwamba Serikali imeongeza wigo wa usafishaji damu kwa kuongeza vituo Zaidi ya 17 ambavyo vinatoa huduma ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa Figo katika hospitali binafsi na Hospitali za Serikali.
“Tumeongeza wigo wa usafishaji damu hadi tunavyoongea, tunavituo Zaidi ya 17 ambavyo vinatoa huduma ya kusafisha damu katika hospitali binafsi pamoja na hospitali zetu za Serikali , Muhimbili kuna vitanda 42, Mloganzira kuna vitanda 12, Bugando vitanda 6, KCMC vitanda 6, Mbeya vitanda 6, bila kusahau Regency, TMJ, Agakhan, Hindumandal,  na tunaendelea kuimarisha huduma”. Alisema Dkt. Ndugulile.
Vile vile Dkt. Ndugulile alisema kuwa Serikali imeanza upandikizaji wa Figo na imeshafanikisha kwa mgonjwa mmoja mpaka sasa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili  na matarajio ni kufanya upasuaji kwa mgonjwa mmoja kila mwezi mmoja.
Aliendelea kusema  mgonjwa mmoja anahitaji wastani wa shilingi milioni 37 kwa mwaka kwa ajili ya kulipia gharama ya kusafisha damu. Aidha, anahitaji kusafiri na kufika kwenye huduma kwa wastani wa safari 126 kwa mwaka sawa na wastani wa safari 3 hadi 4 kwa wiki.
Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile aliendelea kuwa kukumbusha kuwa Serikali ya awamu ya tano imeongeza Bajeti ya Dawa kutoka Bilioni 30 ilipokuwa ikiingia madarakani hadi sasa ni Bilioni 270 kwaajili ya Dawa, vifaa na vifaa tiba kwaajili ya magonjwa yakiwemo magonjwa ya Figo.
“Tumeongeza bajeti kwaajili ya Vifaa, Dawa na Vifaa Tiba kutoka Bilioni 30 wakati Serikali hii inaingia madarakani mbaka Bilioni 270, yaani mara tisa Zaidi, kwahiyo Dawa na Vifaa Tiba kwaajili ya matibabu ya Figo tunazo” alisema Dkt. Ndugulile.
Mwisho Dkt.Ndugulile alitoa wito kwa wananchi kubadili jinsi ya kuandaa vyakula nyumbani, mfano kwa kupunguza kiasi cha chumvi kwenye chakula na kiasi cha mafuta kutasaidia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza magonjwa shinikizo la damu (hypertension), kisukari na unene wa kupindukia, vile vile kuhamasisha familia kufanya mazoezi.
“Watanzania hatujui kula, tunakula bora chakula kuliko chakula bora, Matumizi ya vyakula vya mafuta, matumizi ya chumvi nyingi, matumizi ya vilevi, matumizi ya sigara kama hayana ulazima basi tupunguze, tutumie vyakula vilivyochemshwa na vilivyochomwa, bila kusahau kujenga utaratibu wa kufanya mazoezi angalau mara 3 kwa wiki kwa lisaa limoja inatosha” alisema Dkt. Ndugulile.
CHANZO: WIZARA YA AFYA - WAMJW
Share:

Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji Wa 19 March 14

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu  Machi 14,2018 atafanyiwa upasuaji wa 19 katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven nchini Ubelgiji.

Upasuaji huo ni mwendelezo wa ambazo amekuwa akifanyiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikokuwa amelazwa baada ya kushambuliwa kwa risasi akiwa katika makazi yake mjini Dodoma Septemba 7,2017.

Alipatiwa huduma za awali katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

Taarifa ya Lissu aliyoitoa jana usiku Machi 10,2018 akielezea afya yake amesema licha ya sasa kuweza kusimama bila msaada, amejuzwa na timu ya madaktari wanaomtibu kuwa kasi ya mfupa wa juu ya goti kuunga ni ndogo.

"Madaktari wangu wamesema wasipoingilia kati na kurekebisha mfupa huo itachukua muda mrefu sana kuunga," amesema.

Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) amesema madaktari wamemweleza hata mfupa huo ukiunga baada ya muda mrefu, hautaunga kwa namna utakaoondoa hatari ya kuvunjika baadaye.

"Kwa sababu hizi, madaktari wangu wamependekeza kufanya operesheni nyingine kwenye mfupa wa juu ya goti la kulia Machi 14,2018, nitarudi Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven, Gasthuisberg, kwa ajili ya kufanyiwa operesheni hiyo," amesema.

Amesema yuko katika mikono salama ya kitabibu chini ya madaktari Profesa Stefa Nijs na Profesa Willem-Jan Mertsemakers ambao amesema ni madaktari bingwa wa mifupa wanaosifika barani Ulaya.

"Hivyo, msiwe na hofu. Mungu wetu aliyeniwezesha kuwa hai sasa, ataendelea kutenda miujiza kupitia kwa madaktari bingwa hawa," amesema.

Lissu amesema ataendelea kutoa taarifa za maendeleo ya afya yake kwa kadri itakavyohitajika akiwaomba Watanzania kumuunga mkono yeye na familia yake katika kipindi anachopitia.

Lissu yupo Ubelgiji tangu Januari 6,2018 alikopelekwa akitokea Hospitali ya Nairobi, Kenya.
Share:

DAR ES SALAAM: Mamlaka ya hali ya hewa Yatoa Tahadhari

Mamlaka ya hali ya hewa iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini Tanzania imewatahadharisha wananchi kuwepo kwa hali mbaya ya hewa katika maeneo ya mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara ndani ya saa 24 kuanzia leo.

Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na mamlaka hiyo na kudai kutakuwepo vipindi vifupi vya mvua kubwa ambazo zinatarajiwa kunyesha katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Singida, Dodoma, Morogoro, Ruvuma, Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe, Kilimanjaro, Manyara na Arusha

Mbali na hilo, TMA imesema kutakuwepo upepo mkali unaofikia kilomita 30 kwa saa kutoka Kaskazini- Mashariki kwa Pwani ya Kaskazini na kutokaa Kaskazini-Magharibi kwa Pwani ya Kusini huku hali ya bahari inatarajiwa kuwa na mawimbi makubwa kiasi.
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>