• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

KENYA: Kenyatta, Odinga wakutana Nairobi

Rais Uhuru Kenyatta Ijumaa asubuhi amekutana na mpinzani wake mkuu wa kisiasa na kiongozi wa muungano wa National Super Alliance (Nasa), Raila Odinga katika Jengo la Harambee jijini Nairobi.
Hii ni mara ya kwanza kwa wawili hao kukutana tangu walipotofautiana kuhusu uchaguzi mkuu uliokuwa na upinzani mkali wa Agosti 8, 2017 na wa marudio Oktoba 26 ambao Odinga alisusia.
Agenda ya kikao chao haikuwekwa wazi. Baada ya kikao chao Kenyatta na Odinga walitarajiwa kulihutubia taifa.
Seneta wa Siaya James Orengo, mshirika wa karibu wa Odinga aliliambia shirika la habari la Reuters akithibitisha kufanyika kikao hicho.
“Kinafanyika sasa, lakini tutatoa maelezo zaidi kitakapokuwa kimemalizika,” amesema.
Msemaji wa Ikulu Manoah Esipisu aliwaambia waandishi wa habari kwamba Odinga atakuwa wa kwanza kuhutubia na kisha Rais Kenyatta atatoa maoni yake.
Kikao cha viongozi hao kimefanyika siku ambayo Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex Tillerson anatarajiwa kuwasili Nairobi akiwa katika ziara ya Afrika.
CHANZO: MWANCHI
Share:

DAR ES SALAAM: MAGONJWA YA FIGO YANAATHIRI ZAIDI WANAWAKE

Magonjwa ya figo yanakadiriwa kuwaathiri takribani wanawake milioni 195 duniani kote na yanashika nafasi ya 8 kama chanzo cha vifo vya wanawake duniani na inakadiriwa kuwa wanawake 600,000 hupoteza maisha kutokana na matatizo ya figo duniani kote kila mwaka

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile wakati akitoa tamko la siku ya Figo duniani ambapo huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi.

Dkt.Ndugulile alisema tafiti zilizofanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO), zinaonyesha wanawake wako katika hatari zaidi ya kupata matatizo ya figo ukilinganisha na wanaume. Kwa wastani asilimia 14% ya wanawake wanaathiriwa na matatizo ya figo ukilinganisha na asilimia 12% kwa wanaume

Kwa upande wa Tanzania Naibu Waziri huyo alisema ugonjwa huo umekuwa ukiongezeka  na tafiti zilizofanya Kanda ya Kaskazini mwaka 2014, ulionyesha kuwa kati ya 7% – 15% ya Watanzania wana matatizo sugu ya figo na kwa asilimia kubwa yamekuwa yakichangiwa na magonjwa ya Shinikizo la Damu na Kisukari

Hata hivyo aliongeza kuwa kwa utafiti uliofanywa na Hospitali ya Kanda Bugando, umeonesha kuwa 83% ya Wagonjwa wa Kisukari wana matatizo sugu ya figo na kati ya hawa, 25% walikuwa wanahitaji huduma za usafishaji damu.

“Wagonjwa waliokuwa wanapatiwa huduma ya kusafisha damu kutokana na figo kushindwa kufanya kazi, ambao ni wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) walikuwa 178. Kwa sasa idadi ya Wagonjwa hawa imeongezeka na kufikia 783. 


Aidha, alisema  mgonjwa mmoja anahitaji wastani wa shilingi milioni 37 kwa mwaka kwa ajili ya kulipia gharama ya kusafisha damu. Aidha, anahitaji kusafiri na kufika kwenye huduma kwa wastani wa safari 126 kwa mwaka sawa na wastani wa safari 3 hadi 4 kwa wiki.

Alisema Serikali  imekuwa ikipeleka wastani wa wagonjwa thelathini na tano(35) kwa mwaka nje ya nchi kwa ajili ya kupandikiza figo na idadi ya waliokwishapandikizwa figo na ambao wanafuatiliwa matibabu yao katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili  ni takribani 204.“Gharama za kupandikiza figo nje ya nchi ni wastani wa fedha za Kitanzania milioni 75 hadi 77 kwa mtu mmoja,ikijumuisha upandikizaji,nauli na malazi”Alisema Dkt.Ndugulile

Dkt.Ndugulile alitoa wito kwa wananchi kubadili jinsi ya kuandaa vyakula nyumbani, mfano kwa kupunguza kiasi cha chumvi kwenye chakula na kiasi cha mafuta kutasaidia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza magonjwa shinikizo la damu (hypertension), kisukari na unene wa kupindukia, vile vile kuhamasisha familia kufanya mazoezi.Kaulimbiu ya maadhimisho ya siku ya figo ya mwaka huu wa 2018 ni “FIGO NA AFYA YA WANAWAKE: WASHIRIKISHWE, WATHAMINIWE NA WAWEZESHWE”.

CHANZO: AFYABLOH Na WAMJW. Dar es salaam.
Share:

MASASI:wasichana waonyesha vipaji kwa kusakata "volleyball"


Image may contain: one or more people, people playing sports, sky, cloud, outdoor and natureTimu ya volleyball ya watoto wa kike kutoka shule ya msingi na sekondari MKALAPA Kata ya NDANDA iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya MASASI wameadhimisha siku ya wanawake duniani kwa mchezo wa volleyball.

Wakizungumza baada ya mchezo huo, wamefurahi  na kuiomba jamii kutoa kipaumbele katika michezo inayohusisha jinsia ya kike.

Ikumbukwe kuwa timu ya watoto hao ni moja kati ya timu ambazo zimeupa ushindi Mkoa wa MTWARA katika mashindano ya UMISETA na UMITASHUMTA, hivyo watoto wa kike wakiwezeshwa wanaweza katika kujitelea maendeleo na  kushiriki katika safari ya kuelekea uchumi wa Viwanda kwa kutumia vipaji vyao.


WAKATI HUOHUO

Image may contain: one or more people, people standing and textHalmashauri ya Wilaya ya MASASI imeadhimisha siku ya Wanawake duniani katika Kata ya NDANDA huku Mambo MATATU ya kumwezesha mwanamke ili kushiriki kwa vitendo kuelekea uchumi wa viwanda ifikapo 2025 ikiwemo kuwawezesha kielimu, kuwapa mitaji na kuwashirikisha katika maamuzi yakisisitizwa.

Image may contain: 7 people, people smiling, weddingHalmashauri ya wilaya ya Masasi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya shilingi milioni 79,445,000 zimekopeshwa kwa vikundi 31 vya wanawake ikiwa ni mitaji ya kuendeleza biashara zao na hivyo kuzalisha kwa tija ili kukuza uchumi wa kaya na Taifa kwa ujumla.


Kauli mbiu ya siku ya wanawake duniani mwaka 2018 unasema"KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA: TUIMARISHE USAWA WA KIJINSIA NA UWEZESHAJI WANAWAKE VIJIJINI"

Share:

RUKWA: WAZIRI UMMY AWAONYA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI WASIOTENGA FEDHA ZA UWEZESHAJI WANAWAKE

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewaonya Wakurugenzi wote wa Halmashauri wtakaokaidi agizo la Serikali la kutenga asilimia 4 kwa  ajili ya wanawake na vijana pamoja na asilimia 2 kwa ajili ya watu wenye ulemavu.
Ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mkoa wa Rukwa ambapo amepokea changamoto kutoka kwa wanawake wengi  kuhusu utoaji mdogo wa mikopo na wengine kutopata kabisa mikopo kutoka Halmashauri zao.
Ummy amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashuri zote nchini kutenga asimilia 4 kwa ajili ya wanawake na kutoa mikopo yenye tija itaakayoweza kuwasaidia wanawake kujikwamua kiuchumi na sio kurudi nyuma kiuchumi.
“Mikopo ya laki tatu haina tija toeni kikopo yenye tija itakayoendana na kauli mbiu ya kuelekea uchumi wa viwanda,”alisema  Mhe. Ummy
Mhe. Ummy ameongeza kuwa ili kufikia azma ya Tanzania ya Viwanda basi Halmashauri hazina budi kujiwekea mikakati ya kutoa mikopo mikubwa itakayo wawezesha wanawake na wananchi kwa ujumla kufikia dhana hiyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kalembo Mhe. Julieth Binjula ameiomba Serikali kuendelea kuwawezesha wanawake kwa kuwapa elimu ya jinsi ya kutumia fedha na kuendesha miradi mbalimbali itakayo wakwamua kiuchumi.
Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Bw. Khalfan Haule amesisitiza wadau kushirikiana na Serikali pale ambapo wanaweza kuwawezesha wanawake sehemu walipo ili waweze kujikwamua kiuchumi na kutoa mchangokatika kuchangia kujiletea maendeleo jumuishi.
Siku ya Wanawake Duniani 2018 kilele chake ni siku ya tarehe 8 Machi, 2018 na  Kaulimbiu inayoongoza maadhimisho haya ni‘‘KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA: TUIMARISHE USAWA WA JINSIA NA UWEZESHAJI WA WANAWAKE VIJIJINI”. Dhamira ya Wizara nikuona kila mdau mmoja mmoja anaelewa madhumuni ya kaulimbiu na kuchukua hatua kuchangia utekelezaji wa ujumbe mahususi wa kuwajumuisha wanawake wa vijijini katika maendeleo yao na ya Taifa kwa ujumla.
CHANZO: DEWJBLOG
Share:

UNIDO TAYARI KUSAIDIA TANZANIA YA VIWANDA


Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Viwanda (UNIDO) limesema litasaidia Watanzania kutimiza ndoto za kuwa taifa lenye uchumi wa kati linalotegemea viwanda kwa kuunga mkono utendaji wa pamoja wa sekta ya umma na binafsi.
Kauli hiyo imetolewa katika hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Li Yong ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania na pia ya kwanza nje ya makao makuu ya Shirika hilo baada ya kuchaguliwa kwake kwa mara ya pili mwaka jana.
Alisema katika hotuba yake kwamba moja ya majukumu makubwa ya shirika hilo ni kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs)  hasa lengo namba tisa la  maendeleo na teknolojia kwa ajili ya ustawi wa nchi hizo.
Aidha alisema ili kufanikisha hilo kumesisitizwa ushirikiano ambao ni lengo namba 17 la SDGs.
Alisema sekta binafsi ikishirikiana vyema na serikali ndiyo inayoendesha uchumi hasa katika kutoa fursa za kazi kwani asilimia 80 ya kazi kila mwaka hutolewa na sekta binafsi.
Alisema katika hotuba yake hiyo kwamba amefurahishwa na malengo ya Tanzania na nia ya Shirika hilo kuona kwamba malengo hayo kuelekea uchumi wa kati wa viwanda yanatekelezwa kwa kuangalia vionjo muhimu.
Aidha alisema kwamba wataendelea kushirikiana na sekta binafsi kupitia TSPF kuhakikisha kwamba wananchi wanashirikishwa katika malengo ya maendeleo ili kuwa na malengo endelevu na yanayozingatia mazingira.
Naye Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini- TPSF Dr. Reginald Mengi akizungumza katika hafla hiyo aliitaka UNIDO kusaidia kutengeneza utajiri nchini Tanzania.
Dr. Mengi alisema kwamba ziara ya kiongozi huyo imekuja wakati muafaka, wakati ambapo Tanzania inaelekeza macho yake katika uchumi wa kati na hivyo kuwa na nafasi ya kusaidia ndoto hiyo kufanikiwa.
Alisema wakati nchi nyingi zimekuwa zikipiga maendeleo, zimekuwa na msingi dhaifu wa uchumi wa viwanda kutokana na kusafirisha zaidi bidhaa ambazo hazijasindikwa au zinazotokana na uziduaji.
Alisema hali hiyo pamoja na kuipa utajiri nchi imekuwa haitawanyi utajiri uliopo.
Alisema kutokana na hali hiyo, UNIDO ina kazi kubwa ya kusaidia Tanzania kufikia lengo lake la viwanda hata kusaidia kuanzishwa kwa maeneo ya viwanda (Industrial Park).
Aidha aliishukuru UNIDO kwa kuwezesha sekta binafsi na serikali kukaa pamoja kupitia Baraza la Taifa la Biashara ambako kunakuwa na mazungumzo yenye tija kuhusiana na maendeleo ya biashara na uchumi nchini Tanzania.
Alifafanua kwamba UNIDO ina nafasi kubwa ya kuisaidia Tanzania hasa katika mipango mikakati yake kwa kuunganisha sekta binafsi na umma ili kuiharakisha Tanzania kuelekea uchumi wa kati wenye kutegemea viwanda.
Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda pamoja na Kimataifa Dr Augustine Mahiga, ambaye wizara yake ndiye ilimwalika Mkurugenzi mkuu huyo, pamoja na kumshukuru kwa kuitikia wito huo aliitakabkusaidia kuchagiza maendeleo ya viwanda.
Alisema kwamba viwanda vya Tanzania bado vichanga na vinahitaji kusaidiwa na kupewa nguvu ya kuendelea mbele kwani pamoja na uchanga wake mchango wake katika kuelekea uchumi wa kati ni mkubwa.
Awali kabla ya hafla ya chakula cha mchana UNIDO ilitiliana saini na serikali ya Tanzania waraka wa kusaidia kuitoa Tanzania katika mipango ya kitaifa kwenda kwenye mipango ya nchi na washirika ili kufikia uchumi wa kati.
Makubaliano hayo yalisainiwa jijini Dar es Salaam kati ya  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO, Li Yong huku yakishuhudiwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
Share:

DAR ES SALAAM: WAZIRI NDALICHAKO, ANNA MAKONDA WATOA SOMO KWA WANAWAKE


Ikiwa leo Machi 8, 2018 ni kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Stadi, Profesa Joyce Ndalichako na Spika Mstaafu wa Bunge, Anna Makinda wametoa somo kwa wanawake hapa nchini.
Akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu masuala ya maendeleo endelevu ya Wanawake barani Afrika, Prof. Ndalichako amewataka wanawake kufanya kazi kwa bidi ili waweze kuaminiwa na jamii.
“Wito wangu ni kwamba tuendelee kufanya kazi kwa bidii kwa sababu historia imemuweka mwanamke katika nafasi isiyo nzuri kwa hiyo wanawake tukiendelea kufanya kazi kwa bidii mchango wetu kwa jamii utaendelea kuonekana na kuthaminiwa na hivyo tunaweza tukawa tunapata nafasi kubwa na nzuri ya kulitumikia taifa, hii historia ya kubaki nyuma tutaiondoa wanawake wenyewe kwa kufanya kazi kwa bidi,” amesema.
Naye Makinda amewataka wanawake kujiamini sambamba na kuwa na uthubutu huku akiwasihi kujitika katika utafutaji wa elimu kwani ndiyo mkombozi wa maendeleo ya wanawake.
“Elimu ni kitu muhimu sana, wanawake wengi elimu zao ni ndogo wananyanyasika wananyang’anywa mali sababu hawajui wanaenda wapi, elimu yenyewe siyo ya utaniutani, wenyewe wanasoma lakini hawajui wanasoma nini. Mkombozi wa mwanamke ni kupatikana elimu sahihi ya kuweza kupambanua maisha yake na kujua haki zake ziko wapi na si kumdekeza sababu ukimdekeza hatuwezi kufanya chochote,” amesema na kuongeza.
“Elimu inamfanya mwanamke athubutu, kama huna elimu hijuamini ndiyo unatengeneza mazingira ya kupata mafanikio kwa kupitia mtu, kusoma vizuri kujiamini, kuwa na uthubutu mwengine anataka kwenye kazi apelekwe na mtu.”
Na Regina Mkonde

Share:

DAR ES SALAAM: Jaji Mkuu awataka hawa wajitathimini


Jaji Mkuu wa Tanzania, PROF. IBRAHIM JUMA amewataka watendaji na wataalamu wa Mahakama, nchini kujitathmini na kuona namna wanavyoweza kutoa msukumo wa maboresho wa Mahakama katika suala la kutoa haki kwa wakati
Jaji PROF. JUMA amesema hayo Jijini ARUSHA wakati akifungua Mkutano wa watendaji na wataalam wa Mahakama wenye lengo la kutathmini utekelezaji wa mpango wa maboresho wa Mahakama nchini.

Jaji Mkuu huyo wa Tanzania amesema kuwa kuna tatizo la utoaji wa taarifa muhimu kwa Wananchi kitika MAHAKAMA jambo linalowanyima wananchi haki ya kufuatilia mashauri yao.

Pia Jaji Mkuu amewataka watendaji kufanya Tathmini na kuona namna wanavyeweza kutoa msaada katika kufikia malengo yaliyokusidiwa na Mahakama.
Msikilize hapa chini Jaji Mkuu akiongea zaidi.

Share:

DODOMA: DKT. KALEMANI AIAGIZA TPDC KUHARAKISHA UUNGANISHAJI WA GESI MAJUMBANI

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amelitaka na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ( TPDC) kuharakisha uunganishaji wa huduma ya Gesi asilia katika nyumba za wananchi kwenye maeneo ya jiji la Dar Es Salaam kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Dkt. Kalemani aliyasema hayo tarehe 3 Machi, 2018 ofisini kwake mkoani Dodoma alipokutana na watendaji wa TPDC kwa lengo la kujadili suala la usambazaji wa Gesi asilia katika nyumba za Wananchi pamoja na bei watakayouziwa wananchi hao.
Katika mazungumzo hayo, Dkt. Kalemani aliwataka TPDC kuunganisha nyumba kuanzia Hamsini ( 50) na kuendelea katika maeneo ya Mwenge na Mikocheni kwa kuwa tayari miundombinu ya Bomba la Gesi asilia kwa matumizi ya nyumbani limepita maeneo hayo.
kuhusu suala la bei ya kuwauzia wateja, Dkt. Kalemani alisema kuwa Gesi hiyo itauzwa kwa Wananchi kwa pungufu ya 40% ya bei ya mitungi ya gesi itakayokuwa sokoni kwa wakati huo.
“Hii ni gesi yetu na Bomba ni la kwetu, vyote vinapatikana hapahapa nchini, ni vyema iuzwe kwa bei ya chini zaidi ya ile iliyopo sokoni kwa sasa, ili kila mwananchi aweze kumudu gharama zake pia itasaidia kupunguza matumizi ya mkaa na kulinda misitu yetu,” alisema Dkt. Kalemani.
Dkt. Kalemani pia aliwaagiza TPDC kuendelea na taratibu za kuwaunganisha wananchi wa Mtwara na huduma ya Gesi asilia katika nyumba zao kama itakavyofanyika jijini Dar es salaam hivi karibuni.
Aidha alilishauri Shirika hilo, kutumia wataalam wake wa ndani kupitia Shirika lake Tanzu la kulinda Miundombinu ya Gesi ( GASCO) ili kusambaza Gesi asilia kwenye nyumba za wananchi badala ya kutegemea wakandarasi ambao mchakato wa kuwapata unachukua muda mrefu.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa TPDC, Mhandisi Kapuulya Musomba, alifafanua kuwa gharama za uunganishwaji wa huduma ya Gesi asilia katika nyumba za wananchi itategemea na ramani ya nyumba husika pamoja na umbali wa nyumba kutoka ilipopita miundombinu ya Bomba la gesi asilia linalotumika kusambaza gesi katika maeneo ya makazi.
Vilevile, Mhandisi Musomba aliweka wazi kuwa mfumo wa kusambaza Gesi asilia katika nyumba za wananchi utakuwa kama ule unaotumika kusambaza huduma ya maji, lakini ulipaji wa gharama za matumizi ya gesi hiyo utakuwa kama ule unaotumiwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Lipa Umeme Kadri Unavyotumia ( LUKU) kwa maana kwamba kila mtumiaji atalipia huduma kadri atakavyokuwa akitumia.
Gesi itakayokuwa ikisambazwa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani ni ile inayozalishwa katika Visima vya Gesi vilivyopo katika Mkoa wa Lindi na Mtwara.
Share:

DODOMA: Bashe anena "Lolote Litakalonikuta ni Mipango ya Mungu"


Mbunge wa Nzega (CCM), Hussein Bashe amewahakikishia wananchi wa Tanzania kuwa hoja yake aliyoiwakilisha kwa Katibu wa Bunge kuwa haiwezi kukwamishwa na jambo lolote kwa madai hakuna kisichojulikana kinachoendelea kutoka katika nchi.


Bashe ametoa kauli hiyo jana (Machi 08, 2018) wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuelezea sababu zilizompelekea yeye kama Mbunge kuandika barua ya kutaka kuundwe kwa kamati ya uchunguzi dhidi ya matukio mbalimbali yanayoonesha kutishia umoja, usalama na mshikamano wa taifa la Tanzania.


"Madhumuni ya kikatiba ya Chama cha Mapinduzi  (CCM) ni kuwasemea wananchi, kuwatetea kwa hiyo natimiza wajibu wangu kama Mbunge sioni kama nitapoteza Ubunge wangu katika hili. 

"Mimi ninaamini nitapoteza ubunge wangu kwasababu zifuatazo, endapo nitashindwa kutimiza wajibu wangu ndani ya Bunge, nikishindwa kutimiza wajibu wangu ndani ya Jimbo langu kwa maana nimeshindwa kuisimamia serikali katika kuleta maendeleo, nimeshindwa kutimiza ahadi wakati wa uchaguzi katika jimbo langu na mwisho wanaccm watakaposema kwenye mchakato wa kidemokrasia wa kura kwamba Hussein wewe hapana.


"Mimi ni muumini wa kiislamu ninaamini kila binadamu umauti utamfika (kifo) na chochote kitakachonifika ni kile ambacho amekipanga Mwenyezi Mungu lakini sina hofu yeyote kwasababu hili sio taifa la namna hiyo.

"Nikiwa kama Hussein sidhani hii hoja kama inakwenda kukwama kwasababu unapoikwamisha hoja unapaswa kusema unaikwamisha kwa kutumia misingi gani kama watu wanaamini kwa kila kinachotokea ndani ya ardhi ya Tanzania sioni kama itakwama.


"Bunge limeshafanya maamuzi mbalimbali juu ya masuala mbalimbali katika rekodi ya nchi hii, kwa hiyo mimi nadhani ni muhimu tukatoa fursa jambo hili lifike Bungeni na likifika huko kama litakataliwa basi tujue ni kwasababu zipi na  kama nilivyofanya kuwaambia watanzania ndivyo hivyo nitarudi kuwaambia limekataliwa kwasababu zipi na hapo tutajadili hatua za kufanya".


Kwa upande mwingine, Bashe amesema anasubiria majibu ya barua aliyotuma kutoka kwa Katibu wa Bunge Pamoja na Katibu Chama cha Mapinduzi (CCM) ambayo ameeleza dhamira na nia yake huku akisisitiza zaidi kuwa jambo hilo hajalifanya kwa mihemuko (kukurupuka) bali amefanya kwa umakini wa hali ya juu na utafiti wa kutosha.


Share:

DAR ES SALAAM: Mtuhumiwa wa Maandamano ya CHADEMA awadai polisi gari yake

Mfuasi wa CHADEMA, Ally Rajabu anayekabiliwa na kesi ya kufanya mkusanyiko usio halali ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anaomba arejeshewe gari lake ambalo lipo mikononi mwa polisi.

Ally Rajabu ni mshtakiwa wa 28 kati ya 31 wakiwemo watatu waliopigwa risasi na Polisi ambao ni wafuasi wa chama hicho wanaokabiliwa na kesi ya kufanya mkusanyiko usio halali maeneo ya Kinondoni Mkwajuni Dar es Salaam.

Awali kabla ya kueleza hayo, Wakili wa Serikali Aldo Mkini, amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Naye Wakili wa utetezi, Alex Massaba amedai kuwa wateja wake wawili ni wagonjwa na wameshindwa kufika mahakamani hapo.

Baada ya kueleza hayo, mshtakiwa wa 28, Ally Rajabu ameieleza mahakama kuwa anaomba kurudishiwa gari lake ambalo linashikiriwa na Jeshi la Polisi tangu siku ya maandamano.

Hata hivyo, Hakimu Mashauri amesema kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kuingilia masuala yaliyofanyika Polisi ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi April 4, 2018.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Thabitha Mkude, Khaji Lukwambe, Emmanuel Kimio, Mohamed Juma, Husein Mnimbo na wenzao kwa pamoja wanadaiwa kati ya  February 16, 2018 maeneo ya Mkwajuni Kinondoni DSM walifanya mkusanyiko usio wa halali kinyume cha sheria.

CHANZO: MPEKUZI
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>