KENYA: Kenyatta, Odinga wakutana Nairobi
Hii ni mara ya kwanza kwa wawili hao kukutana tangu walipotofautiana kuhusu uchaguzi mkuu uliokuwa na upinzani mkali wa Agosti 8, 2017 na wa marudio Oktoba 26 ambao Odinga alisusia.
Agenda ya kikao chao haikuwekwa wazi. Baada ya kikao chao Kenyatta na Odinga walitarajiwa kulihutubia taifa.
Seneta wa Siaya James Orengo, mshirika wa karibu wa Odinga aliliambia shirika la habari la Reuters akithibitisha kufanyika kikao hicho.
“Kinafanyika sasa, lakini tutatoa maelezo zaidi kitakapokuwa kimemalizika,” amesema.
Msemaji wa Ikulu Manoah Esipisu aliwaambia waandishi wa habari kwamba Odinga atakuwa wa kwanza kuhutubia na kisha Rais Kenyatta atatoa maoni yake.
Kikao cha viongozi hao kimefanyika siku ambayo Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex Tillerson anatarajiwa kuwasili Nairobi akiwa katika ziara ya Afrika.
CHANZO: MWANCHI
DAR ES SALAAM: MAGONJWA YA FIGO YANAATHIRI ZAIDI WANAWAKE
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile wakati akitoa tamko la siku ya Figo duniani ambapo huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi.
Kwa upande wa Tanzania Naibu Waziri huyo alisema ugonjwa huo umekuwa ukiongezeka na tafiti zilizofanya Kanda ya Kaskazini mwaka 2014, ulionyesha kuwa kati ya 7% – 15% ya Watanzania wana matatizo sugu ya figo na kwa asilimia kubwa yamekuwa yakichangiwa na magonjwa ya Shinikizo la Damu na Kisukari
Hata hivyo aliongeza kuwa kwa utafiti uliofanywa na Hospitali ya Kanda Bugando, umeonesha kuwa 83% ya Wagonjwa wa Kisukari wana matatizo sugu ya figo na kati ya hawa, 25% walikuwa wanahitaji huduma za usafishaji damu.
“Wagonjwa waliokuwa wanapatiwa huduma ya kusafisha damu kutokana na figo kushindwa kufanya kazi, ambao ni wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) walikuwa 178. Kwa sasa idadi ya Wagonjwa hawa imeongezeka na kufikia 783.
Alisema Serikali imekuwa ikipeleka wastani wa wagonjwa thelathini na tano(35) kwa mwaka nje ya nchi kwa ajili ya kupandikiza figo na idadi ya waliokwishapandikizwa figo na ambao wanafuatiliwa matibabu yao katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ni takribani 204.“Gharama za kupandikiza figo nje ya nchi ni wastani wa fedha za Kitanzania milioni 75 hadi 77 kwa mtu mmoja,ikijumuisha upandikizaji,nauli na malazi”Alisema Dkt.Ndugulile
Dkt.Ndugulile alitoa wito kwa wananchi kubadili jinsi ya kuandaa vyakula nyumbani, mfano kwa kupunguza kiasi cha chumvi kwenye chakula na kiasi cha mafuta kutasaidia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza magonjwa shinikizo la damu (hypertension), kisukari na unene wa kupindukia, vile vile kuhamasisha familia kufanya mazoezi.Kaulimbiu ya maadhimisho ya siku ya figo ya mwaka huu wa 2018 ni “FIGO NA AFYA YA WANAWAKE: WASHIRIKISHWE, WATHAMINIWE NA WAWEZESHWE”.
CHANZO: AFYABLOH Na WAMJW. Dar es salaam.
MASASI:wasichana waonyesha vipaji kwa kusakata "volleyball"
Timu ya volleyball ya
watoto wa kike kutoka shule ya msingi na sekondari MKALAPA Kata ya NDANDA iliyopo
Halmashauri ya Wilaya ya MASASI wameadhimisha siku ya wanawake duniani kwa mchezo
wa volleyball.
Wakizungumza baada ya
mchezo huo, wamefurahi na kuiomba jamii
kutoa kipaumbele katika michezo inayohusisha jinsia ya kike.
Ikumbukwe kuwa timu ya watoto hao ni moja kati
ya timu ambazo zimeupa ushindi Mkoa wa MTWARA katika mashindano ya UMISETA na UMITASHUMTA,
hivyo watoto wa kike wakiwezeshwa wanaweza katika kujitelea maendeleo na kushiriki katika safari ya kuelekea uchumi wa
Viwanda kwa kutumia vipaji vyao.
WAKATI HUOHUO
Halmashauri
ya Wilaya ya MASASI imeadhimisha siku ya Wanawake duniani katika Kata ya NDANDA
huku Mambo MATATU ya kumwezesha mwanamke ili kushiriki kwa vitendo kuelekea
uchumi wa viwanda ifikapo 2025 ikiwemo kuwawezesha kielimu, kuwapa mitaji na
kuwashirikisha katika maamuzi yakisisitizwa.
Halmashauri ya wilaya ya
Masasi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya shilingi milioni 79,445,000
zimekopeshwa kwa vikundi 31 vya wanawake ikiwa ni mitaji ya kuendeleza biashara
zao na hivyo kuzalisha kwa tija ili kukuza uchumi wa kaya na Taifa kwa ujumla.
WAKATI HUOHUO
Halmashauri
ya Wilaya ya MASASI imeadhimisha siku ya Wanawake duniani katika Kata ya NDANDA
huku Mambo MATATU ya kumwezesha mwanamke ili kushiriki kwa vitendo kuelekea
uchumi wa viwanda ifikapo 2025 ikiwemo kuwawezesha kielimu, kuwapa mitaji na
kuwashirikisha katika maamuzi yakisisitizwa.
Halmashauri ya wilaya ya
Masasi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya shilingi milioni 79,445,000
zimekopeshwa kwa vikundi 31 vya wanawake ikiwa ni mitaji ya kuendeleza biashara
zao na hivyo kuzalisha kwa tija ili kukuza uchumi wa kaya na Taifa kwa ujumla.
Kauli mbiu ya siku ya wanawake duniani mwaka 2018
unasema"KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA: TUIMARISHE USAWA WA KIJINSIA NA
UWEZESHAJI WANAWAKE VIJIJINI"
RUKWA: WAZIRI UMMY AWAONYA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI WASIOTENGA FEDHA ZA UWEZESHAJI WANAWAKE
Ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mkoa wa Rukwa ambapo amepokea changamoto kutoka kwa wanawake wengi kuhusu utoaji mdogo wa mikopo na wengine kutopata kabisa mikopo kutoka Halmashauri zao.
Ummy amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashuri zote nchini kutenga asimilia 4 kwa ajili ya wanawake na kutoa mikopo yenye tija itaakayoweza kuwasaidia wanawake kujikwamua kiuchumi na sio kurudi nyuma kiuchumi.
“Mikopo ya laki tatu haina tija toeni kikopo yenye tija itakayoendana na kauli mbiu ya kuelekea uchumi wa viwanda,”alisema Mhe. Ummy
Mhe. Ummy ameongeza kuwa ili kufikia azma ya Tanzania ya Viwanda basi Halmashauri hazina budi kujiwekea mikakati ya kutoa mikopo mikubwa itakayo wawezesha wanawake na wananchi kwa ujumla kufikia dhana hiyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kalembo Mhe. Julieth Binjula ameiomba Serikali kuendelea kuwawezesha wanawake kwa kuwapa elimu ya jinsi ya kutumia fedha na kuendesha miradi mbalimbali itakayo wakwamua kiuchumi.
Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Bw. Khalfan Haule amesisitiza wadau kushirikiana na Serikali pale ambapo wanaweza kuwawezesha wanawake sehemu walipo ili waweze kujikwamua kiuchumi na kutoa mchangokatika kuchangia kujiletea maendeleo jumuishi.
Siku ya Wanawake Duniani 2018 kilele chake ni siku ya tarehe 8 Machi, 2018 na Kaulimbiu inayoongoza maadhimisho haya ni‘‘KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA: TUIMARISHE USAWA WA JINSIA NA UWEZESHAJI WA WANAWAKE VIJIJINI”. Dhamira ya Wizara nikuona kila mdau mmoja mmoja anaelewa madhumuni ya kaulimbiu na kuchukua hatua kuchangia utekelezaji wa ujumbe mahususi wa kuwajumuisha wanawake wa vijijini katika maendeleo yao na ya Taifa kwa ujumla.
CHANZO: DEWJBLOG
UNIDO TAYARI KUSAIDIA TANZANIA YA VIWANDA
Kauli hiyo imetolewa katika hafla ya
chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO
Li Yong ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania na pia ya kwanza
nje ya makao makuu ya Shirika hilo baada ya kuchaguliwa kwake kwa mara ya pili
mwaka jana.
Alisema katika hotuba yake kwamba moja ya
majukumu makubwa ya shirika hilo ni kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu
(SDGs) hasa lengo namba tisa la maendeleo na teknolojia
kwa ajili ya ustawi wa nchi hizo.
Aidha alisema ili kufanikisha hilo
kumesisitizwa ushirikiano ambao ni lengo namba 17 la SDGs.
Alisema sekta binafsi ikishirikiana vyema
na serikali ndiyo inayoendesha uchumi hasa katika kutoa fursa za kazi kwani
asilimia 80 ya kazi kila mwaka hutolewa na sekta binafsi.
Alisema katika hotuba yake hiyo kwamba
amefurahishwa na malengo ya Tanzania na nia ya Shirika hilo kuona kwamba
malengo hayo kuelekea uchumi wa kati wa viwanda yanatekelezwa kwa kuangalia
vionjo muhimu.
Aidha alisema kwamba wataendelea
kushirikiana na sekta binafsi kupitia TSPF kuhakikisha kwamba wananchi
wanashirikishwa katika malengo ya maendeleo ili kuwa na malengo endelevu na
yanayozingatia mazingira.
Naye Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini-
TPSF Dr. Reginald Mengi akizungumza katika hafla hiyo aliitaka UNIDO kusaidia
kutengeneza utajiri nchini Tanzania.
Dr. Mengi alisema kwamba ziara ya kiongozi
huyo imekuja wakati muafaka, wakati ambapo Tanzania inaelekeza macho yake
katika uchumi wa kati na hivyo kuwa na nafasi ya kusaidia ndoto hiyo kufanikiwa.
Alisema wakati nchi nyingi zimekuwa
zikipiga maendeleo, zimekuwa na msingi dhaifu wa uchumi wa viwanda kutokana na
kusafirisha zaidi bidhaa ambazo hazijasindikwa au zinazotokana na uziduaji.
Alisema hali hiyo pamoja na kuipa utajiri
nchi imekuwa haitawanyi utajiri uliopo.
Alisema kutokana na hali hiyo, UNIDO ina
kazi kubwa ya kusaidia Tanzania kufikia lengo lake la viwanda hata kusaidia
kuanzishwa kwa maeneo ya viwanda (Industrial Park).
Aidha aliishukuru UNIDO kwa kuwezesha
sekta binafsi na serikali kukaa pamoja kupitia Baraza la Taifa la Biashara
ambako kunakuwa na mazungumzo yenye tija kuhusiana na maendeleo ya biashara na
uchumi nchini Tanzania.
Alifafanua kwamba UNIDO ina nafasi kubwa
ya kuisaidia Tanzania hasa katika mipango mikakati yake kwa kuunganisha sekta
binafsi na umma ili kuiharakisha Tanzania kuelekea uchumi wa kati wenye
kutegemea viwanda.
Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda pamoja na Kimataifa Dr Augustine
Mahiga, ambaye wizara yake ndiye ilimwalika Mkurugenzi mkuu huyo, pamoja na
kumshukuru kwa kuitikia wito huo aliitakabkusaidia kuchagiza maendeleo ya
viwanda.
Alisema kwamba viwanda vya Tanzania bado
vichanga na vinahitaji kusaidiwa na kupewa nguvu ya kuendelea mbele kwani
pamoja na uchanga wake mchango wake katika kuelekea uchumi wa kati ni mkubwa.
Awali kabla ya hafla ya chakula cha mchana
UNIDO ilitiliana saini na serikali ya Tanzania waraka wa kusaidia kuitoa
Tanzania katika mipango ya kitaifa kwenda kwenye mipango ya nchi na washirika
ili kufikia uchumi wa kati.
Makubaliano hayo yalisainiwa jijini Dar es
Salaam kati ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles
Mwijage pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO, Li Yong huku yakishuhudiwa na
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
DAR ES SALAAM: WAZIRI NDALICHAKO, ANNA MAKONDA WATOA SOMO KWA WANAWAKE
Ikiwa leo Machi 8, 2018 ni kilele cha maadhimisho ya siku ya
wanawake duniani, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Stadi, Profesa
Joyce Ndalichako na Spika Mstaafu wa Bunge, Anna Makinda wametoa somo kwa
wanawake hapa nchini.
Akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa
kuhusu masuala ya maendeleo endelevu ya Wanawake barani Afrika, Prof.
Ndalichako amewataka wanawake kufanya kazi kwa bidi ili waweze kuaminiwa na
jamii.
“Wito wangu ni kwamba tuendelee kufanya
kazi kwa bidii kwa sababu historia imemuweka mwanamke katika nafasi isiyo nzuri
kwa hiyo wanawake tukiendelea kufanya kazi kwa bidii mchango wetu kwa jamii
utaendelea kuonekana na kuthaminiwa na hivyo tunaweza tukawa tunapata nafasi
kubwa na nzuri ya kulitumikia taifa, hii historia ya kubaki nyuma tutaiondoa
wanawake wenyewe kwa kufanya kazi kwa bidi,” amesema.
Naye Makinda amewataka wanawake kujiamini
sambamba na kuwa na uthubutu huku akiwasihi kujitika katika utafutaji wa elimu
kwani ndiyo mkombozi wa maendeleo ya wanawake.
“Elimu ni kitu muhimu sana, wanawake wengi
elimu zao ni ndogo wananyanyasika wananyang’anywa mali sababu hawajui wanaenda
wapi, elimu yenyewe siyo ya utaniutani, wenyewe wanasoma lakini hawajui
wanasoma nini. Mkombozi wa mwanamke ni kupatikana elimu sahihi ya kuweza
kupambanua maisha yake na kujua haki zake ziko wapi na si kumdekeza sababu
ukimdekeza hatuwezi kufanya chochote,” amesema na kuongeza.
“Elimu inamfanya mwanamke athubutu, kama
huna elimu hijuamini ndiyo unatengeneza mazingira ya kupata mafanikio kwa
kupitia mtu, kusoma vizuri kujiamini, kuwa na uthubutu mwengine anataka kwenye
kazi apelekwe na mtu.”
Na Regina Mkonde
DAR ES SALAAM: Jaji Mkuu awataka hawa wajitathimini
Jaji Mkuu wa Tanzania, PROF. IBRAHIM
JUMA amewataka watendaji na wataalamu wa Mahakama, nchini kujitathmini na kuona
namna wanavyoweza kutoa msukumo wa maboresho wa Mahakama katika suala la kutoa
haki kwa wakati
Jaji PROF. JUMA amesema hayo Jijini ARUSHA wakati akifungua
Mkutano wa watendaji na wataalam wa Mahakama wenye lengo la kutathmini
utekelezaji wa mpango wa maboresho wa Mahakama nchini.
Jaji Mkuu huyo wa Tanzania amesema kuwa kuna tatizo la utoaji wa
taarifa muhimu kwa Wananchi kitika MAHAKAMA jambo linalowanyima wananchi haki
ya kufuatilia mashauri yao.
Pia Jaji Mkuu amewataka watendaji kufanya Tathmini na kuona
namna wanavyeweza kutoa msaada katika kufikia malengo yaliyokusidiwa na
Mahakama.
Msikilize hapa chini Jaji Mkuu akiongea zaidi.
DODOMA: DKT. KALEMANI AIAGIZA TPDC KUHARAKISHA UUNGANISHAJI WA GESI MAJUMBANI
Dkt. Kalemani aliyasema hayo tarehe 3 Machi, 2018 ofisini kwake mkoani Dodoma alipokutana na watendaji wa TPDC kwa lengo la kujadili suala la usambazaji wa Gesi asilia katika nyumba za Wananchi pamoja na bei watakayouziwa wananchi hao.
Katika mazungumzo hayo, Dkt. Kalemani aliwataka TPDC kuunganisha nyumba kuanzia Hamsini ( 50) na kuendelea katika maeneo ya Mwenge na Mikocheni kwa kuwa tayari miundombinu ya Bomba la Gesi asilia kwa matumizi ya nyumbani limepita maeneo hayo.
kuhusu suala la bei ya kuwauzia wateja, Dkt. Kalemani alisema kuwa Gesi hiyo itauzwa kwa Wananchi kwa pungufu ya 40% ya bei ya mitungi ya gesi itakayokuwa sokoni kwa wakati huo.
“Hii ni gesi yetu na Bomba ni la kwetu, vyote vinapatikana hapahapa nchini, ni vyema iuzwe kwa bei ya chini zaidi ya ile iliyopo sokoni kwa sasa, ili kila mwananchi aweze kumudu gharama zake pia itasaidia kupunguza matumizi ya mkaa na kulinda misitu yetu,” alisema Dkt. Kalemani.
Dkt. Kalemani pia aliwaagiza TPDC kuendelea na taratibu za kuwaunganisha wananchi wa Mtwara na huduma ya Gesi asilia katika nyumba zao kama itakavyofanyika jijini Dar es salaam hivi karibuni.
Aidha alilishauri Shirika hilo, kutumia wataalam wake wa ndani kupitia Shirika lake Tanzu la kulinda Miundombinu ya Gesi ( GASCO) ili kusambaza Gesi asilia kwenye nyumba za wananchi badala ya kutegemea wakandarasi ambao mchakato wa kuwapata unachukua muda mrefu.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa TPDC, Mhandisi Kapuulya Musomba, alifafanua kuwa gharama za uunganishwaji wa huduma ya Gesi asilia katika nyumba za wananchi itategemea na ramani ya nyumba husika pamoja na umbali wa nyumba kutoka ilipopita miundombinu ya Bomba la gesi asilia linalotumika kusambaza gesi katika maeneo ya makazi.
Vilevile, Mhandisi Musomba aliweka wazi kuwa mfumo wa kusambaza Gesi asilia katika nyumba za wananchi utakuwa kama ule unaotumika kusambaza huduma ya maji, lakini ulipaji wa gharama za matumizi ya gesi hiyo utakuwa kama ule unaotumiwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Lipa Umeme Kadri Unavyotumia ( LUKU) kwa maana kwamba kila mtumiaji atalipia huduma kadri atakavyokuwa akitumia.
Gesi itakayokuwa ikisambazwa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani ni ile inayozalishwa katika Visima vya Gesi vilivyopo katika Mkoa wa Lindi na Mtwara.
DODOMA: Bashe anena "Lolote Litakalonikuta ni Mipango ya Mungu"
Mbunge wa Nzega (CCM), Hussein Bashe amewahakikishia
wananchi wa Tanzania kuwa hoja yake aliyoiwakilisha kwa Katibu wa Bunge kuwa
haiwezi kukwamishwa na jambo lolote kwa madai hakuna kisichojulikana
kinachoendelea kutoka katika nchi.
Bashe ametoa kauli hiyo jana (Machi 08, 2018) wakati
alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam kwa lengo la
kuelezea sababu zilizompelekea yeye kama Mbunge kuandika barua ya kutaka
kuundwe kwa kamati ya uchunguzi dhidi ya matukio mbalimbali yanayoonesha
kutishia umoja, usalama na mshikamano wa taifa la Tanzania.
"Madhumuni ya kikatiba ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) ni kuwasemea wananchi, kuwatetea kwa hiyo natimiza wajibu
wangu kama Mbunge sioni kama nitapoteza Ubunge wangu katika hili.
"Mimi ninaamini nitapoteza ubunge wangu
kwasababu zifuatazo, endapo nitashindwa kutimiza wajibu wangu ndani ya Bunge,
nikishindwa kutimiza wajibu wangu ndani ya Jimbo langu kwa maana nimeshindwa
kuisimamia serikali katika kuleta maendeleo, nimeshindwa kutimiza ahadi wakati
wa uchaguzi katika jimbo langu na mwisho wanaccm watakaposema kwenye mchakato
wa kidemokrasia wa kura kwamba Hussein wewe hapana.
"Mimi ni muumini wa kiislamu ninaamini kila
binadamu umauti utamfika (kifo) na chochote kitakachonifika ni kile ambacho
amekipanga Mwenyezi Mungu lakini sina hofu yeyote kwasababu hili sio taifa la
namna hiyo.
"Nikiwa kama Hussein sidhani hii hoja kama
inakwenda kukwama kwasababu unapoikwamisha hoja unapaswa kusema unaikwamisha
kwa kutumia misingi gani kama watu wanaamini kwa kila kinachotokea ndani ya
ardhi ya Tanzania sioni kama itakwama.
"Bunge limeshafanya maamuzi mbalimbali juu ya
masuala mbalimbali katika rekodi ya nchi hii, kwa hiyo mimi nadhani ni muhimu
tukatoa fursa jambo hili lifike Bungeni na likifika huko kama litakataliwa basi
tujue ni kwasababu zipi na kama nilivyofanya kuwaambia watanzania ndivyo
hivyo nitarudi kuwaambia limekataliwa kwasababu zipi na hapo tutajadili hatua
za kufanya".
Kwa upande mwingine, Bashe amesema anasubiria majibu
ya barua aliyotuma kutoka kwa Katibu wa Bunge Pamoja na Katibu Chama cha
Mapinduzi (CCM) ambayo ameeleza dhamira na nia yake huku akisisitiza zaidi kuwa
jambo hilo hajalifanya kwa mihemuko (kukurupuka) bali amefanya kwa umakini wa
hali ya juu na utafiti wa kutosha.
DAR ES SALAAM: Mtuhumiwa wa Maandamano ya CHADEMA awadai polisi gari yake
Mfuasi wa CHADEMA, Ally Rajabu anayekabiliwa na kesi ya kufanya mkusanyiko usio halali ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anaomba arejeshewe gari lake ambalo lipo mikononi mwa polisi.
Ally Rajabu ni mshtakiwa wa 28 kati ya 31 wakiwemo watatu waliopigwa risasi na Polisi ambao ni wafuasi wa chama hicho wanaokabiliwa na kesi ya kufanya mkusanyiko usio halali maeneo ya Kinondoni Mkwajuni Dar es Salaam.
Awali kabla ya kueleza hayo, Wakili wa Serikali Aldo Mkini, amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.
Naye Wakili wa utetezi, Alex Massaba amedai kuwa wateja wake wawili ni wagonjwa na wameshindwa kufika mahakamani hapo.
Baada ya kueleza hayo, mshtakiwa wa 28, Ally Rajabu ameieleza mahakama kuwa anaomba kurudishiwa gari lake ambalo linashikiriwa na Jeshi la Polisi tangu siku ya maandamano.
Hata hivyo, Hakimu Mashauri amesema kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kuingilia masuala yaliyofanyika Polisi ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi April 4, 2018.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Thabitha Mkude, Khaji Lukwambe, Emmanuel Kimio, Mohamed Juma, Husein Mnimbo na wenzao kwa pamoja wanadaiwa kati ya February 16, 2018 maeneo ya Mkwajuni Kinondoni DSM walifanya mkusanyiko usio wa halali kinyume cha sheria.
CHANZO: MPEKUZI
CHANZO: MPEKUZI










