• VIPINDI VYA ELIMU HASA KILIMO

    Tuna vipindi mbalimbali vinavyohamasisha jamii katika kilimo cha Korosho, ufuta na Mhogo. tunaendelea na jamii inafurahia uwepo wa vipindi kwa sababu wanakutana na wataalamu moja kwa moja

  • SAUTI ZA WANAJAMII HUSIKIKA

    Sauti ni muhimu hasa unapohudumia jamii ya vijijini, wasikilizaji hupenda kusikia sauti zao kwakua watu wao wanawafahamu, hivyo huwa kivutio kwako na ni rahisi jamii kuamini kuwa mpo pamoja nao

  • MICHEZO MBALIMBALI

    Afya ni sehemu ya vipindi vyetu kwenye radio, hii husaidia kuwapa fursa watu wanaopenda michezo kuwa pamoja na kubadirishana mawazo, michezo hujenga urafiki na undugu baina mwa jamii

  • WATOTO KATIKA RADIO

    Hupenda kushiriki na hujiona sehemu ya radio kwa kuwa huishi katika jamii, kipindi cha watoto kimekuwa kikifuatiliwa na watu wazima kwasababu kuu moja tu, watoto waishio vijijini huwa hawapewi kipaumbele kama tulivyofanya Jamii fm

  • SIKIKA KATIKA RADIO

    Kipengere hiki hutoa fursa kwa wanajamii wanaotuzunguka kuongea moja kwa moja na kueleza hoja zao ambazo baadae hufuatiliwa kwa undani

“Ni kosa polisi kujichunguza kwa Matukio yanayowahusu”......Hili ni Tamko la Asasi za Kiraia Kuhusu Hali ya Usalama Nchini

WITO WA ASASI ZA KIRAIA KUHUSU HALI YA USALAMA WA RAIA, HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA WA SHERIA NCHINI

UTANGULIZI
Sisi Asasi za Kiraia tulioweka sahihi katika Waraka huu, kwa umoja wetu tumesikitishwa sana na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu, utawala wa sheria na usalama wa raia vinavyoendelea hivi sasa hapa nchini. Asasi za Kiraia (Civil Society Organizations) ni taasisi huru zilizoundwa kwa mujibu wa sheria mbalimbali nchini. Taasisi hizi zinatekeleza majukumu mbali mbali hapa nchini katika kuhakikisha ustawi wa taifa letu.

Hivyo tunawaomba viongozi na watanzania kwa ujumla kutambua juhudi zinazofanywa na asasi za kiraia katika kutetea maslahi ya umma, kuleta maendeleo na mabadiliko mengine katika jamii. Katika nchi mbali mbali zilizoendelea, mchango wa asasi za kiraia umesaidia kuleta mabadiliko makubwa ya kimfumo na kimaendeleo na hivyo nchi/mataifa husika kuona umuhimu wa kuheshimu AZAKI na kuweka ushirikiano mzuri wa serikali na asasi za kiraia. 

Pamoja na changamoto changamoto mbalimbali , AZAKI pia zimetambua na kumpongeza Rais wa Jamhuri wa Tanzania kwa kuonyesha juhudi katika kupamnbana na matumizi mabaya ya rasilimai za umma, kuleta nidhamu katika taasisi za umma na usimamizi mzuri wa mali asili za Watanzania. 

AZAKI zitambua kabisa umuhimu wa maendeleo ya kitaifa katika kulinda na kuheshimu haki za binadamu kwa kuwa vitu vyote hivi huenda pamoja na hutegemeana. Kwa maana hiyo tuko bega kwa bega na Rais wetu katika kuhakikisha Tanzania inapata maendeleo makubwa, kwa kuwa maendeleo hayo ndiyo msingi wa haki za binadamu na maisha bora kwa Mtanzania.

TATHMINI YA HALI YA HAKI ZA BINADAMU, UTAWALA WA SHERIA NA USALAMA
Katika utendaji kazi wa asasi za kiraia, huwa zinapata muda wa kukaa na kufanya tathmini ya hali ya mambo mbali mbali ya kitaifa na kuangalia ni namna gani wao kama wadau na washiriki wa kuleta maendeleo na kuhakikisha mustakabali bora wa taifa unalindwa na kutetewa wakati wote. 

Mnamo tarehe 19/02/2017 Jukwaa la Wakurugenzi wa AZAKI (Tanzania CSOs Director’s Forum-CDF) Ililikaa kikao ili kufanya tathmini ya masuala mbalimbali yenye maslahi na mustakabali mzima wa taifa hili na kubaini masuala kadhaa ya ukiukwaji wa haki za binadamu, hali ya taharuki juu ya amani ya nchi, uhuru wa kujieleza, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa AZAKI, maamuzi yasiyozingatia sheria na taratibu, kuminywa kwa demokrasia ya taifa letu pamoja na chaguzi zisizo na usawa na zenye viashiria za umwagaji damuna kuhatarisha amani ya nchi.
 
Hali hii imetokana na matukio mbali mbali ambayo tumeyashuhudia na kwa kuzingatia historia ya nchi yetu hatukuwahi kuyashuhudia wala kudhani kwamba yangeweza kutokea. Matukio haya yamehusishakuvamiwa (mashambulizi), kuuawawa, kuumizwa, kupotea na kuteswa kwa watetezi wa haki za binadamu, wanahabari, wanasiasa na hata raia wa kawaida. Baadhi ya matukio hayo ni haya yafuatayo;

(i) Mauaji ya Mwanafunzi wa Chuo -Akwlina Baftah
Mnamo tarehe 16/02/2018 taarifa zilisambaa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii juu ya kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Akwilina Baftah ambaye anasadikiwa kuuwawa kikatili akiwa katika daladala na askari polisi waliokuwa wakiwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao walikuwa wanakwenda kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoniambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kwa ajili ya kudai fomu za mawakala wa uchaguzi. 

Jeshi la Polisi kupitia kwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, lilithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kukiri kwamba tukio hilo limetokea wakati polisi wakiwa wanafyatua risasi angani kuweza kuwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
 
Tukio hili limezua taharuki kubwa kwa taifa na jamii ya kimataifa kwani ni moja kati ya matukio mabaya yanayoendelea kutokea katika Taifa letu. Tukio la kuuwawa kwa mwanafunzi huyu limeleta simanzi kubwa sana kwa taifa kwakuwa limetokea kwa mtu asiyekuwa na hatia yoyote ile. 

Ni moja ya tukio ambalo limewaleta watanzania pamoja bila kujali dini zao, mirengo yao ya kisiasa, vyeo vyao, makabila yao au hali zao. 

Tukio hili limewakumbusha watanzania wengi kwamba kumbe ile amani iliyokuwa ikihubiriwa katika taifa hili inaweza potea ndani ya dakika chache bila kutarajia kama tusipoamka wote kudai Taifa kurudi katika misingi ya demokrasia, usawa, utawala wa sharia na haki za binadamu.

Wana AZAKI tunawashukuru wote wanaoendelea kuifariji familia hiyo hasa Waziri wa Elimu Bi-Joyce Ndalichako alieonyesha ukaribu wa kusimamia msiba huu kama waziri mwenye dhamana ya elimu nchini, lakini pia ushiriki wa Serikali katika kusaidia mazishi ya mwanafunzi huyo. 

Tunaipongeza Serikali kwa kuonyesha kujali na kuwafariji familia ya marehemu kutokana na msaada huo. Sisi kama wana Azaki tunaamini Serikali na wananchi wameguswa sana na msiba huo.
 
(ii) Vitendo vya kutekwa, kuuwa, kuumizwa na kupotea kwa watu mbalimbali
• Matukio ya kutekwa na kuuwa kwa viongozi mbalimbali hapa nchini yalishika kasi pale viongozi wa CCM, askari zaidi ya 10 na wananchi karibu 40 katika eneo la Kibiti walivyoanza kushambuliwa na kuuwawa bila wahusika kukamatwa. Matukio haya yameendelea hadi kwenye vipindi vya uchaguzi ambapo mnamo tarehe 11/02/2018 Kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ndugu Daniel John alitekwa na kishaaliuwawa kikatili wakati wa Kampeni za Uchaguzi mdogo wa jimbo la Kinondoni. Matukio haya ni mengi na yamekuwa yakijirudia kote hadi visiwani Zanzibar.
 
• Tarehe 7/09/2017 Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika na Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu alivamiwa na kupigwa risasi hadharani na watu wasiojulikana katika eneo la area D Mkoani Dodoma ambapo mpaka sasa watu hao hawajaweza kubainika na.
 
• Tarehe 21/11/2017 Mwandishi wa habari wa Mwananchi Communications Limited ndugu Azory Gwanda alipotea katika mazingira ya kutatanisha ambapo mpaka sasa hajapatikana licha ya wana AZAKi na waandishi wa habari kupaza sauti zao juu ya kupotea kwake.
 
• Msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Ben Saanane alipotea katika mazingira ya kutatanisha na taarifa za wapi alipo mpaka hazijawahi kutolewa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama wala kuwabaini waliohusika na tukio hilo.
 
• Matukio ya utekaji na uteswaji wa watu yamekithiri katika nchi yetu ambapo hivi karibuni tumeshuhudia matukio kadhaa ya kutekwa na kuteswa kwa wasanii, wanahabari ambao wanaonekana kutoa maoni mbadala juu ya masuala mbali mbali yanayoendelea katika nchi yetu.

(iii) Matumizi ya Sheria Kandamizi na Ukamataji Usiozingatia sheria
• Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 18 inatoa uhuru wa maoni kwa kila Mtanzania ata hivyo kumekuwa na sheria mbali mbali kama vile Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016, Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997, Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 pamoja na sheria zingine ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikiminya uhuru wa maoni kwa makundi mbali mbali pamoja na watanzania kwa ujumla.
 
• Tumeshuhudia katika kipindi kifupi cha utekelezwaji wa sheria kandamizi, magazeti mengi yamefungiwa, wanahabari wamevamia, kutekwa na kunyanyaswa, watu kufunguliwa mashtaka ya kughushi, kuvamiwa ofisi za mawakili, vyombo vya habari kupigwa faini kwa kurusha taarifa ambazo pengine zinaonyesha kasoro za uongozi. Hali hii imezua taharuki kubwa kwa tasnia ya habari ambapo sasa wanahabari wanafanya kazi katika mazingira magumu sana na ambayo sio salama hivyo kusababisha kuogopa kutoa taarifa juu ya uvunjifu wa haki za binadamu na mwenendo wa demokrasia nchini.
 
• Vyombo vya habari vimepigwa marufuku kutoa taarifa za uchaguzi, haza zile zinazonyesha kasoro katika uchaguzi, wengi tumesikitishwa na kitendo cha ITV kutakiwa kuomba radhi kwa taarifa ya kweli waliyorusha wakati wa upigaji kura kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni kwa kuonyesha tukio la wizi wa sanduku la kura wakati uchaguzi ukiendelea.
 
• Utawala wa sheria, Demokrasia na haki za kisiasa vimekuwa havisimamiwi vizuri na vyombo husika. Kwa mfano, Jeshi la Polisi nchini limekuwa likishindwa kutokuwa na upande katika mambo yanayowahusu raia na serikali au vyama vya siasa na hivyo kusababisha madhara na maafa kwa wananchi mbali mbali wa taifa hili.Vyombo hivi vya usalama vinalalamikiwa na wananchi kwa kutokufanya kazi zao kwa weledi, uhuru na usawa na kuonekana kama vinaingiliwa na kufanya kazi kwa maagizo mengi toka nje ya mifumo yao na kuondoa dhana ya kuwa vyombo kwa ajili ya ulinzi wa raia na mali zao.
 
• Tume ya taifa ya Uchaguzi nchini imejionyesha wazi kuwa siyo chombo huru kinachofaa kusimamia au kuwa msimamizi wa chaguzi za mfumo wa vyama vingi kutokana na muundo wake au wasimamizi wanaoteuliwa kuwa na uhusiano na vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi. Hili limeonekana dhahiri kwamba kuna mambo ambayo tume imeshindwa kuyasimamia wakati wa uchaguzi uliopita na hivyo kusababisha kutokea kwa vurugu na vifo/athari mbali mbali kwa viongozi wa vyama vya siasa na wananchi kwa ujumla. Kwa mfano, tukio la juzi la kuuwawa kwa mwanafunzi Akwilina Baftah ni matokeo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzina Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni kushindwa kusimamia vizuri zoezi la uchaguzi. 

Taarifa zaidi kuhusu uangalizi wa uchaguzi huo zitaletwa baadaye na muungano wa AZAKI zilizoshirikikufanya uangalizi wa uchaguzi baada ya taarifa hizo kukaguliwa kwanza na Tume kwa Mujibu wa taratibu mpya. Hili nalo ni jambo geni kabisa katika taratibu za uangalizi wa uchaguzi ambapo waangalizi walikuwa huru kutoa taarifa zao za uangalizi bila ya kusubiri taarifa hizo kuhakikiwa na TUME.
 
(iv) Hali ya Watetezi wa Haki za Binadamu na AZAKI
• Watetezi wa Haki za binadamu wameendelea kufanya kazi katika mazingira ambayo sio rafiki na hatarishi huku wengi wao wakifunguliwa kesi, kushambuliwa, kukamatwa na vyombo vya Dola ikiwemo kupewa majina mabaya na hata kuzushiwa kuwa baadhi yao sio raia wa Tanzania.
 
• Makundi mbali mbali na Asasi za kiraia zimeendelea kufanya kazi katika mazingira ambayo sio rafiki huku uhuru wao wa kufanya kazi na kujieleza ukiwa umeminywa kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria zinazoanzisha na/ama kulinda maslahi ya asasi za kiraia.
 
• Tumeshuhudia asasi za kiraia zikitishiwa kufungiwa huku zikiwa zinatekeleza majukumu yao kisheria. Nafasi ya asasi za kiraia imedhoofika kutokana na kauli mbali mbali za viongozi wa serikali pamoja na hatua zinazochukuliwa na serikali hivyo kufanya Asasi za kiraia kushindwa kutimiza majukumu yake kwa ufasaha na kwa wakati katika maeneo mablimbali ya nchi.
 
• Mfano AZAKI nyingi sasa zimekwama kutoa matangazo kwa vyombo vya habari kutokana na kutakiwa kupata kibali kwanza toka TAMISEMI baada ya kuyawasilisha matangazo hayo kwa viongozi kwa ukaguzi. Matangazo kama yale yaliyokuwa yakitolewa na HAKIELIMU kwa utaratibu wa sasa ni lazima kukaguliwa na kupata kibali ndipo chombo cha habari kiweze kuyatoa kwa umma.
 
• AZAKI zinazokwenda Mikoani kufanya kazi zinakumbana na upinzanimkubwa kutokana na maagizo ya kutaka kupata kibali toka Makao Makuu ya TAMISEMI kabla ya kwenda Mikoani
 
• Pia AZAKI zinashindwa kutoa taarifa zauangalizi wa uchaguzi kutokana na kutakiwa kupeleka kwanza taarifa hizo kwa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi kuzikagua ili kuangalia yaliyomo na kuiridhiwa IKIWAPENDEZA. Changamoto hii imeendana na changamoto ya kupata kibali kwa AZAKI kama waangalizi wa uchaguzi. Mfano yapo Mashirika mengine yalikwenda Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuomba kuwa waangalizi lakini walijibiwa kuwa kuna mashirika mengi yameeomba kufanya uangalizi hivyo nafasi zimejaa.
 
SISI Wana AZAKI tumeona tutumize majukumu yetu kwa kutafuta namna ambayo tunaweza kuijadili kwa pamoja jinsi ya kurekebisha changamoto hizi na kusonga mbele. Tusipofanya hivyo, taifa hili linaweza kuingia katika migogoro ambayo huzaa chuki na hatimaye kupoteza Amani yetu. Kwani kwa sasa kumekuwa na kauli zinazoashiria ubaguzi wa itikadi za kisiasa na kimaendeleo.

WITO WA AZAKI KWA SERIKALI NA TASISI HUSIKA
1. Serikali itazame upya suala la upatikanaji wa Katiba mpya kwani ndiyo suluhisho la matatizo mbali mbali yanayotokea katika jamii kwa sasa, kwani suala la katiba mpya kimekuwa ni kilio kikubwa na hitajio la watanzania wengi ili kutibu hali hii inayojitokeza sasa.Tunashauri Mchakato wa Katiba mpya ufanyike mwaka huu kwa kuwa mawaka 2019 na 2020 Taifa litakuwa bize na mambo ya uchaguzi. Tunamshauri Mhe Rais aitishe kikao cha wadau wote kujadili namna ya kuliweka hili suala kwa maslahi ya Taifa.
 
2. Tunaomba Tume Huru ya Uchaguzi ipatikane kabla ya chaguzi za 2019 na 2020, itakayoweza kusimamia usawa na haki kwa vyama vyote kuepusha madhara ambayo yanaweza kujitokeza kutokana na Tume kushindwa kusimamia misingi ya haki na usawa katika uchaguzi.Tume ya uchaguzi ifungue ofisi zake wilayani na kuajiri wataalam wake kuwa wasimamizi wa uchaguzi na kuachana na mfumo wa sasa unaonekana kuwa na mgonano wa kimaslahi. AZAKI tupo tayari kushirikiana na Serikali na wadau wengine wa maendeleo katika kulifanikisha hili.
 
3. Tunapendekeza iundwe Tume huru ya uchunguzi itakayohusisha AZAKI, Taasisi za Dini, Vyombo vya Habari, Baraza la Vyama vya Siasa, Wanahabari, Majaji/Mahakimu, Polisi, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora kufanya uchunguzi huru juu ya vifo na vitendo vya utekwaji na utesaji vilivyojitokeza wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Kinondoni. Matukio yanayowahusu Polisi kama watuhumiwa ni kosa kubwa kuwaachia wao wenyewe wajichunguze na hili limekuwa sasa chanzo cha matukio kuendelea kutokea na kutochukuliwa hatua.
 
4. Vyombo vya utoaji haki kama Polisi na Mahakama vifanyiwe maboresho na viachweviwe huru katika kutekeleza majukumu yake ili kuepusha wasiwasi na dhana ambayo imeanza kuonekana dhahiri kwamba vyombo vyetu vya utoaji haki haviko huru. Au kuthibitisha ile zana ambayo imeanza kuzoeleka kuwa kuna Mhimili mmoja umejichimbia kwenda chini kuliko mihimili mingine.
 
5. Tunalisihi na kulishauri Jeshi la polisi kutimiza wajibu wake kwa kufanya kazi kwa weledi, taaluma na sheria za nchi pamoja na kuacha kuegemea upande mmoja ili kuepusha lawama chuki na uhasama ambao unajengeka kwa wananchi kwa Jeshi hilo.
 
6. Jeshi la polisi liwe makini katika kutimiza wajibu wake wakati wa kuzuia maandamano, kwani kauli ambazo zimekuwa zikitolewa na viongozi wa Jeshi la Polisi na matumizi ya silaha za moto huonyesha wazi kwamba Polisi inashindwa kutumia njia zilizoanishwa kisheria kukabiliana na waandamanaji wasio na silaha na wasiofanya vurugu. Pia Jeshi la lifanye kazi kwa ushirikiano na wananchi pamoja na Asasi za kiraia na kwa namna yoyote kuepuka kutumia nguvu kubwa ili kuboresha dhana ya ulinzi shirikishi.
 
7. Askari wanaotuhumiwa kuhusika kusababisha kifo cha Mwanafunzi Akwilina wafikishwe katika vyombo vya sheria ili hatua stahiki zichukuliwe kwa aliyehusika na tukio hilo. Taifa liwe na mfumo huru au chombo huru (Oversite body) ya kuchunguza na kusimamia mashtaka yanayohusu vyombo vya usalama badala ya kuwaachia wao kufanya uchunguzi na kuendesha mashtaka.
 
8. Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni ambaye ndiye Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kinondoni ajipime mwenyewe kwa vitendo vyake alivyofanya katika uchaguzi huu kuhusu kuvuruga taratibu za uchaguzi na kuwanyima mawakala wa vyama vingine haki ya kusimamia uchaguzi pamoja na kusababisha uvunjifu wa amani ajipime kama anatsahili kuendelea katika nafasi hizo tena. Viongozi wengine wahusika nao wajitafakari.
 
9. Tume ya Utawala Bora na haki za binadamu nchini iingilie kati vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu nchini kwa kufanya utafiti huru juu ya yale yanayotokea katika jamii na kupendekeza njia sahihi za kushuhulikia ukiukwaji wa haki za binadamuTanzania.
 
10. Tunaziomba asasi za kiraia, asasi za kiserikali, wabunge, wanasiasa, mashirika mengine na wadau mbali mbali wa maendeleo kuendelea kupaza sauti na kuungana kwa pamoja kupigania haki, utawala wa sheria, demokrasia na amani ya nchi hii haswa kipindi hiki ambapo kumekuwepo na uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu.
 
11. Tunashauri kuwepo kwa Mjadala wa kitaifa utakwaowaleta pamoja makundi yote yaliyo kwenye jamii kama viongozi wa dini, taasisi za kitaaluma, vyama vya wafanyakazi, viongozi wa kisiasa, viongozi wa serikali, viongozi wakuu wastaafu na AZAKI ili kujadili amani ya nchi na umoja wetu wa kitaifa ambao uko hatarini kutoweka endapo hatua stahiki hazitachukuliwa.
 
12. Tunawaomba viongozi wa Serikali waone umuhimu kusikia sauti hizi kwa kutoa nafasi ya majadiliano na kundi hili ili kupokea mapendekezo mengi ambayo AZAKIzinawezatoa mapendekezokwa mustakabali wa Taifa letu.
 
13. Tunavishauri Vyama vya siasa kuendelea kutumia njia za amani kudai haki zao pale zinapovunjwa wakati AZAKI zinatafuta njia ya amani na ya mazungumzo na taasisi husika na uongozi kwa ujumla.
 
14. Bunge lirudi katika majukumu yake kama walivyofanya katika matukio ya serikali siku za nyuma kwa kuunda kamati za kibunge kuchunguza hali ya sasa ya utawala wa sheria, haki za binadamu, usalama wa raia na usawa katika jamii.
 
15. Tunaomba viongozi wa serikali (hasa wale wachache wenye mtizamo hasi kuhusu AZAKI) waone Asasi za Kiraia kama wadau wazuri wa maendeleo na hivyo kuondoa vikwazo vya sasa vinazidi kujitokeza wakati AZAKI zinapokuwa katika utekelezaji wa majukumu yao.
 
Mwisho, sisi AZAKI tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa Binti Akwilina na wote waliopoteza wapendwa wao Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi. Amina.
 
Imetolewa na Jukwaa la Wakurugenzi wa AZAKI Tanzania leo 21/02/2018
Share:

Serikali Yaridhia Gharama za Mazishi ya Akwilina


Familia ya marehemu  Akwilina Akwiline inaendelea na maandalizi ya mazishi, huku ikielezwa kuwa Serikali imekubali kuyagharimia lakini si kutoa fedha.

Serikali imefikia hatua hiyo baada ya jana Februari 20,2018 familia ya Akwilina kueleza kuwa bajeti ya mazishi ni Sh80 milioni.

Katibu wa kamati ya mazishi Moi Kiyeyeu, ambaye ni kaka wa Akwilina amesema Serikali imewajibu kuwa haitawapa fedha taslim bali itagharimia vitu vilioorodheshwa katika bajeti ya mazishi hayo.

"Tulipotoa bajeti hatukuwa na maana kuishinikiza Serikali itoe fedha zote bali ilikuwa mahitaji ya msiba hadi pale utakapoisha. Tunashukuru Mungu kwa Serikali kuridhia kugharimia," amesema Kiyeyeu.

Kuhusu hilo, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika taarifa iliyotolewa leo Februari 21,2018  imesema kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Dk Leonard Akwilapo ilipokea makisio ya gharama za mazishi ya Sh80 milioni kutoka kwa msemaji wa familia, Festo Kavishe.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha wizara hiyo, Mwasu Sware alisema baada ya kupokea makisio hayo Dk Akwilapo alitahadharisha kuwa kuna baadhi ya matumizi hayatakubaliwa kwa kuwa kisheria hayagharamiwi na Serikali.

Pia, katika makisio hayo kuna gharama ambazo zilikuwa zimepewa makadirio ya juu.

Alisema katibu mkuu aliagiza kuwe na kikao kati ya wizara na ndugu wa marehemu ili kuweka sawa changamoto hizo na kuwa na bajeti ya pamoja ambacho kilifanyika jana jioni Februari 20,2018 na kufikia muafaka.

“Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa taratibu nyingine za maandalizi ya mazishi zinaendelea vizuri,” amesema.

Wakati huohuo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amefika nyumbani kwa dada wa marehemu Mbezi Luis kuhani msiba.

Dk Mwakyembe amesema tukio la kifo cha Akwilina ni la kusikitisha
Share:

Mwenyekiti Wa Halmashauri Ya Misungwi Na Mwanasheria Wakamatwa

JESHI la Polisi mkoani Mwanza kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana  na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) mkoani hapa  imemkamata Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Bw. Anthony Bahebe.
 
Pia Mwanasheria wa Halmashauri hiyo Bw. Alphonce Sebukoto naye amekamatwa na Jeshi hilo. Viongozi wote hao wanakabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na ubadhilifu wa fedha za umma.
 
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema kukamatwa kwa viongozi hao kunatokana na tuhuma mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na matumizi mabaya ya madaraka.
 
Kamanda Msangi alisema, Bw. Sebukoto alikamatwa Februari 19, 2017 na Bw. Bahebe amekamatwa leo na wote wanaendelea kuhojiwa na Polisi kwa kushirikiana na TAKUKURU.
 
Naye Kamanda wa TAKUKURU wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Ernest Makale alisema Bw. Sebukoto aliidhinisha malipo ya sh.milioni 278 zilipwe katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw. Bahebe.

Alisema Bw. Sebukoto aliidhinisha malipo hayo kwa Bw. Bahebe Novemba 2017 wakati alipokuwa anakaimu nafasi ya ukurugenzi wa Halmashauri ya Misungwi ambapo jumla sh. milioni 138 ziliingizwa katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti huyo. Alisema kiasi kingine cha fedha kinachunguzwa kubaini kilipo.

Kukamatwa kwa viongozi hao kunatokana na juhudi za Serikali katika mapambado dhidi ya matumizi mabaya ya madaraka pamoja na fedha za umma.
 
Februari 19, 2019 akiwa katika ziara yake wilayani Misungwi Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alimsimamisha kazi Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Bw. Sebukoto na kuagiza achungunzwe na vyombo husika.
 
Alichukua hatua hiyo baada Mwanasheria huyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kushindwa kuishauri vyema halmashauri hiyo na kuisababishia hasara ya sh. milioni 278.

Amesema Mwanasheria huyo Novemba 2017 wakati alipokuwa anakaimu nafasi ya ukurugenzi aliidhinisha malipo ya sh.milioni 278 zilipwe katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw. Anthony Bahebe.

Waziri Mkuu alisema Bw. Bahebe aliishtaki halmashauri hiyo akidai kulipwa fedha kwa ajili ya kazi ya ukandarasi wa mradi wa maji Igenge uliojengwa na kampuni ya ukandarasi ya Seekevim.

Alisema mradi huo ulianza 2014 na ulitakiwa ukamilike 2015. Mwanasheria huyo aliidhinisha malipo hayo wakati ambao tayari hati maalumu ya uwakilishi ilikuwa imekwisha tangu Desemba 2015.

Alisema Mwanasheria alimlipa Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kufanya kazi na Halmashauri jambo ambalo ni kinyume na maadili ya utumishi wa umma.

Hivyo alitumia fursa hiyo kuwakumbusha watumishi wa umma kuzingatia maadili ya utumishi na matakwa ya kisheria katika utekelezaji wa majukumu yao.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, FEBRUARI 21, 2018.
Share:

MAKALA: HALMSHAURI YAWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO

Image result for VIJANA MTWARALICHA ya serikali kupitia Mfuko wa kuwasaidia vijana na Wanawake kuendeleza juhudi za kuwainua Kiuchumi vijana mbalimbali,bado vijana hao wanashindwa kutumia vyema fursa hiyo

Kundi hilo la vijana ambalo linawajumuisha wanaomaliza elimu za vyuo vikuu,vijana wasiokuwa na ajira na vijana wote kwa ujumla wenye Umri (18-35) Wanaopatiwa Mikopo kiasi cha 5% kwa vijana na 5% kwa wanawake katika makusanyo ya mapato ya ndani katika halmshauri ili wajiendeleze,bado vijana wanashindwa kutumia fursa hiyo vyema na hatimaye wnabaki kuzurura na vyeti mikononi na wengine kulalamika kukosa ajira au kukosa mitaji ya biashara
Halmashauri ya Manispaa ya mtwara mikindani ni Miongoni mwa halmashauri ambazo hutoa mikopo kwa Vijana na wanawake kila mwaka

Kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Manispaa hiyo imetenga shilingi milioni 487,514,287 kwa jili ya Mfuko wa wanawake na vijana (WDF) Ambayo ni sawa na asilimia 10 ya mapatao yake ya ndani na inatarajiwa kunufaisha vikundi 110

Hivi karibuni afisa maendeleo ya jamii wa halmshauri hiyo Juliana Manyama alikaririwa akisoma taarifa ya utoaji wa Mikopo alisema kuwa kwa awamu ya kwanza Jumla ya Mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 154,180,000 imetolewa kwa vikundi 48 ambavyo kati ya hivyo vya vijana ni nane peke yake

Vikundi hivyo vilivyopatiwa mikopo hujishughulisha na miradi mbalimbali ikiwemo uuzaji wa samaki,uvuvi na ufugaji 
Kati ya idadi hiyo wapo vijana kutoka Makundi mbalimbali ya waliosoma na wasiosoma na kwamba idadi ya vijana wanaojitokeza ni ndogo ukilinganisha na idadi ya vikundi vilivyopo katika manispaa hiyo

Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Bi Beatrice Dominic anasema kuwa kati ya vijana waliopokea Mikopo hiyo wengi wanajishughulisha na shughuli za kilimo,uvuvi na shughuli nyingine za ujasiriamali ambao wanatoka katika kata mbalimbali ndani ya Manispaa hiyo ya Mtwara Mikindani

Hivyo anawaasa Vijana wanaoishi katika manispaa hiyo kuitumia vyema fursa ya Mikopo inayotolewa na halamshauri hiyo,ili kukuza mitaji na kuongeza kipato na ajira,miongoni mwao na kufanya vikundi hivyo kunufaika na kutimiza Malengo ya serikali katika kukuza uchumi wa vijana nchini hususani katika halamshauri hiyo

Bi Dominiki anasema kuwa licha ya vigezo na masharti ya kupata mikopo hiyo iko wazi lakini bado vijana wanaojitokeza na kuomba mikopo hiyo idadi yake bado ni ndogo nikilinganishwa nan kundi la wanawake

Hivyo anaendelea kutoa msisisitizo kwa vijana kutumia vyema fursa hiyo,kukuza mitaji,kuongeza kipato na fursa za ajira Miongoni mwao ili waweze kujikwamua katika umaskini na kuondokana na dhana ya kutegemea kuajiriwa

Mkuu wa wilaya ya Mtwara Evodi Mmanda akizungumza katika hafla ya kutoa hundi kwa vikundi 48 mwanzon mwa mwezi December 2017 katika ukumbi wa Boma anasema kuwa wakati Tanzania ikielekea kwenye viwanda wajasiriamali wanatakiwa wajipange kwa ajili ya kupata ajira kwa wageni watakaokuja kujenga viwanda mtwara lakini ni fursa kwao kutengeneza bidhaa kama nguo,kupika chakula kwa mama lishe,uzoaji wa taka unaozalishwa

VIJANA WANASEMA

MWENYEKITI wa Jukwaa la vijana Manispaa ya Mtwara (MYEF)Na mwasisi wa Jukwaa hilo Salum alfati Ngauja Anasema kuwa changamoto kubwa inayowafanya vijana kutochangamkia fursa hiyo ni kutokana na vijana wenyewe Kutokuwa na utayari na wengine kuwakatisha Tamaa wale wanaoomba mikopo

Licha ya Changamoto hiyo amesema kuwa baada ya kupata Mafunzo mbalimbali yaliyowawezesha kuimarika na hadi kubuni wazo lam kuanzisha Jukwaa la kuwainua vijana Katika manispaa ya mtwara Mikindani,sasa wamebuni Mradi wa kilimo na tayari wametuma Maombi ya Mkopo katika manispaa ya Mtwara Mikindani

Amesema kuwa Kupitia Jukwaa hilo lenye zaidi ya vijana 150 wameomba kiaisi cha Takribani milioni ishirini kwa ajili ya Mradi huo na tayari wametimiza Vigezo vyote na wanatarajia kupata mkopo hivi karibuni

Hivyo anawaasa vijana wengine nchini kujaribu na Kudhubutu,bila ya kukata tamaa kuomba Mkopo Jambo litakalowasaidia kujiajiri na kuinua uchumi,pasipo kuajiriwa

Ngauja anasema kuwa Mafaniko mengi yanatokana na uvumilivu na kwamba vijana wasisubiri ajira bali wajiajiri kwa ubunifu wowote,ili wapambane na changamoto za ukosefu wa ajira,zinazowakumba vijana wengi

Anasema kuwa akiwa kijana aliamua kubuni wazo la kuanzisha jukwaa hilo ili liwe chombo cha kuwasaidia vijana kuelezea matatizo yao

Aidha amesema kuwa waliamua kubuni mradi wa Kilimo kwa kuwa wameona kuwa mradi wa Kilimo ndio unaolipa zaidi

“wengi wanashangaa vijana kufanya kilimo,ila ukweli kilimo kinalipa sana na ni kitu kitakachoweza kuleta manufaa na na kuongez uchumi”anasema Ngauja

“na kilimo tutakachofanya ni tofauti kwani tutalima mazao hasa ya mbogamboga na itakuwa ni kwa mwaka mzima hatutategemea mvua,tutafanya kilimo cha umwagiliajai”anaongeza Ngauja

Ngauja anaongeza kuwa watalima mboga za majani aina zote na viungo ikiwemo nyanya,bamia,hoho n.k

Mmoja wa vijana wa jukwaa hilo Farida abdulrahman,akisoma risala wakati wa uzinduzi wa Jukwaa hilo hivi karibuni anataja malengo ya jukwaa hilo ni pamoja na kutanua wigo wa kuwasaidia vijana wenye fani tofauti tofauti kukaa pamoja na kubadili fikra za vijana na kuondokana na dhana ya kusubiri kuajiriwa

Mtazamo wao ni kupata fedha na kuondoa kabisa hali ya umsikini miongoni mwa vijana wa halmshauri hiyo

Mmoja wa vijana hao Betina Mpinga Amesema kuwa katika mRadi huo changamoto inayowakabili ni pamoja na uhaba wa Ardhi kwani kilimo kinahitaji Ardhi kubwa kutokana pia na idadi kubwa ya vijana kuendelea kujiunga na jukwaa hilo watahitaji ardhi kubwa itakayowawezesha kufanya kilimo ambapo alitoa wito kwa halamshauri kuangalia changamoto hiyo kwa jicho la pili

Pia anasema kuwa licha ya vijana hao kujishughulisha na kilimo pia wapo vijana wengine wenyue fani mbalimbali kama udereva,upishi,ushonaji na hata upambaji hivyo kupatikana kwa mkopo kutoka halamshauri utawainua na kuwawezesha kutimiza lengo la jukwaa hilo

Vigezo vya Vijana kujiunga katika jukwaa hilo ni kijana yeyote mwenye nia ya dhati ya kupambana na umaskin anayeishi ndani ya manispaa ya Mtwara mikindani.

Na John Massawe - Jamii Fm Radio
Share:

Serikali yatoa tamko walimu wa sekondari kufundisha Shule za msingi

#Serikali imesema #mwalimu wa sekondari kufundisha shule ya msingi si kushushwa #cheo na wala si jambo la ajabu.

Taarifa ya mkuu wa kitengo cha mawasiliano Ofisi ya Rais (Utumishi), Florence #Lawrence imesema Serikali kuwapangia baadhi ya walimu wa sekondari kufundisha shule za msingi ni moja ya hatua za kuongeza ufanisi na kuleta mgawanyo sawa wa walimu katika shule hizo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk Laurean Ndumbaro amekaririwa katika taarifa hiyo iliyotolewa leo Februari 20,2018 akisema hatua hiyo haimaanishi kuwa walimu wanaotoka katika shule ya #sekondari kwenda kufundisha msingi wameshushwa cheo.

Dk #Ndumbaro ametoa ufafanuzi huo katika kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako.

Amesema lengo la Serikali ni kuondoa upungufu wa walimu katika shule za msingi na kuimarisha utoaji wa elimu.

Katibu mkuu ameainisha kuwa sifa za kufundisha na kiwango cha elimu zinaendana na mabadiliko yanayotokea duniani, hivyo mwalimu mwenye elimu ya kiwango cha Shahada ya kwanza kufundisha shule ya msingi isionekane ni jambo la ajabu.

Dk Ndumbaro amewaambia watumishi wa umma kuwa, maendeleo katika sekta yoyote, ikiwamo ya elimu yanakuja na mabadiliko hivyo wayapokee na kufanya kazi ili kufikia lengo.
Share:

IARA YA MAKAMU WA RAIS WILAYA YA MEATU MKOANI SIMIYU

17#Makamu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. #Samia #Suluhu Hassan leo ameendelea na ziara yake katika mkoa wa Simiyu ambapo ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa bwawa la maji kwa ajili ya binadamu na mifugo katika eneo la Mwanjolo, wilayani Meatu mkoani Simiyu.
Bwawa hilo la maji litahudumia #wananchi kumi na tatu elfu na mifugo laki moja na elfu nane wa Mwanjolo, mradi huo mpaka kukamilika utatumia shilingi za kitanzania bilioni 1.6 na utahifadhi kiasi cha maji lita 345,129,000.
Makamu wa Rais aliwataka wananchi wa Mwanjolo kulinda vyanzo vya #maji na kutunza mazingira.
Akizungumza na Wananchi waliojitokeza kushuhudia uwekaji jiwe hilo la msingi Makamu wa Rais alisema “ Serikali ya awamu ya tano ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa wananchi wote”
Makamu wa Rais aliwapongeza wananchi wa Wilaya ya Meatu kwa kulima pamba kwa wingi ambapo wilaya hiyo inategemea kilo 84 na kuwaahidi wananchi hao kuwa dawa za kuulia wadudu zitapatikana kwa wingi kuanzia mwisho wa mwezi huu kwani serikali imetoa fedha zaidi ya bilioni 9
Makamu wa Rais aliwaambia wananchi hao kuwa barabara zote ambazo ilani ya uchaguzi imeahidi kuzijenga zitajengwa na zile ambazo hazipo kwenye ilani ila zina umuhimu zitaingizwa kwenye bajeti ijayo.
Wakati huohuo Mbunge wa Jimbo la Kisesa Mhe. Luaga Mpina alisema kuwa kati ya kata 13 ni vijiji vine tu vina maji hivyo alimuomba Waziri wa Maji kusaidia zaidi upatikanaji wa maji.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe aliahidi kusimamia kwa ukamilifu upatikanaji wa maji .
Share:

WAENDESHA BAISKELI ZA ABIRIA WAPINGA AGIZO LA KUONDOKA MJINI GEITA

Waendesha Baiskeli Maarufu kwa jina la daladala wanaosafirisha abiria kwenye halmashauri ya mji wa Geita, wamepinga agizo la Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo la kuwataka kufikia leo wasitishe shughuli zao kwenye maeneo ya mjini badala yake wafanye kwenye maeneo waliyopangiwa.
 
Hatua hiyo imekuja baada ya kupewa muda wa siku tano kupisha maeneo ya mjini kutokana na wimbi la ajali zinazosababishwa na waendesha Baiskeli kwa kutotumia barabara vizuri wanapokuwa kwenye shughuli zao.
 
Baadhi ya waendesha Baiskeli hao Bw Vistusi Maagani, John Maige na Fredy Maganga wamesema utaratibu uliofanyika sio mzuri kwa kuwa hawajapewa maeneo yatakayowasaidia kufanya kazi zao .
 
“Nasikitishwa sanaa na kitendo cha Mkurugenzi kututoa bila ya kutuandalia maeneo mazuri ya kufanyia kazi zetu kwa mfano mimi hapa hii kazi ndio nategemea kulisha familia pia kutuma pesa kwa mama yangu mzazi kwa kuwa sina ndugu leo natolewa kufanya kazi mjini unategemea nitaishi maisha gani jamani na wale ambao wananitegemea nitawaelezaje mimi naomba haya maamuzi wayaangalie kwa umakini”Alisema Maagini.
 
“Nashindwa hata niseme nini najisikia moyo wangu kutoka  kabisa kutokana na taarifa hii ya kuondolewa mjini maeneo ambayo tunaambiwa kufanya kazi akuna abiria sasa sijui tutaishije sisi waendesha daladala”Alisema  Maganga.
 
Bi,Lucia Paul ambaye mume wake anajishughulisha na kazi hizo alisema  kuondolewa mjini kwa waendasha baiskeli kutaleta athari kwenye familia zao kutokana na wengi wao kutegemea shughuli hiyo kukidhi mahitaji ya familia.
 
“Kwasasa hivi nyumbani hapakaliki kila siku mume wangu anamawazo anashindwa afanye nini na uku anafamilia muda mwingine hadi namuonea huruma  serikali ni vyema ikaangalia maana itatupa wakati mgumu sisi wanawake ambao tunawategemea waume zetu kwenye utafutaji”Alisisitiza Lucia.
 
Kutokana na hali hiyo chama cha ACT wazalendo kupitia kwa katibu wa mkoa huo,Bw Ikolongo Otoo  ameitaka halmashauri ya mji wa Geita kuondoa mara moja zuio hilo  kwa kuwa ni la kibaguzi ambalo alijazingatia wala kuthamini vijana masikini na wanyonge ambao wameamua kujipatia vipato kwa njia halali kabisa.
 
Mkurugenzi wa Halmashari ya mji wa Geita,Mhandisi Modest Aporinaly  alisema suala ambalo linafanyika ni la utekelezaji na alilikuwa aliitaji  muda kwani maeneo ambayo wamewapatia kufanya biashara ni makubwa na kwamba hata wangepewa muda  wa kutosha bado wangeombwa kuongezewa.
 
Mbunge wa Jimbo la Geita mjini,Constatine Kanyasu alisema  ahafikiani na makubaliano hayo na kwamba akuna utaratibu wala sheria ambayo inawazuhia waendesha Baiskeli kufanya shughulo zao maeneo ya mjini.
Share:

Sikiliza jamii FM Radio

🎧 Jamii FM Live

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

Blog Archive

WAENDESHA WEBSITE

Contact Form



1 ] )[0]; $title = $recent_post['post_title']; $excerpt = wp_trim_words( $recent_post['post_content'], 20 ); $image = get_the_post_thumbnail_url( $recent_post['ID'], 'full' ); ?>